Kuna uwezekano Aubin Kramo hajui kuwa jina lake limeondolewa kwenye wachezaji wa Simba

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,129
7,897
Pamoja na mapenzi kwa timu yangu, ila mara kwa mara sijasita kuja na malalamiko dhidi ya uongozi wa Simba na moja ya maeneo yanayokera wengi yanahusiana na treatment ya wachezaji wake kuanzia wale walio bora hadi wale ambao wanaonekana mchango wao umepungua mno na wanaigharimu timu. Imefika wakati unashangaa wachezaji walio bora wanapewa huduma mbovu ndani ya timu hadi kuachwa katika mazingira ya kutatanisha, halafu wale ambao viwango vyao vinatia mashaka ndiyo tunaaminishwa ndiyo tegemeo la timu.

Juzi nilikuwa naangalia video moja wakati Simba inakwenda Zanzibar, ukimsiklliza interview ya Aubin Kramo haupati picha kama ni mtu aliye na taarifa kuwa si tena sehemu ya kikosi cha Simba msimu huu. Ukimsikiliza Ahmed Ally anasema jina la Kramo liliondolewa ila anaendelea kulipwa stahiki zake zote. Kama kuna mtu anabisha, mtu ajitokeze amuulize swali hili moja kwa moja Kramo mwenyewe kama anajua kuwa jina lake limeondolewa. Kama anasema anajua natoa 100,000 kwa mwandishi yoyote atakayepewa jibu hilo. Kwa mtazamo wangu Kramo alishapona ila kuna watu wamemkazia ili kulinda wachezaji wao. Majeraha ya Kramo hayakuwa ya kumkalisha nje muda mrefu kiasi hiki.

Huyu ni mchezaji mwingine ambaye msimu ukiisha ataachwa katika mazingira ya kutatanisha halafu ukamkuta upande wa pili anakiwasha. Hii ni story inayojirudia ya Moses Phiri, tulikuwa tunaambiwa hajapona hajapona, mara amepona ila ni maamuzi ya mwalimu kumtumia, mwisho wa siku mchezaji mwenyewe anaona huu ni upuuzi anaonyesha dalili za kutojali maana hata juhudi zake bado hazimpi namba tena, mara anakuja kuachwa. Kuna tatizo kubwa sehemu pale Simba ila hatutaki kulisema.

Kwa kumalizia, kwenye dirisha dogo lililopita kuna mchezaji mwenye sifa ya kuikaba timu ambaye mkataba wake ulikuwa umeisha kulingana na taarifa walizokuwa wametupa hapo kabla ila dirisha dogo likafungwa hatukuambiwa kama ameongezewa mkataba na usishangae mwakani tena tukawa naye huku kina Kramo wakiachwa.
 
Simba inaonekana viongozi Wana wachezaji wao, hata Kakolanya alifanywa kipa wa tatu makusudi ili aondoke.
Wanachama wanaochagua hao viongozi hawana uchungu na timu kabisa.
Kuna shida kubwa sana. Unaweza kusema ni hujuma inafanyika maana haileti mantiki kung'ang'ania mchezaji ambaye kila siku anaigharimu timu na kila mtu anaona halafu yule anayeonekana anaibeba au anaweza kuja kuibeba unampiga vita au unamuacha.
 
Kwa madai yako ni kwamba hata Kramo mwenyewe ameshiriki kwenye mchakato wa kuwa mchezaji hewa pale Simba.

Maana yake umesema alipona kitambo.

Kwasababu hata yeye alikiri kuwa ni majeruhi na akaushukuru uongozi kwa careness iliyompa.

Lakini kingine umenishangaza hapo ulipoandika kuwa inawezekana hata yeye mwenyewe hajui.

Yani kumbe inawezekana swala la majeraha muhusika mwenyewe asiweze kujua kama anaumwa au la mpaka pale atakapo ambiwa na mwingine?

Hivi kwa akili tu ya kawaida, viongozi walimuogopa nani mpaka wafikie uamuzi huo wa kumficha Kramo asicheze kwa visingizio vya majeraha?

Wamfiche kisha waendelee kumlipa mshahara ambao haufanyii kazi.

Kwanini usifikirie swala la Kramo kama sehemu ya uongozi kupewa pongezi kurekebisha makosa yao waliyofanya kwa Dilunga?

Mi nadhani point ya Ahmed Ally kuhusu Kramo kuondolewa hukuielewa vyema.

Kumbuka Simba ilimpa Kramo mkataba wa miaka 2 hapo msimu jana.

Na mind you jamaa alipata majeraha awamu mbili. Awamu ya kwanza ali spend almost Miezi miwili.

Aliporejea akakutana na buyu lingine tena mechi ya kirafiki nukumbuka alifunga na goli hakumaliza hata dakika 45 za kipindi cha kwanza.

Baada ya majeraha hayo ya awamu ya pili yalimchukua muda kupona.

Kulingana na sheria za TFF zinataka wachezaji foreigners wasizidi 12. Na kwa wakati huo nadhani idadi ilikuwa imetimia ukimjumuisha na Kramo.

Wakati wa dirisha dogo Simba ilihitaji kupata wachezaji wengine kwa ajili ya kuongeza nguvu ndio hapo walipoangalia muda wa Kramo ku recovery majeraha na kuona itamchukua muda kupona.

Wakamtoa kwenye mfumo wa usajili wa CAF na TFF ili waweze kupata wachezaji wengine katika kipindi ambacho ataendelea ku recovery.

Kwa hiyo mkataba bado upo ila hawezi kucheza kwasababu aliondolewa kwenye usajili mpaka dirisha kubwa la usajili litapoanza.
 
Kwa madai yako ni kwamba hata Kramo mwenyewe ameshiriki kwenye mchakato wa kuwa mchezaji hewa pale Simba.

Maana yake umesema alipona kitambo.

Kwasababu hata yeye alikiri kuwa ni majeruhi na akaushukuru uongozi kwa careness iliyompa.

Lakini kingine umenishangaza hapo ulipoandika kuwa inawezekana hata yeye mwenyewe hajui.

Yani kumbe inawezekana swala la majeraha muhusika mwenyewe asiweze kujua kama anaumwa au la mpaka pale atakapo ambiwa na mwingine?

Hivi kwa akili tu ya kawaida, viongozi walimuogopa nani mpaka wafikie uamuzi huo wa kumficha Kramo asicheze kwa visingizio vya majeraha?

Wamfiche kisha waendelee kumlipa mshahara ambao haufanyii kazi.

Kwanini usifikirie swala la Kramo kama sehemu ya uongozi kupewa pongezi kurekebisha makosa yao waliyofanya kwa Dilunga?

Mi nadhani point ya Ahmed Ally kuhusu Kramo kuondolewa hukuielewa vyema.

Kumbuka Simba ilimpa Kramo mkataba wa miaka 2 hapo msimu jana.

Na mind you jamaa alipata majeraha awamu mbili. Awamu ya kwanza ali spend almost Miezi miwili.

Aliporejea akakutana na buyu lingine tena mechi ya kirafiki nukumbuka alifunga na goli hakumaliza hata dakika 45 za kipindi cha kwanza.

Baada ya majeraha hayo ya awamu ya pili yalimchukua muda kupona.

Kulingana na sheria za TFF zinataka wachezaji foreigners wasizidi 12. Na kwa wakati huo nadhani idadi ilikuwa imetimia ukimjumuisha na Kramo.

Wakati wa dirisha dogo Simba ilihitaji kupata wachezaji wengine kwa ajili ya kuongeza nguvu ndio hapo walipoangalia muda wa Kramo ku recovery majeraha na kuona itamchukua muda kupona.

Wakamtoa kwenye mfumo wa usajili wa CAF na TFF ili waweze kupata wachezaji wengine katika kipindi ambacho ataendelea ku recovery.

Kwa hiyo mkataba bado upo ila hawezi kucheza kwasababu aliondolewa kwenye usajili mpaka dirisha kubwa la usajili litapoanza.
Sidhani kama kuna sehemu nimesema Kramo hajui kama anaumwa au amepona.
Nimesema hajui kama jina lake limeondolewa kwenye orodha ya wachezaji wa Simba walio hai katika mashindano.

Wengi mpaka dakika hii wanaamini Kramo yupo kwenye usajili wa CAF hata mchangiaji hapo juu anaamini hivyo, wewe unaamini hivyo pia?
 
Sidhani kama kuna sehemu nimesema Kramo hajui kama anaumwa au amepona.
Nimesema hajui kama jina lake limeondolewa kwenye orodha ya wachezaji wa Simba walio hai katika mashindano.

Wengi mpaka dakika hii wanaamini Kramo yupo kwenye usajili wa CAF hata mchangiaji hapo juu anaamini hivyo, wewe unaamini hivyo pia?
Kufuatia ulichoandika kuwa viongozi wanafanya udanganyifu kuonesha Kramo ni mgonjwa angali alipona mapema.

Ndio sababu inayofanya uonekane kuwa umemaanisha kuwa hata Kramo mwenyewe inawezekana hajui kuwa anaumwa na kufanya yeye na viongozi wote lao liwe moja.

Ungesoma vizuri post yangu basi paragraph yako ya pili usingeiandika.
 
Simba inaonekana viongozi Wana wachezaji wao, hata Kakolanya alifanywa kipa wa tatu makusudi ili aondoke.
Wanachama wanaochagua hao viongozi hawana uchungu na timu kabisa.
Kakolanya inadaiwa Mkataba wake ulikuwa upo mwishoni wakati tunamalizia mechi za mwisho za CAF Club bingwa.

Navyosikia Simba wakamuita mezani kumuongezea Mkataba lakini kumbe alikuwa tayari kasaini Mkataba wa awali na Singida ambao ulikuwa na thamani mara mbili ya ule aliokuwa amesaini Simba.

So kuanzia pale ndio Simba ikabidi imchukue Ally Salim na kuanza kumuandaa kama mbadala kwasababu walijua hakuna room ya negotiations ambayo ingeweza kufanyika kumnusuru Kakolanya asiondoke.
 
Ni kweli hayupo sababu wachezaji wa kigeni ni 12 tu wanaruhusiwa kucheza na kusajiliwa.
Ayubu,Chemalone,Inonga,Babacar,Ngoma,Kanute,Saido,Chama,Onana,Saido,Paomar,Fred,Luis.Hee mbona wamezidi
Saido umeandika mara mbili

1.Ayoub
2.Enonga
3. Che Malone
4. Ngoma
5 Kanoute
6. Babacar
7. Pa Omary
8. Onana
9. Saido
10. Chama
11. Fred
12. Luis
 
Kufuatia ulichoandika kuwa viongozi wanafanya udanganyifu kuonesha Kramo ni mgonjwa angali alipona mapema.

Ndio sababu inayofanya uonekane kuwa umemaanisha kuwa hata Kramo mwenyewe inawezekana hajui kuwa anaumwa na kufanya yeye na viongozi wote lao liwe moja.

Ungesoma vizuri post yangu basi paragraph yako ya pili usingeiandika.
Kichwa cha habari kinatosha kusema kile ninachotaka kusema na nimekuwa direct sana kwenye ujumbe wangu bila kupindisha maneno. Sikuacha mwanya wa mtu kupata maana tofauti au zaidi ya kile nilichoandika kama ulivyofanya wewe.

Mchezaji anaweza kusema yuko tayari na amepona lakini akaambiwa aendelee kufanya recovery. Hivi Kramo amefanyiwa matibabu yake lini? Wewe unaamini bado hajapona? Achana na sasa, unaamini wakati wa dirisha dogo alikuwa hajapona?

Najua hautaki kuyasikia haya hasa kipindi hiki kuelekea mechi ngumu ila jiandae kisaikolojia. Kuna ukweli wa kinachoendelea pale na kila mtu anauona ila watu wanaogopa kuongea ili wasionekane kama kina Mchome.

Turudi kwenye swali kuu la mada hii, Kramo anajua kuwa jina lake liliondolewa katika mashindano yote?
 
Kichwa cha habari kinatosha kusema kile ninachotaka kusema na nimekuwa direct sana kwenye ujumbe wangu bila kupindisha maneno. Sikuacha mwanya wa mtu kupata maana tofauti au zaidi ya kile nilichoandika kama ulivyofanya wewe.

Mchezaji anaweza kusema yuko tayari na amepona lakini akaambiwa aendelee kufanya recovery. Hivi Kramo amefanyiwa matibabu yake lini? Wewe unaamini bado hajapona? Achana na sasa, unaamini wakati wa dirisha dogo alikuwa hajapona?

Najua hautaki kuyasikia haya hasa kipindi hiki kuelekea mechi ngumu ila jiandae kisaikolojia. Kuna ukweli wa kinachoendelea pale na kila mtu anauona ila watu wanaogopa kuongea ili wasionekane kama kina Mchome.

Turudi kwenye swali kuu la mada hii, Kramo anajua kuwa jina lake liliondolewa katika mashindano yote?
Kramo aliondolewa Jina kwenye NBC ila caf champions league Jina lipo, Maana caf hakuna idadi ya wachezaji wa kigeni. Tulishakua na Junior Lokosa pia miaka kama 3 ilopita alikua kasajiliwa caf ila hachezi ligi kuu
 
Barbakar
Saidoo
Fredi
Luis
Kamati ya Usajiri wa Simba iwaondoe dilisha kubwa.

Ni wachezaji wastaafu kwa sasa.
Aikili inataka kucheza mwili unakataa.
Hao Tandika wako wengi tu wa kucheza Bonanza.
Chasambi anawazidi mala elfu
 
Pamoja na mapenzi kwa timu yangu, ila mara kwa mara sijasita kuja na malalamiko dhidi ya uongozi wa Simba na moja ya maeneo yanayokera wengi yanahusiana na treatment ya wachezaji wake kuanzia wale walio bora hadi wale ambao wanaonekana mchango wao umepungua mno na wanaigharimu timu. Imefika wakati unashangaa wachezaji walio bora wanapewa huduma mbovu ndani ya timu hadi kuachwa katika mazingira ya kutatanisha, halafu wale ambao viwango vyao vinatia mashaka ndiyo tunaaminishwa ndiyo tegemeo la timu.

Juzi nilikuwa naangalia video moja wakati Simba inakwenda Zanzibar, ukimsiklliza interview ya Aubin Kramo haupati picha kama ni mtu aliye na taarifa kuwa si tena sehemu ya kikosi cha Simba msimu huu. Ukimsikiliza Ahmed Ally anasema jina la Kramo liliondolewa ila anaendelea kulipwa stahiki zake zote. Kama kuna mtu anabisha, mtu ajitokeze amuulize swali hili moja kwa moja Kramo mwenyewe kama anajua kuwa jina lake limeondolewa. Kama anasema anajua natoa 100,000 kwa mwandishi yoyote atakayepewa jibu hilo. Kwa mtazamo wangu Kramo alishapona ila kuna watu wamemkazia ili kulinda wachezaji wao. Majeraha ya Kramo hayakuwa ya kumkalisha nje muda mrefu kiasi hiki.

Huyu ni mchezaji mwingine ambaye msimu ukiisha ataachwa katika mazingira ya kutatanisha halafu ukamkuta upande wa pili anakiwasha. Hii ni story inayojirudia ya Moses Phiri, tulikuwa tunaambiwa hajapona hajapona, mara amepona ila ni maamuzi ya mwalimu kumtumia, mwisho wa siku mchezaji mwenyewe anaona huu ni upuuzi anaonyesha dalili za kutojali maana hata juhudi zake bado hazimpi namba tena, mara anakuja kuachwa. Kuna tatizo kubwa sehemu pale Simba ila hatutaki kulisema.

Kwa kumalizia, kwenye dirisha dogo lililopita kuna mchezaji mwenye sifa ya kuikaba timu ambaye mkataba wake ulikuwa umeisha kulingana na taarifa walizokuwa wametupa hapo kabla ila dirisha dogo likafungwa hatukuambiwa kama ameongezewa mkataba na usishangae mwakani tena tukawa naye huku kina Kramo wakiachwa.
Asante shabiki unayejitambua. Juzi kuna Mtu kakurupuka kaweka Uzi wake humu akiwa hajui haya yote. Pale Simba pale! Kuna shida si kidogo. Kuna michongo na mitikasi mpaka Wachezaji wanajiona hawafai wanajiondoa. Nachelea kusema hata issue ya Ulevi inawezekana ilitokana na kunyimwa 10%. Sina shida Mangungu maana na yeye ni ceremonial figure. Tatizo la Simba linaanzia Kwa Jaribu Tena. Huyu usipomnyenyekea uwanjani utapasikia tu. Naongea Kwa ushahidi nilionao Kwa issue ya Kakolanya alipoumia Manula. Saidoo mtaendelea kuwa naye mwakani labda muitishe Uchaguzi upya mwaka huu.
 
Back
Top Bottom