Duru za siasa - Matukio

Mkuu Mchambuzi
Wakati tukisubiri uendelee kuhusu asasi za kirai na kijamii |(civil society) nitumbukize senti moja hapo mstari wa mwisho kuhusu vyombo vya habari.

Sheria ni kweli ina matatizo kwakuzingatia iliwekwa ili kukidhi haja ya mfumo wa wakati huo.
Sheria hiyo imetumika ndivyo sivyo na kuwa mpini wa kuua demokrasia.

Kwa upande mwingine tuna tatizo kubwa sana la waandishi wa habari. Fani ya habari bado ipo nyuma kwa kutoa waandishi ambao nadiriki kusema wengi hawakidhi viwango. Waandishi wamebadilika kutoka katika kiini cha kazi zao ikiwa ni kutafiti, kuhakiki na kutaarifu na sasa wamekuwa reporters.

Nachelea kusema sijui wangapi wanaweza kuona maana halisi ya bandiko kama lako na nini wanaweza kupata kutoka hapo. Fani ya uandishi mara nyingi hutegemea inputs ndipo mambo kama research yanafuata.
Kwamba mwandishi anatakiwa akione kitu halafu akifuatilie mbali na kinavyoonekana (Investigative jouranalism).

Tunatakiwa tuwe na waandishi ambao ni wataalam wa fani na si 'one size fits all'
kwa mantiki hiyo uwezekano wa mtu kueleza nini civil society na role yake katika jamii inaweza kuandikwa na kueleweka.

gfsonwin
katika bandiko lako hapo juu kuna kitu kimenigusa. Kuhusu mzozo wa EAC nadhani rais anamchango mkubwa wa kuzorota kwa hali. Simaanishi maamuzi yake ninamaanisha jinsi anavyokabliana na suala hilo.

Kwa mfano, rais JK amefanyakazi kama waziri wa mambo ya nje kwa miaka 10.
Amefanya kazi na marais 2 na hivyo kuingia katika vikao vikubwa vya maamuzi yakiwemo yaliyohusu EAC.

Rais JK alikuwa mwenyekiti wa jumuiya kwa nyakati fulani. Kwa maneno mengine ana uzoefu wa hali ya juu kuhusu EAC.Sielewi imekuaje hadi imefikia kiwango hicho bila yeye kufahamu au kuwasiliana na umma ili uelewe nini kinatokea.

Kuna uwezekano maamuzi yake yakawa sahihi na pia yaweza kuwa siyo. Hiyo si hoja, hoja kubwa ni kuwa na communication breakdown kati ya serikali na wananchi hivyo kuwafanya wabaki wanahisi hisi na si kuwa na uhakika na hali iliyopo. Hii ni failure kwa uongozi the least to say.
 
Mkuu Mchambuzi
Wakati tukisubiri uendelee kuhusu asasi za kirai na kijamii |(civil society) nitumbukize senti moja hapo mstari wa mwisho kuhusu vyombo vya habari.

Sheria ni kweli ina matatizo kwakuzingatia iliwekwa ili kukidhi haja ya mfumo wa wakati huo.
Sheria hiyo imetumika ndivyo sivyo na kuwa mpini wa kuua demokrasia.

Kwa upande mwingine tuna tatizo kubwa sana la waandishi wa habari. Fani ya habari bado ipo nyuma kwa kutoa waandishi ambao nadiriki kusema wengi hawakidhi viwango. Waandishi wamebadilika kutoka katika kiini cha kazi zao ikiwa ni kutafiti, kuhakiki na kutaarifu na sasa wamekuwa reporters.

Nachelea kusema sijui wangapi wanaweza kuona maana halisi ya bandiko kama lako na nini wanaweza kupata kutoka hapo. Fani ya uandishi mara nyingi hutegemea inputs ndipo mambo kama research yanafuata.
Kwamba mwandishi anatakiwa akione kitu halafu akifuatilie mbali na kinavyoonekana (Investigative jouranalism).

Tunatakiwa tuwe na waandishi ambao ni wataalam wa fani na si 'one size fits all'
kwa mantiki hiyo uwezekano wa mtu kueleza nini civil society na role yake katika jamii inaweza kuandikwa na kueleweka.

gfsonwin
katika bandiko lako hapo juu kuna kitu kimenigusa. Kuhusu mzozo wa EAC nadhani rais anamchango mkubwa wa kuzorota kwa hali. Simaanishi maamuzi yake ninamaanisha jinsi anavyokabliana na suala hilo.

Kwa mfano, rais JK amefanyakazi kama waziri wa mambo ya nje kwa miaka 10.
Amefanya kazi na marais 2 na hivyo kuingia katika vikao vikubwa vya maamuzi yakiwemo yaliyohusu EAC.

Rais JK alikuwa mwenyekiti wa jumuiya kwa nyakati fulani. Kwa maneno mengine ana uzoefu wa hali ya juu kuhusu EAC.Sielewi imekuaje hadi imefikia kiwango hicho bila yeye kufahamu au kuwasiliana na umma ili uelewe nini kinatokea.

Kuna uwezekano maamuzi yake yakawa sahihi na pia yaweza kuwa siyo. Hiyo si hoja, hoja kubwa ni kuwa na communication breakdown kati ya serikali na wananchi hivyo kuwafanya wabaki wanahisi hisi na si kuwa na uhakika na hali iliyopo. Hii ni failure kwa uongozi the least to say.

mkuu Nguruvi3 nakushukuru kwa mchango wako wenye kina katika bandiko lako hili. Lakini hapa naomba nirudi tena kusema jambo moja dogo sana amablo mie binafsi linanitatiza.

Leo hii imeripotiwa kwamba Mhe Samwel Sitta amesema kwamba rais atakwenda kushiri katika mkutano wa marais wa EAC. HOJA YAKE binafsi mie nimeielewa lkn imeniach ana mswali kadhaa juu yake;

mie najiuliza hivi rais wetu huwa anawajibika kwa nani?? ni wazi kwamba anawajibika kwa wananchi kama ndivyo kwann sisi ambao ndo tunaomuwajibisha yeye kama yeye hasemi na sisi?? umesema swala la communication breakdown lakin mimi silioni kwa maana unayoiona wewe ila mimi kwa mara ya kwanza naomba nitamke wazi kwamba rais wetu anatudharau sisi wananchi wake na ndio maana kauli zake hata pale inapobidi atoe kauli yeye humuacha mtu kutoa kauli hiyo.

Kama raisi anagelisema haya basi maswali mengi ambayo yako kwenye vichwa vyetu tungemuuliza tofauti na sitta alivyomsemea na kusema yeye hana la kusema juu ya Tanzania kutengwa................

Nimekuwa mfuatiliaji wa maswala ya Marekani kwa muda mrefu sana lijapo swala la maslaha ya wananchi utamwona raisi kasimama anawaambia wananchi nini kinachofwata, tumeona majuzi tu Obama akihutubia wanachi wake juu ya kuivamia serbia, na hata aliposimamisha kwa muda shughuli za serikali kwasababu ya bajeti.

nimependa sana hii tabia yake kwasababu huulizwa maswali na hutoa majibu ya kina kwa wananchi wake sasa leo hii sisi raisi hana muda wa kutusikiliza wala hana muda wa kuongea na sisi. ukichunguza hotuba zake za kila mwezi ambazo na yeye pi aliziiga kwa Mkapa sawa huwa zina address matukio ya mwezi huo lkn bado hazitoi majibu ya kina wakati mwingine.

Kitendo cha sisi kuanza kuisi umetengwa EAC yeye alipaswa ashtuke manake si anasoma habari?? kisha afanye uchunguzi wake binafsi na aje na majibu kwetu sisi wananchi, na sio kusemewa na Sitta wakati Sitta mwenyewe anasema hana la kusema juu ya nchi kutengwa EAC.
 
Last edited by a moderator:
YAH: Nafasi Na Changamoto Zinazozikabili Asasi Za Kiraia na Kijamii Katika Kuleta Mabadiliko Ya Kweli Tanzania

Wakuu Nguruvi3 et al, Naomba mniwie radhi kwa kutorudi kwa wakati kujadili hoja zangu viporo; Naomba niingie moja kwa moja kwenye hoja husika, nikilenga hasa suala la Mabadiliko kupitia Katiba Mpya;

Mjadala kuhusiana na nafasi na changamoto zinazozikabili Asasi Za Kiraia/Kijamii (Civil Society) itaeleweka Zaidi iwapo tutaijadili katika muktadha unaosisha Serikali (STATE) na Jamii (Community); Katika nchi kama Tanzania, pande mbili hizi (STATE & COMMUNITY) traditionally zimekuwa zikikinzana kimsimamo na kimtazamo katika suala zima la siasa na nafasi yake katika maendeleo ya nchi – kijamii na kiuchumi, kama ifuatavyo:

Kwa upande mmoja – State (Serikali) ina characteristics na pia inahusika Zaidi na masuala yafuatayo: ·

-
Legacy ya ukoloni pamoja na incorporation ya serikali (state) katika jumuiya ya kimataifa ya nchi huru duniani (international community of the so called ‘sovereign states'); ·
-
Uamuzi wa kupendelea Zaidi ‘top-down approach' to development or change katika taifa (mfano, sera za maendeleo, mabadiliko kama vile ya katiba n.k); ·
-Na katika miaka 25 iliyopita, kushindwa kwa serikali kuhimili pressure kutoka kwa umma kutokana na serikali kushindwa kusimamia ipasavyo liberalization & globalization kwa faida ya walio wengi nchini.

Kwa upande pili wa mlinganyo (equation) huu ni Jamii (Community) ambayo ina charecteristics na pia inahusika Zaidi na masuala yafuatayo: ·

-Pre-colonial past (kwa mfano rejea maamuzi ya Mwalimu kuingiza nchi kwenye Ujamaa ndani ya miaka sita ya uhuru wa Tanganyika); ·
-Reciprocity culture ambayo ina mizizi mirefu katika jamii yetu – kwa mfano, uwepo wa long term interdependent exchanges between partners (both between individuals and also individuals and institutions), na moja ya mifano mizuri ni mahusiano baina ya chama tawala (CCM) na jamii wakati wa chaguzi ambapo reciprocity culture uonekana wazi; Hali hii haitakiwi kuwepo katika jamii iliyopiga hatua – yani huwa hakuna long term relations between exchange partners, badala yake, wapiga kura huwa ni rational and incorrupt, and if you don't deliver, mwingine anapewa fursa; ·
-
Pia, tofauti na characteristic ya state kuhusiana na ‘top – down' approach to development, kwenye upande wa JAMII, huwa ni preference ya ‘bottom – up' approach to development. ·
-Vile vile, tofauti na Serikali (state), kwenye jamii kuna matumaini ya kweli ya african renaissance/revival kwa manufaa ya walio wengi, na jamii constantly inakuwa ikitafuta platform ambayo inaonekana ni more effective kufanikisha hilo (je, mbadala wa kweli wa CCM ni Chadema?);

Katika muktadha wa mahusiano baina ya pande hizi mbili, serikali (state) stands to abuse power kwa faida ya wachache na pia kuondoa matumaini ya maisha bora kwa watanzania walio wengi, hukku jamii (community), pamoja na changamoto inazokabiliana nayo, stands for a better and a brighter future. Nadhani hadi hapa tunaweza kuona kwa urahisi kwanini Serikali (state) na jamii (community) wanakuwa na mvutano na mara nyingine uadui, na hali hii inakuwa manifested in the state – civil society relationship.

Sasa tukihamishia mjadala wa hapo juu kwenye suala la katiba: Tangia uhuru, kinachowashikilia watanzania kuwa pamoja haijawahi kuwa ni suala la national constitution & legal framework; Badala yake imekuwa ni a perceived need to guard against a common enemy (nje na ndani ya nchi); hadi leo hii, chama tawala kinaendelea kujenga hoja kwamba ‘national unity' (tena unconditionally), is a pre-requisite for national development; Katika muktadha huu, serikali (kupitia a top-down approach) inaona kwamba ndio yenye mamlaka ya mwisho ya kuamulia wananchi sera, priorities, na pia pace ya mabadiliko, ikiwa ni pamoja na suala la katiba mpya; Chini ya mazingira haya, criticisms are intolerable, vinginevyo nguvu ya serikali inaweza kutumika to eliminate yoyote mwenye kupingana na serikali;

Ndio maana, licha ya matumaini makubwa miongoni mwa watanzania wengi kuhusiana na mchakato wa katiba mpya, binafsi naamini kwamba we still have a very long way to go before we turn into a true ‘liberal democracy'. Kuna kila aina ya ushahidi kwamba uongozi wan chi (CCM) hauna haraka ya kufikia lengo hili. Katika kipindi chote tangia uhuru wan chi yetu, serikali imekuwa ikipendelea Zaidi to manage the process of transition carefully, na kujaribu ku - balance the pursuit of political liberalization na wasiwasi waku juu ya madhara ambayo yanaweza kutokea katika civic peace and social harmony, two values ambazo ndio pekee zilizobakia kuipa serikali ya CCM legitimacy mbele ya umma. Kwa hali hii, demokrasia nchini Tanzania is more likely kuendelea kuchechemea kwa muda kwani kuna dalili kubwa kwamba itaendelea kuwa managed from the ‘top down', huku serikali ikifanya kila hila ili civil society isinyakue mchakato husika, kwani ikitokea hivyo, given the antagonism discussed hapo juu baina ya JAMII na SERIKALI, ruling elite na taasisi zao zinazoendesha nchi kwa mtindo wa informal institutions kuliko formal institutions, watakuwa katika hali mbaya sana;

Itaendelea...
 
Wana duru tulisimama kidogo kutoa nafasi kwa Mchambuzi kumalizia mada yake akipata wasaa.
Wakati tunamsbiri tutarejea kwa uchache yaliyojitokeza hasa hotuba ya rais.
 
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, ALIYOITOA BUNGENI KUHUSU JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI, 7 NOVEMBA, 2013, DODOMA


Mheshimiwa Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Mheshimiwa Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni;
Waheshimiwa Wabunge;
Mabibi na Mabwana;

Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kukubali ombi langu na kutenga muda wenu ili niweze kuzungumza na Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuhusu masuala muhimu kwa uhai, ustawi na maendeleo ya nchi yetu na watu wake.

Mheshimiwa Spika;
Nimeambiwa kuwa taarifa ilipotolewa kuwa ninaomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge, kumekuwepo na dhana mbalimbali. Wapo waliodhani kuwa nakuja kuzungumzia mchakato wa kuunda Katiba mpya na hasa matukio ya wiki chache zilizopita. Wapo waliodhani nakuja kuzungumzia "Operesheni Tokomeza". Tena wapo waliokwenda mbali na kufikiria kuwa nakuja kuwakaripia Waheshimiwa Wabunge waliotoa maoni yao kuelezea kasoro zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni hii muhimu. Na wapo pia waliodhani ninakuja kuzungumzia ushiriki wa majeshi yetu ya Tanzania katika Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa nchini Kongo.

Mheshimiwa Spika;
Hayo si makusudio yangu. Kinachonileta mbele ya Bunge lako Tukufu ni kuzungumzia Jumuiya ya Afrika Mashariki na mustakabali wa Tanzania katika Jumuiya hiyo. Lakini, kwa sababu ya umuhimu wa masuala hayo niliyoyataja na rai niliyopewa kuwa niyasemee japo kidogo. Nimeona ni vyema nifanye hivyo.

Mheshimiwa Spika;
Kuhusu mchakato wa Katiba mpya, napenda kusema kuwa tumefikia hatua nzuri katika utekelezaji wake. Kama mjuavyo Tume ya Mabadiliko ya Katiba imekamilisha, kwa mafanikio, hatua ya mwanzo ya kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu Katiba wanayoitaka. Pia walishatoa Rasimu ya Kwanza ya Katiba na kukamilisha mchakato wa Mabaraza ya Katiba. Kinachosubiriwa kwa hamu na sisi wote, ni Rasimu ya Pili ya Katiba ambayo inatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 15 Desemba 2013 au kabla ya hapo.

Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa Bunge lako Tukufu, tunategemea kupata mambo mawili kutoka kwenu yatakayowezesha mchakato kutekelezwa vizuri katika hatua zinazofuata. Jambo la kwanza ni kutungwa kwa Sheria ya Kura ya Maoni na pili kufanyika kwa marekebisho ya nyongeza ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kuhusu Bunge Maalum ili kuboresha utekelezaji wake. Baada ya Bunge kukamilisha kazi yake hiyo itafuatia uteuzi wa Wajumbe wa Bunge Maalum ili kazi ya kujadili Rasimu ya Pili ya Katiba ifanyike na kutupatia Rasimu ya Mwisho. Rasimu ambayo ikikubaliwa na wananchi katika Kura ya Maoni itakayofanyika wakati wo wote mwakani, tutakuwa tumepata Katiba Mpya. Hivi sasa katika Serikali tunaendelea kufanya tafakuri na tunachukua hatua za kuwezesha Bunge Maalum na Kura ya Maoni kufanyika kwa mafanikio.

Operesheni Tokomeza

Mheshimiwa Spika;
Napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuwa sikukasirishwa na maoni yao kuhusu madai ya kuwepo kasoro katika utekelezaji wa Operesheni Tokomeza. Shabaha ya Operesheni hii ni kuokoa maliasili za misitu na wanyamapori dhidi ya uvunaji haramu ambao umefikia kiwango kinachotishia kutoweka kwa raslimali hizo. Kwa kweli hali inatisha. Miti inakwisha na ndovu na faru wanaangamia.

Mheshimiwa Spika;
Wakati, tunapata Uhuru Tanzania ilikuwa na ndovu waliokadiriwa kuwa takribani 350,000. Lakini, kwa sababu ya ujangili uliokithiri katika miaka ya 1970 na 1980 ilipofika mwaka 1989 kulikuwa na ndovu wapatao 55,000 tu. Ilipofikia hali hiyo Serikali ikaanzisha Operesheni Uhai iliyohusisha Jeshi la Ulinzi na kuongozwa na Meja Jenerali John Walden (ambaye sasa ni marehemu) kuendesha mapambano dhidi ya majangili. Kutokana na hatua hiyo na uamuzi wa Shirika linalosimamia biashara ya wanyama walioko kwenye hatari ya kutoweka (CITES) kupiga marufuku biashara ya pembe za ndovu duniani, idadi ya ndovu nchini iliongezeka na kufikia 110,000 mwaka 2009.

Tumewaomba Fankfurt Zoological Society ambao ni wabia wetu katika uhifadhi wa wanyama pori kwa miaka mingi wafanye sensa maalum ya ndovu katika Hifadhi ya Selous na kote nchini ili tujue hali halisi ikoje. Kazi hiyo inaendelea hivi sasa.

Mheshimiwa Spika;
Baada ya mwaka 2009 kumezuka wimbi jipya, tena la nguvu kubwa, la kuua ndovu na faru nchini na kwingineko katika Bara la Afrika ambako wanyama hao wapo. Idadi kubwa ya meno ya ndovu yaliyokamatwa na yanaoendelea kukamatwa nchini na kwingineko duniani inathibitisha ukweli huo. Kwa mfano, kati ya mwaka 2010 na Septemba, 2013, hapa nchini, kwa jitihada zetu vipande 3,899 vya pembe za ndovu vyenye uzito wa kilo 11,212 na vipande 22 vya pembe za ndovu zilizochakatwa zenye uzito wa kilo 3,978 vilikamatwa. Aidha, katika kipindi hicho vipande 4,692 vya pembe za ndovu vilivyotokea Tanzania vyenye uzito wa kilo 17,797 vilikamatwa nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika;
Kama nilivyokwisha sema hapo awali matatizo ya kuuawa kwa wingi kwa ndovu na faru lipo pia katika nchi nyingine Afrika zenye wanyama hao. Nchi za Gabon, Kenya, Afrika ya Kusini, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Uganda, Zimbabwe, Zambia na nyinginezo nazo zinakabiliwa na matatizo kama yetu. Tatizo limekuwa kubwa kiasi cha kuifanya Jumuiya ya Kimataifa kushtuka na kuamua kuingilia kati kwa namna mbili. Kwanza kuunga mkono juhudi za uhifadhi wa ndovu na faru katika nchi zenye wanyama hao. Na, pili, kuchukua hatua thabiti kudhibiti biashara ya meno ya ndovu duniani. Ni ukweli ulio wazi kuwa kama hakutakuwepo na wanunuzi wa meno ya ndovu na faru hakuna ndovu au faru atakayeuawa.

Mheshimiwa Spika;
Kutokana na ukweli ulivyo uamuzi wetu wa kuendesha Operesheni Tokomeza ni sahihi kabisa. Manufaa yaliyopatikana baada ya Operesheni Uhai ya mwaka 1989 yanatupa imani kuwa na safari hii pia tutafanikiwa. Tusipochukua hatua kama hii sasa ni sawa na kuwapa kibali majangili waendelee kumaliza ndovu na faru nchini. Hakika wanyama hao watakwisha. Itakuwa ni aibu kubwa kwetu na historia itatuhukumu vibaya.

Mheshimiwa Spika;
Tumeyasikia maelezo ya Wabunge kuhusu kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni Tokomeza. Nawaahidi kuwa tutayafanyia kazi. Serikali imeahirisha kwa muda Operesheni hii ili kujipa muda wa kurekebisha kasoro hizo na kujipanga upya. Watendaji wasiokuwa waadilifu na wale wasiokuwa waaminifu wataondolewa. Halikadhalika, kasoro za kimfumo nazo zitasahihishwa ili tutakapoanza upya Operesheni itekelezwe kwa mafanikio yaliyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika;
Miongoni mwa mambo yaliyozungumzwa kwa uchungu ni ukamataji wa mifugo iliyokutwa kwenye mapori ya hifadhi za wanyama na vitendo vibaya walivyofanyiwa wenye mifugo na mifugo yenyewe. Narudia kusisitiza kuwa taarifa zote hizo zitafanyiwa kazi na waliohusika watachukuliwa hatua zipasazo. Pamoja na hayo, napenda kuwakumbusha ninyi watunga sheria wetu kuwa sheria ya hifadhi za wanyamapori hairuhusu mifugo kuchungwa katika maeneo ya hifadhi.

Naomba tuwakumbushe wananchi tunaowaongoza wajiepushe na kufanya hivyo. Ni uvunjifu wa Sheria za nchi. Naomba pia, wananchi waelimishwe ili wajue kuwa wakifanya hivyo na kukutwa katika maeneo hayo na mifugo yao kuna adhabu iliyotamkwa kwenye sheria. Hivyo tusiwalaumu wala kuwaona maafisa wanyamapori kuwa ni watu wabaya. Wanatekeleza Sheria iliyotungwa na Bunge hili. Pale wanapotenda visivyo tuseme, watawajibishwa ipasavyo.


Jeshi la Umoja wa Mataifa Kongo

Mheshimiwa Spika;
Mapema mwaka huu (2013) Umoja wa Mataifa uliomba nchi yetu ichangie kikosi kimoja cha wanajeshi katika Brigedi Maalum iliyoundwa na Umoja huo kuongeza nguvu ya kudhibiti waasi Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Lengo la msingi ni kuiwezesha nchi hiyo kupata amani ya kudumu ambayo imekosekana kwa muda mrefu kutokana na kuibuka kwa uasi mara kwa mara.

Mheshimiwa Spika;
Tulikubali, kwani hata kabla ya kuombwa na Umoja wa Mataifa tulishakubali maombi kama hayo yaliyotolewa kwenye Mkutano wa Nchi za Maziwa Makuu. Ni miezi saba (tangu Aprili) sasa tangu wanajeshi wetu waende Kongo na wamekuwa wanatekeleza majukumu yao vizuri tena kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu. Sifa hiyo kwa wanajeshi wetu imekuwa inatolewa na viongozi wa juu wa Umoja wa Mataifa, viongozi wa juu wa Jeshi la Umoja wa Mataifa Kongo (MONUSCO) na viongozi wa juu wa Serikali ya Kongo.

Mheshimiwa Spika;
Majeshi ya Umoja wa Mataifa hupewa majukumu na mamlaka ya namna mbili. Yapo yanayopewa jukumu la kulinda amani tu. Wanajeshi wake huwa hawapewi majukumu ya kimapigano na hata pale wanaposhambuliwa wanatakiwa kujihami tu. Kwa kawaida majeshi yenye jukumu hili hupelekwa mahali ambapo kumekuwepo na makubaliano ya kuacha mapigano. Wanapelekwa kusaidia kuona Mkataba unatekelezwa ipasavyo.

Aina ya pili ni ile ya majeshi yanayopelekwa mahali ambapo hakuna amani hivyo wanapewa jukumu la kuchukua hatua za kufanya amani ipatikane. Majeshi haya hupewa mamlaka ya kutumia nguvu ya kijeshi dhidi ya wanaosababisha amani ikosekane kama ni lazima kufanya hivyo. Maana yake ni kwamba wanayo ruhusa kuingia katika mapigano dhidi ya watu au vikundi vinavyovuruga amani. Tofauti na wenzao wa kundi la kwanza, wanajeshi wa kundi la pili wako kwenye hatari zaidi ya kupoteza maisha au kujeruhiwa kuliko wenzao ingawaje wapo wengi nao wameuawa na kujeruhiwa.

Mheshimiwa Spika;
Wanajeshi wetu wamekwenda Kongo chini ya utaratibu huu wa pili ambao unahusu kuingia kwenye mapigano dhidi ya waasi kama hapana budi kufanya hivyo. Wametekeleza majukumu yao vyema na kwa ujasiri mkubwa na weledi wa hali ya juu. Bahati mbaya tumepoteza vijana wetu watatu shupavu. Daima tutawakumbuka na tutawaenzi ipasavyo mashujaa wetu hawa. Tuzidi kuwaombea kwa Mola awape mapumziko mema. Ameen.

Wakati huo huo, Mheshimiwa Spika, napenda kutumia nafasi hii kumpongeza Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa mafanikio ya kihistoria waliyoyapata hivi majuzi dhidi ya waasi wa M23. Tunamtakia yeye na wananchi wa Kongo kila la heri katika kazi ngumu iliyo mbele yao ya kujenga upya eneo hilo na kujenga mahusiano mapya miongoni mwa watu wa Kongo. Pia nawapongeza sana wanajeshi wa Brigedi Maalum ya Umoja wa Mataifa kwa kazi nzuri waliyoifanya iliyowezesha mafanikio kupatikana. Wanajeshi hao ni kutoka Afrika Kusini, Tanzania na Malawi wanaoongozwa na Brigedia Jenerali James Aloisi Mwakibolwa wa JWTZ.


Jumuiya ya Afrika Mashariki

Mheshimiwa Spika;
Kama nilivyosema awali, haya mambo matatu siyo hasa makusudio yangu nilipoomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge wetu. Nimeyachomekea tu kwa sababu ya umuhimu wake katika jamii kwa wakati tulio nao. Jambo lililonileta hapa leo ni kuzungumzia hali ilivyo sasa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na nafasi ya Tanzania katika Jumuiya hiyo. Nimeona nifanye hivyo kutokana na maswali mengi ambayo Watanzania wanajiuliza kufuatia matukio ya hivi karibuni ya viongozi wa nchi tatu wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaani Uganda, Rwanda na Kenya kukutana bila ya ushiriki wa viongozi wa Tanzania na Burundi. Viongozi wenzangu hao wamefanya mikutano mitatu yaani: tarehe 24-25 Juni, 2013 mjini Entebbe, Uganda; tarehe 28 Agosti, 2013 mjini Mombasa, Kenya; na tarehe 28 Oktoba, 2013 mjini Kigali, Rwanda.

Mheshimiwa Spika;
Naomba kwanza niweke wazi jambo moja, kwamba nchi mbili wanachama au zaidi hazikatazwi kuwa na makubaliano ya ushirikiano katika kufanya mambo mbalimbali. Hata sisi Tanzania tunao ushirikiano wa namna hiyo na nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Lakini, nchi wanachama zinatakiwa kufanya hivyo kwa yale mambo ambayo hayako kwenye shughuli za Jumuiya kwa maana kwamba hayamo katika Mkataba au Itifaki au hakuna uamuzi wa msingi uliofanywa na vikao au taasisi za Jumuiya kuyashughulikia. Pia, tunaweza kufanya hivyo kwa mambo ambayo yalishaamuliwa na Jumuiya yatekelezwe na ruhusa imetolewa kwa nchi yo yote iliyokuwa tayari kutekeleza ama peke yake au kwa kushirikiana na nchi nyingine.

Mheshimiwa Spika;
Kwa mujibu wa matamko ya pamoja (Communique) yaliyotolewa baada ya mikutano hiyo, kuna mambo yapatayo manane ya msingi yaliyoamuliwa kufanywa na nchi hizo kwa lengo la kuendeleza utengamano wa nchi hizo wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mambo hayo ni haya yafuatayo:
(1)Kujenga reli ya kisasa kutoka Mombasa hadi Kampala, Kigali na Bujumbura.
(2)Ujenzi wa Bomba la Mafuta la kutoka Kenya hadi Uganda na Sudani ya Kusini.
(3)Kujenga Kiwanda cha kusafisha mafuta nchini Uganda.
(4)Kuanzisha Himaya Moja ya Ushuru wa Forodha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kutekeleza vipengele vyote;
(5)Kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki na kwamba itaundwa Kamati ya kuandaa rasimu ya Katiba ya Shirikisho.
(6)Kuharakisha uanzishwaji wa Visa ya pamoja ya Utalii ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (Single East African Community Tourist Visa);
(7)Kuandaa utaratibu wa kutumia vitambulisho vya taifa kama hati ya kusafiria katika nchi zao; na
(8)Kuongeza uzalishaji na usambazaji wa umeme.

Mheshimiwa Spika;
Ni dhahiri kwamba orodha hiyo imechanganya mambo yale ambayo ni ya Jumuiya na yale yasiyo ya Jumuiya. Kwa mfano, mambo manne kati ya hayo manane hayamo kwenye masharti ya kutokufanyika bila ya kuihusisha au kupata ridhaa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Jambo la kwanza ni uzalishaji na usambazaji wa umeme. Ni kweli kwamba tunao mkakati wa kuwa na akiba ya pamoja ya nguvu ya umeme (East African Power Pool). Hata hivyo, bado jukumu la kuzalisha na kusambaza umeme huo limeachiwa nchi wanachama zenyewe kuamua. Lakini, hivi ndugu zetu hawa wanao muhali kuishirikisha Tanzania katika mpango ambao kimsingi umebuniwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo sote ni wanachama?

Jambo la pili, ni ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta nchini Uganda. Hili si suala la Jumuiya bali la nchi ya Uganda kuamua yenyewe peke yake au kwa kushirikiana na wadau wengine. Rais Yoweri Museveni alituarifu mpango huo na sote tuliupokea kwa furaha kwamba sasa tutapata mafuta karibu na nyumbani. Alitualika kushiriki katika ujenzi wake sijui sasa amebadili mawazo kwamba Tanzania siyo muhimu.

Mheshimiwa Spika;
Jambo la tatu ni ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Kenya hadi Sudani ya Kusini na Uganda. Hili si jambo linalobanwa na masharti ya Jumuiya. Ni juu ya nchi hizi tatu kuamua kufanya ili kuwezesha mafuta yao kufika kwenye masoko. Hata hivyo, nimeambiwa kuwa Jumuiya imeshazungumzia bomba la mafuta kutoka Eldoret hadi Uganda, Rwanda na Burundi kuwa nalo lifike Tanzania kupitia upande wa Kaskazini Magharibi mwa Tanzania. Inaelekea mpango huo sasa haupo maana hatujausikia kutajwa katika ujenzi wa bomba hilo.

Mheshimiwa Spika;
Jambo la nne ni ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Mombasa – Kampala – Kigali – Bujumbura. Hili nalo hatuna tatizo nalo. Si mradi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ni jambo lililo chini ya mamlaka ya nchi wanachama husika. Hata hivyo, ni vyema kutambua ujenzi wa miundombinu ya reli, barabara na usafiri wa anga na majini kuunganisha nchi za Afrika Mashariki ni miongoni mwa mambo ya kipaumbele cha juu yanayoshughulikiwa na Jumuiya yetu. Jumuiya hutengeneza mikakati ya pamoja na ndiyo maana tuna East African Railway Masterplan, tuna East African Road Network, na tuna Lake Victoria Development Programme kwa ziwa Victoria.

Kwa ajili hiyo, nilitegemea kuwa reli ya kutoka Mombasa hadi Kigali na Juba ingekuwa na tawi linalounganisha reli hiyo na reli ya Tanzania kama ilivyo reli ya Moshi – Voi – Taveta aliyotuachia mkoloni. Tulitegemea hivyo kwa minajili ya kuunganisha soko la Afrika Mashariki ambapo naamini Tanzania ni mdau muhimu. Lakini inaelekea kwa maoni ya wenzetu hivyo sivyo.

Mheshimiwa Spika;
Lazima nikiri kuwa inashangaza na tunayo kila sababu ya kuuliza kwa nini wenzetu wameamua kufanya hivi. Kumetokea nini toka tukutane pale Arusha Aprili 28, 2013 na Juni 24, 2013 walipokutana kuamua kufanya mambo ya kujenga na kuimarisha utengamano wa Afrika Mashariki kwa kubaguana, Haijawahi kuwa hivi kabla.

Mheshimiwa Spika;
Katika mambo manne yaliyosalia ambayo yaliamuliwa na kuwekewa utaratibu wake wa utekelezaji na Jumuiya ya Afrika Mashariki mawili hatuna maneno nayo. Mambo hayo ni matumizi ya vitambulisho vya taifa kama hati ya kusafiria na Visa ya Pamoja ya Utalii kwani tuliamua kwa pamoja kuwa nchi wanachama zilizokuwa tayari waanze. Lakini, kwa upande wa kuanzishwa kwa Himaya Moja ya Ushuru wa Forodha (Single Customs Territory) na Shirikisho la Afrika Mashariki tunadhani wenzetu wamekiuka uamuzi wetu wa pamoja.

Mheshimiwa Spika;
Katika Mkutano Maalum wa 11 wa Wakuu wa Nchi wanachama uliofanyika tarehe 28 Aprili, 2012 Jijini Arusha, tulipokea na kuridhia mapendekezo ya kuanzisha Himaya Moja ya Ushuru wa Forodha (Single Customs Territory). Kwa mujibu wa mapendekezo hayo kila nchi mwanachama itasimamia shughuli zake za kiforodha na kukusanya mapato yake kama ilivyo sasa. Hata hivyo, kwa bidhaa zinazopitia nchi moja kwenda nchi nyingine mwanachama, ukaguzi na ukusanyaji wa mapato utafanyika katika kituo cha kwanza bidhaa hizo zinapoingilia. Mapato hayo yatawasilishwa kwa nchi husika baada ya kuthibitisha kuwa bidhaa zilivuka mpaka.

Mheshimiwa Spika;
Kutokana na uamuzi huo, Wakuu wa Nchi waliagiza Baraza la Mawaziri kuunda Kikosi Kazi cha kujadiliana na kuandaa utaratibu wa utekelezaji wa mfumo huo. Taarifa ya kikosi kazi inatakiwa kutolewa katika Mkutano wa 15 wa Wakuu wa Nchi utakaofanyika Kampala, Uganda tarehe 30 Novemba, 2013. Iweje leo nchi tatu wanachama ziamue peke yao kuanza kutekeleza? Wanatekeleza nini na kwa nini wafanye hivyo?

Mheshimiwa Spika;
Kuhusu Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki hadithi yake inafanana na hii ya Himaya ya Forodha. Katika Mkutano wa 14 wa Wakuu wa Nchi wanachama uliofanyika tarehe 30 Novemba, 2012, Nairobi, tulipokea taarifa ya hatua iliyofikiwa kuhusu mchakato wa kutaka kuanzishwa kwa Shirikisho. Mkutano huo uliagiza nchi wanachama kujadiliana zaidi kuhusu mpango kazi wa kufikia Shirikisho la Kisiasa na mpango wa kutekeleza mapendekezo mengine yaliyotolewa na Timu ya Wataalamu. Inategemewa kuwa Baraza la Mawaziri litawasilisha mapendekezo ya majadiliano hayo katika Mkutano wa 15 wa Wakuu wa Nchi mwezi Novemba, 2013. Iweje leo wenzetu hawa waamue kuanzisha mchakato wao wa kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Spika;
Kwa kweli huwa najiuliza maswali mengi na kukosa majibu kuhusu nini kinachoendelea kufanywa na viongozi wenzangu watatu na kwa nini! Nakosa majibu ya uhakika. Je wenzetu wamekosa imani na Jumuiya ya Afrika Mashariki na je wanataka kuunda yao? Je wanaichukia nchi yetu na hivyo wameamua kutufanyia vitimbi tutoke! Au sijui wanachuki na mimi! Napenda kuwahakikishia Waheshimiwa Wabunge kuwa hatuna mpango wa kutoka (kama vijana wasemavyo hatoki mtu hapa). Tupo na tutaendelea kuwepo!

Mheshimiwa Spika;
Tanzania haijafanya jambo lo lote baya dhidi ya Jumuiya au nchi yo yote mwanachama. Na ukweli ni kwamba ni mwanachama mvumilivu, mtiifu na mwaminifu kwa Jumuiya. Tunatimiza ipasavyo wajibu wetu kwa Jumuiya na kushiriki kwa ukamilifu katika ujenzi wake na utengamano ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Sabahu ya wenzetu watatu kuamua kufanya mambo yahusuyo Jumuiya yetu peke yao kwa kweli haieleweki.

Mheshimiwa Spika;
Tunasikia eti kuwa baadhi yao walipoulizwa kwa nini wengine hatupo wakasema kuwa wao wametangulia na sisi tutakapokuwa tayari tutajiunga. Yaani wana Umoja wa Waliokuwa Tayari (Coalition of the Willing). Hivi ni nani hayuko tayari (who is not willing?) Haiwezekani watu waitane wenyewe bila ya kutualika halafu wadai kuwa wao ndiyo wako tayari na kujenga dhana kuwa sisi wasiotualika ndiyo ambao hatuko tayari. Madai hayo hayana ukweli. Ni vyema waseme ukweli. Kama walitualika tukakataa ndiyo wanaweza kusema hayo.

Mheshimiwa Spika;
Kumekuwepo na madai kutoka kwa baadhi ya wenzetu, eti kwamba Tanzania haina moyo wala dhamira ya dhati ya kuendeleza utengamano wa Afrika Mashariki. Kwa sababu hiyo inasemekana eti nchi yetu imekuwa kikwazo kwa maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwamba Tanzania tunawachelewesha wengine kupiga hatua za haraka. Wanadai kama siyo hivyo Jumuiya ya Afrika Mashariki ingekuwa mbali kwa maendeleo. Maneno hayo yamekuwa yanarudiwa au kujirudia mara nyingi kiasi cha kuwafanya baadhi ya watu wa Afrika Mashariki na hata kwingineko duniani waamini hivyo.

Mheshimiwa Spika;
Napenda kusema kwa dhati ya moyo wangu kwamba madai hayo hayana ukweli wo wote. Isitoshe hata sababu zinazotolewa kuthibitisha ukweli wake hazina mashiko. Hazifanani na ukweli kuhusu Tanzania na Watanzania walivyo. Tanzania ni muumini wa dhati wa umoja na utengamano wa nchi za Afrika Mashariki na Afrika. Tumethibitisha hivyo kwa vitendo kwa kuunganisha nchi zetu mbili huru yaani Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika na kuwa taifa moja liitwalo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Muungano wa nchi zetu mbili ndio pekee uliodumu kwa muda mrefu kuliko yote Afrika.

Mheshimiwa Spika;
Tanzania ni mwanachama mwaminifu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa maana ya kutekeleza Mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo, kwa Itifaki zake na maamuzi halali ya vikao na taasisi za Jumuiya. Kama lipo jambo ambalo hatujalifanya ilivyotakiwa itakuwa ni kwa sababu za msingi na siyo kwa sababu ya kupuuza Jumuiya. Tunaithamini sana Jumuiya na tumeipa kipaumbele cha juu. Hatuwezi kuhangaika kwa gharama kubwa ya muda wetu, fedha zetu na kutoa mchango wa hali na mali kuianzisha, kujenga na kuifikisha Jumuiya hapa ilipo halafu tuwe ni watu tunaoongoza kutokuipenda na kudhoofisha maendeleo na ustawi wake. Ni maneno ya kushangaza na wala hayaingii akilini. Ama kweli akutukanae hakuchagulii tusi.

Mheshimiwa Spika;
Nionavyo mimi msimamo wetu kuhusu kuharakisha Shirikisho na masuala ya ardhi, ajira, uhamiaji, pengine ndiyo yanayotuletea hisia zisizokuwa sahihi juu yetu. Mimi siamini kama kuna mengine. Hata hivyo, napata taabu kuamini kwamba kutofautiana kwa mawazo katika mambo hayo kutapelekea baadhi ya wenzetu wasipende hata kushirikiana nasi kwa mambo ambayo hayana matatizo na tumekuwa tunashirikiana vizuri.

Mheshimiwa Spika;
Tanzania imekuwa inawasihi wanachama wenzetu kuwa tujenge Jumuiya yetu hatua moja baada ya nyingine kama ilivyo kwenye Mkataba ulioanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hatuna tatizo la kuongeza kasi ya ujenzi wa Jumuiya lakini tusivuke hatua yo yote. Tusiende kasi ya kupindukia. Mkataba unaelekeza tunaanza na Umoja wa Forodha, inafuatia Soko la Pamoja kisha Umoja wa Kifedha na hatimaye Shirikisho la Kisiasa.

Mheshimiwa Spika;
Ni kweli kabisa hatukuunga mkono kuharakisha Shirikisho la Kisasa kabla ya kukamilisha baadhi ya hatua. Na, tulifanya hivyo kwa nia njema ya kutaka Shirikisho lijengwe juu ya msingi imara. Na, msingi huo si mwingine bali utengamano wa kiuchumi kwa maana ya Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja na Umoja wa Kifedha zilizojengeka vizuri na kufanya kazi ipasavyo na kunufaisha wanachama wote sawia.

Mheshimiwa Spika;
Lazima tutambue ukweli kuwa kunufaika kiuchumi ndicho kichocheo kikubwa cha nchi kujiunga na kuendelea kuwa mwanachama wa Jumuiya yetu. Kama mambo ya kiuchumi yakipangika vizuri na kila nchi ikanufaika sawia, unajenga msingi imara kwa Shirikisho la Kisiasa kustawi na kudumu. Kama ngazi hizi tatu za awali hazitashughulikiwa vizuri na nchi wanachama zikahisi hazinufaiki ipasavyo, Shirikisho litayumba au kuyumbishwa hivyo kudumu kwake kutakuwa kwa mashaka.

Mheshimiwa Spika;
Tanzania ni kati ya zile nchi zinazotaka ngazi zote za mchakato wa utengamano zitekelezwe moja baada ya nyingine bila kuruka hata moja. Kwa msimamo na mtazamo wetu, Shirikisho iwe ndiyo hatua ya mwisho. Na huo siyo msimamo wangu au wa Serikali peke yake, ndiyo msimamo wa Watanzania walio wengi.

Bila ya shaka sote tutakumbuka kuwa mwaka 2006 Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya waliunda Kamati Maalum katika kila nchi kukusanya maoni ya wananchi kuhusu kuharakisha Shirikisho la Afrika Mashariki. Kwa hapa nchini Kamati hiyo iliongozwa na Profesa Samwel Wangwe na katika taarifa yake, Kamati ilieleza kuwa asilimia 74.4 ya Watanzania wanaunga mkono kuwepo kwa Shirikisho lakini ni asilimia 25.4 tu ndiyo waliunga mkono kuharakishwa kwake.

Mheshimiwa Spika;
Takwimu hizi zinaelezea ukweli kuhusu hisia za Watanzania, kuhusu kuwepo kwa Shirikisho na kasi ya utekelezaji wake. Watanzania wengi sana wanaunga mkono kuwepo kwa Shirikisho la Afrika Mashariki lakini wanataka jambo hilo lisifanywe haraka haraka. Wanataka lifanywe kwa umakini mkubwa na tuende hatua kwa hatua kama ilivyoainishwa katika Mkataba uliounda Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Spika;
Sera na msimamo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakwenda sambamba na ile ya wananchi wa Tanzania. Ndiyo maana tumeafiki mapendekezo ya Kamati ile ya mwaka 2004 iliyoongozwa na Mheshimiwa Amos Wako wakati ule akiwa Mwanasheria Mkuu wa Kenya. Kamati hiyo iliundwa kupendekeza namna ya kuharakisha utekelezaji wa mchakato wa utengamano wa Afrika Mashariki.

Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki umetamka muda wa kutekeleza ngazi ya Umoja wa Forodha lakini uko kimya kuhusu ngazi zilizofuata. Ili kuondoa kasoro hiyo na kwa nia ya kuharakisha Shirikisho Kamati ilipewa jukumu la kutoa maoni na mapendekezo juu ya namna ya kufanya hivyo. Kamati ilifanya kazi nzuri ya kupata maoni na hisia za watu wa makundi mbalimbali katika nchi wanachama kuhusu ujenzi wa Jumuiya na utengamano.

Mheshimiwa Spika;
Kwa upande wa Tanzania kwa mfano, Kamati ya Mheshimiwa Amos Wako ilitambua hisia za Watanzania kuhusu ardhi na ajira na kupendekezwa kuwa masuala hayo yabaki kwenye mamlaka ya nchi wanachama kuamua. Kuhusu mchakato wa utengamano Kamati ilipendekeza kwanza kwamba mchakato wa ujenzi wa Umoja wa Forodha uachwe mpaka ufike ukomo wake wa miaka mitano. Baada ya hapo muda wa kutekelezwa ngazi zinazofuata unaweza kupunguzwa. Kwa mfano walipendekeza kuwa matayarisho ya kuunda Soko la Pamoja yaanze hata kabla ya mchakato wa Umoja wa Forodha kufika mwisho ili mara wakati huo ukifikiwa Soko la Pamoja linaanze. Hivyo hivyo mara baada ya ngazi hiyo kuanza matayarisho ya kuanza ngazi ya Umoja wa Kifedha yanaanza. Ngazi hiyo nayo ikianza matayarisho ya kuunda Shirikisho yanaanza. Kamati pia imetoa mapendekezo ya namna ya kufikia uamuzi kuhusu Shirikisho kwamba wananchi wa nchi wanachama wataamua kwa kura. Tukifuata mapendekezo ya Kamati ya Mheshimiwa Amos Wako na wenzake kama tufanyavyo sasa Tanzania haina matatizo nayo.

Mheshimiwa Spika;
Baada ya kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na wana-Afrika Mashariki kuhusu ujenzi wa Jumuiya yao inasikitisha kuona vinafanyika vitendo vinavyoanzisha mivutano kuhusu mambo yaliyokwisha fanyiwa kazi na kuamuliwa. Tunapata taabu zaidi pale watu wanapobagua wenzao na wanapofanya mambo yanayopingana na Mkataba wa Jumuiya na Itifaki zake. Kwa kweli kama mwenendo huu hautabadilika sijui mambo yatakuwaje mbele ya safari.

Mheshimiwa Spika;
Nchi yetu inapenda kuona kuwa tunakuwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyo imara na iliyo endelevu. Jumuiya ambayo inaendeshwa vizuri, mambo yake ni mazuri na nchi zote wanachama na watu wake wananufaika nayo, na hivyo wanaifurahia. Tanzania haina tatizo na kuharakisha mchakato wa utengamano, lakini tunapata taabu kuruka baadhi ya hatua kabla hazijakamilika. Tunawaomba wenzetu kuwa makini katika kila hatua tunayochukua. Bila ya kufanya hivyo, Jumuiya yetu itakuwa imejengeka katika msingi dhaifu hivyo ustawi na uhai wake utakuwa na changamoto nyingi. Hatupendi ya mwaka 1977 yatokee tena.

Mheshimiwa Spika;
Napenda kuwahakikishia kuwa Tanzania itaendelea kushiriki katika shughuli za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuimarisha utengamano wa Afrika Mashariki kwa kuzingatia matakwa ya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Itifaki zake. Tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha kuwa Jumuiya haidhoofiki wala kufa. Na iwapo itadhoofika au kufa kamwe hatutaki Tanzania inyooshewe kidole kuwa chanzo wala kichocheo chake. Ndiyo maana, hatutachoka kuzungumza na wenzetu kuhakikisha kuwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki inaendelea kustawi.

Tutaendelea kukumbushana umuhimu wa kufanya mambo yanayojenga na kuepuka yale yanayoweza kubomoa. Tutakumbushana umuhimu wa kuheshimu matakwa na masharti ya Mkataba ulioanzisha Jumuiya, Itifaki zake na maamuzi halali ya vikao rasmi na asasi za Jumuiya. Tukifanya hivyo Jumuiya ya Afrika ya Mashariki itadumu, itazidi kustawi na kunufaisha nchi wanachama na watu wake kama yalivyo malengo na madhumuni ya kuundwa kwake.

Mungu Ibariki Afrika

Mungu Ibariki Tanzania

Idumu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Mheshimiwa Spika na
Waheshimiwa Wabunge;
Asanteni sana kwa kunisikiliza.
...........................
 
Mkuu @JokaKuu hili la media zao ni two way traffic. Ni kweli kama ulivyosema lakini pia ni kweli kuwa media zetu hazipo makini katika kulieleza suala hili.Sijasoma analysis yoyote ya maana zaidi ya nukuu za nani kasema na kasema nini.

Pili, kuna tatizo ambalo Tanzania inalifanya sasa hivi.
Ni muda mrefu suala hili lipo na serikali inalifahamu. Na ni ukweli kuwa JK ni kiongozi anayeifahamu EAC zaidi baada ya Museveni. Amekuwa waziri wa mambo ya nje na Rais kwa miaka kwa 10+8.
Ni wazi chochote kilichokuwa kinaendelea alikifahamu.

Katika muda wote amekuwa kimyaa kuwasiliana na wananchi kuwaeleza nini msimamo wa nchi.
Wengi waliamini kuwa suala hilo linafanyiwa kazi na serikali hasa baada ya waziri wa mambo ya nje ambaye pia ni mzoefu katika EAC kulitolea kauli.

Ukimya huo umeonekana kama ni hatu za kidiplomasia zaidi kuliko za kuibuka na kauli.
Na ukimya huo ulipeleka maswali zaidi kwa hao wenzetu kwa kutojua Tanzania inafikiria nini

Siku za karibuni kumetokea mambo ya kila waziri kutoa kauli, waziri wa mambo ya nje kutoa kauli, wa EA kutoa kauli na wabunge.Ukisoma kauli zao ni kama knee jerk reaction kitu ambacho si kweli.
Hili linatokana na kutokuwa organized na pengine kukosa mwongozo kutoka kwa Rais.

Waziri Membe alisema serikali itapeleka suala hilo bungeni kwa wakati muafaka ikisubiri majibu kutoka sekretariati na mwenyekiti wa EAC. Aidha serikali imesema kuna kikao cha wakuu ambacho suala hilo litaongelewa.

Nimemshangaa Spika Makinda akiruhusu jambo hilo lizungumziwe bila maandalizi au utaratibu.
Na kibaya alimtaka waziri husika kutoka kauli za namna hiyo. Hapa tayari kuna kujichanganya.

Wabunge wanaongea kwa namna wanavyojua wao.
Kwavile nia ya wenzetu ni kuikashifu Tanzania wao watachukua kauli ya mbunge kama Komba na kuifanya kama kauli ya serikali.

Hoja ya kuwa na ushirikiano na Burundi au DRC si core issue.
Hakuna hakuna sababu za kuwa na kauli tofauti kila siku.

Nadhani rasi Kikwete anatakiwa atoke awaeleze wananchi nini kinaendelea.
Hii habari ya kukwepa hoja nzito na kuwaachia mawaziri kila mmoja akiongea lake inazidi kuleta picha kuwa kuna kuhaha kwa Tanzania.

Hapa leadership haipo ndio maana Spika anaruhusu mijadala ambayo serikali haijafikia tamati, waziri Sitta anasema hili, Membe anasema lile ili mradi tu kuna a kind of disorganization.

In this situation the buck stops with Mr President JK
Rais ametoa hotuba pengine kwa kuzingatia ukweli huo hapo juu
 
Duru za Siasa - Matukio inalitazamaje suala la mpambano wa viongozi wa Chadema kushambuliana wenyewe kwa wenyewe kwenye mitandao ya kijamii kwa mustakabali wa Chadema na taifa zipi athali zake.
@Ritz kwa muda duru imelifuatilia suala hili kwa uangalifu, umakini na kwa kina.

Duru imefikia hatua nzuri kabisa ya kulizungumzia kwa kuzingatia mambo yafutayo.
1. Historia ya tatizo
2. Chimbuko la vurugu za sasa (kwanini sasa)
3. Sababu za mtinange unaondelea CDM (sababu kuu tatu)
4. Makundi yanayohusika
5. Hatima na mustakabali wa vurugu hizi kwa taifa
6. Nini CDM wafanye kujinusuru.

Tunaomba wana duru uvumilivu wa masaa 48 tu tutakuwa mtandaoni. Hataonewa mtu hata hurumiwa mtu, ukweli utatamalaki.
 
MTAFARUKU, MPAMBANO NA KUSIGISHANA KWA CHAMA CHA CHDEMA
MZOZO WA VIONGOZI NA UONGOZI


Sehemu ya kwanza

Katika siku za karibunu Chadema imejikuta katika mtafuruku unaohusisha viongozi na kutikisa uongozi mzima. Kuna wanosema mtafaruku huu ni mdogo na wengine wakidai ni kukua kwa chama.
Ukweli usio na shaka mgogoro huu ni mkubwa, mzito unaotishia uhai wa Chama kwa vigezo vya kijamii na kisiasa.


Kuna sababu kuu mbili zainazopelekea hali kutotulia na kuongezeka kwa uhasama.
1. Sababu kutoka ndani ya chama
2. Sababu kutoka nje ya Chama.

Hatuwezi kuliongelea tatizo bila kujua chanzo chake japo kwa uchache. Kwa muktadha huo tutakuwa na sehemu tatu zinazohusu mada hii. Tunatanguliza samahani kwa urefu wa mada, uhuhimu wa kufanya hivyo ni mkubwa kuliko kuliangalia tatizo kijuu juu.

A: Kuasisiwa kwa chama:
Tunafahamu waasisi wa chama ni wale waliokataa kukubaliana na sera za chama tawala nayakati hizo.
Wengi walipoteza nafasi zao kwa kupingana na 'establishment' ndani ya CCM.

Kwa bahati mbaya kutokana na mvuto wa Mwalimu wakati huo ,nyota zao zilifunikwa na wao kuonekana kama 'wahaini\. Mmoja wapo ni mwasisi mzee Edwin Mtei.

Chadema kikawa chama cha watu wasiokubaliana na CCM na wenye 'resentment' kikiungwa mkono na watu wa mikoa ya kaskazini zaidi. Kuungwa mkono si kutokana na asili ya viongozi bali mwamko na kiwango kikubwa cha uelewa kuliko sehemu nyingi za nchi. Uasi wa mikoa ya kaskazini dhidi ya CCM ni wa kihistoria.

Mzee Mtei aliendeleza chama katika ngazi ya kitaifa tbila kuingia mikoani au vijijini.
Mrithi wake marehem Bob Makani hakuwa tofauti sana na Mtei, pengine utofauti wake ulikuwa kukijenga chama katika bunge kwa kiasi fulani. Na hatimaye akachukua Mbowe ambaye ni mwenyekiti hadi sasa.

Kitu kimoja kikubwa kilichofanywa na Mtei na Makani ni kuwajenga vijana kujiunga na chama.
Hapo ndipo walipowapata akina Mbowe .

Tofauti na watangulizi wake Mbowe aliamua kukieneza chama katika taasisi kama vyuo ambako alifanikiwa kuwaingiza akina Zitto n.k.

Mbowe ana sifa kubwa ya kukisambaza chama. Alipogombea urasi alifahamu hawezi kushinda lakini hiyo ndio ilikuwa njia rahisi ya kukieneza chama. Kwa hilo ni credit ambayo haiwezi kuondolewa kwake.

Chadema ni chama chenye historia ya kubadilisha viongozi bila migogoro.
Ni chama chenye historia ya kuteua mgombea wa nafasi ya Urais kwa mwanachama wa kawaida wa chama.

B:
Mgogoro ulianza katika uchaguzi wa Mwenyekiti kipindi cha pili. Ni wakati huo vijana walioingia CDM walishakuwa maarufu kwa ujenzi wa hoja bungeni. Mmojawapo ni Zitto. Vijana hao walitaka nafasi zaidi ndani ya chama pengine kwa kutaka kufanya mageuzi ya haraka au kwasababu za uongozi tu kwa kuzingatia umaarufu.

Wazee wa CDM kwa kuzingatia utaratibu waliokuwa nao wa kuchagua viongozi waliona chama bado ni kichanga kukabidhi vijana wasio na uzoefu na pengine hilo lingepunguza nguvu za chama.

Walizingatia jitihada za Mbowe na kudhani alihitaji muda zaidi kukijenga chama.
Hata hivyo uamuzi huo ulikinzana na dhana ya demokrasia ambao ni msingi wa chama chao.
Ingawa suala lilimalizwa ukweli ni kuwa halikumalizwa kwa maridhiano bali wengi wape.

Mtafaruku wa pili ni ule wa kuwania nafasi ya kuongoza upinzani.
Huu pia ulimhusisha Mbowe na Zitto . Maamuzi yaliyotolewa hayakuonekana kufuata misingi ya demokrasia(principles) bali kanuni za mardhiano' consensus'
Hili likazidisha ufa kati ya Mwenyekiti Mbowe na Naibu katibu mkuu Zitto

Ykatokea makundi mawili makubwa ndani ya chama.
Kundi la Mwenyekiti linalotetea uendelezaji wa chama kwa kufuata misingi ya waanzilishi na kundi la Zitto linalodhani kuna umuhimu wa mageuzi ya uongozi na kwamba ni wahanga'victims' ndani ya chama.

Kundi la pili la Zitto likaamua kujiimarisha ili kujenga himaya kwa kukusanya vijana.
Ni kundi hili lililojaribu kufanya mapinduzi batili likiwa na akina Kafulila.

Hakuna siri kiongozi wa kundi hilo ni Zitto. Ndipo ulipotokea mtafaruku wa pili uliopelekea akina Kafulila na Sungura kujiondoa ndani ya chama baada ya kunyang'anywa madaraka.
Walitambua wazi kuwa bila madaraka wasingeweza kufikia lengola mageuzi kwa njia za haraka

Zitto anaamini kuwa kutofanikiwa kwake ni matokeo ya kutokuwa katika kundi la 'wazee' au inner cicricle na njia rahisi ni kuanzisha makundi ili yapenyeze katika uongozi wa taifa.

Ni kwa msingi huo aliunda kundi jingine ambalo leo tunaijua kama Chadema 'Masalia'.
Kundi hili lilikuwa na makamu mwenyekiti wa BAVICHA na wanachama wengine.

Kundi hilo lilifanikiwa sana kupenya katika ngazi na ofisi kuu za chama.
Mbinu za kuwachafua viongozi zikaanzia na kila mara kukawa na taarifa za kuchafuana ambazo zilikuwa zinatoka ndani ya chama.Baadhi ya wanachama wakaodnolewa katika nafasi hizo akiwemo Mwigamba.

Kutokana na kuvunjika kwa kundi la masalia na lile la viongozi ndani ya ofisi za chama, ukaanzishwa mtandao mwingine unaohusu viongozi katika ngazi za mikoa.
Lengo likiwa ni lile lile la awali la kutengeneza mazingira ya kukabiliana na kundi la uongozi 'establishment'

CHIMBUKO LA VURUGU ZA SASA.

Itaendelea sehemu ya pili mchana huu......
 
CHIMBUKO LA VURUGU ZINAZOENDELEA

Inaendele...
Chimbuko la vurgu zinazoendelea sasa ni kutokana na kufukia ukweli wa mzozo nilioueleza hapo juu na ni baina ya makundi mawili, kundi liliko madarakani likiwa na mwenyekiti na katibu mkuu, na kundi la Naibu katibu mkuu, mshauri wa Chama na mtandao uliojengeka wa kimikoa.

Makundi haya yana wapiga debe ambao ndio wameleta mtafaruku huu uonekane dhahiri.
Mtifuano uliopo kati ya Lema na Zitto ni uwakilishi tu wa matatizo ya muda mrefu.

Uongozi wa juu umegawanyika katika makundi yafuatayo
1. Kundi linaloamini kufanya kazi kwa kuleta mageuzi (Neutral)
2. Kundi linalowania uongozi kwa matamanio kuwa sasa ni wakati wao(Power struggle)
3. Kundi linaloamini katika CDM kama ilivyoasisiwa na misingi yake (establishment)
4. Kundi la wasaliti ambao wanatumiwa kukihujumu CDM (Traitors)

Kundi la 1 linakereka sana na hali ilivyo ndani ya chama na kwa bahati mbaya hili lina wapiganaji kindaki ndaki wasio na sauti sana ndani ya chama.

Kundi la 2 linajenga mtandao wa kukabliana na kundi la 3 kwa kuamini kuna mambo kama ukanda n.k. na njia
rahisi ni kujenga mtandao wao. Ndilo limekuwa chimbuko la matatizo kila mara.

Kundi hili haliamini katika mageuzi kama hatua(process) linaamini katika hatua za nguvu (radical intervention) na lipo tayari kutumia mbinu chafu hata kama kufanya hivyo kutaumiza chama(bomoa leo tutajenga kesho)

Kundi la 3 linaamini mageuzi ni hatua na linafuata taratibu za makubaliano (consensus) zaidi kuliko demokrasia. Kwasasa limegundua kupungua kwa nguvu yake kutokana na mtandao wa kundi 2 kuwa mkubwa.
Limeamua kujibu mapigo

Kundi la 4 ndilo hatari sana. Hili linawashirikisha watu kutoka chama tawala ili kuhakikisha CDM inakufa kabla ya uchaguzi ujao.

Kundi hili linaungwa mkono na wana CCM kwasababu linafanya kazi iliyokusudiwa.Wapo wanachama wa kundi la 2 ambao ni washiriki wa kundi hili katika jitihada zile zile za kuwania uongozi(power struggle)

Tatizo lililozushwa na Mwigamba halimhusu yeye binafasi.
Mwigamba ni mwakilishi wa mtandao uliojengeka ambao unaona muda unazidi kwenda na mkakati haujafikia mhali pa zuri.

Ni kwa msingi huo madai ya Mwigamba kama 'mkulima masikini' ni kuwepo kwa uchaguzi kwavile mtandao umeimarika vema. Mwigamba si tatizo bali wale walioko nyuma yake ambao ni viongozi.
Mwigamba alipochukuliwa lap top ghafla likatokea kundi lililotaka kumuunga mkono hadarani la wenye viti wa mikoa. Ikumbukwe kuwa kuna katibu mkuu wa mkoa aliwahi kukihama chama kwasababu zile zile za Mwigamba

Tatizo la Lema kumshambulia Zitto si la kisera au misimamo ya chama.
Ni kundi la uongozi linajibu mapigo kwa kushambulia chanzo.
Ndio maana husikii Lema akijibishana na Mwigamba, tumtemeke au mwingine na uongozi umekaa kimya kushughulikia jambo hili.

Tatizo ambalo tumewahi kulisema hapa duru za siasa siku nyingi sasa lipo wazi.
Chadema imejengwa katika misingi ya personality. Kuna watu ambao ni chama na chama ni wao.
Laiti taratibu zingekuwa zinaongoza chama wala tatizo lisingefika hapa lilipo.

Kungekuwa na uwazi katika kuendesha shughuli za chama na kuruhusu mawazo mbadala hata kama hawakubaliani,
kusingekuwa na viongozi wanaojenga makundi yanayotishia uhai wa chama.

Na kwavile kuna ufa, CCM inautumia vema ufa huo kudhoofisha chama.
Inatumia maneno na kashfa zinazotokana na wanachadema kuufanya mtafaruku kuwa mkubwa zaidi.

Tazama jinsi shughuli za CDM zilivyozorota(M4C) na uenezaji wa chama ulivyofifia.
Haya ndiyo CCM inayapenda na imetumia vyombo vya habari rasmi na vya kijamii katika kuendeleza mgogoro ambao ni mkubwa hata bila kuongeza nguvu kutoka nje.

Kibaya kinachoimaliza CDM ni kuvunjika moyo kwa wanachama(political base) ambayo imekuwa inafanya kazi kwa moyo na sasa ikijikuta haina viongozi wa pamoja bali makundi.
Hili linaimaliza sana CDM na linahitaji kuangaliwa kwa ukaribu.Huwezi kufanikiwa kisiasa bila kuwa na strng political base. Si kundi la uongozi au linalowania likalofaulu kwa kuua political political base.

Personality zinaweza kusaidia tu kwa muda mfupi,kwa muda mrefu ni maafa makubwa sana. Ndicho kiliikumba NCCR na CUF na hakuna shaka kama hakuna umakini CDM ipo katika orodha

NINI MUSTAKABALI WA CHADEMA KWA TAIFA

Itaendelea
 
NINI MUSTAKABALI WA CHADEMA NA TAIFA

Mustakabali wa CDM utategemea sana hatua za haraka na za makusudi watakazochukua. Kwa upande wa taifa mstakabali utaangaliwa kwa namna mbili.

1. Kwa chama tawala CCM na wale wasiopenda mabadiliko ya kiuchumi na kijamii kifo au mtafaruku ndani ya CDM ni faraja kwao. Hiyo ni njia rahisi ya kuhakikisha kuwa chama tawala kinaendelea kutawala tena katika hali tuliyokuwa nayo miaka kadhaa kabla na baada ya vyama vingi.
Ni fursa kwa kundi au makundi ya watu kufanya watakavyo 'business as usual'

2. Kwa upande wa umma wa wananchi wenye kupendelea mabadiliko ya kiuchumi na kijamii hili litakuwa ni pigo kubwa. Ni kurudi katika zama za serikali kulala, wezi kutamalaki na kila aina ya uchafu kushamiri.
Uwepo wa vyama vya upinzani ni sehemu muhimu sana ya check and balance.

Tumeshudhudia jinsi bunge lililosheheni wabunge wa chama kimoja likipitisha maazimio kwa njia za masilahi yao na si masilahi ya umma. Tuanzo kumbu kumbu za jinsi bunge lilivyoficha habari zinazoathiri maisha ya wananchi kila siku. Leo watu hawajui kwanini tunalipa umeme kwa bei ya juu kuliko nchi zote za EA.

Ni kutokana na sababu namba 1 duru tunaamini kuwa pamoja na kuwa na mzozo wa ndani wa CDM, kuna uchochezi unaotaka nje. Uchochezi unaopenyezwa kwa kuangalia safu za uongozi wa juu wa CDM.
Kwavile CDM imejengwa kwa personality atakayetikisa personality hizo atakuwa ameleta kishindo kikubwa

Kwa mfano mwenyekiti wa CCM anapoanadama na mwanachama wa CDM na kueleza wazi kuwa huuni wakati wa vijana kutawala nchi, ni dhahiri alikusudia kuwatia kichwa vijana hao ili wajisikie kuwa sasa ni wakati wao na inapaswa wafanye jambo. Ndiyo haya tunayoyaona ya vijana kuacha siasa za uchumi na jamii na kujiingiza katika siasa za 'uharamia' kwa kutumia mitandao, kuchafuana na kuchafua viongozi wengine.

Lakini pia ikumbukwe kuwa CCM wametumbukiza mbegu za ukabila ambazo zimeota vema ndani ya CDM.
Kundi linalopinga uongozi linatumia hiyo kama hoja muhimu sana hata kama linafahamu hakuna ukweli.
Hii ni mbegu waliyopanda akina Nchemba na Nape na sasa inachanua.
CDM wakubali au wakatae huo ni ukweli.

CCM imetumbukiza mbegu ya udini. Nayo pia inatumika katika kubomoa chama.
Mbegu hiyo inatumiwa na baadhi ya viongozi wa CDM kujilinda kwa namna fulani. Inawalinda kwasababu hatua zozote zinaweza kutafsiriwa katika maana isiyokusudiwa na kuleta mantiki isiyokuwa na ukweli.

Mgogoro wa Chadema unachagizwa sana na CCM, hata hivyo ni lazima CDM wajilaumu kwa kutoa nafasi kwa mahasimu wao kutumia udhaifu wao.
Kwavile haionekani kama CDM wanajielewa suala hilo linaweza kuamua mustakabali wao kama ilivyokuwa kwa NCCR na CUF.

CHADEMA WAFANYE NINI KUJINUSURU
Itaendelea.....
 
CHADEMA WAFANYE NINI KUJINUSURU

Gogoro la Chadema ni kubwa na lenye mizizi mirefu na mizito.
Ni mgogoro unaoweza kukivuruga chama kama hatua za haraka na makusudi hazitachukuliwa.


Hakuna busara kwa viongozi kuwa katika hali ya kukataa 'state of denial' ya uwepo wa tatizo kubwa.
Na hakuna hekima wala busara kwa viongozi kuamini kuwa kukaa kimya ni njia ya kumaliza tatizo.


Umuhimu wa kulishughulikia tatizo ni mkubwa kwasababu muda si mshiriki mzuri.
Mzozo wote unaofukuta umejikita katika viongozi na uongozi na wala si wanachama.

Kuelekea uchaguzi wa 2015 mzozo huo utakuwa mkubwa zaidi. Harakati za akina Zitto, Lema, Mwigamba na Tuntemeke ni kiashirio kizuri kuwa kadri muda unavyosonga bomu linakarikibia kulipuka.

Tatizo si wanchama na wapenzi wa CDM. Tatizo lipo katika viongozi na uongozi.
Chama kimejengwa katika mardhiano'consensus' badala ya demokrasia.
Kimejengwa katika personalities badala ya wanachama.

Ili kuweza kukabiliana na tatizo, baada ya kukubali kuwa kuna tatizo(kuacha state of denial) mambo yafuatayo yafanyike haraka sana kabla ya mwezi March 2015 kama CDM ingependa kushamiri.

1. Chama kikubali uwepo mgongano wa mawazo ndani yake na kwamba hilo si kosa bali ni sehemu ya demokrasia.
Kuwepo na uwazi wa uendeshaji wa chama na taratibu zifuatwe ikiwemo kalenda ya shughuli za chama.

2. Uchaguzi wa chama ufanyike haraka ili kukijenga chama tayari kwa hatua zinazofuata.

3. Kukirudisha chama nikononi mwa wanachama
Kuwepo na jitihada za makusudi kabisa kuvunja nguvu ya personality( s) zinazodhani chama ni wao na wao ni chama.

Personality hizo zidhibitiwe kwa kutumia kanuni na sheria za chama bila kujali umhimu wao.

Hakuna personality iliyo juu ya chama na kwamba chama kwanza na watu na haiba zao baadaye.

4. Chadema izingatie demokrasia ya kutoa uhuru wa kushiriki katika mambo ikiwemo chaguzi
Iachane na utamaduni wa chama kuongozwa kwa misingi ya maridhiano 'consensus'.

Chadema kimekuwa na wala hakina upungufu wa viongozi na hakuna sababu za maridhiano bali demokrasia iachwe ichukue mkondo wake.


5. Kuvunjwa kwa makundi
Baraza la wadhamini na ile la wazee waingilie kati na

a)kuvunja uongozi uliopo na kuitisha uchaguzi kama njia ya dharura ya kutafuta muafaka

b) Kuwachukulia hatua madhubuti wanakaokiuka misingi ya uendeshaji wa chama hata kama ni viongozi
c) Kuwafukuza wanaoendesha kampeni chafu dhidi ya wanachama na chama chao

d) Kwaonya na kuwataka
i) Mh Mbowe avunje kundi lake la vijana linaloshambulia viongozi wengine.
Akina Lema wachukulie hatua za kinidhamu kwa kukiuka misingi ya chama na uongozi.

ii)Zitto achukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuwa kinara wa migogoro kwa kutumia vijana ndani ya ofisi za Chadema , katika mitandao na avunje mtandao anaoujenga kwa nia ya kuvuruga chama.

6. Wasaliti wote wa chama wapewe nafasi ya kujieleza na ikidhihirika vinginevyo wafukuzwe ndani ya chama mara moja.

7. Uongozi kupewa jukumu la kuchukua hatua za haraka pale kunapotokea fununu za ukorofi kuliko kusubiri mgogoro ufukute kama uliopo.

Katika kutekeleza hayo lazima kuwepo na hatua za ukakasi (radical intervention) ambazo hazitaangalia personality ya mtu ndani ya chama bali ushiriki wake katika kuzua au kueneleza migogoro.
Hilo halitarajiwi kuwa jambo jepesi lakini ndio jibu la kudumu la tatizo lililopo.

Hatutegemei mwanachama wa kawaida aje na jibu lakini wanachama wana majibu.
Wachague viongozi kwa kuzingatia sifa za uongozi, historia zao za mambo ya kisiasa na ushiriki wao katika ujenzi wa chama.
Wanachama wachukue ownership ya chama na kuwatuma viongozi watende na wala isiwe kinyume chake.

Na wala CDM wasitegemee kuwa Mbowe na Zitto wanaweza kuvunja kambi zao kirahisi.
Ni wanachama wanaoweza kuvunja ngome hizo kwa kuwakataa wale wanaoongoza na wapiga debe wao.

Duru tunamalizia kwa kusema mgogoro uliopo si wa Cahadema kama chama, ni wa viongozi wawili wenye makundi ndani ya chama, mwenyekiti Mbowe na naibu katibu mkuu Zitto. Hawa ndio wachawi wa CDM.

Hadi pale wanachama watakaposimama na kusema Mbowe na Zitto hatutaki mnayoyafanya, CDM inaelekea kule CUF na NCCR walipopumzika.

Wanajamvi tusemezane
 
Nguruvi3,

Mkuu wangu lazima ufahamu kwanza mzizi wa fitna unatoka wapi kisha unapofanya mabadiliko unakuwa unajenga badala ya kuziba nyufa ilihali nguzo hazipo tena.
Mimi mtoto wa mujini nafahamu fika kwamba hizi zote ni jitihada za kukiua chama na hao kina Mbowe na Zitto ni sababu au nyenzo zinazotumika kuukuza mgogoro ambao kusema kweli haupo.

CCM ina mbinu nyingi sana za kukimaliza chama au mtu yeyote anayekuwa threat kwao. Na moja ya mbinu zake ni kuingiza majasusi chamani ambao wameingia hadi ktk mishipa ya damu ya chama, sasa wanaifanya kazi yao. Niliwahi kusema zamani ya kwamba hapakuwa na mgogoro baina ya Zitto na Mbowe isipokuwa uliundwa na ukashika moto.

Tatizo kubwa la CDM ni uendeshaji wa chama hiki kama NGO ambapo kuna watu wanajua fika kwamba wakiwa karibu na Mbowe watafaidika kisiasa iwe madaraka ya ndani ya chama au kupewa nafasi ya kugombea Ubunge, udiwani na kadhalika. Hawa watu wote ni wachumia tumbo ambao wepesi kumeza lishe wanayopewa ili kujipendekeza kwa Mbowe.

Mimi binafsi namfahamu Mbowe vizuri sana, na namuaminia sana japo tayari jina lake limekwisha haribiwa kisiasa lakini bado ni kiongozi mzuri na bora kisiasa. naweza sema Mbowe ni mwanasiasa bora kuliko vijana wote wa CDM, isipokuwa tatizo lake image yake imekwisha tiwa dosari kulingana na sifa wanazo ziamini Watanzania.

Kwa upande mwingine Zitto ni shupavu, mzalendo na kwa siasa za CCM yeye ni weakest link yao maana hafanani na wengineo maana yeye toka zamani ni muumini wa mfumo wa kihafidhina, lakini viongozi wengi wa CDM ni wajamaa kiitikadi japo wamejiunga na Chadema ili wapate kupanda majukwaani. Na hili utaliona ktk hotuba zao,majigambo yao lakini mimi husema hawa wote ni wanafiki maana wanapopewa nafasi za uongozi, huo Ujamaa wao hukoma pale pale na kuwa hawana tofauti na viongozi wa CCM maana hupingana na Zitto hata ktk matumizi ya fedha za walipa kodi.

Kwa kumalizia tu, ni kwamba haya yote yamepangwa na CCM kama mbinu mojawapo ya kukimaliza chama kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015. Na kinachokosekana CDM ni Hekima na Busara maana kumejaa vijana wasiofikiri na kupima uzito kabla ya kusema ama kuandika. Kwa nini ikiwa mtu ana mashtaka yoyote kuhusu Zitto au Mbowe malalamiko hayo yasipelekwe ktk vikao vya chama isipokuwa inaanzia ktk magazeti na mitandano wakati huyo mlalamikaji ni kiongozi ndani ya chama?. Huyu mtu huwa ana lengo gani haswa kama sio kutumika ili kukivuruga chama kabla ya 2015. Wengine huanza kutoa tuhuma zao baada ya kufukuzwa madaraka, hii kweli inaingia akilini! tena basi bila aibu hujiunga na CCM na kunadi ati anazo siri za Chadema, hizo siri gani hizo uloficha hadi ufukuzwe na CDM wasiwe na wasiwasi kukufukuza. Na mbona hao wengine walotoka CCM hawakuja na siri za CCM au huko hakuna siri?.
 
Mkuu Mkandara , ahsante kwa bandiko
Kama umenisoama vema nimeeleza kwa kina kuhusu chagizo la mgogoro kuanzia nyakati hizo hadi sasa.

Nimeelaza kuwa CCM walitumia karata ya ukanda na ukabila. Karata hiyo imekufa baada ya kuonekana kuwa CDM ina nguvu sehemu nyingine kuliko katika kanda yao. Mfano ni Mwanza.

Wakatumia kete ya udini ambayo imekufa baada ya kuona CDM inaungwa mkono na sehemu kubwa ya Watanzania bila kujali itikadi zao.

Kwasasa wanatumia udhaifu wa viongozi ndani ya CDM kukidhoofisha chama.
Karata hii inaonekana kufanya kazi.Kwa mfano, iweje CCM wamalize masuala yao kama ya mafisadi kimya kimya lakini waunge mkono wana CDM wanaokichafua chama chao kwa mgongo wa demokrasia ndani ya chama?

Kuna demokrasia gani CCM wanaweza kuieleza kama mfano. Si uhuru wa kusema au wa kutenda lakini wameshikilia bango hasa wanapotokea watu ndani ya CCM kutenda yale yale CCM isiyokubaliana nayo.

Ni makosa kuilaumu CCM kwasababu ndio kazi wanaotarajia kuifanya baada ya kukosa hoja licha ya kuwa madarakani.Kinachofanywa na CCM ni 'survival' tu kwasababu mbinu za kihoja hazina mashiko tena.

Watu wa kulaumiwa ni viongozi wa CDM na vijana wao ambao hawatafakari kwa kina yale yanayotokea bali kuongozwa na hisia tu.

Mbowe, nimeeleza ni mwanasisa na mchango wake kwa chama ni mkubwa.
Hata hivyo chama kimefikia mahali pa kujitanua zaidi na lazima mbinu na taratibu zibadilike kutokana na ukuaji wake.

Chama kiendeshwe kwa taratibu na viongozi wawe tayari kukabiliana na changamoto.
Huu si muda wa kuendesha chama kwa 'consesus' yaani maridhiano.
Kuna mapungufu kwa upande huo na katika kuziba mapungufu hayo Mbowe amevutika katika matumizi ya vijana badala ya kuchukua hatua za kisheria, kanuni na nidhamu kuimarisha chama.

Kwa upande wa Zitto, naye ni mwanasiasa mahiri na mchango wake katika chama unathamaniwa kama sitakosea.
Tatizo linalojitokeza kwa Zitto ni kutengeneza makundi ndani ya chama.
Mgogoro wa akina Kafulila, Zitto alitajwa.Mgogoro wa masalia Zitto alitajwa. Na huu mgogoro wa Mwigamba Zitto ametajwa.

Tatizo ambalo wengi hawapendi kuliongelea ni kuwa sasa hivi CDM inajiimarisha kuelekea vijijini.
CDM ina hazina kubwa ya viongozi kwa bahati mbaya utamaduni wa kutegemea Personality unakimaliza chama.
Na CCM wanajua vema ukitikisa 'personality ABC' chama kinayumba na wanapiga hapo kwa mapigo.

Ni kwa msingi huo nimeshauri uitishwe uchaguzi ili uongozi mpya upewe nafasi ya kurejesha nidhamu na utokane na wanachama wenyewe. Hili litasaidia sana kuvunja makundi yaliyopo.

Mimi siamini kuwa CCM ni tatizo, nina amini kuwa tatizo ni CDM wenyewe wanaojenga ufa na CCM kuutumia kuwavuruga.

Mkuu Mkandara hakuna shoka linalokata bila mpini, kwa hili nasema CCM ni mpini tu shoka lenyewe lipo ndani ya CDM.

Mgogoro huu ni mkubwa hata kama watu wanakataa. Umehusisha vijana ambao sasa hawafugiki tena.
Vijana hao ni wa makundi ya Mbowe na Zitto.
 
RE: MGOGORO WA UONGOZI NDANI YA CHADEMA

Nguruvi3,

Wengi tulikuwa tunasubiri umalizie mada yako kuhusiana na mfarakano inayoendelea ndani ya Chadema. Umefanya kazi nzuri sana, hasa ya kutuelimisha juu ya masuala mengine ambayo hatukuwa tunayatazama kwa undani kiasi hicho. Naomba nichangie kidogo kwenye mada ifuatavyo:

Kwa mujibu wa maelezo yako, kinachoendelea ndani ya Chadema ni uwepo wa makundi mbalimbali madogo ndani ya kundi kubwa au kwa lugha ya wenzetu, factions. Mara nyingi, hasa katika demokrasia zilizokomaa, uwepo wa factions ni feature ya kawaida katika demokrasia ya vyama vingi, na sio lazima iwe ni kitu ni kitu ‘destructive' kwani katika siaza za Vyama - huwa kuna constructive factions & destructive factions. Kwa upande mmoja, Constructive factions mara nyingi (sio mara zote) revolves around zaidi onindividuals/personalities, and on the other hand, Destructive factions mara nyingi (sio mara zote), revolves Zaidi around Issues;

Kwa maelezo yako hapo juu, factions zilizopo Chadema hivi sasa ni mchanganyiko wa constructive and destructive factions. Swali linalofuatia ni je:

· Ni factions zipi zina "a constructive function" na factions zipi zina "a destructive function" kwa Chadema na
Demokrasia ya Tanzania kwa ujumla?

Binafsi sina majibu Zaidi ya maoni tu kwamba kundi ulilifafanua kama kundi namba moja ndio kundi pekee lenye "pure constructive function" yani:

Kundi linaloamini kufanya kazi kwa kuleta mageuzi (Neutral)

Kundi llingine naona kama vile lipo kwenye border line baina ya kuwa constructive and destructive factions, na hili ni kundi namba mbili, yani:

Kundi linalowania uongozi kwa matamanio kuwa sasa ni wakati wao(Power struggle)

Naliweka kundi hili katika border line kwa sababu kuu moja kwamba - zaidi ya kutaka generational changes in leadership, kundi hili halina mtazamo/sera ambazo zinatushawishi kwamba zitakuwa ni mbadala wa kweli kwa CCM. So far, linaonekana ni kundi ambalo linataka kwenda kufaidi madaraka na resources zinazoendana na uongozi wa juu wa chama, na sio kitu kingine.

Kundi ambalo kwa mtazamo wangu naliona ni "pure destructive faction" ni kundi namba nne ulilojadili hapo juu, yani:
Kundi la wasaliti ambao wanatumiwa kukihujumu CDM (Traitors)
.

Na sababu juu ya kwanini kundi hili ni pure destructive faction for Chadema na ujenzi wa demokrasia ya vyama vingi kwa ujumla nchini, ni sababu ambazo zipo wazi, hivyo sina haja ya kuingia katika mjadala huo kwa kina.

Kundi namba tatu linaweza kuwa either way – pure constructive or pure destructive, yani kundi ulilojadili kama:

Kundi linaloamini katika CDM kama ilivyoasisiwa na misingi yake (establishment)

Kundi hili linaweza kuwa "pure constructive faction" iwapo nia yake ya dhati ni pamoja na kudhibiti kundi namba nne yani:
Kundi la wasaliti ambao wanatumiwa kukihujumu CDM (Traitors)
,

Lakini pia iwapo nia yake ya dhati ni kuhakikisha kuendeleza ‘conservatism' juu ya masuala Fulani Fulani mpaka wakati muafaka ufike.

Lakini pia linaweza kuwa "pure destructive" iwapo nia yake ni kutoruhusu chama kiende mikononi mwa wengine kwa sababu za ovyo ovyo tu kama ukabila, ukanda, ukoo na mambo yanayofanania na haya.

Katika nchi za wenzetu wenye demokrasia zilizokomaa, madhumuni makuu ya factions huwa ni pamoja na haya yafuatayo:

1. Kushinikiza sera Fulani au Policy agenda Fulani.
2. Kuzuia sera Fulani au policy agenda Fulani mbadala isipite.
3. Kuunga mkono watu Fulani Fulani ndani wenye malengo ya uongozi ndani ya chama.

Swali linalofuatia ni je:

· Madhumuni haya matatu yana uhusiano na kundi lolote ulilojadili hapo juu?

Kwa haraka haraka, binafsi naona makundi yote manne uliyojadili yanahusiana na dhumuni namba tatu hapo juu yani
Kuunga mkono watu Fulani Fulani ndani wenye malengo ya uongozi ndani ya chama.
Pengine ndio maana mijadala mingi juu ya factions ndani ya vyama vya siasa inatuelimisha kwamba factions politics mara nyingi revolves around personalities ambapo watu wachache play key roles, acting like magnets kwa watu wengine wenye similar mindsets or interests. Vinginevyo madhumuni ya factions niliyojadili kama namba moja na namba mbili hapo juu, yani:

· Kushinikiza sera Fulani au Policy agenda Fulani, na
· Kuzuia sera Fulani au policy agenda Fulani mbadala isipite.

Sijafanikiwa kuona kama madhumuni yana uhusiano wowote na makundi uliyojadili. Sana sana labda kama ni kuhusiana na kundi namba nne kutumika na CCM Kimkakati (sio Kisera) kuhakikisha kwamba Chadema haifanikishi malengo yake ya kuchukua utawala wan chi, 2015.

Mwisho nikuulize, je, kuna uwezekano wowote kwamba chanzo cha factions ndani ya Chadema kinatokana na:

· Failed expectations ambazo zimepelekea polarization and divisions within the party?
· Politics of exclusion within the party?

Na je, kama haya yapo, ufumbuzi wake ni nini: Politics of accommodation au Politics of Compromise?

Kama tunakumbuka vizuri historia ya TANU, chama hiki kilipata misukosuko mingi kutokana na intergenerational conflicts. Ni bahati tu kwamba chini ya mfumo wa chama kimoja, ikawa ni rahisi kwa TANU na baadae CCM kuwapatia Vijana ajira katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya chama – UVCCM, ambapo wengi pia wakawa wanapata fursa ya kupenya kwenye nafasi mbalimbali kama vile ubunge, ukuu wa wilaya, n.k. Utamaduni huu bado unaendelea hadi leo vinginevyo CCM ingeshakufa siku nyingi kutokana na kushindwa to accommodate factions.

Tofauti na CCM, Chadema haina resources za kutosha to accommodate factions ndani ya Chama. Matarajio ya umma kwa chadema yamekuwa ni makubwa sana kuliko uwezo wa Chadema kukidhi matarajio hayo na pia kuliko uwezo wa Chadema kupambana na CCM, hasa pale CCM inapotumia resources and organizational capacity yake kupambana na mafanikio ya Chadema in the electorate. Chadema ifanye uamuzi wa haraka: je, kuelekea 2015,

· Chama Kiegemee Zaidi upande wa Political Party au upande Political Movement?

VariablePolitical OrientationPolitical Party
OrientationCauseIssues
Level of operationRegimeGovernment
Main area of operationSocietyParliament
Method of OperationMobilizationPersuasion
Member orientationDiffuseSpecific
Claims to resourcesNo formal limitsConstrained by rule of law

Chadema ichague sasa, kwani haiwezekani kutumikia mabwana wawili. Hata TANU (1950s), mafanikio yake kutokomeza Chama tawala cha mkoloni (UTP) yalitokana na TANU kujipanga Zaidi kama a political movement kuliko chama cha siasa; kwa kufanya hivyo, kulipunguza incentives za umma (plus viongozi wa TANU) kupoteza muda katika kushabikia na kuchochea mapungufu ya TANU kama vile poor organization, lack of financial resources and factionalism; Lengo likabakia moja tu kwamba – kumtoa mkoloni na kuikomboa nchi irudi mikononi mwa maskini ambao ndio walikuwa ni wengi; Kuitoa CCM madarakani ni muhimu kwa demokrasia ya Tanzania kwa maana moja tu: Kukipa Changamoto CCM, na kuzaa vyama viwili vikuu vya siasa nchini kwani hiyo ndio njia pekee ya CCM kujirekebisha; CCM haiwezi jirekebisha ikiwa madarakani:

cc Ritz, Zinedine, gfsonwin, Mkandara
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi na Nguruvi3 nashukuru sana kwa michango yenu juu ya hali ya mgogoro ndani ya CDM.

nimesoma michango yenu na kuikubali sana lakini sasa kuna mambo nami pia ningependa kuongezea ambayo naona hayapo.

kwanza kabisa CDM inatakiwa ijue kwamba ni chama chenye nguvu na kimeweza kuwin trust ya watua akwa kiwango cha hali ya juu. lakin pia kwa chenyewe kuwa chama basi lazima misukosuko itatokea tu manake wao sio malaika useme hawata tofautiana hata lugha tu.

kama ndivyo basi CDM wanatakiwa waichukue hii kama changamoto kwao na sio kama adhabu ama uonevu kwao ili wasimamie misingi imara ya upinzani ili kuleta tija kwenye demokrasia ya kweli.

CCM ukweli inahitaj kupata mbadala japo wa 5 yrs ili sasa ijipange upya lakin hii haiguarantee kwamba CCM wako kimya kwenye kusaka nafasi ya kuendelea kubaki madarakani. kama ndivyo lazima wajue kwamba cdm wanakazi kubwa kuwaondoa na wanaye taka kumwondoa hawata mwondoa kwa nguvu ya mtutu ama ya bomu bali kwa nguru ya kuwa na political stability ndani ya chama na kuwa na sera nzuri zenye ushawish wa kutekelezeka na sio zile za kuifanya Kigoma dubai miaka 10 sasa bado hata hadi ya jiji la tanga haijafikia.

jambo jingine CDM wala isihangaike kupambana na maadui zake kwa kuwa-attack maadui bali ipambane nao kwa sera, utendaji mzuri na kuwa na watu clean wanaoweza kushika mshumaa wa chama. iachane kabisa na siasa za kusema nani anastahili kuwa mwenyekiti wa chama bali igeukie kwenye kura iwe mwamuzi na mtu achagulkiwe na watu.

Lakin pia CDM itambaue kwamba trust ambayo wananchi wanayo juu yake ni kubwa sana na hivyo kushindwa kufanya kile kinachokusudiwa na wananchi wengi basi ni kuwaonea sana na kuwavunja moyo haw ambao wanawaamini.
 
Last edited by a moderator:
Binafsi sikupendezwa na kile kili/nachoendelea Chadema, hata hivyo nikubaliane na Mchambuzi kwamba, Chadema hakina budi kubadilika na kuwa na ukomavu zaidi wa ku-focus kwenye kujenga imani ya uthabiti na uimara wa uongozi utakaoweza kuwatofautisha na chama kilichopo madarakani. Na zaidi, mimi nitakuwa na -attention na siasa za nchi yetu mpaka tutakapokuwa na chama kimoja tu (chenye nguvu zaidi) cha upinzani. Hii itaifanya siasa iwe katika sifa za ushindani wa kweli kuliko sasa hivi ambapo kuna vyama vipo kwa ajili ya kutawanya kura za upinzani ili kukipa ushindi chama kimoja tu. Naamini ushindani wa pande mbili zaidi kuliko tatu, nne, na kuendelea
 
Last edited by a moderator:
gfsonwin
Hoja zako mbili nazitamana kwa mitazamo miwili
1. Chadema imepata umaarufu si kwasababu ya watu bali watu waliosimama vema kutetea sera na umma.
Watu waliojipambanua na jamii kuwaona kama wasemaji wao.

2. Kwa kusimamia masilahi ya umma kama chama cha upinzani, CDM ili 'win' nyoyo za watu kwa matumaini yao

Badala ya kuchukua imani kama changamoto wamechukua nafasi hiyo kama sehemu ya kutaka ukubwa, umaarufu wa mtu binafsi na kusahau bila watu hakuna chama.

Unapoungwa mkono na mamilioni ya Watanzania automatic unapata uhalali wa uongozi wa umma, wao ni viongozi wa umma. Tatizo ni pale kila mmoja anaon uwepo wa CDM ni kwasababu yake. Ubinafsi umeshaingia.

CCM wanafahamu kuwa kuushaiwshi umma kwamba wanaweza kufanya jambo tofauti na miaka mingi iliyopita ni ndoto.Wanachokifanya ni kudhoofisha anayeonekana ni tatizo. Hapa si TLP au CUF ni CDM, wanatumia udhaifu wa ubinafsi kukabiliana na CDM na hadi sasa wamefaulu sana.

Mfano, Nape amesikika akisema CDM wafanye uchaguzi ama sivyo atawashtaki kwa msajili.
Haiwezekani Nape anayeshinda na kula na wahalifu wa nchi hii aone umuhimu wa CDM kufanya uchaguzi. Haiwezekani Nape anayezuia demokrasia ndani ya chama chake aone demokrasia ndani ya CDM.

Anachokifanya Nape ni kutumia madhaifu ya siku za karibuni kuendeleza mgogoro.
Anafahamu uchaguzi kwa wakati huu CDM ikiwa mapande utawafaidisha CCM.

Yeye yupo mikoani anaimarisha CCM huku CDM wakiwa wamesimamisha kampeni zao kama M4C.
Hata ziara zao mikoani sasa hivi zimegubikwa na malumbano ya wanachama na viongozi ngazi za kitaifa.
Hii ni destruction ya hali ya juu sana.

CCM wanafahamu wakati huu chama kikiwa kimegawanyika, chaguzi ambazo naturally hugawa vyama kama CCM itazidi kupigilia msumari wa moto juu ya donda bichi.

Ni makosa kumlaumu Nape. nachokifanya ndicho anachokitaka. Makosa ni ya CDM kuanza malumbano tena ya kipuuzi kabisa katika mitandao, kukashfiana na hata kutuhumiana katika mambo yenye itikadi za chama kama suala la posho za bunge. Leo nani anaweza kusimama na kusema CDM wanasimama wapi katika suala hilo.
Zinedine , nafasi ya kuwa na chama kikuu imejitokeza mara tatu.

Kwanza NCCR, pili CUF na sasa CDM. Mara zote hizo wananokiangusha chama si wananchi ni wanachama viongozi.
Hakuna sababu ya wananchi kusubiri kizuke chama kingine kama uyoga.
Nadhani wanapaswa kuchukua ownership ya mambo ya kisiasa.

Ownership ni kama sasa ambapo badala ya watu kulumbana kwa hoja za kitoto, wangesimama kwa pamoja na kusema hili ndiyo hili hapana. Huyu anasema kweli huyu muongo na wawakatae watu hao mara moja
 
Mkuu Mchambuzi
Kwanza niseme uwepo wa factions ndani ya chama ni jambo la afya kabisa.
Kinachotakiwa ni factions kutimiza majukumu kama ulivyo aanisha na niongeze ziwe na lengo la kukiinua chama

Hivyo sivyo ndani ya CDM kwa sasa. Kinachoendelea ni factions za kuumizana bila kujali gharama za chama.

Nimeandika mara nyingi kuwa kupingana kwa mawazo ndani ya chama tena kwa uwazi ndio demokrasia na uhai w. Nimemuunga mkono Zitto katika baadhi ya hoja na kumpinga zingine bila kumhukumu kwanini ana mtazamo tofauti pengine na chama chake.

Kilichoimaliza CCM ni kutokubaliana na mawazo tofauti. Kila aliyepinga kama Kolimba aliitwa na kutishiwa kitumbua.Nadhani wao wamebadilika kiasi, najaribu kufikiria ingekuwa enzi hizo akina Filikunjombe, Lugora, Mwambalwasa wasingekuwa viongozi. Bado safari yao ni ngumu lakini basi wanajaribu.

Factions zilizpo CDM si za kujenga chama ni za kuua chama. Factions za kujificha na kutoa tuhuma nyuma ya mitandao ni destructive force. Imefika mahali CDM hawawezi kupingana bila kutumia mitandao.
Hivi kiongozi wa CDM hawezi kusimama na kuuambia uongozi hili si jema ni hadi ajifiche kwa majina bandia.


Factions inanyowakilisha 'neutral' ninaionea hurum. Hii imejaa watu wanaoamini katika mabadiliko bila kujali nafasi zao siku za baadaye. Utawakuta Shinyanga, Singida, Ukonga katika mashina wakifanya kazi ya chama
Ni nadra kuwasikia katika mizozo wanaamini katika matokeo mazuri.


Factions zilizobaki ni 'pure destructive'
1. Lile kundi linaloangalia uongozi umeeleza vema kabisa na wala siongezi kitu.

2. Kundi linaloamini CDM ya asili lina tatizo moja. Linaamini katika kutenda mazuri, kwabahati mbaya limejaa wahafidhina 'extreme conservative' ambao hawawezi kukubaliana na mabadiliko hata kama ni chanya.

3. Wasaliti" Hili ndilo linazamisha CDM lina ukaribu sana na kundi la 1 hapo juu.

Je, ufumbuzi ni politics of accommodation au politics of compromise?
Niseme hakuna accommodation wala compromise,. Makundi hayo yanaweza kuua chadema kama yatapewa fursa.

Nitatoa mfano, CCM wanafanya politics of accomodation. Tazama jinsi inavyowatesa na ni suala la muda utaona ufa mpana sana ambao ndio utakuwa kaburi lake kama kutakuwa na mbadala.

CUF wanafanya politics of compromise ona chama kilivyokosa msimamo na mwelekeo. Mwenyekiti anasema hili, katibu mkuu lile, kiongozi wa CUF bungeni hili, msemaji wa chama lile, naibu katibu mkuu vile n.k. ilimradi tu kuna compromise ya kuishi kama wana CUF

NCCR ilitokea radical intervention, chama kikadhoofika sana lakini bado kipo na kinajikongoja.

CDM hakihitaji politics of accommodation kwasababu kufanya hivyo kukiwa na makundi matatu yanayokinzana ni kulea ugonjwa. Wamejaribu sana ku accomodate kiongozi wa kundi linalowania uongozi wa CDM kwa kutomchukulia hatua na amekuwa ndiye 'culture media' ya waasi wa CDM na kila siku anawaletea matatizo.

Wamejaribu politics of compromise kwa vikao vya kuondoa tofauti zilizopo katika makundi.
Hiyo ime feli kwasababu hakuonekani kuwa na muafaka bali ni chuki za chini chini na kuchekeana kinafiki.

CDM wanahitaji radical intervention kama NCCR. Kuna namna mbili
1. Kuwaweka pembeni katika uongozi viongozi wa makundi yanayoleta uharibifu usio wa lazima
3. Kuwaondoa katika chama kwa kuwafukuza.

Hakuna kiongozi wa CDM anwyeweza kutenda hayo hapo juu kwasababu uongozi mzima upo katika accomodation na compromise hata kama kuna hatari. Ndicho kinaendelea sasa hivi kwa mwenyekiti, katibu mkuu, kamati kuu na vyombo vingine kujifanya hakuna mzozo wakati mzozo ni mkubwa sana.

Wanaoweza kuisadia CDM ni wanachama. Na wafanye haya
1. Wakubali kuwa kuna tatizo linalosababishwa na viongozi kuvurugana.(waache denial state)
2. Washinikize yawepo maongezi ya wazi juu ya tatizo
3. Waondoe tofauti zao zinazojengwa na mirengo ya viongozi, watambue kuwa umoja wao ndio salama ya chama.
4. Wameze ukweli kuhusu makundi wanayoshabikia na wayanyooshee vidole bila aibu au haya
5. Wachukue hatua nilizozisema hapo juu
a) Kuwaweka kando viongozi wanaoleta ghasia na uchochezi hata kama ni personality za chama
b)Kuwafukuza katika chama wanaohusika kama wasaliti n.k.

Hii ndiyo salama ya CDM. Vinginevyo August 2014 tutakuwa tunaongelea CDM kwa njia nyingine.
Nimewahi kuwaonya kuhusu mgogoro wa masalia, nikaeleza chanzo chake na watu walioko nyuma yake.
CDM wakapuuza maoni na miezi 5 baadaye wakaonja shibiri ya akina Shonza. Na hili nasema ni suala la muda.

Nitaendelea na hoja zaingine ulizozianisha.

 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom