Duru za siasa - Matukio

DR SEZIBERA AENDELEZA MASHAMBULIZI DHIDI YA TANZANIA.
KASHFA SASA BILA KIFICHO

Tumeshaeleza katika mabandiko mengi na hata la mwisho#340 ya kuwa katibu mkuu wa Jumuiya ya EA anachangia sana katika kuzorotesha Jumuiya.

Juzi alihojiwa Nairobi kuhusu mkutano unaotarajiwa kufanyika kati ya tarehe 28-29 Oktoba mjini Kigali ukiwashirikisha marais watatu (Uhuru, Museveni na Kagame). Sezibera amesema 'hana taarifa za Tanzania kutengwa ndani ya shirikisho. Kufanyika kwa mikutano ya washirika si uthibitisho wa Tanzania kutengwa au kuondolewa katika shirikisho' alisema.

Katika mahojiano na waandishi, Sezibera alitoa kauli ikiashiria kushiriki vema katika hujuma dhidi ya Tanzania.
Alisema 'From the secretariat point of view, we are not aware. I can't say if Tanzania has been sidelined or is a reluctant partner in the bloc'.

Kwa mtazamo Dr Sezibera anaihukumu Tanzania kuwa reluctant bila kueleza kwanini.
Katika lugha ya kidiplomasia reluctant ni neno kali linaloonyesha Tanzania ni Wakaidi.
Tanzania haiwezi kuwa kaidi bila sababu, lugha aliyotumia ni mwendelezo wa mashambulizi dhidi ya Tanzania.
Ikumbukwe Sezibera ni raia wa Rwanda.

Sezibera hakuishia hapo aliendelea kuinanga Tanzania vilivyo '
He added that it could not be claimed that Tanzania was paying lip service to EAC aspirations by differing with its partners on issues such as the use of national IDs as valid travel documents.''

Jambo asilotaka kulisema ni kuwa kutumika kwa vitambulisho ni suala linalohitaji umakini.
Sezibera anafahamu nchi yake ni miongoni mwa nchi zenye wahamiaji haramu Tanzania na vi itambulisho ni njia rahisi ya kuingiza raia wa nchi nyingine kirahisi ili kukamilisha mpango wa iliobuniwa awali na kukwama wa kuhusu ardhi

Suala la vitambulisho lilishatolewa uamuzi kuwa nchi zinazoona inafaa ziendelee hadi sasa Kenya na Rwanda wana mapngo huo. Hakuna sababu za kuburuza wanachama wengine na hilo si kazi yake.
Kwanini ameshupalia vitambulisho? Soma maneno yake yafuatayo

Dr Sezibera said yesterday that the bloc should urgently address the issue of immigration, adding that the recent expulsion of illegal immigrants in Kagera, Kigoma and Geita regions was done "haphazardly" and it should be done in the right manner where human rights are not violated''

Dr anasema zoezi la kuondoa wahamiaji haramu limefanya hovyo na kipuuzi na Tanzania kwa maana hiyo na kuwa upo ukiukaji wa haki za binadamu. Asichokileza ni haki gani zimekiukwa kwa wahamiaji kurudishwa kwao.
Dr anailaumu Tanzania kuchukua hadhari dhidi ya yale yanayoleta taabu Goma na kwingineko.

Kauli yake imesukumwa na Unyarwanda zaidi kuliko spirit ya EA. Huyu ni kiongozi hatari sana ambaye Tanzania na nchi nyingine zinapaswa kumuangalia. Endelea kusoma matusi na kashfa za Sezibera dhidi ya Tanzania. Anasema

Dr Sezibera confirmed that the team sent by the EAC secretariat to Kagera Region in August gather facts on the deportation of illegal immigrants had completed its task.
Earlier, the Kenyan Cabinet Secretary for East African Affairs, Ms Phyllis Kandie, urged Rwanda andTanzania to meet urgently to resolve the issue of illegal immigrants.

Dr Sezibera ameshawishi nchi za jirani kuamini kuwa zoezi hilo lililenga Wanayarwanda pekee.
Dr Sezibera anazidi kutia chuki ambayo haipaswi kuwepo kwa nchi Mwanachama kulinda mipaka yake.

UNHCR imeiomba radhi Tanzania kwa taarifa juu ya kukimbizwa kwa wakimbizi na kuna kila sababu ya kuamini kuwa Dr Sezibera alikuwa na ushaiwshi kwa UNHCR kuhusiana na hilo. Hakubali ukweli bali kuendelea kuchochea utengano.

Kutoka na msimamo wa Dr Sezibera kuishambulia Tanzania na kuacha facts nyingine muhimu tunashawishika kusema ni 'nyoka' ambaye Tanzania inapaswa kumuangalia kwa macho mawili.

Kauli zake za kashfa na hata matusi dhidi ya Tanzania zinatuleza hali ilivyo na ni wakati sasa serikali ya Tanzania ikahoji kama Sezibera ni katibu wa Jumuiya au ni waziri wa serikali ya Rwanda.

Tunadhani wakati umefika Dr Sezibera aende kuhudumia KKK na kuiacha EAC.
Hakuna taifa linaloweza kuvumilia matusi ya wazi tena bila 'ku balance'.

Kwa hisani ya The citizen

Tusemezane.

 
HOTUBA YA RAIS YA MWEZI

Tuiangalie taasisi ya Urais inayoongizwa na Rais. Taasisi hii huwezeshwa kujitosheleza kwa mahitaji ya bajeti malipo ya wafanyakazi na wahudumu wengine.Kwa kutambua majukumu mazito Ikulu ina kila ngazi ya watumishi.


Wapo wafanyakazi wa kawaida,washauri wa Rais kutoka serikalini na ashauri binafsi wa rais wengine wakiwa si sehemu ya serikali ingawa wanahudumiwa kimafao na serikali.


Ikulu ina uhusiano na vyombo vya nchi kwa ukaribu kuliko taasisi nyingine hii ni katika mtazamo wa uzito wa majukumu na unyeti wake.Taarifa za Ikulu zinapaswa ziwe za uhakika bila shaka au chembe ya sintofahamu.


Kauli ya rais huchukuliwa kama sheria kwa kutambua kuwa itakuwa imefanyiwa kazi na wasaidizi wake kama mawaziri, mwanasheria mkuu, katibu mkuu kiongozi na wasaidizi binafsi.


Hakuna jambo linalotia shaka na wasi wasi kama habari kutoka Ikulu zitakuwa hazina utofauti na kauli nyingine za kusikia au kusemwa ‘hearsay'.


Kwa mtazamo huo hotuba ya Rais ya mwanzo wa mwezi iliyoandaliwa na Ikulu kwa kushirikisha vyombo vya dola ,wasaidizi na washauri imeacha umma katika lindi zito la mshangao na mkanganyiko.


Duru za siasa tuanzie hapo kwa kuiangalia hotuba hiyo hasa katika maeneno tata au yaliyoleta sintofahamu.

1.Rais ametumia maneno ' nimeambiwa/Nimeelezwa' si chini ya mara 9.
Kauli hizo zinamaanisha Mh Rais anaeleza kitu ambacho ima hana uhakika nacho au ana uhakika usiothibitika kutoka katika vyanzo vyake.

Swali la kujiuliza inakuwaje Rais mwenye access na kila eneo la nchi na chombo chochote kama bunge apewe habari asizoziamini yeye mwenyewe na kutueleza.


a)Haieleweki akilini pale mhe. Rais anaposema ameambiwa utaratibu uliotumika katika kupeleka mswada Zanzibar hauna ulazima wa kupitiwa na kamati za huko. Hivi Mwanasheria mkuu alimshauri nini Rasi kuhusu suala hilo.
Mh Rais anaposema ameambiwa na si kuongea kimamlaka inatia shaka kama alishauriwa na watu husika au alikuwa na wasi wasi na ushauri wao.

Hata kama kisheria haipo,bado wasaidizi na washauri wa rais wanapaswa kumshauri atumie maneno ya busara katika kuongelea masuala nyeti na muhimu kama hili la Znz.


b)Hata hao ‘waliomwambia' ilikuwaje hawakumwambia kuwa waziri wake wa sheria amekiri kupeleka vifungu pingufu Zanzibar kujadiliwa.


Je waziri na Mwanasheria akiwemo katibu mkuu kiongozi walifanya kazi zao inavyopaswa?

Hakuna shaka alichokisema Rais na kilichosemwa na wasaidizi haviwiani na vimemweka Rais katika hali ya kuonekana ni muongo, mzushi au anajichanganya yeye na wasadidizi wake (Disorganized) jambo la aibu kwa taasisi ya Urais.


Tuna kila sababu ya kuwa na wasi wasi kuhusu umakini wa ofisi hii kubwa ya nchi hasa watendaji wake. Rais anaongea kwa mamlaka na si kwa kutumia maneno ya ‘nimeambiwa/nimesikia n.k.' kama sisi watu wa mitaani.


Kutokana na maelezo tuliyotoa awali hakuna sababu zozote za kuifanya taasisi ya Urais ionekane katika hali inayoonekana.
Kuna tatizo kubwa hasa kwa wasaidizi wa rais wa ngazi zote, wale wa serikali na binafsi.

Tutaendelea na hoja ya 2 Kuhusu hotuba ya Rais



 
2. Bandiko lililotangulia tumeona jinsi Rais alivyoshauriwa vibaya au kupotoshwa kutokana na udhaifu ima wa vyombo vyake alivyochagua au yeye mwenyewe kukubali hali hiyo.

  1. Mwanasheria mkuu wa SMZ na waziri wa sheria wameeleza hadharani mswada ulivyopelekwa kwa ujanja wa kuondoa vifungu. Hii ina maana kuwa viongozi hao wana mchalenji Rais wa JMT hadharani tena wakiwa na takwimu na ushahidi.
2 Makamu wa pili wa rais SMZ alikwenda Dodoma na kuetetea mswada ambao ulikuwa pungufu kwa maana ya ulaghai
3.Waziri mkuu Pinda alikuwepo bungeni wakati mswada unapitishwa. 4.Mwanasheria mkuu, waziri wa sheria na waziri ofisi ya rais na utawala bora wote walikuwepo.

Waziri mkuu, kiongozi wa serikali bungeni akishirikiana na mawaziri na mwanasheria mkuu wote ni wateule wa Rais. Kisichojulikana ni kama hawa viongozi waliwasiliana na rais wakati wa mtafaruku au walikuja na suluhu zao za ulagahai na kumwingiza Rais mwishoni!!


Hakuna namna inayoweza kueleza kuwa hawa siyo waliompa Rais ‘maneno' hadi akasema nimeambiwa nimesikia n.k.
Kama ndio basi wamemwadhiri vibaya Rais kwasababu ya taarifa potofu.


Na kama wao walikuwa na msimamo uliopo wa kushinikiza mswada, Rais atakuwa amewageuka kiujanja na kuwaadhiri. Kitendo cha kusema suala ABC yarudi bungeni ni dhalili kwa Waziri mkuu na viongozi wenzake wakiwemo wa Bunge.


Ni aibu kwa taifa Rais anaposema bunge lilijadili vema mswada kifungu hadi kiufungu huku dunia ikijua kuwa kilichofanyika ni matusi dhidi ya wapinzani, inasikitisha.
Pengine rais alipewa taarifa potofu na wasaidizi wake au alipewa taarifa sahihi akaamua makusudi kupotosha habari hizo.


Leo ni nani anayeweza kuamini maneno ya viongozi wetu ikiwa wao wenyewe hawaaminiani na kila mmoja anaongea suala lake bila kuwa na team work.

Katika mazingira yaliyopo Rais ana machaguo mawili


  1. Kuwawajibisha viongozi waliompa taarifa potofu
  2. Kubaki na msimamo wake ambao una mashaka kuliko uhakika machoni mwa wananchi.

Kwa upande mwingine baadhi ya viongozi wanapaswa kuwajibika kumsaidia Rais atoke katika aibu iliyopo.


  1. Waziri mkuu kwa kushindwa kuongoza serikali kupata suluhu hadi Rais kutoa maamuzi yasiyohitaji hata kikao. PM alikuwa na nafasi ya kumuomba Spika muda wa kujadiliana na mh Rais.
Hakufanya hivyo akiamini anachokifanya ni sahihi. Je, ni sahihi kutokana na mwenendo uliopo?

2.Waziri Lukuvu, Chikawe na Wasira anapaswa kuwajika kwa kumuingiza Mh Rais katika timbwili la aibu.
Waziri wa SMZ na mwanasheria mkuu wanapotoa ushahidi wa kumsuata Rais wa JMT hakuna namna bali mawaziri
husika waliopeleka mswada feki kuwajibika ili kumnusuru rais na aibu hii.


Kutokana na utamaduni wan chi yetu sidhani kuna lolote kati ya hayo linaloweza kufanyika.
Tunajua utendaji wa viongozi wetu ni ule wa nifae kwa jua nikufae kwa mvua.


Hii itaacha jambo moja kubwa, kwamba wale watu waliokuwa na mashaka kuhusu udhaifu wa serikali ya JK na udhaifu wake kama kiongozi wataondokewa na mashaka.
Umma utapoteza imani kwa rais na pengine mchakato wa katiba ukaingia katika machafuko kutokana na upotoshaji.


Sehemu inayofuata tutaangalia kauli zaidi katika hotuba na nia ya hotuba hiyo kama ilifanikiwa au imezidi kuleta uharabifu.


Tutaendelea

 

Sehemu ya tatu

HOTUBA YA RAIS

Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanasema Rais JK hupenda kuridhisha kila upande .
Kisiasa ni mkakati mzuri hasa kiongozi anapohitaji muda wa kumalizia ajenda zake. JK hana sababu hizo kwasababu huu ni mhula wake wa mwisho.


Kiongozi hapaswi kuwa na sura mbili wakati wa kuongoza.
Anatakiwa asimamie kile anachoamini ni sahihi na kukemea kisicho sahihi.


Katika hotuba ya JK kuna eneo amesema wapinzani walitoa mawazo mazuri hata kukwamua baada ya kukwama. Halafu akasema Wapinzani wameamua kutoka bungeni bila kujadili rasimu na hivyo kukosa fursa.
Hapa alikuwa anawapendeza wapinzani halafu akarudi kuwafiriji CCM kwa kauli yao.


Kiongozi anapokuwa na double standard anauchanganya umma.
Ilikuwa ni vema mh akaeleza kwanini wapinzani waliokuwa na mawazo mazuri waliamua kutoka.
Kusema walitoka tu ni kama kusema walienda kunywa chai au bia na kuacha mswada.


Rais ameshindwa kuelezwa kuwa wabunge zaidi ya 134 hawakuwemo.
Kusema mswada ulijadiliwa kwa kina wakati akidi haikutimia ni kuongoza kwa namna ya ajabu kidogo.

Suala zito la katiba halijadiliwi na wabunge 100 tena wakitoa matusi halafu Rais wa nchi afurahi kuwa umejadiliwa kwa kina. Hansard za bunge zipo wazi sijui kipi kilishindakana kumshauri Rais kuhusu hilo.


Rais akaendelea kumnanga mh Tundu Lisu kama mnafiki, mzandiki na mzushi.
Alichokisahau ni kuwa Rais hapaswi kuleta malumbano na Raia mmoja mmoja tena kwa lugha ya kashfa.


Lakini pia Tundu aliongea kama waziri kivuli wa kambi ya Upinzani.
Kama alitaka kutukana angewatukana Wapinzani na si Tundu Lisu.
Pengine kwa mwenendo wa Rais JK kutaka kumpendeza kila mtu alihofia kusema wapinzani akaamua kumshambulia raia mmoja kwa kupitia. Hizi zote ni dalili za udhaifu wa hoja pengine na uongozi kama si serikali.


Wapinzani wamemjibu kwa ushahidi kuwa TEC na Walemavu hawakushirikishwa.

Kilichobaki ni Rais wan chi kuwa na malumbano na raia kwa jambo ambalo laiti anagekuwa na wasaidizi makini wala asingefika hapo. Hii inasikitisha sana.


Kwa yale mambo aliyosema yanaweza kuzungumzika yarudi bungeni bado kuna maswali yanayoonyesha udhaifu wa serikali. Mfano, ni serikali ya JK iliyoandaa mswada wa awali uliotoa muda kwa tume ya Warioba kumaliza kazi . Katikati ya mchakato serikali hiyo hiyo inasema ukomo uwe wakati wa bunge la katiba.


Rais JK anaelewa hoja za akina Warioba kuhusu muda wa tume na kwanini iendelee hadi kumalizika kura ya maoni. Wakati huo huo hataki kuudhi wana CCM wanaotaka kuteka mchakato kupitia bunge la katiba.

Kwa kuwa JK hupenda kupendeza maeneo yote ili abaki kuwa mzuri kwa kila upande, suala hilo hakusema lirudi bungeni yeye ana maoni gani. Ukisoma kwa undani amesema kuhusu ukomo kabla ya bunge halafu akauliza ikihitajika nani aje tume au mwenyekiti wa Tume.


Maana yake anakubaliana na wana CCM kuwa tume ya Warioba ikome wakati wa bunge la katiba, lakini kwa ujanja anauliza na kusema litaamuliwa na wabunge.
Hii si aina ya uongozi unaotakiwa katika nyakati hizi ngumu.

Kilichonikitisha zaidi katika hotuba ni pale aliposema hahitaji kazi ya kuteua kwasababu ile ya kwanza ya kupata wajumbe 15 ilikuwa ngumu sana.

Hivi Rais wa watu milioni 40 alitegemea kupata jambo gani rahisi. Hivi si alizunguka nchini akiomba kazi ya Urais, leo iweje alalamike kuwa kuna mambo magumu. Nani alisema Urais ni jambo rahisi!


Tunasisitiza hotuba ya rais ukiisoma kwa undani na kuielewa umeonyesha udhaifu hasa wa serikali ya leo madarakani.

Tutaangalia ni wapi serikali imedhoofika, wapi mafisadi wamepata ushindi na Wapinzani waende Ikulu kunywa Togwa kama ilivyokuwa siku za nyuma.


Itaendelea….

 
KUDHOOFIKA KWA SERIKALI YA JK
Hotuba ya JK imeendelea kuonyesha udhaifu wa serikali kwa mambo mengi. Athari zake zinaweza kupelekea hali ya vurugu au kutekwa kwa mjadala wa kitaifa unaohusu katiba.

  1. Makamu wa pili wa rais wa SMZ , waziri wa sheria na mwanasheria mkuu wanajisikia kudanganywa na wenzao wa serikali ya muungano.Hili linafanya uungwaji mkono kutoka Zanzibar kupungua na kuwa na athari kubwa kwa wahafidhina wa CCM ingawa ni nafuu kiwa taifa.
  2. Viongozi wa serikali bungeni ,waziri mkuu na Wabunge waliotetea mswada huo kwa nguvu za chama sasa wanajisikia kusalitiliwa na mwenyekiti wao licha ya kudhalilika.
  3. Wabunge wa CCM kutoka Zanzibar wanajihisi kudanganywa na kuisaliti nchi yao kama wanavyoelezwa na wapinzani ndani ya mikutano
  4. Kundi la ‘mafisadi' wanaojipanga kwa uongozi 2015 limepata nguvu zaidi,JK anabaki mwenyewe bila uungwaji mkono isipokuwa kwa ''wajinga'' wachache wasio na aibu wanaoweza kutetea upuuzi hata kama ni matusi
  5. Wananchi wameingiwa na shaka kuhusu uaminifu na utayari wa JK kusimamia katiba mpya hasa wale walioamini kuwa kulikuwa na nia njema.

KITATOKEA NINI?

  1. Wapinzania wanaendelea kuungwa mkono pande zote za muungano. Tumeona jitihada zao za kuwaleta Wazanzibar pamoja ili kupunguza nguvu kubwa ya CCM bara.
Mkakati wa wapinzani kuwatumia waznz ni mahususi kwa kutambua kuwa turufu yao ndani ya bunge la JMT haina
nguvu kutokana na mikakati na ubabe unaonendelea.

Maana yake ni kuwa nguvu ya JK kuudhibiti mchakato kwa kutumia inapambana na upinzani mkubwa zaidi wa vyama na wazanzibar.Hicho kimepelekea JK kuwaita wapinzani ili kupunguza nguvu inayoungwa mkono na umma wa pande zote


  1. kwavile keshapoteza idadi kubwa ya wabunge wanaounga mkono serikali yake, nguvu ya JK imebaki katika wajumbe 166 anaotakiwa awachague watiifu sana.Wajumbe 166 nao sasa ni mwiba kutokana na shinikizo la wapinzani, na hata wakipatikana wale wa znz hawategemewi kuwa watiifu kutokana na udanganyifu ulioonekana.
  2. Kundi linalowania 2015 ambalo limewekeza sana katika serikali 2 linaonekana kupata nguvu.
Kundi hili halikuathirika na mgogoro uliopo kwasababu kuparaganyaika kwa mshikamano katika serikali ya JK ni
faraja kubwa kwao.

Kundi hili litaelekeza nguvu katika bunge la katiba. Endapo litafanikiwa kupenyeza watu wao ndani
ya bunge huo utakuwa mwiba kwa wananchi na wapinzani kwa ujumla.
Utakuwa ni mpambanio wa mafisadi na wananchi kwakuwa seriakali ya JK imeshapoteza nguvu.
Ni kutokana na udhaifu wa serikali ya JK katika kushughulikia masuala mazito ya kitaifa, sasa uwezekano wa kuvunjika muungano ni mkubwa kuliko wakati mwingine. Na kama wazanzibar wanataka hilo litokee hii ndiyo nafasi pekee, serikali imeshadhoofika na hakuna wa kuzuia hilo kutokea.

Kwa kutambua kuwa ajenda ya katiba mpya si ya CCM na maamuzi yalikuwa ya JK, jambo hili likiingia katika NEC ya CCM ambayo JK hana ushawishi litamsumbua sana.

Lengo la JK kuteka mjadala wa katiba mpya ilikuwa kuhakikisha serikali inabaki na nguvu wa kulinda mambo kama muungano, kwa bahati mbaya hilo sasa lipo hatarini na JK keshapoteza nguvu na udhibiti.

KWANINI KUNA KUYUMBA YUMBA KWA MCHAKATO?
Mchakato haukufuata kanuni za uandikaji katiba. Katiba haiandikwi na serikali, inaandikwa na wananchi na serikali inabaki kuwa mdau kama taasisi au vyama vingine vya kiraia.

Serikali ilitakiwa kuandaa mazingira kama ulinzi na huduma za kifedha ikibidi, ili wadau kutoka sehemu mbali mbali waanze na mkutano wa kitaifa, kuangalia tunataka taifa la namna gani, tuandae vipi katiba na akina nani wasimamie.
Serikali ingekuwa mdau kama taaisi nyingine na pengine ingebaki kuwa na ushawishi kuliko kilichofanyaika sasa hivi.

Hebu tuangalie 'safari' ya wapinzani ikulu na nini wafanye au wasifanye, je, watakunywa Togwa kama kawaida yao!!. Itaendelea….
 
Mkuu Nguruvi3,

Asante sana kwa hoja nzuri juu ya yanayojiri katika suala zima la mchakato wa katiba; Nimekuwa nikikufuatilia kwa muda mrefu sana kuhusiana na mada husika;siku nyingi ulishasema upinzani ulishakosea na taifa halitapata katiba itakayotokana na wananchi;je, unadhani safari ya pili ya upinzani kwenda ikulu kuonana na Rais (JK) inaweza zaa matunda ambayo yatabadilisha mtazamo wako wa awali? Na je, hivi tunaweza thibitisha kwamba Rais alishatia 'sign' muswada husika kuwa sheria na kuelekeza urudi bungeni kwa marekebisho? Marekebisho yepi hasa? Kilichoenea mitaani ni uvumi lakini ni vigumu kuhakikisha juu ukweli uliopo; pengine una taarifa sahihi zaidi, nipo kijijini kwahiyo mengi yamenipita;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,Asante sana kwa hoja nzuri juu ya yanayojiri katika suala zima la mchakato wa katiba; Nimekuwa nikikufuatilia kwa muda mrefu sana kuhusiana na mada husika;

siku nyingi ulishasema upinzani ulishakosea na taifa halitapata katiba itakayotokana na wananchi;je, unadhani safari ya pili ya upinzani kwenda ikulu kuonana na Rais (JK) inaweza zaa matunda ambayo yatabadilisha mtazamo wako wa awali?

Na je, hivi tunaweza thibitisha kwamba Rais alishatia 'sign' muswada husika kuwa sheria na kuelekeza urudi bungeni kwa marekebisho? Marekebisho yepi hasa? Kilichoenea mitaani ni uvumi lakini ni vigumu kuhakikisha juu ukweli uliopo; pengine una taarifa sahihi zaidi, nipo kijijini kwahiyo mengi yamenipita;
Mkuu Mchambuzi ahasante na salaam zao huko nyumbani.

Kuhusu hoja ya katiba na matatizo yatokanayo bado ninasimama na hoja kuwa mchakato hautatupa katiba tunayoihitaji kama wananchi. Kosa la kwanza la wapinzani ni kuachia serikali ichukue umiliki wa mchakato.

Safari ya kwanza ya wapinzani Ikulu zipo kumbu kumbu kuwa tuliwaasa wasikubali lolote isipokuwa hoja moja tu ya kurudisha mjadala mikononi mwa wananchi. Tuliwaambia kuwa kitendo cha JK kuchukua agenda ya katiba kilikuwa na lengo moja tu kuhakikisha udhibiti wa mchakato. Wapinzani wakaridhika na maneno matamu bila kujua repercussions zake.

Wapainzani wakapoteza fursa ya kurudisha mjadala kwa wananchi na hoja ikatekwa na CCM. Hili ni kosa kubwa na gharama zake ndizo kama hizi tunazoshuhudia sasa.

Mswaada haujasainiwa na Rais kwasababu maalumu kabisa. Kwanza anataka akutane na wapinzani ili 'waweke' mambo sawa. Nia yake ni kutaka kuwashawishi kuwa yale wanayoyagomea kama uteuzi wa wabunge 166 hayana maslahi kwa taifa, ukweli ni kuwa hayana masilahi kwake kwasababu anahitaji wajumbe 166.

Mswada haupo katika ratiba ya vikao vya bunge, 'on technical ground' ukisubiri matokeo ya kikao cha Rais na Wabunge. Mh Rais anaogopa kuwa kurudisha mswada kutawaudhi zaidi wabunge wa CCM ambao tayari wameudhika sana hasa wahafidhina wa CCM.

Mambo yanayoleta matatizo ni hili la wajumbe 166. Wapinzani wanasema Rais atangaze majina bila kupewa uwezo wa kubadili, kuondoa au kufanya chochote. Rais na CCM wanataka wajumbe 166 kwasababu kati ya 230 waliopo sasa idadi imeoungua sana. Wengi wanaunga mkono hoja za wapinzani.

Hoja ya pili ni ile ya kurudisha 2/3 badala ya simple majority. Kutokana na kupungua kwa idadi ya wabunge wa CCM wanaounga mkono hoja za akina Nape CCM inataka ushindi hata wa 51. Wapinzani wanasema hapana! katiba haiamuliwi kwa kura moja.

Jambo la tatu ni kuwashirikisha Wazanzibar. Wazanzibar walipelekewa mswada vifungu pungufu waliposhtuka vimeshatinga bungeni kwa Makinda na Ndugai ambao waliandaliwa kuhakikisha mtego unafanikiwa. Hili ndilo chimbuko la ugomvi wa Mbowe na Ndugai na hata Sugu.

Nne, serikali ya JK inataka tume ya Warioba ikome kazi baada ya kuanza bunge la katiba. Hii maana yake ni kuwapa uwezo CCM kubadili, kutengua, kuandika na kufanya watakalo kwasababu kuu mbili.
1. Wingi wao wa sasa 2) Idadi ya wabunge 166.
Haya yote yatawapa nafasi ya kuwa na Spika wanayemtaka ili wajipange na kutengeneza katiba yao.

Madai yote ya mswada yametengenezwa na serikali ya JK. Mswada ulipita katika baraza la mawaziri na JK aliridhia. Hakuna namna ya kuweza kusema yeye hahusiki. Hizi kauli za ;nimeambiwa' nimesikia n.k. ni kutaka kujivua majukumu. Rais huongea kwa mamlaka si kama mtu wa mitaani.

Hata baada ya kupata ukweli, Rais hajachukua hatua dhidi ya Lukuvi, Chikawe au Wasira kwasababu anajua walifanya alichowatuma. Huyu ni JK wa double standard na wa kupendeza watu.

Na kimalizia maswali au hoja zako hapo juu, safari ya pili ya Wapinzani Ikulu itakuwa na sura mbili.
1. JK atawasihi wakubaliane asaini mswada ili vifungu vyenye matatizo virudishwe kama sheria inayofanyiwa marekebisho. Hapa anataka kuwaridhisha wapinzani na wahafidhina wa CCM kwa wakati mmoja.

2. Wapinzani wasipokubaliana na hoja zake JK atawageuzia kibao na kuchomeka hoja kuwa wao wanataka kuchukua mchakato na kufanya spinning nyingi kwasababu atakuwa na media. Unakumbuka mkutano wa kwanza wa Togwa Ikulu ilitoa taarifa ya wapinzani kukubaliana na kila jambo baada ya wao kunywa Togwa na kuondoka

Wapinzani wana nafasi moja tu ya kujikwamua kwa kutaka yafuatayo.
1. Kumtaka rais awawajibishe mawaziri walioleta mtafaruku
2. Kukataa mswada usirudishwe kwa vipande vya sheria bali urudi mzima kama ulivyo
3. Kuitaka serikali ikae mbali na shughuli za kuratibu mambo ya katiba
4. Tume ya Warioba iendelee hadi siku ya mwisho.
5. Kusifanyike marekebisho tena ya sheria baada ya mswada uliopo kukubalika kurudishwa bungeni.
6. Kuismamia hoja ya wajumbe 166 wasitokane na rais

Nimesikiliza hoja za wapinzani katika mikutano yao sidhani kama wataktoka na kitu tofauti na mkutano wakwanza wa Ikulu uliomalizika kwa Togwa.
Hii ndio nafasi iliyobaki hasa serikali ikiwa imedhoofika sana ndani ya chama na kwa wananchi. Wapinzani wakishindwa kuitumia vema ndio mwisho wa mchezo!

 
Last edited by a moderator:
Katika duru hapo kesho tutaangalia mkuatano wa wapinzani na Rais
1. Nini tliongelea na imekuwaje
2. Wapi wapinzani walipoingia mkenge tena
3. Double standard za JK
 
MKUTANO WA RAIS NA WAPINZANI

USULI (FEEDBACK)
Mkuu Mchambuzi aliuliza swali akiwa kijijini iwapo mswada ulishasainiwa na hoja zingine bandiko#347 hapo juu.Bandiko#348 tulijaribu kueleza kile kinachotokea na kitakachotokea.

Ni kweli Rais alikuwa hajasaini mswada kuwa sheria kama tulivyosema. Sababu kubwa ilikuwa hofu ya maandamano ya tarehe 10. Lengo la rais lilikuwa kusaini mswada huo ili kutowaudhi wahafidhina wa CCM waliomshinikiza ausaini kwa nia zao ovu na za hila na kuzuia maandamano yaliyotishia kusimamisha nchi

Mkutano na wapinzani ulipangwa tarehe baada ya 10 kwa makusudi ili kutoa nafasi ya rais kuzuia maandamano na kumpa mwanya wa kusaini mswada asiudhi wahafidhina wa CCM.

Tunakumbuka habari zilipovuja haraka Ikulu mawasiliano walikanusha kwa kujua kuwa kusaini kabla ya tarehe 10 kusingezuia maandamano nchi nzima na kungeamsha hasira kwa wananchi.

Katika hotuba ya mwezi Rais aliwafariji wapinzani kwa maneno matamu huku pia akiwatukana ili kuwaridhisha wahafidhina wa CCM kwa upande mwingine. Huyo ndiye JK anayeweza kucheza na maneno kiujanja ujanja

Leo tunafahamu kuwa mswada ulisainiwa tarehe 10 baada ya kuridhika hakuna maandamano ya wapinzani. Alitegea wakubaliane na mwaliko wake halafu arudi ndani kuwafariji wana CCM. Ndicho kilichotokea.

Tuliwaonya wapinzani kuwa Rais Kikwete hupenda kumpendeza kila mtu na hivyo si mtu wa kuaminika kwa kauli. Tunakumbuka aliwahi kuwakemea Wabunge Diamond Jubilee kwa kutuma wazee wa CCM wasome risala ya kuwatuhumu. Leo tunajua Rais yule yule aliyewatuhumu wabunge diamond alisaini ongezeko la mafao ya wabunge.

Tuliwawatahadhirisha wapinzani kuwa lazima wawe na mawasiliano ya wazi kati yao na wananchi.
Leo ni takribani siku ya nne tangu mkutano huo hakuna kinachojulikana kwa wananchi.

Kinyume chake taarifa ya mawasiliano Ikulu imeeleza kuwa wapinzani walikuwa na taarifa ya kusainiwa kwa mswada kabla ya tarehe 10.

Tayari Ikulu imeshawazunguka wapinzani kwa kuwatupia mzigo kuwa walikuwa na taarifa kabla ya tarehe 10, wakati ambapo Ikulu hiyo hiyo ilikataa kusainiwa kwa mswada kwa press release

Ikulu imesema wapinzani na rais wamekubaliana mswada usainiwe kama sheria kisha urudishwe bungeni kwa marekebisho. Wamewataka wapinzani kupeleka mapendekezo yao haraka serikali ili sheria irudishwe bungeni.

Hapo JK ameshawazunguka tena kwasababu tayari kasaini mswada ambao wapinzani waligomea asiusaini.
Kwa maneno mengine JK ame buy time huku akisema wapinzani wana time yeye ana clock.
Kilichopelekea uwepo wa maandamano ni kuzuia mswada usisainiwe, sijui kwanini wapinzani hawalioni hilo!

Lakini muhimu ni kuwa kila mara mambo yanapogoma wapinzani hukimbilia kwa wananchi na kuwaeleza waungwe mkono. Vipi leo wapinzani wametoka Ikulu na hawajajitokeza kuwaeleza wananchi kile walichokubaliana Ikulu?

Kwanini wapinzani wadhani kuwa mawasilaino Ikulu inatoa habari kwa uhakika tukijua kile ni chombo cha propaganda cha rais! Kwanini hawajajitokeza kueleza wamesema nini.

Wapinzani wamekubali kukaa pamoja na akina Wasira, Chikawe na Lukuvi. Hawa wamewatukana sana kiasi kwamba nashindwa kuelewa inakuwaje na kwa kigezo gani wadhani kuwa uwepo wao mbele ya rais utabadili tabia zao za ajabu katika jamii. Wapinzani walitakiwa wagomee uwepo wa watu hao wasio na tija kwa taifa.

Mtego wa kuambiwa kila chama kiandike mapendekezo yake ni mkubwa sana. Wapinzani walikubaliana kuwa na ajenda ya pamoja. Kwanini serikali itake kila chama kilete maoni yake. Kwani JK alikutana na wapinzani kwa sababu zipi. Kwanini hoja zao zisichukuliwe pale pale na kufanyiwa kazi.

Kinachoendelea ni kuwagawa ili watawaliwe. Serikali ya JK itakuja na maoni kuwa kutokana na hoja ABCD zinaozpingana za wapinzani ni vema jambo ABC likafanyika kwa utaratibu serikali inaoona unafaa.
Kwa maneno mengine kwa utaratibu wa CCM na siyo nchi.

Hoja zitapelekwa kwa Makinda na Ndugai ambao watapewa ushauri waachie wapinzani waongee kwa kadri ya wingi na uwezo wao. Mwisho itaamuliwa kura ambayo CCM ina wingi na kwavile tayari rais ameshawaridhisha basi watashinda. Wapinzani hawatakuwa na pa kutokea tena.

Serikali inasema vyama vya siasa vikae pamoja kupitia kituo cha demokrasia kwa majadiliano.
Huu ni ulaghai wa hali ya juu sana. Kama vyama 5 vyenye uwakilishi bungeni havikuweza kukaa pamoja na kuwa na muafaka hatudhani genge la vyama 20 linaweza kuwa tofauti tena likiwa halina sheria za kuliongoza kama ilivyo kwa bunge.

Wapinzani hawaoni huu ni mtego wa kuweza kuleta vyama vya wenye njaa ili kuwepo na kuvurugana miongoni mwao tofauti na ushirika wao wa sasa. Huu ni Mkenge mwingine wameingia.

Kwanini kituo cha demokrasia kionekane kuwa na nguvu za kuleta umma pamoja zaidi ya bunge linalogharamiwa na lenye heshima kama mhimili wa nchi. white elephant !!! na ni mbinu za kuwapumbaza wapinzani.

Kwa muktadha huo duru za siasa tunaweza kusema swali la mkuu Mchambuzi kuhusu tija kwa safari ya wapinzani linajibika sasa kama ilivyokuwa hapo awali.

Hakuna tija bali ulaghai na wapinzani wameuza silaha kwa maneno matamu ya JK.
Miaka mingi JK anajulikana kwa double standard na kwamba ni mtu asiyeweza kuaminika, nashangaa bado wapinzani wanamwamini. Wanampa heshima anawajibu kwa ujanja wa kuwafanya majuha.

Hakuna njia bora kama waliyokuwa wanaitumia ya kushtaki kwa mahakama ya wananchi.
Kuachia nafasi hiyo ni kosa kubwa. Maandamano hayakupaswa kusita, ilitakiwa kuwepo na makubaliano kuwa mswada usisainiwe hadi mazungumzo yamalizike.

Wao wakakubali kichwa kichwa kumbe wanategewa tarehe yao ya maandamano JK anawapa salam kuwa ni majuha na hawamwezi. Akasini mkataba siku ile ile ya maandamano to prove them wrong and to show them the power vested to him.

Tatizo halijatatuliwa na wapinzani wakiamka na kubaini walichezewa shere sijui watarudi wapi maana wananchi hawajui nini kimeongelewa na hakuna anayewaambia.
Pengine tofauti na nyakati nyingine safari hii hawakunywa juisi hicho ndicho nakiona kama mafanikio.

Itaendelea.....
 
Last edited by a moderator:
Duh! Hatuna budi kujipa pole wanaTz! Lakini kwa aina ya siasa ambazo tumekubali kuwa nazo, HAKUNA JIPYA!

Werevu na wenye busara mlishatahadharisha, tukawasikia, sadly tulishakubali kushikishwa makali na wanasiasa! Hapa ndipo napoikubali na kuililia sana BOTTOM-UP APROACH, alikwisha isemea Mkuu Mchambuzi. Mkuu wangu Nguruvi3, tujipe pole tu, maana tunashuhudia namna sisi wenyewe tunavyowachimbia kaburi wajukuu wetu. INAUMA SANA!
Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
KWANINI MAKUBALIANO YA JK NA WAPINZANI NI GHILBA
Inaendelea....

Tumesema hakuna kipya katika mazungumzo kati ya Rais na wapinzani. Jipya ni mbinu za ulaghai zilizotumika.
Kusainiwa mswada siku ya maandamano ambayo iliahirishwa kama 'good gesture' ni kibao cha usoni kwa wapinzani.

Hii ni mara ya pili rais anaingilia mchakato wa katiba. Kwasas ndiye mwenye ufunguo wa kuandika katiba.
Tumeshasema Rais na serikali ni wadau wa katiba na wala si kuongoza mchakato. Leo hatujui hata mamlaka ya tume ya Warioba, kila kitu kinamalizwa Ikulu tunaambiwa katiba inayoandaliwa ni ya wananchi.

Haiwezekani serikali iandike mswada, ipeleke baraza la mawaziri halafu leo rais yule yule aliyeridhia mabadiliko aje na maoni tofauti ya maridhiano! hicho ni kiini macho,mwenyekiti wa baraza la mawaziri vipi hakuona kasoro hizo!

Katika kikao cha kwanza na wapinzani rais alisema kutakuwepo na mawasiliano ya mara kwa mara kuhusiana na mchakato.
Japo hilo ni kosa kwasababu ya kuuteka mchakato, ingekubalika kama yasingetokea haya ya sasa.
Kilichomlamlazimisha rais kukutana na wapinzani ni hofu ya maandamano wala si nia njema kama inavyosemwa.

Eti wameamua sheria irudi kufanyiwa marekebisho. Atakayepeleka sheria hiyo ni Wasira, Lukuvi na Chikawe na ndio wale wale walioleta matatizo tutegemee wataleta neema. wapinzani wamefanywa ndondocha! inasikitisha.
Wapinzani wajiulize kama rais ana nia njema mbona hakutani na tume ya Warioba iliyo na malalamiko kutafuta muafaka.

NINI USHAURI KWA WAPINZANI
1. Wakatae hoja ya kupeleka maoni kama vyama binafsi. Wapeleke maoni kama ushirika wa vyama hivyo ili kuondoa uwezekano wa kuwagawa ambalo ni lengo la kwanza la rais Kikwete.

2.Wagomee sheria kufanyiwa marekebisho na akina Wasira kama ishara ya kuonyesha kutoridhishwa na wasimamizi. Wasira, Lukuvi na Chikawe walipaswa wajiuzulu. Kwavile wametumwa hilo halitatokea,wapinzani wawakatae kwasababu, kwanza wamepeleka mswada uliotishia amani ya taifa na hawapaswi kuaminiwa tena na umma.
Pili, kumjibu rais kuwa kitendo cha 'kuwatukana'kwa kusaini mswada chini ya viongozi hao

3. Wapinzani wagome kutumia kituo cha demokrasia( TCD).Kituo kinatumika kama tawi la serikali . Haiwezekani kituo cha demokrasia kitambuliwa kati kati ya mchakato! kuna jambo hapo.Wingi wa vyama utaharibu mkakati vinginevya 'briefcase' vinanunulika kwa bei rahisi.

4. Wapinzani waendele kuuhabarisha umma kwa njia ya mikutano kila hatua. Mapendekezo yawekwe hadharani wananchi waone uhuni, ulaghai na ujahili wa serikali ya CCM katika kuwadhulumu haki yao ya kuandika sheria zinazowatawala

5. Wamwambie rais JK hawana imani naye. Vitendo vya kuwazunguka havionyeshi nia njema au utayari wa maridhiano.
Kusaini mswada siku ya maridhiano ni kuwadharau na kuwadhalilisha.

Leo akina Ndugai na wahafidhina wa CCM wanashangilia kwa rais kutia saini na kuridhia hoja zao itakayobandikwa jinala katiba ya wananchi. Rais kawafurahisha watu wake kwa kibao cha puani kwa wapinzani. Kawaita wamekwenda, kawapa furushi la mitego na kuwasukumia kibao cha usoni! wakaondoka kwa picha na basha sha.

Kilichotokea hakina tija kwa wapinzani, wamebabaishwa na wamekubali! Inasikitisha sana.
Jk na serikali yake wataendelea kuwacheza shere kila watakapowahitaji hadi katiba ya CCM itakapoandikwa kwa jina la wananchi.

Mchakato mzima ulikuwa na matatizo. Hakuna mahali katiba imeandikwa na serikali.
Serikali inaweka mazingira ya kuandika katiba na si kusimamia katiba.

Kibaya hapa kwetu hilo halikuwa wazo la kundi la watu, ni hoja ya wapianzani iliyotekwa nyara na mtu mmoja, Rais Kikwete, bila idhini ya chama chake na kutangaza kuanza mchakato.

Inawezekanaje rais aone sasa ni muda wa kuandika katiba na si wananchi?
Mwaka 2020 rais mwingine atakapokuja na wazo lake tutakataa kwa msingi upi?

Ni kutokana na kukiukwa kwa taratibu za kuandika katiba leo tupo hapa tulipo.
Wananchi wana hasira ingawa haisemwi, hatujui lini hasira hizo zitajitokeza juu.

Ni kwa msingi huo duru tunasema na kutahadharisha kuwa mchakato umeliweka taifa rehani.
Hali si njema wala si shwari. Mbele ya safari kuna dalili za machafuko!

Tusemezane
 
Duh! Hatuna budi kujipa pole wanaTz! Lakini kwa aina ya siasa ambazo tumekubali kuwa nazo, HAKUNA JIPYA!

Werevu na wenye busara mlishatahadharisha, tukawasikia, sadly tulishakubali kushikishwa makali na wanasiasa! Hapa ndipo napoikubali na kuililia sana BOTTOM-UP APROACH, alikwisha isemea Mkuu Mchambuzi.

Mkuu wangu Nguruvi3, tujipe pole tu, maana tunashuhudia namna sisi wenyewe tunavyowachimbia kaburi wajukuu wetu. INAUMA SANA
JingalaFalsafa Ni masikitiko kwa vizazi vyetu na sisi wenyewe huko mbeleni. Tunashindwa kusimamia utajiri, uchumi na sasa tumeshindwa kuweka sheria za kukosoa makosa ya nyuma.

Naukumbuka sana mjadala na Mchambuzi kuhusu Bottom up approach au top to bottom. Moja kati ya mambo tuliyokinzana ilikuwa ni bottom up. Mimi nilisema bottom up ndiko tunatakiwa tuelekeze nguvu. Mchambuzi akasema je tuna civil society za kutosha na zenye uwezo wa kuifanya hiyo bottom up?

Approach yangu ndio hiyo unayoisema na hadi leo nabaki kusema tunahitaji bottom up approach. Pamoja na hayo hoja ya mchambuzi kuwa je tuna civil society za kutosha kuibea bottom up approach imejidhihirisha mapema zaidi kuliko alivyosema. Ukweli ni kuwa thamani ya hoja yake tunaiona less than a year tangu aitoe! Nitafafanua

Endapo tungekuwa na civil society za nguvu mchakato huu pamoja na kutekwa bado ungeweza kurudi mikononi mwa wananchi. Tunachokiona ni kuvutana kwa vyama vya kisiasa kwa jambo ambalo hakika si la kisiasa.
Hili ni la societies, approach yake ingekuwa na nguvu sana kuliko ilivyo sasa.

Kitu ninachotaka kuumuliza Mchambuzi ni je, tumechelewa kuwa na hizo civil societies!
Na pili how do we build them tukijua ni civil na uwepo wake unatakiwa kuwa natural tunachohitaji ni ku nuture!

cc Mchambuzi
 
Last edited by a moderator:
Sawia kabisa Mkuu wangu Nguruvi3.
JingalaFalsafa Ni masikitiko kwa vizazi vyetu na sisi wenyewe huko mbeleni. Tunashindwa kusimamia utajiri, uchumi na sasa tumeshindwa kuweka sheria za kukosoa makosa ya nyuma.

Naukumbuka sana mjadala na Mchambuzi kuhusu Bottom up approach au top to bottom. Moja kati ya mambo tuliyokinzana ilikuwa ni bottom up. Mimi nilisema bottom up ndiko tunatakiwa tuelekeze nguvu. Mchambuzi akasema je tuna civil society za kutosha na zenye uwezo wa kuifanya hiyo bottom up?

Approach yangu ndio hiyo unayoisema na hadi leo nabaki kusema tunahitaji bottom up approach. Pamoja na hayo hoja ya mchambuzi kuwa je tuna civil society za kutosha kuibea bottom up approach imejidhihirisha mapema zaidi kuliko alivyosema. Ukweli ni kuwa thamani ya hoja yake tunaiona less than a year tangu aitoe! Nitafafanua

Endapo tungekuwa na civil society za nguvu mchakato huu pamoja na kutekwa bado ungeweza kurudi mikononi mwa wananchi. Tunachokiona ni kuvutana kwa vyama vya kisiasa kwa jambo ambalo hakika si la kisiasa.
Hili ni la societies, approach yake ingekuwa na nguvu sana kuliko ilivyo sasa.

Kitu ninachotaka kuumuliza Mchambuzi ni je, tumechelewa kuwa na hizo civil societies!
Na pili how do we build them tukijua ni civil na uwepo wake unatakiwa kuwa natural tunachohitaji ni ku nuture!

cc Mchambuzi

Jambo muhimu hapa ni kutambua suluhisho sahihi na kulipigania kwa nguvu zote! Kama suluhisho bora ni Bottom-up Aproach, lakini hatuna civil societies si kigezo cha kuikacha, ila ni kuzianzisha na kuzi-empower hizo civil societies kufikia namna tunavyotaka ziwe kukidhi haja ya mchakato!

Bottom-Up Aproach, mimi naamini hufanywa na civil societies ambazo ziko out of power enthronement movements, ni zile zinazopigania society welfare! Hawa wapiganiao Ikulu, hawawezi fanya chochote nje ya mbio zao za kuendelea kuwepo au kuingia Ikulu!

Pia ninaamini hizo societies zipo, ila tu zimekuwa tuned kucheza ngoma za wanasiasa, We have to Change them, and make them stand on their own! Hatuwezi sema zimeshindwa kwani hata ushiriki wao ulibebwa mno na wanasiasa! Hizi sizo tunazozitaka. Tunataka zile zinazojitambua katika kutekeleza wajibu wao katika kuleta ustawi wa Taifa.

Hatujachelewa wala kuwahi, TUPIGANIE KILICHO BORA WAKATI WOWOTE!
Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Afrika na ICC: Ubeberu wa Mataifa Makubwa na Uharamia wa Viongozi wetu[/B]


Na Ben Saanane[/B]

Mwishoni mwa wiki iliyopita Viongozi wa Nchi za Africa walikua Makao Makuu ya Umoja huo Mjini Addis Ababa nchini Ethiopia kujadili mpango wa kujiondoa katika mkataba wa Roma unaoongoza Mahakama ya kupambana na uhalifu wa kivita na makosa makubwa ya Jinai dhidi ya Ubinadamu duniani, ICC (International Criminal Court).

Hoja kuu ni kuwa mahakama hii inawalenga Viongozi kutoka Mataifa ya Afrika tu. Hii ni hoja yenye ukweli kwa kiasi Fulani, maana asilimia kubwa ya kesi zilizoko kwenye Mahakama hii kwa sasa ni kutoka Afrika huku rekodi zikionyesha hata Kesi nyingi za nyuma zilizowahi kushughulikiwa na Mahakama hiyo zinahusu Watuhuniwa kutoka Afrika zaidi.

Ukiacha sababu hizo lakini pia Viongozi wa Afrika nao wana ajenda yao juu hili azimio lao la kutaka kujitoa ICC, azimio ambalo halikupata uungwaji mkono wa kutosha katika Kikao hicho cha juzi japo kuliibuliwa azimio jipya mwishoni mwa kikao la kumtaka Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kutohudhuria Mahakamani wakati wa Kesi yake inayopangwa kusikilizwa mwezi ujao.

Nchi 34 kati ya 54 za Umoja wa Afrika zimesaini Mkataba wa Roma wa kukubali kuanzishwa kwa Mahakama hii. Wakati Viongozi wa Nchi hizo waliposaini haraka haraka mkataba wa ICC na kuziingiza nchi zao walidhani wanazuia mapinduzi dhidi yao kutoka kwa waasi, na walikwenda hatua mbele zaidi ya kujifanya kuwa hawatatambua matumizi ya mtutu katika kubadilisha utawala kwa njia ya kupindua serikali.

Hawakufikiria wala kutilia maanani kuwa ili kukomesha ‘mapinduzi ya kijeshi’ ni lazima kuimarisha utawala bora wa sheria bila kuminya demokrasia ili sauti huru zisikike na pia kujali zaidi maslahi ya wananchi wan chi hizo. Mapinduzi ya kijeshi Afrika yanachochewa kwa kiwango kikubwa na tawala kandamizi zilizominya uhuru wa maoni na kuzuia sauti za wananchi wenye mawazo kinzani pamoja na wanaharakati.

Jambo la kufurahisha ni kuwa wapo Viongozi zaidi ya 12 wa Nchi za Afrika waliopo Madarakani na ambao ni wanachama wa AU ambao waliingia madarakani kwa mtutu wa Bunduki na wengine wakisalia madarakani kwa kupora chaguzi. Kipindi wanapitisha azimio la kutotambua mapinduzi ya kijeshi idadi hii ilikua kubwa zaidi na hao hao walioingia madarakani kijeshi au kwa wizi wa kura ndiyo waliotangaza kutotambua mapinduzi hayo ya kijeshi.

Kwa mujibu wa Maandishi ya Vitabu vya Kitafiti kuhusu Mapinduzi ya Kijeshi katika Mchi za Kiafrika kama ‘Coup D’Etat’ cha Mwandishi Edward Luttwak na ‘Political Order In Changing’ kilichoandikwa na Samuel P.Huntngton, ilionekana kuwa pamoja na ushawishi kutoka mataifa ya nje lakini Upendeleo,Ufisadi na hali ngumu ya kiuchumi na kijamii ni mojawapo ya vichocheo vikubwa kwa mapinduzi ya kijeshi yaliyoikumba Afrika.

Kwa kipindi cha karibia miaka 60 tangu Nchi za Kiafrika zipate Uhuru, Afrika Imeshudia Mapinduzi ya Kijeshi zaidi ya 40 huku Nchi ya Nigeria ikiongoza kwa kukumbwa na Mapinduzi 10 ya kijeshi Kati ya mwaka 1966-1999 ikifuatiwa na Ghana iliyokumbwa na zaidi ya Mapinduzi 9 ya Kijeshi.

Kwa hiyo badala ya kufikiria namna ya kuondoa sababu na vichocheo vinavyochochea uwezekano wa Mapinduzi ya Kijeshi huko baadae, Viongozi wetu hawa wa Afrika waliamua kufumba macho na kuchagua njia waliyoiona ni rahisi zaidi kwa wakati huo bila kutazama athari zake kwao pia, yaani Mkataba wa Roma wenye kuasisi Mahakama ya ICC.

Kwa mfano suala la Uchaguzi kwa nchi za Afrika ni kichocheo kikubwa cha uvunjifu wa amani na mapinduzi kwa njia ya mtutu. Viongozi wa Afrika wanaogopana kuambiana ukweli au hawaheshimiani kwa kuwa tabia zao za ukiukaji wa sheria na kutowajali raia wao zinafanana. Labda tuangazie kwa kifupi tu nchini Kenya ambako ndipo chanzo cha hatua hizi za AU.

Wakati Mwai Kibaki, Uhuru Kenyatta na wanasiasa wengine wa kilichokuwa Chama Tawala cha Kenya cha PNU walipofanya udanganyifu kwenye uchaguzi wa Rais na wabunge nchini Kenya Mwaka 2007, hali iliyosababisha wapinzani kutoka chama cha ODM wakiongozwa na Willium Ruto na Raila Odinga kwa upande mwingine kuingia barabarani kupinga kuporwa uchaguzi huo na kusababisha mauaji ya watu zaidi ya 1000 na wengine zaidi ya 600,000 ya wasiokuwa na hatia kukosa makazi, Umoja wa Afrika, AU haukutangaza moja kwa moja kumchukulia hatua Mwai Kibaki na Watawala wengine.

Umoja huu haukutangaza kumtenga Mwai Kibaki na serikali yake na hata Rais Benjamin Mkapa wa Tanzania na Dk. Koffi Annan walipopelekwa kusuluhisha mgogoro huo walipata wakati mgumu kwa kuwa Kibaki alikuwa akiwadharau wote wawili kwa sababu ya rekodi zao za Ufisadi wakati wakiongoza Tanzania na Umoja wa Mataifa. Mkapa akituhumiwa kwa kufisadi mgodi wa Kiwira na Annan akitajwa kwa kashfa ya ‘Mafuta kwa chakula’ ya Iraq.

Wakati wote huo wa vurugu za Kenya waliokuwa wanapoteza maisha ni raia wanyonge tu kutoka maeneo mbalimbali wan chi hiyo. Sasa’ swali la kujiulia ni kuwa kuna haja gani ya kufanya uchaguzi ikiwa aliyeshinda uchaguzi anaporwa ushindi? Kuna tofauti gani kati ya Mapinduzi ya kijeshi (Coup d’tat) na wizi wa kura? Unapopora haki ya raia kuchagua,unapopora haki ya raia kutoa sauti. Hayo ni mapinduzi ya matakwa ya umma (coup D’Civillien). Hayo ni mapinduzi mapya baada ya Coup d’tat. Viongozi wa Afrika wamelibariki hilo.Unafiki ulioje?

Mara zote mapinduzi ya aina hii yasipofanikiwa kwa asilimia kubwa husababisha vita ya wenyewe kwa wenyewe.Tulishuhudia jaribio hili kule Cot de’Ivore. Laurent Gbagbo alishindwa uchaguzi na Mpinzani wake Allasaine Outtara, akaamua kufanya ‘Coup de’ civillien’.Afrika haikufua dafu,walitoa sauti za kinafiki kukemea na hali ilizidi kuwa mbaya na kuhatarisha amani kiasi kilichopelekea uwezekano wa kuzuka vita ya wenyewe kwa wenyewe hadi jumuiya ya kimataifa ikiongozwa na Mkoloni wa zamani wa nchi hiyo, Ufaransa walipoingilia kati na hatimaye Gbagbo akakamatwa akiwa amejificha kwa aibu. Leo anashtakiwa mbele ya mahakama ya ICC, Mahakama hii ndiyo ambayo Viongozi hawa wanataka kujitoa ili kujiepusha na haya yanayomkuta Gbagbo.

Kwa hiyo tunaona kwamba mjadala wa Viongozi wa AU na nia yao ya kujadili suala la kujiondoa ICC linalenga pia kuwalinda viongozi hawa ambao wengi wao wamekiuka haki za binadamu na pia kuua na kutesa wapinzani wao. Ni azimio la kikatili.

Mbona hawajitoi kwenye Shirika la Fedha Duniani (IMF), Benki ya Dunia (WB) na kwenye Shirika la Biashara Duniani (WTO)? Inatambulika kuwa Benki ya Dunia na Shirika la fedha Duniani ni nyenzo kuu za mabeberu zinazotumika kuzinyonya nchi zinazoendelea na hasa zile nchi zenye viongozi wasiofikiria mbele. Heri yao wananchi wa Venezuela waliojiondoa kutokana na ushupavu wa Rais wao Kamaradi Hugo Chavez.Vyombo hivi vya mabeberu (IMF, WB na WTO) ni hatari kwa Afrika na Ustawi wa wananchi wa Afrika kuliko Al-Qaeda na Al-Shaabab ambayo ni makundi hatari kwa Mabeberu, Vibaraka na maslahi yao popote pale duniani. Jambo kubwa la kinafiki kutoka kwa viongozi wetu hawa ni kuwa Viongozi wengi wa Afrika walioshitakiwa ICC walipelekwa huko na serikali za nchi zao ambazo viongozi wake walikusanyika huko mjini Addis Ababa kulalama kuwa ICC inawashtaki wao tu.

Serikali zilizopeleka kesi na watuhumiwa wenye asili ya kiafrika huko ‘The Hague’ ni pamoja Serikali za nchi za Jamhuri ya Afrika ya Kati, Cote d’Ivoire, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda. Kesi nyingine mbili za Darfur na ile ya Libya zilipelekwa mbele ya mahakama hiyo na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mamlaka yake zikiwa na sapoti ya wanachama wa baraza hilo kutoka barani Afrika.

Nilishawahi kusema baadhi ya viongozi wa Afrika ni ‘mambumbumbu’. Hata Makao Makuu mapya ya AU walipokaa kujadili hili la kujitoa ICC yamejengwa kwa Msaada wa ‘Beberu Mpya’ wa dunia, UCHINA, ambaye rekodi yake juu ya ukiukwaji wa haki za binaadam inajulikana namna ilivyo mbaya, zaidi sasa Nchi hiyo imekuwa bingwa wa kuzuia Demokrasia Duniani. Viongozi wa Afrika ni wabinafsi na hawawezi kuona mbele hadi hatari iwaguse wao binafsi. Hawajali maslahi ya nchi zao. Si wale Viongozi wa kaliba ya kina Kwame Nkrumah, Julius Nyerere, Nelson Mandela, Ahmed Sekou Toure, Thomas Sankara, Gamal Abdel Nasser, Patrice Lumumba. Viongozi tunaowaheshimu katika ujengaji wa hoja kwa maslahi ya nchi na bara la Afrika kwa vitendo tofauti na hawa madikteta waoga.

Viongozi wa sasa wa Afrika walipotia saini mkataba wa Roma walikuwa na akili zao timamu, waliona namna Marekani, China na Urusi ambao ni Wajumbe watatu muhimu wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa aidha walipokacha kusaini mkataba wote au hata kujiwekea sharia zao za ndani za kuzuia matumizi ya Mkataba huo wa Roma kwa raia wao. Leo wanalalamika na kuhoji uhalali wa wajumbe hao wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wasioikubali ICC kisheria kupitisha kukamatwa kwa Rais Omar Hassa Al-bashir wa Sudan kwa kadhia ya Darfur.

Makala hii inaendelea.....
 
Afrika na ICC: Ubeberu wa Mataifa Makubwa na Uharamia wa Viongozi wetu[/B]


Na Ben Saanane[/B]

Mwishoni mwa wiki iliyopita Viongozi wa Nchi za Africa walikua Makao Makuu ya Umoja huo Mjini Addis Ababa nchini Ethiopia kujadili mpango wa kujiondoa katika mkataba wa Roma unaoongoza Mahakama ya kupambana na uhalifu wa kivita na makosa makubwa ya Jinai dhidi ya Ubinadamu duniani, ICC (International Criminal Court).

Hoja kuu ni kuwa mahakama hii inawalenga Viongozi kutoka Mataifa ya Afrika tu. Hii ni hoja yenye ukweli kwa kiasi Fulani, maana asilimia kubwa ya kesi zilizoko kwenye Mahakama hii kwa sasa ni kutoka Afrika huku rekodi zikionyesha hata Kesi nyingi za nyuma zilizowahi kushughulikiwa na Mahakama hiyo zinahusu Watuhuniwa kutoka Afrika zaidi.

Ukiacha sababu hizo lakini pia Viongozi wa Afrika nao wana ajenda yao juu hili azimio lao la kutaka kujitoa ICC, azimio ambalo halikupata uungwaji mkono wa kutosha katika Kikao hicho cha juzi japo kuliibuliwa azimio jipya mwishoni mwa kikao la kumtaka Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kutohudhuria Mahakamani wakati wa Kesi yake inayopangwa kusikilizwa mwezi ujao.

Nchi 34 kati ya 54 za Umoja wa Afrika zimesaini Mkataba wa Roma wa kukubali kuanzishwa kwa Mahakama hii. Wakati Viongozi wa Nchi hizo waliposaini haraka haraka mkataba wa ICC na kuziingiza nchi zao walidhani wanazuia mapinduzi dhidi yao kutoka kwa waasi, na walikwenda hatua mbele zaidi ya kujifanya kuwa hawatatambua matumizi ya mtutu katika kubadilisha utawala kwa njia ya kupindua serikali.

Hawakufikiria wala kutilia maanani kuwa ili kukomesha ‘mapinduzi ya kijeshi' ni lazima kuimarisha utawala bora wa sheria bila kuminya demokrasia ili sauti huru zisikike na pia kujali zaidi maslahi ya wananchi wan chi hizo. Mapinduzi ya kijeshi Afrika yanachochewa kwa kiwango kikubwa na tawala kandamizi zilizominya uhuru wa maoni na kuzuia sauti za wananchi wenye mawazo kinzani pamoja na wanaharakati.

Jambo la kufurahisha ni kuwa wapo Viongozi zaidi ya 12 wa Nchi za Afrika waliopo Madarakani na ambao ni wanachama wa AU ambao waliingia madarakani kwa mtutu wa Bunduki na wengine wakisalia madarakani kwa kupora chaguzi. Kipindi wanapitisha azimio la kutotambua mapinduzi ya kijeshi idadi hii ilikua kubwa zaidi na hao hao walioingia madarakani kijeshi au kwa wizi wa kura ndiyo waliotangaza kutotambua mapinduzi hayo ya kijeshi.

Kwa mujibu wa Maandishi ya Vitabu vya Kitafiti kuhusu Mapinduzi ya Kijeshi katika Mchi za Kiafrika kama 'Coup D'Etat' cha Mwandishi Edward Luttwak na 'Political Order In Changing' kilichoandikwa na Samuel P.Huntngton, ilionekana kuwa pamoja na ushawishi kutoka mataifa ya nje lakini Upendeleo,Ufisadi na hali ngumu ya kiuchumi na kijamii ni mojawapo ya vichocheo vikubwa kwa mapinduzi ya kijeshi yaliyoikumba Afrika.

Kwa kipindi cha karibia miaka 60 tangu Nchi za Kiafrika zipate Uhuru, Afrika Imeshudia Mapinduzi ya Kijeshi zaidi ya 40 huku Nchi ya Nigeria ikiongoza kwa kukumbwa na Mapinduzi 10 ya kijeshi Kati ya mwaka 1966-1999 ikifuatiwa na Ghana iliyokumbwa na zaidi ya Mapinduzi 9 ya Kijeshi.

Kwa hiyo badala ya kufikiria namna ya kuondoa sababu na vichocheo vinavyochochea uwezekano wa Mapinduzi ya Kijeshi huko baadae, Viongozi wetu hawa wa Afrika waliamua kufumba macho na kuchagua njia waliyoiona ni rahisi zaidi kwa wakati huo bila kutazama athari zake kwao pia, yaani Mkataba wa Roma wenye kuasisi Mahakama ya ICC.

Kwa mfano suala la Uchaguzi kwa nchi za Afrika ni kichocheo kikubwa cha uvunjifu wa amani na mapinduzi kwa njia ya mtutu. Viongozi wa Afrika wanaogopana kuambiana ukweli au hawaheshimiani kwa kuwa tabia zao za ukiukaji wa sheria na kutowajali raia wao zinafanana. Labda tuangazie kwa kifupi tu nchini Kenya ambako ndipo chanzo cha hatua hizi za AU.

Wakati Mwai Kibaki, Uhuru Kenyatta na wanasiasa wengine wa kilichokuwa Chama Tawala cha Kenya cha PNU walipofanya udanganyifu kwenye uchaguzi wa Rais na wabunge nchini Kenya Mwaka 2007, hali iliyosababisha wapinzani kutoka chama cha ODM wakiongozwa na Willium Ruto na Raila Odinga kwa upande mwingine kuingia barabarani kupinga kuporwa uchaguzi huo na kusababisha mauaji ya watu zaidi ya 1000 na wengine zaidi ya 600,000 ya wasiokuwa na hatia kukosa makazi, Umoja wa Afrika, AU haukutangaza moja kwa moja kumchukulia hatua Mwai Kibaki na Watawala wengine.

Umoja huu haukutangaza kumtenga Mwai Kibaki na serikali yake na hata Rais Benjamin Mkapa wa Tanzania na Dk. Koffi Annan walipopelekwa kusuluhisha mgogoro huo walipata wakati mgumu kwa kuwa Kibaki alikuwa akiwadharau wote wawili kwa sababu ya rekodi zao za Ufisadi wakati wakiongoza Tanzania na Umoja wa Mataifa. Mkapa akituhumiwa kwa kufisadi mgodi wa Kiwira na Annan akitajwa kwa kashfa ya ‘Mafuta kwa chakula' ya Iraq.

Wakati wote huo wa vurugu za Kenya waliokuwa wanapoteza maisha ni raia wanyonge tu kutoka maeneo mbalimbali wan chi hiyo. Sasa' swali la kujiulia ni kuwa kuna haja gani ya kufanya uchaguzi ikiwa aliyeshinda uchaguzi anaporwa ushindi? Kuna tofauti gani kati ya Mapinduzi ya kijeshi (Coup d'tat) na wizi wa kura? Unapopora haki ya raia kuchagua,unapopora haki ya raia kutoa sauti. Hayo ni mapinduzi ya matakwa ya umma (coup D'Civillien). Hayo ni mapinduzi mapya baada ya Coup d'tat. Viongozi wa Afrika wamelibariki hilo.Unafiki ulioje?

Mara zote mapinduzi ya aina hii yasipofanikiwa kwa asilimia kubwa husababisha vita ya wenyewe kwa wenyewe.Tulishuhudia jaribio hili kule Cot de'Ivore. Laurent Gbagbo alishindwa uchaguzi na Mpinzani wake Allasaine Outtara, akaamua kufanya ‘Coup de' civillien'.Afrika haikufua dafu,walitoa sauti za kinafiki kukemea na hali ilizidi kuwa mbaya na kuhatarisha amani kiasi kilichopelekea uwezekano wa kuzuka vita ya wenyewe kwa wenyewe hadi jumuiya ya kimataifa ikiongozwa na Mkoloni wa zamani wa nchi hiyo, Ufaransa walipoingilia kati na hatimaye Gbagbo akakamatwa akiwa amejificha kwa aibu. Leo anashtakiwa mbele ya mahakama ya ICC, Mahakama hii ndiyo ambayo Viongozi hawa wanataka kujitoa ili kujiepusha na haya yanayomkuta Gbagbo.

Kwa hiyo tunaona kwamba mjadala wa Viongozi wa AU na nia yao ya kujadili suala la kujiondoa ICC linalenga pia kuwalinda viongozi hawa ambao wengi wao wamekiuka haki za binadamu na pia kuua na kutesa wapinzani wao. Ni azimio la kikatili.

Mbona hawajitoi kwenye Shirika la Fedha Duniani (IMF), Benki ya Dunia (WB) na kwenye Shirika la Biashara Duniani (WTO)? Inatambulika kuwa Benki ya Dunia na Shirika la fedha Duniani ni nyenzo kuu za mabeberu zinazotumika kuzinyonya nchi zinazoendelea na hasa zile nchi zenye viongozi wasiofikiria mbele. Heri yao wananchi wa Venezuela waliojiondoa kutokana na ushupavu wa Rais wao Kamaradi Hugo Chavez.Vyombo hivi vya mabeberu (IMF, WB na WTO) ni hatari kwa Afrika na Ustawi wa wananchi wa Afrika kuliko Al-Qaeda na Al-Shaabab ambayo ni makundi hatari kwa Mabeberu, Vibaraka na maslahi yao popote pale duniani. Jambo kubwa la kinafiki kutoka kwa viongozi wetu hawa ni kuwa Viongozi wengi wa Afrika walioshitakiwa ICC walipelekwa huko na serikali za nchi zao ambazo viongozi wake walikusanyika huko mjini Addis Ababa kulalama kuwa ICC inawashtaki wao tu.

Serikali zilizopeleka kesi na watuhumiwa wenye asili ya kiafrika huko ‘The Hague' ni pamoja Serikali za nchi za Jamhuri ya Afrika ya Kati, Cote d'Ivoire, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda. Kesi nyingine mbili za Darfur na ile ya Libya zilipelekwa mbele ya mahakama hiyo na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mamlaka yake zikiwa na sapoti ya wanachama wa baraza hilo kutoka barani Afrika.

Nilishawahi kusema baadhi ya viongozi wa Afrika ni ‘mambumbumbu'. Hata Makao Makuu mapya ya AU walipokaa kujadili hili la kujitoa ICC yamejengwa kwa Msaada wa ‘Beberu Mpya' wa dunia, UCHINA, ambaye rekodi yake juu ya ukiukwaji wa haki za binaadam inajulikana namna ilivyo mbaya, zaidi sasa Nchi hiyo imekuwa bingwa wa kuzuia Demokrasia Duniani. Viongozi wa Afrika ni wabinafsi na hawawezi kuona mbele hadi hatari iwaguse wao binafsi. Hawajali maslahi ya nchi zao. Si wale Viongozi wa kaliba ya kina Kwame Nkrumah, Julius Nyerere, Nelson Mandela, Ahmed Sekou Toure, Thomas Sankara, Gamal Abdel Nasser, Patrice Lumumba. Viongozi tunaowaheshimu katika ujengaji wa hoja kwa maslahi ya nchi na bara la Afrika kwa vitendo tofauti na hawa madikteta waoga.

Viongozi wa sasa wa Afrika walipotia saini mkataba wa Roma walikuwa na akili zao timamu, waliona namna Marekani, China na Urusi ambao ni Wajumbe watatu muhimu wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa aidha walipokacha kusaini mkataba wote au hata kujiwekea sharia zao za ndani za kuzuia matumizi ya Mkataba huo wa Roma kwa raia wao. Leo wanalalamika na kuhoji uhalali wa wajumbe hao wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wasioikubali ICC kisheria kupitisha kukamatwa kwa Rais Omar Hassa Al-bashir wa Sudan kwa kadhia ya Darfur.

Makala hii inaendelea.....
Excellent ! nasubiri umalizie!
 
Excellent ! nasubiri umalizie!

Kwa mujibu wa Mtandao wa Vyombo vya Usalama vya Marekani,Mei 6, 2002 Utawala wa Rais George Bush wa Marekani ulimtaarifu rasmi Katibu Mkuu wa umoja wa mataaifa juu ya Uamuzi wa Taifa la Marekani kujitoa katika mkataba huo. Kulingana na matamshi ya aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani wakati huo Donald Rumsfeld alisema kulikua na uwezekano wa baadhi ya maofisa wa Marekani wakiwemo maofisa wa jeshi la nchi hiyo kushtakiwa na mahakama hiyo na pia Marekani haikubaliani na baadhi ya vipengele vinavyoinyima Marekani kutekeleza wajibu wake hasa katika kipindi ambacho taifa hilo lilikuwa linakabiliana na vita dhidi ya ugaidi.

Marekani walidhamiria kulinda maslahi yao na mwanya wa kuendelea kupelea majeshi yao popote duniani pale wanapoona maslahi yao yapo hatarini. Hapa viongozi wa Afrika hawakushtuka na pia tangu muda huo walibweteka na hawakufikiria namna bora na mbadala wa kujiandaa kitaasisi ili kuwa na chombo chao cha kimahakama chenye hadhi, imani na uwezo wa kushughulikia masuala kama ICC ili kuepuka matatizo kama haya wanayoyajadili leo hii. Kwao waliona busara na ufahari kuwaomba CHINA kuwajengea jengo la kifahari la makao makuu ya Umoja huo badala ya kufikiria ujenzi wa mahakama na taasisi zenye hadhi na uwezo wa kushughulikia matatizo yetu

Kuna kila dalili kuwa Mabeberu wanaitumia ICC kwa maslahi yao. Lakini pia kupitia udhaifu wa viongozi wa Afrika kutoheshimu mifumo ya kutoa haki kama mfumo wa kimahakama, mataifa haya ya kibeberu yanapata mwanya wa kujenga hoja kuwa Afrika haina mfumo thabiti wa kushughulikia kesi bila kulindana(Impunity).

Kwa mfano,Viongozi wa Kenya walitoa taswira hii pale walipoamua kupeleka kesi ya Uhuru na Ruto wenyewe huko ICC. Kipindi hicho Uhuru na Ruto hawakuwa Marais. Viongozi wa Umoja wa Afrika walikaa kimya kwasababu hawa hawakuwa marais wenzao. Nilikerwa sana lakini wao hawakukerwa. Fedheha ya Afrika. Leo wanasema mahakama ya Afrika inalenga Viongozi wa Afrika? Hoja hii itaonekana nyepesi kwa kuzingatia mazingira niliyoyaainisha.

Inatambulika kuwa Haki za Binadamu ni kanuni ya msingi kwenye Mkataba wa umoja wa Africa (AU Chatter) na imepewa uzito katika mkataba huo maarufu kama ‘Banjul Charter . Kwa hiyo jitihada zozote za kutaka kujiondoa au hata hili la kujadili kama Marais wa Afrika waliopo madarakani wasishtakiwe mbele ya mahakama ya kimataifa ya ICC kupitia Umoja wa Afrika (AU) itatuma ujumbe mzito na mbaya juu ya dhamira ya dhati ya viongozi na umoja huo katika kulinda haki za binadamu na kukataa utamaduni wa kulindana (culture of impunity) ambazo ni tunu na nguzo kuu katika madhumuni ya Uanzishwaji na uwepo wa Umoja huu.

Hii ni ajenda iliyojaa hila na ubinafsi kwa viongozi dhidi ya raia wa bara hili. Naungana na msimamo wa mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel, Askofu Desmund Tutu wa Afrika Kusini kuwa Nigeria na Afrika Kusini zikiwa kama mataifa yenye nguvu na ushawishi ndani ya umoja huu ziongoze katika mjadala kuzuia azimio hilo lenye sura mbaya na aibu kwa bara hili. Wito ambao pia umetolewa naye Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Dk. Koffi Annan.

Kama viongozi wa Afrika wanaona uchungu kweli basi waimarishe taasisi zetu na hasa mfumo wa Mahakama ambazo mara nyingi viongozi wa Afrika wamekuwa wakizitumia kuwaadhibu wapinzani wao. Mahakama hizi haziheshimiwi na hazipo huru kiasi cha kubeba matumaini na imani kwamba zitatenda haki. Hii ndiyo sababu kuu kwamba hata baada ya uchaguzi na inapotokea utata wa udanganyifu wa kura wapinzani wanaamua kuingia barabarani kudai haki kuliko kwenda mbele ya mahakama hizi ambazo zinaoneka kutumika kama mkono mwingine wa watawala kunyonga haki

Waafrika ni lazima tusimame imara na kujenga misingi ya kitaasisi. Hakuna wa kulitetea bara la Afrika zaidi ya Waafrika wenyewe na ili tupate mafanikio ni lazima tuachane na kasumba chafu ya kutegemea suluhisho la matatizo yetu kutoka nje ya bara la Afrika. Hatuwezi kuingiza suluhisho la matatizo yetu kutoka nje kama tunavyoagiza bidhaa kutoka nje kwa ajili ya kutatua matatizo tuliyojitengenezea wenyewe. Tuache kutegemea Mataifa makubwa ya kibeberu maana maumivu ya Afrika ni nafuu ya mataifa hayo ya Kibeberu.

ICC ina changamoto kama lilivyo Baraza la Usalama la umoja wa Mataifa .Baraza hili la kudumu nalo lina changamoto ambazo tumekua tukizipigia kelele hasa juu ya upanuzi wa wigo wa kidemokrasia na utendaji wake unaozingatia maslahi ya wachache na hivyo kubeba ajenda za mataifa yenye nguvu kuaamua juu ya masuala mazito ya dunia. Amani ya dunia imewekwa rehani kwa mataifa haya matano tu.

Kwa hiyo ICC inatakiwa pia iangalie uhalifu uliofanyika Iraq, Afghanistan, Palestina na Lebanon. Ukweli ni kuwa ‘Silaha za Maangamizi' za Iraq ya Saddam Hussein hadi leo hii hazijawahi kuonekana kama ilivyonenwa na Wavamizi wa Nchi hiyo, lakini Bush na Blair walioendesha vita yenye uharibifu mkubwa kwa madai ya kumnyang'anya Saddam Hussein silaha za maangamizi wapo huru mtaani tu.

Ukweli ni kuwa tunaishi katika mazingira yaliyojaa laana ya uhalifu dhidi ya binadamu uliofanyika pia sehemu nyingine duniani kama vile Iraq, Lebanon, Libya na Palestina uliofanywa na unaondelea kufanywa na Israel, Marekani, Uingereza, Ufaransa na Washirika wao wa Umoja wa kujihami wa nchi za Magharibi na Marekani (NATO) ambao haukuvuta hisia na dhamira ya kiutendaji ya ICC pamoja na kuwa uhalifu huo pengine ni mkubwa na wa kutisha zaidi kuliko kesi zilizofanyiwa na zinazoendelea kufanyiwa uchunguzi za Afrika Kwa hiyo Viongozi wa Afrika kutumia sababu hii ya madai ya kuachwa kwa uhalifu mwengine duniani iwe ni kwa lengo la kutaka ‘hatua zichukuliwe kwa kila upande' na si kwa lengo la kupinga hatua kuchukuliwa kwao kwa udhalimu wao kwa raia wao kama alivyokuwa akidai Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn wakati wa Kikao cha juzi. Hailemariam amekwenda mbali zaidi kwa kuongeza sababu nyingine ya ubaguzi wa rangi (Racism) kuwa ni miongoni mwa vigezo ambavyo ICC inatumia ili kuwashughulikia zaidi Viongozi wa Kiafrika huku wakisahau kuwa Mwendesha mashtaka Mkuu wa Mahakama hiyo, Fatou Bensouda ni Mwafrika Mwenzao kutoka Gambia ikiwa pamoja na uwepo wa baadhi ya Majaji wa Mahakama hiyo ambao ni Waafrika.

Kama nilivyosema hapo awali ni jambo la kawaida kwa Viongozi wa Afrika kutumia mfumo wa mahakama zetu dhaifu kuendekeza utawala dhalimu, jambo linalopelekea kuoza zaidi kwa mfumo mzima wa mahakama. Kwa vyovyote vile hadi ninapoandika makala hii, wanaharakati na hata vyama vya upinzani haviwezi kupeleka visa vya uchaguzi au madai yao ya msingi kwenye mahakama hizi zinazolinda watawala na badala yake siku zote mahakama kuu kwao ni zile "Mahakama za Umma" ambazo ni tishio kwa watawala.

Kwa hiyo linapotokea jambo kama hili la "Mahakama za Umma" mara moja watawala hawasiti kutumia majeshi na hata silaha za kivita kuzima maandamano na mikutano itakayotishia utawala wao dhalimu na hivyo kupelekea mauaji ya kutisha kwa raia wasiokuwa na hatia wanaodai haki zao za msingi. Hapa ndipo mahakama ya Kimataifa ya ICC inapowakamata viongozi dhalimu wa Kiafrika na kuwashikisha adabu bila kujali kama Bush na Tony Blair wamewajibishwa kwa makosa yao ama la.

*Mwandishi ni Mhitimu wa Shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,na pia shahada ya Uzamili katika Uchumi. unaweza kuwasiliana naye kupitia barua pepe; saananeben@gmail.com au +255768078523

NB:Makala hii imechapishwa Katika Gazeti la SURA YA MTANZANIA,Pia Baadhi ya Vyombo vya Habari vya Kenya Vimeomba kuichapisha Makala hii
 
Ben Saanane
Ahsante sana kwa bandiko lenye kina na vina lililosheheni fikra.
Ni mara chache viongozi wa Afrika kushikamana katika masuala ya pamoja. Utashangaa mgawanyiko uliopo kuhusu Mugabe na Zimbabwe, DRC, Sudan n.k. lakini kwa hili la ICC wote wanaonekana kushikamana.

Kitu kimoja knachokuja akilini ni kuwa kama mtu anatenda jema na kwa wema kwanini aogope mahakama?
Jibu lipo katika bandiko lako kuwa wengi wapo madarakani kwa njia zisizo halali na wanalindwa na vyombo vya umma kwa njia zisizo halali na wanatenda uhalifu. Hofu kuu ndipo ilipo.

Yapo mengi nitayarejelea kutoka katika bandiko lako.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu Nguruvi3, JingalaFalsafa,

Naomba mniwie radhi kwa kupotea kidogo kutokana na majukumu ya hapa na pale, lakini napenda niwahakikishie kwamba pamoja na haya, bado nimekuwa nafuatilia sana mijadala ya humu kwenye duru za siasa; Ningependa kujadili kidogo suala la 'role of civil society' katika kufanikisha mageuzi ya kweli kidemokrasia, kupitia muktadha wa mchakato wa katiba mpya; Ningependa zaidi kujadili kwanza changamoto zilizopo kwa nchi yetu kufanikisha hilo:

Uwepo wa a strong civil society katika taifa lolote lile huitaji uwepo wa 'associational life', kitu ambacho kwa Tanzania kipo very weak ikifananishwa na nchi nyingi za Afrika; Moja ya sababu kubwa juu ya weakness hii ni demographic characteristics za nchi yetu ambapo sisi ni taifa kubwa (land mass & population) lakini wananchi walio wengi wanaishi pembezoni (in the periphery) mwa nchi, huku wachache wakiwa kwenye centre na maeneo mengine machache, hasa yale yenye ardhi yenye rutuba; Ni kwa maana hii, Tanzania ni nchi ya mwisho katika nchi tano za Jumuiya ya Afrika mashariki (EAC) in terms of population density, ambapo hata rwanda na burundi wametupita; kwa maana hii, associational life katika mataifa ya kenya, uganda, rwanda, burundi, ni more significant, hivyo kuwaweka katika nafasi bora zaidi yetu kuwa na a stronger civil society kuliko Tanzania;

Kutokana na hali hii, pamoja na wananchi wengi kuwa vijijini na pia uwepo wa rapid urbanization nchini kwetu (tanzania), tofauti na nchi tajwa hapo juu, kwetu Tanzania, organized efforts ni ngumu sana kufanikisha on a large scale - kwa maana nyingine, ni watanzania wachache sana ambao wanaweza kufanikiwa to engage in a collective action kwa nia ya ku-promote/defend a certain idea/cause (mfano, kudai mabadiliko ya kweli from the bottom - up);

Suala lingine ni kwamba, Tanzania has a weak social capital ambayo by definition (see wikipedia), ni - the expected collective or economic benefits derived from the preferential treatment and cooperation between individuals and groups;Hii weakness (nchini kwetu) inatokana na ukweli kwamba, tofauti na miaka y anyuma (enzi za mwalimu), lack of trust among Tanzanians imejengeka sana, kutokana na ukosefu wa rule of law, patrimonial relations zinazozengwa na viongozi wa chama tawala, ukosefu wa mfumo rasmi wa kuwaongoza wananchi to progress kimaisha (badala yake kufanikiwa ni bahati bahati na ujanja ujanja tu kuliko formula inayoeleweka), jamii kujaa utapeli, ufisadi n.k; Katika mazingira kama hayaa, ni rahisi sana kwa watanzania kugeukana, kuchongeana, kusemeana, hasa iwapo fedha zinatumika kuwanunua na umaskini wao kufanikisha mambo hata yasioyokuwa na tija kwa maisha ya wananchi wenyewe; Liberalization kwa bahati mbaya haijasaidia kujenga 'strong associational life', badala yake imejenga individualism, hivyo kufanya things kuwa even worse; Mfumo wa sasa wa maisha uliojengwa na CCM (kwa makusudi au bahati mbaya), unafanania na ule uliojengeka nchini itali in the 1950s, i.e "Amoral Faminism", na CCM imekuwa inafaidika nao sana to creep democratization, lakini hasa, to determine the process in a 'top-down' fashion;

Mwisho ni kwamba, serikali ya CCM imekuwa ikiweka juhudi kubwa kukwamishia efforts za watu kujenga strong independent organizations na hata NGOs ambazo ni muhimu katika kuchochea mabadiliko ya kweli katika taifa; Any organized efforts zinazolenga to develop collective action zinakuwa closely monitored na vyombo vya ulinzi na usalama; Vile vile serikali imekuwa makini sana katika kuhakikisha kwamba independent organisations (non partisan) zenye mvuto kwa wananchi wengi, mfano autonomous baraza la wanawake na baraza la vijana, hazifanikiwi kuanzishwa nchini;

Pengine paltform iliyobakia kusaidia ujenzi wa a strong civil society ni vyombo vya habari, lakini navyo, kama tunavyoona kila siku, magazeti yanabanwa na sheria ya 1976, huku Television ikipunguzwa kasi na new legislation ya digital migration; Radio inabakia kuwa platform pekee katika hili ingawa nayo ipo closely monitored in terms of content;

Nitarejea kwa mengine zaidi;
 
mkuu Nguruvi3, Mchambuzi kwanza nianze kwa kumba samahan kwa kutoonekana hapa jukwaaani kwa muda mrefu. Naomba mniwie radhi sana kwa hili.

Napenda sana kuwashukuru kwa mda pevu zilizojaa fikra na hekima za hali ya juu, lkn pia napenda zaid kumshukuru Ben Saanane kwa bandiko lake zuri sana juu ya ICC.

mie leo nimekuja hapa nikiwa na mawazo ambayo ni from anecdote tuu na wala siyo kwamba nina reference ya makala fulan.

Mie nimejiuliza maswali mengi sana kutoka na makala zetu na moja ya swala ambalo ambalo mimi binafsi nimeona linanitatiza ni hali ya EAC ilivyo kwa sasa. Nikimnukuu Nguruvi3 juu ya rais wetu kuwa na double standard na nikinukuu pia alivyo tueleza juu ya Dr sezibera hapa napata akili kuchanganyikiwa kabisa.

ninaona jinsi ambavyo kwa rais kutokuwa na msimamo ndio matokeo ya hiki tunachokipata leo hii kwenye EAC. mimi nimefikiri kwamba mbona Tanzania kama taifa huru lina fursa na lina uwezo wa kijismamia lenyewe?? kwann tukae tusubiri watu kama Sezibera wajr kutuamulia??

Nimepata bahati ya kumili kaduka mshenzi huko kkoo, nilichogundua ni kwamba wateja wetu wengi ni wa congo, warundi, wakenya, na waganda. hawa ni watu ambao hutununuza kuliko hata wenyeji kutokana na hili nikaona kumbe basi sisi kama nchi tunaweza kusimama peke yetu na kuimarisha fursa tulizo nazo na tukafanya biashara vizuri tu?? sasa kama ndivyo kwann tunang'ang'ania kukaa EAC??

Sikatai shirikisho ni jema sana na bora sana kama wote mlioko kwenye shirikisho mnania mamoja na wala si kupelekeshwa pelekeshwa kama punda.. sasa kwa hali ilivyo naona kwamba sisi tunapelekeshwa tuu na kwa upole wa rais wetu hakuna anachokisema na mpaka sasa sisi tunaonekana ni wakaidi kwenye EAC.

sijui ni kwann lkn nafikiri zaid ya fursa zeetu hakuna kitu ambacho wenzetu kwenye shirikisho wanakipenda kutoka kwetu, wanana kabisa Tanzania kuna fursa za kibiahsara, kilimo na uwekezaji na wao wanaona huu ndio mtaji ambao sisi tunaingia nao ndo mana wakaanza mara tutumie tu vitambulisho vya uraia na wala sio pasporti ninakasirika sana manake naona kama vile sie tunaumia ila hatusemi...

nafikiri ukweli tujiangalie kwa upya na kama bado tunaona kwamba hatunasababu za kuwa kwenye hii EAC basi tujiondoe kwanza kisha tujipange upya.

fikiria nchi yetu inatumia gharaa kiasi gani kwaajili ya wizara ya AFRIKA MASHARIKI na kumbe hata kwenye mikutan yao sisi hatupo zaid ya kulaumiwa na kutukanwa, hebu tuache michezo ya kitoto tufikiri kwa umakini kwamba tunahitaj kufanya kitu. sion faida yyte ya wizara hi manake kwenye jumuiya yenyewe sisi ni kama hatupo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom