Nimedonoadonoa hoja yako na ukweli ni kwamba nafikiri madhaifu ya awamu ya nne yanatokana na "mamlaka ya juu" kukosa vision ya kitaifa hata kutumia kwa ufanisi mawazo ya PM wake kujenga taifa imara kupitia mfumo mzuri wa Elimu na KIlimo.
Utashi wa Lowassa wa elimu na wa Pinda wa kilimo, ulitakiwa ufanyiwe tathmini ya makini ya dharura na kupewa kipaumbele cha hali ya juu na hata kufanyiwa micro management na watu kama BRN walipaswa kuwa wanaouliza maswali yote ya kwanini kwanini na ilikuwa kwanini mpaka kieleweke.
Lakini hata kama nikimpa tano kwa sera ya kulitangaza Taifa kuwa mahali poa pa kuja kutalii na kufanya biashara, wenzetu wanatarajia kuwa watakuja kwenye nchi yenye fluid movement, si ukiritimba na umangimeza.
Wanatarajia wakija, kuna umeme, maji, competent labor force, functional systems za miundombinu, uchukuzi na kujali muda (time is Money).
Sasa tunaitangaza nchi kuwa kuna neema, hata watalii kuja kuangalia Tembo wananza kuuliza tembo wamejificha? kisha huamua kupitia kenya maana fluidity ya mambo Kenya ni bora kuliko Tanzania.
Hivyo kwa miaka 10, Kikwete amewekeza kuitangazia Tanzania kwa wawekezaji na kuwa kuna vivutio vya kutosha, lakini kama umeme na maji ni shida, basi projection zangu za income na growth lazima zifidiwe na hapo ndipo mtu anaomba msamaha wa kodi na ushuru kwa miaka 5 na anapewa!
Kama tunataka kuendelea, lazima tuwe na viongozi wenye vision na weneye uwezo wa kuweka sera zinazoeleweka na kuzifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kuunda timu na kuzimamia Sera ifanikiwe na si kuachwa kwa wengine waifanyie kazi!
Mkuu , nadhani JK hajaitangaza Tanzania kwa njia muafaka.
Alichotekeleza ni sera/Ilani ya CCM ya kuomba omba. Safari 410 hazina tija ukilinganisha na alipoikuta na kuiacha nchi
Kwa ufupi, safari 410 katika wastani wa siku 1 kwa safari ni sawa na siku 410 ambazo ni sawa na mwaka 1.
Tukifanya wastani wa siku 1 kwa safari, ina maana Rais hakuwa ofisini kwa mwaka 1 katika 10 aliyokaa madarakani
Jaribu kufanya wastani wa siku 5........
Katika muda huo tunaambiwa alikuwa anavutia FDI n.k. Takwimu za kimataifa zinaonyesha tupo nyuma ya mjirani zetu ambao marais wao hawasafiri na hata kama wanafanya , katika miaka 10 hawajafikia hata safari 50
Wawekezaji wanataraji kuwekeza katika mazingira yanayohakiklisha usalama wa mitaji yao.
Pale wanapogundua kuwa hakifanyiki kitu ila kwa rushwa, wanaposikia madili yanayohusisha serikali , wanakosa imani ya kuweka mabilioni yao katika 'volatile and hostile environment ' kama ya Jserikali ya JK
Lakini pia wanajiuliza, kama kuna sababu za kubebea jenereta wakija na mitaji yao.
Wanajiuliza kama kuna sababu za 'simtank' kwasababu hakuna maji.
Wanapoangalia eneo kama Nairobi, hawana sababu za kuwekeza Dar
Ndio maana mashirika mengi na balozi nyingi zina ofisi Nairobi.
Katika mtazamo huo, kiongozi hakuwa na vision wala mission. Mawaziri wakuu waliojaribu hawakuweza kwasababu zile zile za mazingira mabovu ya uongozi. Kama walivyo wawekezaji hata mawaziri wakuu yamewakuta
Haionekani kama Watanzania wamejufUnza jambo.
Mwaka 2005 tuliambiwa kiongozi ni mzuri anapendeza.tukiangalia nyuma Watanzania ni masikini na fukara kuliko 2005.
Sasa tunaambiwa kuna baunsa wa push up. Hatujiulizi , tunashangilia tu.
Hatujishughulishi kufikiri kuwa tunataka Baunsa wa kichwa ili tuondoke hapa tulipo
Hatujiulizi , miaka 50 nguo inaongezeka viraka badala ya kupata mpya. Tunakazana kuweka viraka! hatufikirii zaidi hapo