Cannabis
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 8,943
- 25,284
Wakuu hii nawaletea baada ya dogo fulani kunitafuta huku amefura analalamika ameingia kwenye biashara ya kudownload pesa na kampuni fulani inaitwa 360 Capital na kushindwa kutoa pesa zake. Nikazama kwenye mitandao ya kijamii na kuitafuta kiundani maana jina lake ni kama niliwahi kulisikia.
Katika pita pita zangu nikaiona ni Kampuni iliyoanzishwa na kijana wa kitanzania mpambanaji na mtafutaji almaarufu kama jina fulani la mji fulani huko Canada, wakongwe wa humu mtakuwa mmeshamjua.
Sasa nikazama zaidi kwenye page zao za instagram na twitter na kukuta malalamiko ya wa wadau wengine kuwa wanashindwa kutoa hela (withdrawal) kwa uelewa wangu mdogo wa forex ni kama wameingiza hela na kufanya trading sasa faida waliyoipata haitoki...na wengine wanasema akaunti zao zilizokuwa verified zimeondolewa hiyo status.
Hapo nikaishia kucheka tu na kumwambia dogo hiyo hela yake afanye kuachana nayo, labda kama kuna technical issues tu za kiungwana baadaye anaweza kuipata, ila kwa historia ya huyu mtafutaji kuna uwezekano mkubwa imeshaondoka.
Nimeweka baadhi ya screenshot za wadau hapo chini , natoa tu angalizo hii si kwa ajili ya kuchafua biashara ya mdau yoyote bali ni kutoa tahadhari, huyu dogo nilimuonya kuhusu kufanya hizo biashara kama hana uelewa wa kutosha akanivimbia nikamuacha afanye kitu roho inataka, pia natoa angalizo kwa wabongo kama mnaanzisha biashara mtandaoni basi jitahidini kuweka technical issues sawa, kama mambo yakienda vibaya hakuna mfumo utakaofanya kazi at 100% siku zote basi mijitahidi kutoa mawasiliano na kujibu wateja wenu kwa haraka, kukaa kimya huku watu wanashindwa kupata huduma kunatengeneza picha kwamba wamepiga, bado naendelea kufuatilia maendeleo ya hii kitu, kama kuna wadau mnajua kinachoendelea njooni huku mtujulishe, mjini kuna mambo mengi na muda ni mchache
Katika pita pita zangu nikaiona ni Kampuni iliyoanzishwa na kijana wa kitanzania mpambanaji na mtafutaji almaarufu kama jina fulani la mji fulani huko Canada, wakongwe wa humu mtakuwa mmeshamjua.
Sasa nikazama zaidi kwenye page zao za instagram na twitter na kukuta malalamiko ya wa wadau wengine kuwa wanashindwa kutoa hela (withdrawal) kwa uelewa wangu mdogo wa forex ni kama wameingiza hela na kufanya trading sasa faida waliyoipata haitoki...na wengine wanasema akaunti zao zilizokuwa verified zimeondolewa hiyo status.
Hapo nikaishia kucheka tu na kumwambia dogo hiyo hela yake afanye kuachana nayo, labda kama kuna technical issues tu za kiungwana baadaye anaweza kuipata, ila kwa historia ya huyu mtafutaji kuna uwezekano mkubwa imeshaondoka.
Nimeweka baadhi ya screenshot za wadau hapo chini , natoa tu angalizo hii si kwa ajili ya kuchafua biashara ya mdau yoyote bali ni kutoa tahadhari, huyu dogo nilimuonya kuhusu kufanya hizo biashara kama hana uelewa wa kutosha akanivimbia nikamuacha afanye kitu roho inataka, pia natoa angalizo kwa wabongo kama mnaanzisha biashara mtandaoni basi jitahidini kuweka technical issues sawa, kama mambo yakienda vibaya hakuna mfumo utakaofanya kazi at 100% siku zote basi mijitahidi kutoa mawasiliano na kujibu wateja wenu kwa haraka, kukaa kimya huku watu wanashindwa kupata huduma kunatengeneza picha kwamba wamepiga, bado naendelea kufuatilia maendeleo ya hii kitu, kama kuna wadau mnajua kinachoendelea njooni huku mtujulishe, mjini kuna mambo mengi na muda ni mchache