Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

KUJUIZULU KWA Ms.WASSERMAN

Democrats wamefanya damage control mapema kwa kumshinikiza Ms Wasserman ajiuzulu. Licha ya kujiuzulu,ameonekana ukumbini akiendelea na maandalizi ya mwisho

Habari hii haimgusi Bi Clinton moja kwa moja kama mhusika.
Inamgusa kupitia maandalizi ya mkutano,kampeni na distractions zinazoambata nalo

Bado details za nini kimetokea zinasubiriwa, lakini ni mpango mahususi kuamkia siku muhimu kwa Democrats

Nani anahusika, linabaki swali, tunaona siasa zikiwa na timing! 'mchezo mezani'

Madhara kama tulivyoeleza bandiko la hapo juu yapo katika maeneo haya

1. Kupoteza Focus: Habari iliyotanda imefunika mkutano mkuu kwa siku nzima.
Na haineokani kama itapotea siku za karibu.

Hii inaweza kuwa kibwagizo na pengine kati kati ya mkutano yakatokea makubwa

Kesho anaongea Michelle Obama na Benie Sanders miongoni mwa wengi.

Ilitarajiwa wa set tome ya mkutano, kinyume chake emails zimechukua nafasi.
Hili ni pigo kubwa kwa kampeni ya Clinton

2. Trump apata silaha: Kama anavyomwita crooked Clinton na sasa hili linahusu Democrats, Trump atasema Sanders hakutendewa wema a system ipo rigged.

Hili atalifanya kila siku na athari zake ni kama namba 1 hapo juu
Lengo ni kuwavuta wafuasi wa Sanders ambao bado wana uchungu na chaguzi

3. Vidonda kuvuja damu: Sanders amesha mui endorse Clinton,tofauti na Cruz aliyesababisha timbwili bila endorsement.

Hata hivyo Sanders alisema Bi Wasserman anampendelea Clinton katika hatua za awali

Hoja ya Sanders ililenga kumshinikiza Wasserman akubali wazo la kuwa na chaguzi kwa taratibu anazotaka. Kwamba, kwenye closed elections, zifanywe open.

Hii ni kwasababu aliamini kushinda katika open na si closed. wasserman alikataa

Hoja ya pili,'super delegates' wasihesabiwe kabla ya mkutano mkuu,nalo lilikataliwa

Hoja ya wasserman ilikuwa kuwa, kubadili kanuni mchezo ukiendelea halikuwa jambo la haki. Kwamba, Sanders alifahamu taratibu, akazikubali na ku sign

Sasa, hili la emails Sanders anasema. 'alishasema hatendewi haki'
Na kwavile zime leak, hakuna atakayejali ni haki gani hakutendewa bali kuona hakutendewa haki tu.

Wafuasi wake wenye machungu wataamka kwa hasira na litawagawa democrats.
Trump atakapoisukuma hoja hiyo, hasira na vidonda vilivyoanza kupona vitaibuka upya.

Nini kitatokea Sanders atakapoongea kesho haijulikani.
Je, atamwaga mboga kama Cruz? Atafanikiwa kushawishi wafuasi wapuuze suala hili?

Ikizingatiwa wafuasi wa Sanders walikuwa waandamane kudai sera ya dollar 15 kwa saa kama kima cha chini, huenda kesho kukawa na maandamano zaidi

Katika fukuto hilo democrats wapo katika mtafaruku pengine mkubwa kuliko wa Trump. Tusubiri nini kitatokea

Tutawaletea habari za mkutano in 'real time' mambo yakienda kama tunavyotaraji

Tusemezane
Ni kweli DNC imeanza kwa vituko. Pamoja na kuachia ngazi kwa aliyekuwa mwenyekiti, Debbie Wasserman Schultz, mambo bado si shwari ndani ya DNC na leo kaonja joto la jiwe kwa wanaoaminiwa ni wafuasi wa Bernie Sanders. Hao wafuasi ambao wanaonekana kutokubali tamko la Sanders la kumuunga mkono Clinton, wameshikilia kwamba kama matakwa yao hayatimizwi hawako tayari kubadili msimamo wao. Kwenye Breakfast Club wamemzomea Debbie hadi ikabidi akatishe hotuba yake.

Bernie-goes-to-the-DNC-1.jpg
Picha hii hapo juu inatoa taswira ya hao wapenzi wa Bernie Sanders ambao hawakumbali Clinton na swala la Emails limezidi kukuza madai yao kwamba uongozi wa DNC ulimpendelea Clinton. Wapo baadhi yao bado hawaamini Clinton alishinda kihalali na kwenye ukumbi walionekana wamebeba mabango yaliyoandikwa E-MAILS na mengine yanayomsifu Sanders. DNC itabidi watafute mbinu ya kuwatuliza hawa mashabiki wa Sanders.
 
Kinachofurahisha ni namna watu walivyo huru kutetea misimamo yao bila bugdha...wanaoshangilia na wanaozomea wamesimama bega kwa bega bila ugomvi. Kinachosubiriwa leo baada ya kufunguliwa rasmi kwa Convention ni namna DNC itakavyoweza kukabiliana na hali hiyo iliyojitokeza. Maandamano yanayotarajiwa kufanyika yamegawanyika katika makundi mbalimbali yenye malengo tofauti.

Kundi la kwanza ni la wapenzi wa Sanders ambao hawakuridhika na ushindi wa Clinton. Kundi la pili ni la Black lives matter ikiwa na maana ya hatari inayowakumba weusi mikononi mwa vyombo vya usalama na hasa polisi. Kundi la tatu ni la wanaharakati wanaodai msimamo wa Democrats katika swala la mazingira. Yapo pia makundi mengine zaidi yanayosubiriwa kuwepo mjini Philladelphia, wakati wa Convention.

Inakadiriwa kuwa idadi ya waandamanaji wote inaweza kufikia elfu kumi.
 
Mkuu Mag3
Katika mkutano wa ndani ya DNC kutengeneza platform kule Orlando, wafuasi wa Sanders walishinikiza kila madai yao yatekelezwe ikiwemo Sanders kuwa VP.

Mengine yalitekelezwa katika kuleta unity, mengine hayakutekelezwa.

Majuzi walipanga kuandamana kushinikiza minimum wage katika kiwango cha Sanders

Hili lilikuwa lifanyike kwa mtindo wa 'Never Trump' ya Republican, mkutano ukiendelea

Hivyo, bila emails tayari kulikuwa na mtafaruku unaoendelea.

Hili la emails ni kama lime cement reservations walizokuwa nazo.

Basically tuhuma dhidi ya upendeleo zilikuwa katika kushinikiza
1. Chaguzi zote ziwe katika open isipokuwa caucus alizoshinda Sanders! Debbie akataa
2. Uchaguzi uende DNC kwa kuondoa wajumbe 'super delegates'. Debbie akakataa

Hili la emails wanalichukulia kama sababu, ndiyo maana hawawezi kueleza ni uchaguzi gani au ni njia zipi zimetumika kumpendelea Clinton zaidi ya madai yao 1 na 2 hapo juu

Kwa takwimu, Obama ndiye aliyewahi kupata popular vote/delegates kuliko wengine

Hillary alikuwa wa pili kwa popula vote/delegates na super delegates kwa takwimu za Dem

Hivyo maelezo na madai yao yana base katika emails na siyo takwimu zilizopo

Kosa mbalo DNC wamelifanya ni kuendelea kumwacha Debbie katika mipango ya leo

Alitakiwa akae pembeni kuanzia jana. Uwepo wake unahusishwa na Clinton na ni doa

Wafuasi wa Sanders wapo tayari kuona Dem inazama, na hapo ndipo DNC walipo na tatizo

Kinachosumbua DNC, leo Sanders akizungumza katika Cruz fashion, DNC will crumble

DNC wanona hili ni ammunition kwa Republican.

DNC wanaona unity going forward itakuwa questionable

Wapo katika tatizo kubwa kuliko la Melania au Ted Cruz.

Melania na plagiarism iliondoa tu ladha ya hotuba yake bila madhara kwa mgombea.

La Cruz lilikuwa ni ''vendetta'' kati ya wawili Trump vs Cruz.

Hili la DNC ni family feud, lita dissect voters na kuacha madhara makubwa

Tusemezane
 
Kinachofurahisha ni namna watu walivyo huru kutetea misimamo yao bila bugdha...wanaoshangilia na wanaozomea wamesimama bega kwa bega bila ugomvi.

Kundi la kwanza ni la wapenzi wa Sanders ambao hawakuridhika na ushindi wa Clinton.
Kundi la pili ni la Black lives matter ikiwa na maana ya hatari inayowakumba weusi mikononi mwa vyombo vya usalama na hasa polisi.

Kundi la tatu ni la wanaharakati wanaodai msimamo wa Democrats katika swala la mazingira. Yapo pia makundi mengine zaidi yanayosubiriwa kuwepo mjini Philladelphia, wakati wa Convention.

Inakadiriwa kuwa idadi ya waandamanaji wote inaweza kufikia elfu kumi.
Hakuna kutishana watu wapo huru.

Hakuna anayeahidi kuondoa wenzake katika chama, hakuna kuzuia maandamano kama haki ya msingi yakujieleza. Watu wanatumia haki zao za kidemokrasia

Katika makundi matatu uliyosema, kundi hatari ni la Sanders.
Hili limebeba agenda ya kundi la tatu kuhusu mazingira, yaani two in one.

Msimamo wa Dem kuhusu mazingira upo wazi na Clinton akiwa secretary wakati wa maandalizi ya Paris conference inampa upper hand, isingekuwa tatizo kubwa

Balck lives matter nalo lina tatizo kubwa.
Linashinikiza kupewa kipaumbele katika agenda za mkutano.

Kibaya ni kuwa mauji yanayotokea ya Polisi yanahusishwa na kundi hili.
Hivyo ku balance kati ya haki zao na haki za Polisi kuna tatizo kubwa sana

Republican wamejipambanua kuwa na Polisi ' blue lives matter' bila kujali madai ya black lives matter' na kundi la BLM linatafuta mhali pa kutokea ambako ni Democrats

Ugumu ni pale ambapo BLM linapokuwa sehemu kubwa ya 'electoral college' ya Democrats

Wana balance vipi kuzima hoja ya law and order at the same time ku accommodate BLM?

DNC ina tatizo kubwa na huenda mkutano ukaisha kukiwa hakuna clear message
 
Mkuu Nguruvi3, ni kweli kundi la hatari kwa DNC ni la wanaojiita wafuasi wa Bernie Sanders. Mpaka sasa hili kundi, pamoja na kuhusishwa na Sanders, halijulikani linafadhiliwa na nani. Kinachoanza kuwashtua watu ni tamko lao kwamba kwa sasa Sanders hata akisema nini sasa hawatajali na wameanza kumlaumu kwa ahadi yake ya kumuunga mkono Clinton na kusema amewasaliti kama walivyosalitiwa na Elizabeth Warren.

Lingine la wasiwasi ni kuhusu taswira linaloanza kujitokeza kuhusu hili kundi...sura zote kwa asilimia zaidi ya 98% ni weupe na mpaka sasa hakuna mweusi aliyejitokeza mtaani kuwaunga mkono. Wanapopewa tahadhari kwamba kuipa kura Green Party ni sawa na kumpa kura Trump, msemaji wao naye katoa tahadhari kuwa kama Trump atashinda wasilaumiwe wao, walaumiwe viongozi wa DNC waliomteua mgombea dhaifu, Bi Clinton.
 
Mkuu Mag3 swali ulilozungumzia kuhusu nani yupo nyuma ya Sanders,tuliwahi kuliuliza katika uzi wa Uchaguzi wa Marekani.

Tulisema, nguvu ya kundi la Sanders ipo kwa weupe, kwanini?

Na kwanini ameshindwa ku attract colored kama black na Latino?
Hawa wanatengeneza sehemu kubwa ya 'electoral college' ya Democrats.

Tuliuliza kwanini linapata media coverage na 'interest' na kundi hilo.

Emails zinaeleza kwa kiasi fulani who is behind Sanders campaign

Sasa hivi breaking news, FBI wanachunguza nani alifanya 'hacking' na kwanini

Kuhusu kundi la Sanders
Maandamano ni kumpinga Debbie. kuna hoja ya mazingira ambayo Sanders alimtuhumu Clinton kuchukua fedha za makampuni yanayofanya 'fracking'

Hivyo ni kundi moja limejigawa mara mbili, kwa Debbie na mazingira

Kundi la Black lives matter lina mkono wa Sanders pia.

Utakumbuka Bill Clinton alipopingwa na BLM kuelekea uchaguzi wa New York

Hivyo makundi matatu uliyosema in fact ni moja lililojigawa kuweka pressure

Kinachoonekana ni frustrations za plan A na B ya Sanders kufeli.

Plan A kumshinikiza Debbie abadili chaguzi kuwa open, na kumshinikiza uchaguzi- DNC

Plan B, kutumia emails akiwa secretary of state katika DNC kama ingekubalika, au kumuengua kupitia FBI. La FBI haiku materialize wala DNC

Hili la emails za Debbie, lilikuwa litumike na emails za Benghaz kama uchaguzi ungeenda DNC. Haikufanikiwa, na sasa kundi linajigawa mara tatu
 
Mkuu Mag3 swali ulilozungumzia kuhusu nani yupo nyuma ya Sanders,tuliwahi kuliuliza katika uzi wa Uchaguzi wa Marekani.

Tulisema, nguvu ya kundi la Sanders ipo kwa weupe, kwanini?

Na kwanini ameshindwa ku attract colored kama black na Latino?
Hawa wanatengeneza sehemu kubwa ya 'electoral college' ya Democrats.

Tuliuliza kwanini linapata media coverage na 'interest' na kundi hilo.

Emails zinaeleza kwa kiasi fulani who is behind Sanders campaign

Sasa hivi breaking news, FBI wanachunguza nani alifanya 'hacking' na kwanini

Kuhusu kundi la Sanders
Maandamano ni kumpinga Debbie. kuna hoja ya mazingira ambayo Sanders alimtuhumu Clinton kuchukua fedha za makampuni yanayofanya 'fracking'

Hivyo ni kundi moja limejigawa mara mbili, kwa Debbie na mazingira

Kundi la Black lives matter lina mkono wa Sanders pia.

Utakumbuka Bill Clinton alipopingwa na BLM kuelekea uchaguzi wa New York

Hivyo makundi matatu uliyosema in fact ni moja lililojigawa kuweka pressure

Kinachoonekana ni frustrations za plan A na B ya Sanders kufeli.

Plan A kumshinikiza Debbie abadili chaguzi kuwa open, na kumshinikiza uchaguzi- DNC

Plan B, kutumia emails akiwa secretary of state katika DNC kama ingekubalika, au kumuengua kupitia FBI. La FBI haiku materialize wala DNC

Hili la emails za Debbie, lilikuwa litumike na emails za Benghaz kama uchaguzi ungeenda DNC. Haikufanikiwa, na sasa kundi linajigawa mara tatu
Breaking News!
Sanders anaongea na wafuasi wake...ngoja tusikilize!

Update!
Mmmh, inaoenekana kama vile toka aanze kampeni hakujua zimwi alilokuwa akilifungulia mlango. Pamoja na kuwaomba wafuasi wake wamuunge mkono Clinton, bado wako baadhi ya wafuasi wameonesha kutounga mkono kauli yake hiyo. Na sasa wanaandamana wakihoji na kupinga zoezi zima la uchaguzi ndani ya Democratic party.

Na hii ndiyo sababu inayowapa viongozi wa DNC wasi wasi, je hawa watu wanataka nini hasa! Mojawapo anayehojiwa sasa hivi amesema atampigia kura Donald Trump akidai heri miaka minne ya Donald Trump kuliko ya Clinton.

Tutaendelea kuwajuza...
 
Breaking News!
Sanders anaongea na wafuasi wake...ngoja tusikilize!

Update!
Mmmh, inaoenekana kama vile toka aanze kampeni hakujua zimwi alilokuwa akilifungulia mlango.

Pamoja na kuwaomba wafuasi wake wamuunge mkono Clinton, bado wako baadhi ya wafuasi wameonesha kutounga mkono kauli yake hiyo.

Na sasa wanaandamana wakihoji na kupinga zoezi zima la uchaguzi ndani ya Democratic party.

Na hii ndiyo sababu inayowapa viongozi wa DNC wasi wasi, je hawa watu wanataka nini hasa!

Mojawapo anayehojiwa sasa hivi amesema atampigia kura Donald Trump akidai heri miaka minne ya Donald Trump kuliko ya Clinton.

Tutaendelea kuwajuza...
Mkuu keshafunga Pandora's box

Wakati wanasema Bernie or Bust alidhani ilikuwa jambo jema

DNC wana wasi wasi kuwa hawaweza ku 'harvest' na ku recover post convention. Hii ni 'distraction' kubwa sana, hata hivyo Sanders hakwepi lawama
 
Mkuu keshafunga Pandora's box

Wakati wanasema Bernie or Burst alidhani ilikuwa jambo jema

DNC wana wasi wasi kuwa hawaweza ku 'harvest' na ku recover post convention. Hii ni 'distraction' kubwa sana, hata hivyo Sanders hakwepi lawama
Ni kweli alifungua pandora box...baadhi ya waliokuwa wafuasi wa Sanders, msimamo wao ni huu;

Nothing' will make me vote Clinton. Bernie or Bust' is as strong as ever, if not stronger. If the Democratic Party does not select him, we are having a de-registration party at the DNC.
103814286-RTSJG0Z.530x298.jpg

Kaazi kweli kweli...!​
 
Update

Katika mkutano na wafuasi wake, yupo anayeitwa Jeff Cohen mwenye kundi linalojulikana root action and the Bernie Sander network, mwenye wajumbe 1900.

Huyu anasema yeye si kundi lile la Sanders, utashangaa kundi lake limefanya kazi kwa Sanders!!!

Anachotaka ni kuwa na VP mwingine badala ya Tim Kaine.
Wanapendekeza E.Warren au Sherod Brown

Huyu si mjumbe wa mkutano mkuu lakini yupo 'kuongoza' mambo

Hoja ya emails inaonekana kufunikwa na duku duku jingine la VP

Unaweza kuona Sanders alivyoitibua Democrats siku hizi muhimu

DNC wana kazi nzito katika siku nne.

Tutaendelea kuwaleta kinachojiri Philly
 
DNC LIVE

Convention imeanza kwa mizengwe. Wazungumzaji wanaendelea
Tunawasubiri Michelle Obama, Elizabeth Warren na B.Sanders

Tutaendelea kuwaleta habari kama hakutakuwa na usumbufu wa mawasilia
 
Theme ya leo ni Families

Katika wazungumzaji wanaotarajiwa, Elizabeth Warren anategemewa sana kutuliza hali ya mambo. Wakati wa kuombea mkutano mkuu, kelele za kuzomea alipotajwa Hillary zilisikika huku za kumshangilia nazo zikisika

Kwa mtazamo huo kuna mchangnyiko wa hali ya mambo unaotokana na kuwepo kwa kundi la Bernie Sanders. Mwanzoni walijitambulisha kama wanaharakati k, kadri muda unavyosonga mbele ndivyo wanajidhhiri kuwa wafuasi wa Sanders

Live kutoka Philly
 
SENETA KUTOKA OREGON

-Trump ni tajiri kwa kuchukua advantage ya Waamerika

-Anadhulumu makampuni madogo na kutengeneza mipango feki'scan'

-Hajawahi kufanya kazi kama Amerika worker kama alivyodai katika mikutano

-Watu wanahangaika kulipa mortgage au kupeleka shule

-Suluhisho si kulaumu bali kutfatua suluhu

-Tumemsikia Sander akihamasisha katika hali, na ni hamasa kubwa

- Clinton na Sander wametengeneza common plaform

- Wametengeneza renewable energy, na affordable school fees

-Tunataka kuwa pamoja katika usawa ikiwemo LBGT

-Tufanye kazi nao kuondoa ubaguzi

-Tunataka kufanya kazi kwa pamoja na kukataa bada trade bill kama anvyosema Clinton.

- Pamoja tupiganie serikali ya watu kwa ajili ya watu na siyo wenye fursa

-Tutafanikiwa tukifuata sera za Sanders na Clinton

-Tuungane, iwe kwa Sander au Clinton lazima tusimame pamoja

-Tuwe pamoja katika nguvu ya kura, kama Sander na Clinton wallivyofanya

Ahsanteni
 
Karla Ortis na Fransisca

- Binti mdogo anaeleza experience yake kuhusu uhamiaji

-Amezaliwa Nevada, na kila asiku ana hofu, muda wowote baba na mama yake watalazimika kuondoka. Anataka kukua kuwa lawyer

-Clinton amesema nisiwe na hofu, atakuwa na hofu kwa ajili yetu

Mama anaongea
-Anaongea kilatini

-Hillary for president, ahsante sana
 
Astrid Silva

Anaeleza kuhusu safari yake ya immigration

-Nimemaliza chuo cha Neavada baada ya safari ya miaka 10

-Familia ipo hapa kwasababu ya watu kama seneta Reid.

-Trump akiongea kuondoa watu milioni 11, anaongea kutenganisha watu

-Hillary anafahamu hiyo siyo thamani ya familia na Amerika

Ahsante
 
Muongeaji mwingine

-Nimekulia Puerto Rico, hawakuwa na elimu wala winter coat nilipozaliwa katika mji wa Chicago.

-Mtu mmoja anataka kuzingira watu na kuwaondoa

-Tuungane katika vita na Clinton

-Amerika inabaki welcoming nation

- wahamiaji wanachangia uchumi wa nchi, na wanatoa maana ya waanzilishi wa Taifa. 'We the people'

-Wahamiaji milioni 11 wanaishi na kulipa kodi, sikilizeni, bila kujali unaonekanje, immigration system ya Amerika ni muhimu kwa mabadiliko

-Hillary ndoto yake ni kuwatoa immigrants kutoka gizani na kuhakikisha wanalipa kodi zao

-Hillary anapigani unity ya watu wa rangi zote na anajua climate change is real. Tunaendelea kufanyia kazi nadhari za kina Louis na MLK

-Tunaamini katika nchi ambaye mzaliwa wa Puerto Rico anaweza kuzungumza katika mkutano kama huu katika 'heart of America'

Ahsanteni
 
Jeissen na mwenzake

Tuna watoto watatu mimi na mke wangu

-Nataka watoto wangu wajue kila kitu kinawezekana Amerika

-Utawaambia nini watoto ukiwa Bully kama Trump, ukidharau wahamiaji

Nina heshima kumkaribisha mwenzangu

Anayeongea sasa ni Gay
Mchezaji wa NBA aliyejitokeza, na anasema shukrani kwa familia ya Clinton, iliyojua kipaji chake cha kucheza

-Hillary amefanya kazi na LBGT. Wote kama Afrika Amerika na LBGT tunatambua umhimu wa mabadiliko

Anamaliza
 
Jesen kutoka N. Carolina

-Namshangaa Trump

-Nilianzisha kampuni yangu nikiwa na umri wa miaka 26 na leo tupo nchi nyingi

-Trump haelewi hakuna kinachotisha investment kama hate

-Kutisha watu kumegharimu N.Carolina

-GOP wanadhani wanaweza kuwaambi watu choo gani waingie, lakini soko gani wasiende

-India , Mike Pence ali approve ubaguzi dhidi ya LBGT

-Clinton anajua kile CEO anachojua, tuna nguvu tukiwa pamoja

-Cl ataka tax kwa small businee kukua

Anamaliza
 
Alfranklin kutoka Minnesota (Seneta)

-ANdhihaki kuhusu Trump University,anasema alichukua mortgage kulipia ada
Alitapeli watu wengi. Unajua Trump Univ inapora watu na ni namba mbili kitaifa

- Pride of Trump Univ ni library iliyopo Trump tower yenye kila kitabu chake

- Trump hajafanya chochote kwa mtu isipokuwa peke yake, ni vema tukajielekeza kwa mtu aliyetoa maisha yake kutumikia watu

-Najivunia kumwita rafiki na si wezi kusbiri kumwita Madame President

-Siku 102 ndizo zitaamua nani awe Rais. Ninatoa hotuba kwasababu nilishinda kwa tofauti ya kura 312, ambazo kuna watu walizifanyia kazi

-Future belong to those who are passion and work hard.
Wengi mna kazi, mna family. Mna kazi ya kufanya, pigeni hodi, pigeni simu.

Ahsanteni
 
Sarah Sillverman akiwa na Senta Franken

Huyu ni comedian, anajaribu kuleta pande zote mbili pamoja
Anasema yeye ni Sanders supporter lakini anajivunia Clinton na atampigia kura

Anazungumzia katika hali ya 'comedy'

Wanamkaribisha Paul Simon, mpiga piano na wimboBrid ge over troubled water

Mziki unaendelea
 
Back
Top Bottom