Duru : Utangamano, Amani na Ustawi. Taifa linaelekea wapi?

Duru : Utangamano, Amani na Ustawi. Taifa linaelekea wapi?

Nguruvi3

Platinum Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
16,301
Reaction score
33,751
Ustawi
Taifa lolote linalotazama Ustawi na maendeleo yake huzingatia utangamano na Amani.

Utangamano '(compatibility ) ni uwepo wa pamoja(coexist) licha ya tofauti za Raia katika rangi, Imani, itikadi za siasa na Utamaduni. Amani ni utulivu unaoletwa na uwepo wa maridhiano na haki.
Amani si Ukimya unaoletwa na shinikizo (subdue)

Katika miezi michache kuna hali, matukio na kauli zinazoacha swali, Tanzania kama Taifa, je, tuna utangamano na Amani ! Taifa linaelekea wapi katika hali ya mivutano na mishuano iliyopo!

Ni kawaida kwa 'shughuli za tasnia au fani fulani kuwa na lugha zake.
Mfano, utani wa Simba na Yanga una lugha zenye karaha kwa asiye elewa lugha ya mpira.

Utani katika siasa kama kuitana nyumbu au zero brain ni wa kawaida nchini.

Pamoja na hayo utani wa simba na Yanga una mipaka yake. Mwisho wa siku Watani hukaa pamoja na kula, hujumuika kuuguzana, na hushirikiana kuzikana. Ni utani wa mpira usiohusisha ubinadamu

Siasa za vyama vingi hazijawahi kusimama bila matatizo, lakini, matatizo yaliyojitokeza yalishughulikiwa na viongozi. Ni ukweli usio na shaka kwamba kuanzia 2020 siasa zetu zimebadilika kwa ubaya!

Tulimsikia kiongozi mmoja ambaye sasa ni RC akitamka '' Wapinzani wapigwe risasi''
Hivi katibuni tukasikia kiongozi mwingine akisema '' Wapinzani wakipotezwa'' polisi wasiwatafute
Kiongozi mwingine akisema ' Wapo Watanzania wanaodhamiria kubeba vidudu vya maradhi.. ''

Tumesikia gari la kiongozi likichomwa moto , wafuasi wa vyama wakirushiana makonde n.k.
Tumesikia watu kutekwa, kupotezwa n.k. katika mazingira yanayoashiria siasa.

Katika hali ya kujengeka chuki na kauli za kichochezi zikihamasisha uhasama, tulitegemea sheria zichukue mkondo kwa wahusikam kwasababu sheria ndio msingi wa HAKI inayoleta Amani.

Hata hivyo, vyombo husika katika kusimamia na kutoa HAKI ima vimefumbia macho au KUWA NA makengeza kwasababu za kisiasa kwa masilahi ya viongozi wa kisiasa na si Taifa kwa upana wake

Hali ni mbaya , makundi ya jamii yanaingia katika mivutano yakiwemo ya Dini bila kutaraji

Viongozi wamejikita kutumia nguvu na vyombo vya Dola kutafuta 'Ukimya'' na si Amani.
Viongozi wanahubiri uwepo wa Amani wakijua fika hilo ni Tunda la HAKI isiyokuwepo

Ni katika mivutano iliyopo vyombo vya Dola vilivyonyooshewa vidole kwa muda mrefu kuhusu matukio mabaya ya utekaji, mauaji na dhulma vimejikuta ''viki watoa shaka kwa ushahidi '' waliohisi vinahusika

Kwa mwendo huu, Taifa linaelekea wapi?

Inaendelea
 
Sheria gani imevunjwa?
Jeshi la Polisi limepata wapi mamlaka ya kisheria kuadhibu Wananchi!
Ya Mabwepande na Coco Beach yanaliweka jeshi katika nafasi gani!


Kwa miezi kadhaa vyama vya siasa vimendelea na shughuli za mikutano ya hadhara bila tatizo.
Amani ilitamalaki na kila awaye alitenda aliyokusdia.
Hoja iliyozua sintofahamu ni kauli ya ''no reforms no election' ya CHADEMA. inayosemwa ni uchochezi

Kwa taratibu za nchi, ni Mahakama yenye mamlaka ya kutafsiri si sheria tu bali hoja zinazohitaji matumizi ya sheria.Hakuna aliyekwenda Mahakamani kuhusu ''no reforms no election''

Tukio la Kukamatwa viongozi wa Upinzani limeletwa taswira hisia tofauti.
Mwenyekiti Tundu Lissu (TAL) amefikishwa Mahakamani, Makamu wake alikamatwa kwa kufanya mkutano Kariakoo. Zipo taarifa barua ya kuitaarifu Polisi ilipelekwa mapema kabla ya tukio
Polisi walimkamata wakiwa na Barua ya majibu.

Mahakama ni chombo chenye sheria na kanuni zake, kiukwaji wake hujibiwa kwa adhabu papo hapo.
Mahakama ni eneo huru kwa wote, wanaotuhumu na Wanaotuhumiwa.
Usikilizaji wa kesi ni suala la wazi isipokuwa kwa mashauri yaliyoanishwa kwasababu maalumu.
Kesi ya TAL si moja ya shauri maalumu. Miaka ya 1980 tulisikiliza kesi za Uhani hadharani

Polisi wamezuia Wananchi kusikiliza kesi ya TAL. Mahakama haijalalamika ukiukwaji wa sheria au taratibu kutokana na ''wingi'' wa wasikilizaji. Swali, Polisi wanasheria gani za kuzuia Wananchi?

Kilichofuata siku ya kesi ni madai ya Wanachama wa CHADEMA kupigwa na kutupwa Mabwepande, wengine Coco Beach. Picha mitandaoni (hazijakanushwa) ni za Wanachama kuumizwa.
Hadi sasa hakuna Mwanachama aliyefikishwa Mahakamani miongoni mwao.

Swali, ni sheria gani ilivunjwa kukusanyika Mahakamani. Ni sheria gani inayowapa Polisi haki ya ''kuadhibu'' watuhumiwa na si kuwakamata kwa mujibu wa sheria.

Kwanini wliachwa Mabwepande na Coco Beach? Kuna ujumbe gani unatumwa!

Tukio la kukamatwa Makamu Mwenyekiti pale Kariakoo lili isha kwa kuachiwa bila kufunguliwa mashtaka. Swali, ni sheria gani inayozuia mikutano katika maeneo kama Kariakoo?
Makamu alivunja sheria gani iliyomnyima ''uhuru' akiwa chini ya Polisi bila kufikishwa mahakamani?

Matukio hayo mawili yanaonyesha kinachoitwa linaloitwa ''extrajudicial''.
Kwamba Jeshi la Polisi linavunja sheria. Kumvunja mtu mifupa ni uhalifu kama uhalifu mwingine.

Pili, kushindwa kuwafikisha wahusika Mahakamani ni kuwanyima haki ya kikatiba ya kupata sheria.

Tatu, matukio mabaya yaliyopita yalihusisha maeneo ya Coco Beach na Mabwepande.
Kwa haya yanayoendelea, wenye shaka na uhusika wa Polisi, watakuwa wamekosea wapi?
Kuna utetezi gani kuhusu yaliyopita !!! viongozi wa serikali wapo katika nafasi gani ! na jamii inawatazama kwa mboni ipi!

Tunarejea, AMANI ni Tunda la HAKI. Haki inapatikana kupitia sheria . Sheria hazibagu1.
'' Utii wa sheria bila shuruti'' si kwa Wananchi bali wasimamizi pia.

Kunapotokea ukiukwaji wa sheria, HAKI inapotea na zao lake ambalo ni AMANI linatoweka.

Kama Taifa, tunaelekea wapi?

Inaendelea
 
Viongozi wa Dini
Wanasiasa na kauli ya '' Dini na Siasa''


Chimbuko la siasa za Dunia ni Imani (Dini) . Mitume na Manabii waliofika Duniani kwa nyakati tofauti walikuta Imani zimeshatengeneza mifumo ya Tawala (siasa), nao walipita katika tawala za siasa, Dini ikiwa sehemu yake

Kauli za Wanasiasa wa Tanzania za kutochanganya Dini na siasa zinashangaza. Mifumo ya siasa imetengenezwa kwa taswira ya Dini. Lakini pia Dini na siasa zinakutana katika maisha ya Wanadamu.

Lengo la Dini ni kuhuisha nyoyo za Wanadamu kuabudu, kutenda mema na kukataza mabaya
Mengine kama ujenzi wa shule, Hospitali n.k ni kufanya kazi ya Ibada itoe matokeo mazuri na ya haraka.

Tatizo la Wanasiasa Nchini ni kuchagua(cherry picking), wakati gani Dini ni sehemu ya siasa au la.
Dhana hii ni potofu imelenga ubinafsi zaidi. Shughuli za Serikali zimewahusisha viongozi wa Dini.

Bunge linaanza vikao kwa Dua za kumuomba Mungu si Wanasiasa.
Tumeona Viongozi wa Dini wakishirikishwa katika maombezi ya Taifa, iwe mvua au Amani.

Kunapokuwa na mmomonyoko wa Maadili, kama ongezeko la Vibaka, makahaba n.k. Viongozi wa Dini huombwa kusaidia katika kufundisha na kusimamia maadili mema.

Tatizo linaanza hapa !
Mathalan, ongezeko la Vibaka linahitaji Viongozi wa Dini kufundisha Maadili kwa Vijana wasiumizwe au kufungwa Magereza. Wanasiasa wata andaa mazingira mazuri ya kazi hiyo.

Hata hivyo, wanapoiba wenye suti na Tai maofisini kama inavyoonyesha ripoti ya CAG suala la Maadili na Imani vinawekwa pembeni. Viongozi wa Dini wanaokemea wizi wa Kalamu wanaambiwa wasichanganye Dini na Siasa!

Kasema Askofu mmoja, kwamba, Dini zinapojenga Shule , Hospitali na Vituo vya Mayatima, wanaokwenda kufungua maeneo hayo ni Wanasiasa. Hakuna kuchanganya Dini na Siasa hapo.

Viongozi wa Dini wanaombwa kusambaza na kuhamasiaha neno la ''kujiandisha na kupiga kura'' kwa Waumi wao . Viongozi wa Dini wanapokemea wizi wa kura wanaambiwa wasichanganye Dini na Siasa!

Majuzi, Viongozi wa Dini wamezungumzia HAKI wakieleza mifumo ya Utawala ya Katiba na mifumo ya Uchaguzi isivyo na mizania. Kauli yao ilisimama suala la Haki , maadili na kutenda mema kama Dini zinavyofundisha. Wanasiasa wakaja juu wakisema ''Viongozi wasichanganye Dini na Sias''

Mabaraza ya Dini kama ya Idd, Paska, Chrismas, Maulidi n.k. waalikwa ni Wanasiasa.
Wakiwa huko wanaomba Dini zisaidie Serikali katika mambo ya Maadili, ujenzi wa Shule na Hospitali. Viongozi wa Dini wanapokekeme utovu wa maadili Serikalini kama wizi wa kalamu, hilo ni kuchanganya dini na Siasa.

Kwanini kukemea kukiukwa HAKI isiwe kazi ya Dini? Kwanini kukemea wizi wa Kura lisiwe suala la Maadili?
Tofauti ya mwizi wa Simu na Mwizi wa kura kimaadili ni ipi!

Hatari ya jambo hili ni pale Wanasiasa wanapotumia Dini kama vichaka vya kuwagawa Raia.

Kuna hoja mbona kiongozi akiwa hivi inakuwa hivi.
Huu ushindani hauna afya kwa Taifa, ni kwa masilahi ya Viongozi wa Siasa.

Wanasiasa hutegemea kunufaika zaidi panapotokea migawanyo ya Dini bila kujali madhara yake.
Lakini, hali inapoharibika, Wanasiasa hao huita Viongozi wa Dini waliombee Taifa, si kwasababu wanalipenda Taifa ni kwasababu wana hofu, yakiharibika hawatakuwa na nafasi ya kujinafsi ! Hapo hakuna kuchanganya Dini na Siasa

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
Matukio yanaashiria nini?
Wiki 'ngumu' kwa Jeshi la Polisi


Mabandiko yaliyopita tulieleza kuumizwa kwa Wana CHADEMA, kunakodaiwa kulifanywa na Jeshi la Polisi. Kamanda-Kanda Maalumu Dar , amekanusha kuumizwa kwa Wanachama au jeshi kushiriki.

Katibu Mkuu wa CHADEMA aliitisha mkutano akiwa na Video zinazoonyesha Watu wakipigwa na uwepo wa Polisi, hakuna aliyekanusha 'Video' hizo, si polisi au kwingine.

Maelezo ya Kamanda ''tukio halikutokea'' ! Maelezo ya Walioumizwa na Video tukio limetokea likihusisha Polisi. Wananchi wamemsikia Kamanda kama walivyowasikiliza watuhumiwa na wameona video

Tukio 2
Mabinti wa Chuo Kikuu wamekamatwa kwa tuhuma za shambulio ''kugombea' Mtu mmoja maarufu na Mume wa Mtu. Hatutaongelea suala lililo ''mahakamani''

Kinachoeleta mvuto ni jinsi '' Mtu maarufu anapokamatwa'' kwa kugombewa na Mabinti.
Je, suala hilo lilipaswa kupewa uzito na Jeshi la Polisi kama ilivyotokea?

Kugombewa na Wapenzi ni kosa gani kisheria?
Sheria gani inayolipa Jeshi la Polisi nguvu ya kukamata '' Wachepukaji'' katika ndoa!

Tukio 3
Ni kushambuliwa kwa Fr Katima, Katibu mkuu (TEC)Maaskofu Tanzania, siku chache baada ya kutoa kauli kuhusu mambo yanayoligusa Taifa kwa niaba ya TEC. Mitandaoni , Kitima alishambuliwa na meseji zinazofikirishwa zinazozunguka mitandaoni ikiwemo JF.
Jeshi la Polisi, kwa ''haraka sana'' limemkamata mtu mmoja akihusishwa na shambulio

Uchunguzi wa tukio unaweza kuchukua muda mrefu, suala litakuwa mahakamani na halitaongelewa. Tusubiri vyombo vya Dola vifanye kazi yake! Ni uchunguzi mgumu unaotakiwa kubaini wahusika, dhamira na msukumo . Ni shauri litakalochukua miaka kadhaa kama ilivyokuwa lile la Bomu la CHADEMA Arusha, na lile lililomhusisha Mwanamalundi lililotokea Dar es Salaam.

Tofauti na matukio ya kisiasa, hili lina ''sensitivity'' kwasababu linahusisha kiongozi wa Dini. Linahusisha mazingira yaliyopo nchini ! linahusisha maadili na Haki! linahusisha masuala ya kiroho

Kuna habari mitandaoni kwamba mhusika ni Mwanachama wa CHADEMA kindaki ndaki.
Hiabari hizi za hatari si za kufumbiwa macho na Wanaozizua.

Kwamba, Mwanachama wa Chama cha Siasa akifanya uhalifu, uhalifu wake unahusishwa na Chama!!

Ipo siku Mwanachama wa ACT atajifungua na kutupa kichanga. Tukio hilo litahusishwa na ACT Wazalendo kufanya mauaji ya vichanga.
Ipo siku majambazi yenye kofia za CCM yatafanya ujambazi, na hilo litahusishwa na CCM

Kuhusisha matukio ya uhalifu na vyama ni jambo la hatari sana kuliko uhalifu wenyewe.
Ni jambo linaloweza kusambaa katika jamii kama moto wa nyika, likiunguza kila kilichomo!

Tukio 3
Ni kupotea kwa Mwanaharakati wa CHADEMA Mikoa ya nyanda za juu. Mke wake anasema wazi, waliomchukua ni Polisi. Polisi wanakana kumshilia bila kufanya mahojiano na Mke huyo kama sehemu ya uchunguzi. Je, si haki Mke wa Mwanaharakati huyo kusikilizwa akiwa sehemu ya uchunguzi?

Katika tukio hilo amejitokeza Raia aliye eleza namna Polisi wanavyomtafuta Mwanaharakati huyo siku mbili zilizopita. Raia ametaja majina ya Polisi waliomshawishi awasaidie kumpata Mwanaharakati.

Je, Polisi hawaoni Raia huyo kuwa mtu muhimu katika uchunguzi?
Je, hawaoni umuhimu wa kuwahoji waliotajwa kwavile wanahusishwa na Jeshi la Polisi!

Maoni ya Wananchi na mazungumzo yanabaisnisha kwamba Raia wana elimu na ufahamu mkubwa wa kuelewa mazingira yao. Si rahisi kupewa habari na kuzimeza bila kuzichakata.

Wiki hii imekuwa ngumu kwa Jeshi la Polisi, kwasababu si tu linaonekana kupoteza '' Trust'' lakini pia ''Integrity' yake ipo katika hali ngumu. Kuna suala la ''credibility'' nalo ni tata

''Trust, integrity, credibility'' ni maneno yanayofanana kimtazamo lakini yenye maana tofauti. Tutafafanua

Swali la kujiuliza, kama Taifa tunaelekea wapi?
 
'' Trust, Integrity, Credibility ''
Jeshi la Polisi lanyooshewa kidole tena
Polisi warudia makosa yale yale ya kujichunguza


Hapa chini kuna link ya hotuba ya Mzee Jaji Warioba katika kongamano la TLS

View: https://www.youtube.com/watch?v=OCLDXl-xRkE

Kabla ya kujadili hotuba ya Jaji, tupitie maneno matatu yenye maana zinazofafana lakini ni tofauti kwa mantiki. Trust ( kwa tafsiri isiyo rasmi ni aminika, au kuaminika ) Mtu mwenye ''trust' ni anayeweza kuchukua dhamana ya jambo fulani.

Integrity ( Uaminifu/uadilifu), kwa maana ya kuaminika katika uadilifu.
Halafu kuna credible '' sadiki, sadifu) kwa maana ya jambo lenye sadifu

Mtu anapokuwa na trust, anakuwa na integrity na anachosema kinakuwa credible.

Katika link, Mzee Warioba amehoji Jeshi la Polisi kwa mambo kadhaa. Moja, kwanini walikamata Watu waliokwenda Mahakamani kwa amani na wengine kama Heche kukamatwa hata kabla ya kufika.

Jaji anauliza kwanini hawakufunguliwa mashtaka zaidi ya kuzungushwa na magari kisha kuachwa.
Mzee Warioba akasema wapo waliotupwa Mabwepande, halafu jeshi limekanusha !

Jaji Warioba akasema Polisi wanatumika kisiasa. Lakini kubwa zaidi ni pale alipohoji '' halafu wanataka waaminiwe'' kwa maana ya kwamba habari zao zinakinzana , hazina ithbati kulingana na vitendo.

Kwa maneno mengine , Mzee alihoji, trust ya Jeshi, integrity katika utendaji na credibility.
Hili ni jambo zito kutoka kinywani mwa mstaafu Waziri Mkuu, Mwanasheria mkuu , waziri wa sheria.

Jeshi la Polisi limesema linafanyia kazi tuhuma za Raia kushirikishwa na Askari katika ''ujasusi' dhidi ya Mwanaharakati ailiyetekwa. Jeshi la Polisi limeunda kikosi kazi.

Kwamba tuhuma zinaelekezwa kwa Polisi halafu kikosi kazi ni cha Polisi ili kimchunguze Polisi!

Taarifa yoyote itatiliwa shaka kwasababu hakuna trust, integrity au credibility ya Jeshi la Polisi
Na hii inatokea kwasababu RPC keshasema Polisi hawamshikilii Mwanaharakati.

Kwa maneno mengine RPC amewasafisha Askari wake. Halafu kuna kikosi kazi cha kumchunguza RPC na Askari wake kinachoundwa na Polisi. Hapa integrity, trust na credibility inatoka wapi?

Kwa mtazamo huo, ili Jeshi liaminike na kuaminiwa na kusadikiwa taarifa za kukinzana, zisizothibitika zinaliondolea uaminifu mbele ya Umma.

Tuhuma za Askari Polisi zichunguzwe na chombo huru!
Hakuna haki ya Polisi kujichunguza, na hilo tu linazidi kupoteza imani ya Wananchi.

Hata kama Mwanaharakati huyo ametekwa na ''kaka au Baba au nduguye'' hakuna atakayeamini taarifa ya Kikosi kazi cha Polisi hasa katika wiki hii ambayo taarifa za Polisi zimekinzana, zisizoaminika na kuoenekana zinapootosha Umma. Mzee Warioba kaeleza kwa kina haya ! asikilizwe

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
Spika wa Bunge achagua mifano kwa '' convinence''
Waliomhoji hawana weledi, walitoa ''air time'' si kuhoji
Polisi wajikuta na Utata mwingine, wawapa ''kauli'' wanaowanyooshea vidole


Spika wa Bunge amehojiwa na Wasafi TV. Moja ya hoja ilihusu matukio ya Utekeaji. Spika alieleza matumizi ''mabaya'' ya neno kutekwa akisema utekaji unahusu matumizi ya nguvu iwe silaha au kutokuwa na silaha.

Akitetea hoja zake, spika alitoa mifano ya waliopotea kwa 'stoway'' , wengine wakitafutwa na kukutwa kwa waganga wa kienyeji, wafanyabishara waliokutwa kwa mganga, matukio ya Mbeya na Mwanza n.k.

Spika hakuzungumzia matukio yaliyokuwa na matumizi ya nguvu japo kwa ushahidi.
Mh akawatetea Polisi kwa kusema wapo wahalfu katika matukio wenye pingu. Spika alipaswa kuelewa Raia hawapaswi kuwa na pingu. Ikiwa alibaini hilo, hiyo peke inaeleza hali ya usalama, na hoja ya dharura inapata mashiko.

Spika alifanya '' cherrypicking '' ili ku 'fit narrative'' yake kuhusu hoja kukataliwa Bungeni.

Ni wazi kwamba '' Waandishi'' kutoka TV ya Wasafi hawakuwa na weledi wa kuhoji, hawakufahamu kwanini wanauliza, hawakujua ''follow up questions'' . Ni kama walikwenda kutoa '' free airtime''.

Wiki hii kumeonekana magari ya Polisi yakiwa na askari wakati wa mikutano ya CHADEMA.
Hakuna tatizo la walinzi wa amani kufika maeneo yenye watu, hilo ni jambo la kawaida na jema.

Kilichoshangaza ni kuhusu uvaaji wa baadhi ya Askari katika magari wakifunika nyuso zao.
Moja ya mambo yanayomtofautisha Polisi na Tapeli ni utabulisho '' ID'' ikiwa ni pamoja na mavazi na sura.

Mitandaoni kuna hoja zinazozungumzwa , kwamba, ikiwa Polisi walikuwa na nia njema, kwanini walifika eneo la tukio wakiwa wamefunika nyuso? Nini mantiki ya kufunika nyuso na kwanini walinzi wa amani hawataki nyuso zao zionekane. Tofauti yao na wale ''wenye pingu'' za kitapeli inakuwa wapi!

Katika mazingira yaliyopo ambapo Jeshi la Polisi limenyooshewa vidole ikiwemo kutoka kwa Waziri Mkuu mstaafu, kufunika sura hakulisaidii . Wenye shaka na Jeshi wanakosea wapi katika mazingira hayo? Wananchi wanamtofautisha vipi mhalifu na Polisi?

Kama Taifa tunalekea wapi!
 
Spika wa Bunge achagua mifano kwa '' convinence''
Waliomhoji hawana weledi, walitoa ''air time'' si kuhoji
Polisi wajikuta na Utata mwingine, wawapa ''kauli'' wanaowanyooshea vidole


Spika wa Bunge amehojiwa na Wasafi TV. Moja ya hoja ilihusu matukio ya Utekeaji. Spika alieleza matumizi ''mabaya'' ya neno kutekwa akisema utekaji unahusu matumizi ya nguvu iwe silaha au kutokuwa na silaha.

Akitetea hoja zake, spika alitoa mifano ya waliopotea kwa 'stoway'' , wengine wakitafutwa na kukutwa kwa waganga wa kienyeji, wafanyabishara waliokutwa kwa mganga, matukio ya Mbeya na Mwanza n.k.

Spika hakuzungumzia matukio yaliyokuwa na matumizi ya nguvu japo kwa ushahidi.
Mh akawatetea Polisi kwa kusema wapo wahalfu katika matukio wenye pingu. Spika alipaswa kuelewa Raia hawapaswi kuwa na pingu. Ikiwa alibaini hilo, hiyo peke inaeleza hali ya usalama, na hoja ya dharura inapata mashiko.

Spika alifanya '' cherrypicking '' ili ku 'fit narrative'' yake kuhusu hoja kukataliwa Bungeni.

Ni wazi kwamba '' Waandishi'' kutoka TV ya Wasafi hawakuwa na weledi wa kuhoji, hawakufahamu kwanini wanauliza, hawakujua ''follow up questions'' . Ni kama walikwenda kutoa '' free airtime''.

Wiki hii kumeonekana magari ya Polisi yakiwa na askari wakati wa mikutano ya CHADEMA.
Hakuna tatizo la walinzi wa amani kufika maeneo yenye watu, hilo ni jambo la kawaida na jema.

Kilichoshangaza ni kuhusu uvaaji wa baadhi ya Askari katika magari wakifunika nyuso zao.
Moja ya mambo yanayomtofautisha Polisi na Tapeli ni utabulisho '' ID'' ikiwa ni pamoja na mavazi na sura.

Mitandaoni kuna hoja zinazozungumzwa , kwamba, ikiwa Polisi walikuwa na nia njema, kwanini walifika eneo la tukio wakiwa wamefunika nyuso? Nini mantiki ya kufunika nyuso na kwanini walinzi wa amani hawataki nyuso zao zionekane. Tofauti yao na wale ''wenye pingu'' za kitapeli inakuwa wapi!

Katika mazingira yaliyopo ambapo Jeshi la Polisi limenyooshewa vidole ikiwemo kutoka kwa Waziri Mkuu mstaafu, kufunika sura hakulisaidii . Wenye shaka na Jeshi wanakosea wapi katika mazingira hayo? Wananchi wanamtofautisha vipi mhalifu na Polisi?

Kama Taifa tunalekea wapi!
Inasikitisha sana kuona spika wa bunge amegeuka kuwa msemaji wa serikali. Ni aibu zaidi kwa mtu anaejitanabaisha kuwa msomi wa sheria kiwango cha PHD lakini anatoa hoja dhaifu kiasi kile. Hakika huyu anaenda kuweka rekodi kuwa ni spika mbovu kabisa kuwahi kuhudumu kiti kile toka tupate uhuru!
 
Inasikitisha sana kuona spika wa bunge amegeuka kuwa msemaji wa serikali. Ni aibu zaidi kwa mtu anaejitanabaisha kuwa msomi wa sheria kiwango. cha PHD lakini anatoa hoja dhaifu kiasi kile. Hakika huyu anaenda kuweka rekodi kuwa ni spika mbovu kabisa kuwahi kuhudumu kiti kile toka tupate uhuru!
Kiwadhifa Spika ni kiongozi wa juu sana Nchini. Kitaaluma ni Mwanasheria mbobezi (PhD).
Kijamii ni Mwakilishi wa Watu (Mbunge), ni Mke na Mama wa Watoto n.k.

Kwa kauli anazo toaSpika, ule msemo wa Rais Lincoln una maana
'' If you want to test a man's character give him power'' akimaanisha ukitaka kujua tabia ya mtu mpe madaraka. Kile kilichojificha kuhusu maadili na tabia yake kitajitokeza kwasababu ya madaraka

Bw Matshona akasema '' If you want to know the character of a person, observe how he treats those who don't matter'' akimaanisha ikiwa unataka kujua tabia ya mtu mwangalie anavyo watendea wasio mhusu.

Msemo mwingine '' absolute power corrupts aboslutely'' kwamba nguvu zisizo na mipaka au udhibiti humfanya awaye kuharibika kimaadili.

Mh Spika ana ''define'' kutekwa ni kudhuriwa kwa nguvu au kwa silaha.

Mh anafahamu nini kilimtokea Kijana aliyeumizwa na kutupwa Sumbawanga, kilichotokea Tegeta na nini kinaendelea jimboni kwake. Spika kachagua mifano inayofaa hoja yake '' fit the narratives'' na siyo inayo ''fit' definition yake

Spika akatoa mfano wa aliyetekwa kiluvya akisema '' watu wangesema Polisi kwasababu waliojaribu kumteka walikuwa na Pingu'' . Spika anafahamu pia aliyetekwa ndani ya basi kulikuwa na Pingu.

Pingu inatumiwa na Polisi tu! Spika alitakiwa kujiuliza ikiwa '' Raia'' wana pingu na wanazitumia hali ya usalama ipoje? Je, hilo halikutosha kuwa hoja ! Si kazi ya Spika kuwa msemaji wa Polisi na Serikali.

Waafrika tunasikitisha sana! Tumepoteza Utu, tunajijali sisi , ubinafsi ndio hoja!
Hatujali Wenzetu bali nafsi na nafasi zetu.

Swali, ni kwanini tunawatukana Wakoloni?. Kuna ''electronic footpirint'' ipo siku wataulizwa walisema nini!


Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
Alichosema Mbunge wa Kawe Mh Askofu Gwajima

Habari zinataradadi mitandaoni ni mkutano wa Mh Gwajima na Waandishi. Maoni ya Wananchi yamegawanyika, wapo wanaosema amesema hali ilivyo, wanaosema amekwepa ukweli na wanaouliza alikuwa wapi

Tupitie kwa uchache alivyoeleza Mh Gwajima (Gjm). Kwanza, mada ya utekaji, mauaji na kupotea ni ngumu, si viongozi wanaoweza kuiongelea kwasababu alizoeleza Gwajima, unyeti (sensitivity)

Gwj ametembelea unyuzi ( fine lines) kati ya anachosema na masilahi, akiongea kama Raia si Askofu, Mbunge, m-NEC au Mwanchama wa CCM, akitumia haki ya Kikatiba kuzungumzia masuala ya Nchi kama Raia.

Gjm hawezi 'kutuhumiwa'' kutumia dini , au siasa au Ubunge katika maongezi. Msajili wa Taasisi za dini hawezi kumchukulia hatua, CCM hawawezi kumchukulia hatua wala Bunge haliwezi kumwita. Ni Raia.

Pili, Gwj haamini kama vyombo vya Dola akivitaja kama Polisi, Idara ya Usalama, Magereza au JWT kuhusika na matukio. Gwj ameongea kwa kutumia mifano akisisitiza haina uhusiano na uhalisi.

Gwj akasema, ikiwa Watoto wa Rais, IGP, TISS na JWT wangetobolewa macho, je hali hiyo ingenyamaziwa? Gwj kasema ikiwa sivyo kwanini Wanaotekwa sasa ionekana kama ni Mbuzi!

Mfano mwingine ni wa Wakuu wa TISS kubadilishwa ndani ya miaka 3 akihoji kulikoni?
Gwj anasema huenda kuna kikundi ndani ya vyombo vya ulinzi chenye nguvu ya Wanasiasa.
Kikundi hicho huenda kinazuia vyombo vya ulinzi kufuatilia yanayotokea, akasisitiza.
Gjm akasema viongozi wanaogopa kuondolewa nafasi zao kwenda Ubalozini.

Askofu Gjm akahoji, inakuwaje Watu wanaojitambulisha ni vyombo vya dola wafike Hotel Maarufu na kumchukua mtu kisha kumtupa mpakani? Mwingine mwanamke akidai kudhalilishwa?

Askofu akahoji ikiwa yanatokea katika Hotel yenye hadhi inaeleza hali ya usalma. Akisistiza Gwj ana amini kwa dhati vyombo vya usalama vinafahamu, na kama hivfahamu, kama Nchi hatupo salama!
Gwj alifunga mkutano akisema '' nitasema kama wengine watakaa kimya shauri yao''.

Tumefafanua ili waliosmsikiliza watoe maoni wakiwa na ufahamu wa wakati aliokuwa nao.
Dhamira inamtuma aseme, lakini kama alivyosema viongozi wana Familia, bila shaka naye anayo.

Jitihada za kutembea kwa uangalifu akitazama pande zote , ni mtego. Gwj alifikisha ujumbe wake

Gjm anasema '' kama hatasema biblia inasema, mawe yatasema''. akituhumu eneo analodhani ni haki ya kujadiliana '' Bunge''. '' Hii ni Nchi yetu sote, Tanzania kwanza mengine yanafuata'' alimalizia

Hoja ya safu:
Bunge ni chombo cha Uwalilishi wa Wananchi. Bungeni kuna ''control' ya maongezi yanayohusu masuala ya kijamii wakati huo huo Bunge likitoa uhuru wa maoni.
Bunge linaposusa hoja nzito za utekaji , mauaji n.k. hicho ni kibali cha Raia kuongea .

Tunajua maoni ya Raia ''court of public opinion' hayana control, kanuni au sheria.
Hoja inaweza kuwa ''skewed' kulingana na nguvu za watoa hoja na si nguvu zahoja.

Tumefika mahali tatanishi, lakini, Bunge haliwezi kukwepa lawama kwa chochote kitakachotokea kisichopendeza Umma au kuharibu taswira ya Nchi. Bunge limetelekeza wajibu, limesusa Umma, halioni hatari ya mazungumzo katika ''court of public opinion'' hata hivyo '' Vox Populi vox dei'' kauli ya Umma ni kauli ya Mungu! Ikifika wakati huo Bunge halitakuwa na kauli tena!!

Kama Nchi tunaelekea wapi?
 
Gwajima hajajibiwa hoja !
Bungeni ''self inflicted wound, self incrimination''


Kauli ya Askofu Gwajima, Mbunge wa Kawe imezua mjadala ndani ya jamii na Bungeni kwa hisia kali.
Jamii inatazama hoja zake kama tatizo lililopo linalohitaji ufumbuzi hata kama sio alioupendekeza.

Kwa upande wa CCM na Serikali, hoja ya Gwj inaonekana kama uchonganishi na Jamii

Rais Kikwetwe alimnukuu Mwalimu Nyerere akisema '' hoja hujibiwa kwa hoja, haipigwi rungu''
Wanaompinga Gwj wanamtuhumu kuhusu hali ya kisiasa jimboni kwake kuelekea uchaguzi.

Wengine wakimkejeli kwa kauli alizoahidi wakati Kampeni. Hakuna anayemjibu hoja kwa hoja, yule aliyekuja na 'press conference'' hakukujibu hoja au kufafanua ni wapi Gwajima alikosea

Kada na DC Ikungi alieleza historia ya idara ya usalama, akitetea utekaji kwa hoja za waganga wa wakienyeji, kauli ya Dr Slaa n.k. kama alivyoeleza Spika. Utetezi kwamba hakuna utekaji unatoa nafasi hoja za Gwajima kutamalaki. Mathalani, watetezi wa utekaji hawaelezi yaliyowazi kama tukio la Tegeta.

Ni kwa mtazamo huo hafifu wa makada wa CCM, Gwajima anaungwa mkono na Jamii
Kwamba Jamii haiangalii makando kando ya Gwajima, inataza hoja kama tatizo la jamii .

Bungeni nako hali haikuwa tofauti, kwavile Spika alikataa suala lisijadiliwe, jana limejadiliwa kupitia Gwajima. Bunge limejadili si hoja zake bali kumkejeli , kumdhihaki n.k. ukweli unabaki hoja imeingia Bungeni kupitia Gwajima. Spika alipokataa isijadiliwe kistaraabu imejadiliwa kibubusa na kulidhalilisha Bunge

Katika tukio jingine, wakijadili wizara ya mambo ya ndani Wabunge wamewashambulia Wanaharakati na Watu kutoka Nchi jirani. Hoja ya Bunge si kuhusu nini kimejiri bali Serikali kutukanwa na Gen Z wa Kenya.

Hakuna aliyeeleza kwa ushahidi tatizo ni nini na kwanini kusikiliza kesi iwe kosa!
Wabunge waliongea kwa mihemuko bila point zenye ushawishi.

Kwanza, serikali ni kitu kikubwa sana kujibizana na Gen Z wa mitandaoni. Kwa hili Gen Z wa Kenya wamefaulu kwa kuligeuza Bunge sehemu ya mjadala wao. Haikuwa na ulazima wa aina yoyote kuwajadili

Kubwa zaidi ni Mbunge wa Pandani -Unguja aliidhalilisha Bunge na Nchi akisema ilikuwa ni makosa watu kurudishwa wazima akimaanisha ima waumize au wapotezwe.
Aka mbeza anayechechema na kutaka Waziri asifanye kosa wakati mwingine.

Kauli za Mbunge huyo katika mazingira yaliyopo nchini zinatafsriwa kwamba '' serikali inashughulikia watu bila kufuata sheria'' kauli ya Mbunge ilikuwa ''self inflicted wound '' akishauri '' extra judicial''

Mbunge wa Mjini Magharibi akashauri ''Mtanzania fulani '' anatosha kuwatukana majirani.
Kwamba, Mbunge ameona kuna Mtanzania maarufu kwa matusi na huyo anaweza kutuwakilisha.

Hayo yakitokea Uongozi wa Bunge ulikuwa kimya! ukiruhusu Wabunge wazungumze watakavyo bila kujua kauli zingine ni '' self incrimination'' zimeiacha serikali na wakati mgumu mbele ya jamii.

Wabunge wamethibitisha hoja ya Gwajima, ndio maana tunasema, kwa haya yanayotokea Gwajima kawapiga home and away! anaonekana ni shujaa, si shujaa kwasababu ya ushujaa bali ni shujaa kwa kusimama pale Umma ulipo akipambwa na hoja dhaifu za wanaompinga kama za Wabunge wetu.

Kama Taifa tunalekea wapi?
 
Spika akana mjadala Bungeni
Maji ya kimwagika hayazoleki ni la Spika halikwepeki


Spika aliombwa ijadiliwe hoja ya Watu kupotea au kutekwa katika mazingira tatanishi.
Hoja ya Spika, Bunge halitaweza kutoa ''resolution' yaani azimio baada ya mjadala.

Hoja ya Mh Spika haina ukweli. Kilichopaswa ni kuruhusu hoja iletwe na ijadiliwe. Ikiwa hoja haina mashiko iachwe au ina mashiko ifuatiliwe kwa Bunge kutumia kamati zake au kuunda kamati kama ilivyokuwa kwa Richmond na Korosho Mtwara n.k. kisha ripoti ya kamati ndio itaamua kama kunahitajika azimio la kusimamia serikali. Spika hataki lijadiliwe, hiyo resolution ingepatikanaje?

Spika akagoma Bunge la CCM halikuhoji. Spika akitoka nje ya Bunge analijadili suala la utekaji akichagua mifano inayo ''fit narrative'' kama Waganga wa kienyeji! Suala husika ni nyeti kuna Familia zinalia , zinaomboleza, zina mayatima na Wajane. Kiroho jambo zito si la kufanyia mzaha.

Katikati ya mtifuano ulioanza na kesi ya Tundu Lissu kisha kushika Wanaharakati, Wtaanzania wamegawanyika. Ndani ya mgawanyiko Askofu Gwajima akazungumzia utekaji na kupotezwa.
Kwa njia za ''kiroho'' , Wabunge wa CCM wakaanzisha mjadala Bungeni kupitia Gwajima.

Hoja ya Gen Z wa Kenya na Gwajima zikalivuruga Bunge. Bajeti ya Wizara ya mambo ya ndani ikageuka kituko. Wabunge wakipambana na Gen Z wengine wakimzodoa Gwajima! ikawa dhalili

Wabunge wakatueleza namna ''serikali ilivyozembea'' hadi Wakenya na Waganda wanarudi wazima.
Wabunge wakatoa ushauri apelekwe ''mtaalamu wa matusi'' mmoja apambane na Gen Z.

Bunge likapoteza staha, heshima na kuwa mithili ya mkusanyiko wa wapita njia!! wakibwabwaja

Hoja ya Askofu Gwajima ikapata miguu kuhusu utekaji , kupigwa watu na kupotea.
Kwamba, serikali ihakikishe ''hairudii kosa, Wamerudi wazima! Tumalizane nao'' walisema Wabunge

Ni wapi Gwajima amekosea ikiwa Wabunge wanatuthibitishia kwamba hakuna sheria ila '''kumalizana na watuhumiwa, hata wanaochechemea wanajifanya' na kwamba Serikali isirudie kosa''

Spika amekana yaliyojadiliwa si msimamo wa Bunge akiwataka Wabunge wafuate kanuni.

Sauti ya Umma ni sauti ya Mungu (vox populi vox dei). Umma ulitaka tatizo lijadiliwe, Spika akakataa!
Spika anazuia hoja, anaruhusu ''trolling'' ya Wabunge kwa Gwajima, lakini ukweli unabak, alichosema Gwajima ni kauli midomoni mwa UMMA. Hata kama itafichwa , itapotezwa na kuzuiwa Bungeni, hoja itajitokeza tu kwa njia zisizo rasmi kama ilivyotokea Bungeni !


Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
Kinachoendelea katika jamii Kinafikirisha
Nyerere aliwahi mabadiliko wakati yanaombwa na si kudaiwa


''Video clip'' inayozunguka katika mitandao ya jamii ikimuonyeshwa Mwalimu Nyerere akizungumza juu ya mabadiliko (reforms) akisema '' Wanyonyaji hawataki mabadiliko, lakini kwa Wanyonge mabadiliko ni lazima. Wanyojaji wanaposikia Wanyonge wana mkutano husema , Wanyonge wana mkutano! mamaweee''

Mwalimu anaeleza Wanyonyaji hawataki mabadiliko kwa manufaa yao, akiwaonya kuhusu subira inapofikia kikomo kwa wanyonge, kwamba, kwa ulazima wa mabadiliko wanyonge wanaweza kukaa vikao kwa shari

Katika Mkutano mkuu wa CCM 1995 Mwalimu alizungumzia mabadiliko wanaohitaji Watanzania akionya wasipoyapata ndani ya CCM watayatafuta nje ya CCM.

Kauli za Mwalimu zinatueleza jambo katika wiki za misuko suko ya aina tofauti katika jamii.
Suala linalotawala maongezi ni utekaji, kupotea watu na vifo visivyoelezeka linaongelewa wazi zaidi na kila siku wanajitokeza wasemaji wapya. Ni wazi jamii inaguswa, vyombo vya dola vikiwa kimya au havina majibu.

Kama alivyosema Mwalimu Nyerere 1995 upepo unavuma wa mabadiliko na sasa yakichagizwa na ''No reforms No election'' ya CHADEMA. Kuna uhusiano usio rasmi wa kauli mbiu na matukio.
Hoja ya '' NRNE imetekwa'' na kuwa kauli mbiu ya jamii ikionyesha ghadhabu na hasira za WananchI.
Ni ngumu kutenga mabadiliko ya uchaguzi na mabadiliko yanayodaiwa kutokana na matukio !

Hata kama viongozi watadharau wakisema ni ''kikundi kidogo'' wakichimbia vichwa mchangani kama mbuni, kuna somo la Nyerere. Miaka ya 1990 mabadiliko ya mifumo ya kidunia yaliegemea demokrasia ya vyama vingi. CCM iliandaa ''white paper'' 20% ilisema vyama vingi, 80% kimoja

Mwalimu kwa kutazama mvumo katika jamii aliwaambia CCM, 20% ipo siku watakuwa wengi hamtaweza kuwazuia, ni bora muanze mageuzi msisubiri yaliyomkuta Rais wa Romania aliyesubiri wachache wakawa wengi na kumuondoa madarakani. CCM ikakubali mfumo wa vyama vingi.

Kuna kitu kinatokea katika jamii,viongozi hawaoni au wanaopaswa kuwapa taarifa hawaelezi ukweli.

Katika zama za ''wasiojulikana'' Wananchi wanapoweka picha zao au video au majina au kusimama katika mikutano na kusema bila kificho '' No reforms No Election'' inafikirisha!!!

Ima Wananchi hao ndio wanyonge aliosema Mwalimu Nyerere wamefikia''tipping point' kwamba hawaogopi tena! Viongozi wanaofikiri wanaliona jambo! wasiofikiri wanasema ni ''upuuzi''
Ukweli unabaki, kuna jambo linazizima katika jamii yetu!

Je ni Wapinzania pekee! na mbona wanaungwa mkono na sauti yao ina mashiko ndani ya jamii!
Je wapo CCM wanaoona muda umefika, hali si shwari, na Chama kimepoteza uelewekeo!

Utekaji, upoteaji na mauaji yasiyo elezeka yamejenga hasira kiasi cha Wananchi kuunganisha matukio hayo na No reforms No election. Hii ni perefect storm inayoikabili CCM na Serikali yake.
Itafika mahali nguvu ya Umma itatamalaki! Hakuna tawala iliyowahi kushinda nguvu ya Umma Duniani.

Nyerere alipoona jambo alitangulia kulikabili ! hakuwa kaidi wala kusubiri kuona matunda ya ukaidi.

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
Jaji Mkuu astaafu
Jaji Mkuu Prof Ibrahim Juma kiongozi wa Mhimili wa Mahakama amestaafu. Nyakati zilizopita kustaafu kwa Jaji Mkuu ni gumzo katika jamii, hali si kama ilivyozoeleka.

Ukweli kwamba Jaji aliongezewa muda, kustaafu kwake kumebeba hisia . Kwanza, kuongezewa muda ilileta mtafaruku ndani ya Mahakama ukipingwa na Majaji wengine kwa kukosa ''uhalali'

Kwa Umma, Jaji Juma ni kiongozi aliyebadili mtazamo wa Wananchi kuhusu Mahakama kama Mhimili. Mathalani, tangu chaguzi za 201, 2010 zilizolalamikiwa, kesi hazikufunguliwa Mahakamani na walalamikaji. Hoja ni kwamba hakuna haki Mahakamani, ni kupoteza muda.

Ni katika kipindi cha Jaji Juma, kesi zilifanyiwa mizengwe mfano ile ya kiongozi wa Upinzani kuhusu kuondolewa CAG ilipigwa dana dana hadi Mlalamikiwa alipofariki. Hakukuwa na ulazima kwasababu ilikuwa kesi yenye 'public interest''.

Kipindi cha Jaji Juma kesi ya Wakili mmoja dhidi ya serikali kuhusu Wakurugenzi kusimamia uchaguzi ilitoa majibu yaliyoiacha jamii na mshangao na vicheko. Kwamba, kula kiapo kunazuia uhalifu! ..,

Hayo ni machache yanayoinyima Mahakama ile hadhi iliyokuwa nayo. Wananchi wanakata tamaa lakini Mahakama ni moja. Hili ni doa, Mahakamani inapotiliwa shaka kuna tatizo. Hili linasemwa wazi.

Katika uongozi wa Jaji Ibrahim Juma, Mahakama imeshindwa kujiweka ''huru'' kwa rasilimali ikitegemea Bajeti yake kutolewa na Mhimili mingine. Hili limeifanya Mahakama ikose ''independence''

Ni katika uongozi wake, Mahakama imetoa kauli ya '' kutoa maamuzi kwa kuangalia Mihimili 'mingine.
Kauli inayotafsiriwa kwamba HAKI inategemea Mihimili mingine! Jaji hakufafanua hadi anastaafu

Jaji Juma amesimamia maboresho ya Mahakama , kuifanya ya kisasa na kusimamia kuhamia Dodoma.
Wananchi hawazungumzii au kuyaona hayo kwasababu Mahakama imetia doa jukumu lake la utoaji haki.

Wananchi ni Wateja wa Mahakama, wanapokosa imani ina maana Mahakama ''imeshindwa kuuza bidhaa ''' yake ambayo ni utoaji wa HAKI

Jaji Juma, tumtakie heri kwa mema aliyofanya, atakumbukwa kama kiongozi aliyeshindwa kutetea hadhi na heshima ya Mhimili wa HAKI , kutoilinda Mahakama kuingiliwa na wana siasa na kuifanya Mahakama ipoteza imani kwa Wananchi.

Mahakama imekuwa ''chaka la kuficha au kutetea ''badala ya Mwanga wa Haki, chini ya uongozi wa Jaji Ibrahim Juma
 
Yanayotokea yanalisaidia vipi Taifa? Yana ulazima?

Wiki hii Rais ameongeza muda wa Bunge hadi Agosti 3 litapovunjwa rasmi. Katika kumbu kumbu zakraibuni tukio kama hilo halikuwahi kujitokeza. Kuna minong'ono, Bunge linatakiwa kufanya shughuli nyingine kabla ya Agosti 3.

Ikiwa ni hivyo na hasa kama inahusu siasa, swali la kujiuliza, nini kipya au kilichokuwa hakijulikani takribani mwaka mzima. Ni kipi ambacho hakijazungumzwa na watu wenye busara ambacho kimepata mwenye busara leo!

Tukio la pili ni mtifuano kati ya Waumini wa Askofu Gwajima na Vyombo vya Dola. Ni chururu kila Jumapili, ikionekana kuna majeruhi. Ni kitu gani kinachotishia amani kwa kuruhusu Waumini hao wafanya ibada zao?

Ikiwa kuna kiongozi au muumini anayekiuka sheria za nchi, huyo akabiliwe na mkono wa sheria kama mtu binafsi.
Kutoa hukumu ya kundi kuna madhara makubwa kwa jamii.

Akitokea kiongozi wa KKKT, BAKWATA, Catholic, Baraza kuu la Waislam, Sabato, Ismailia, Shia, Ahmadiya au Pentecost akatamka yasiyoipendeza serikali, je, itakuwa sababu ya kufungia makanisa au misikiti kwa ujumla wake?

Inahitaji busara, si vyema Taifa kuingia katika mitafaruku isiyo na maana! Hatuamini kama Watanzania tumeshindwa kukaa na kutafakari vipau mbele vya Taifa . Tunatumia muda mwingi wa kupambana na 'nyakati' badala ya changamoto.

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
Ni 'Law of the Jungle''
Yanga Sports Club Vs CHADEMA
Mbunge wa Vyama viwili ndani ya Bunge la Jamhuri


Nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania zinasemwa kuto kuwa na nidhamu (discipline) katika jamii zake

Ipo nadharia ya 'the law of the jungle au the rule of the jungle'' ikimaanisha kutokuwepo na taratibu au sheria katika jamii kama ilivyo mwituni ambako mwenye nguvu ndiye mwenye sheria ya wakati husika.

Nidhamu katika jamii yetu ni ya kiwango cha chini cha kutisha kwasababu wanaopaswa kuisimamia wanatekeleza '' the rule of the jungle'' bila mtima wa aibu, ni wasiotahayari wakihubiri hili na kutenda lile bila soni.

Miezi michache iliyopita viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam walizuia na kuwakamata viongozi CHADEMA kwa madai ya kufanya mikutano ya hadhara eneo la Kariakoo.
Hoja ikiwa ni kwamba Kariakoo ni eneo la Biashara , mikutano ya siasa inawalazimu Wafanyabiashara kufunga shughuli zao! Hakukuwa na ushahidi wa madai hayo lakini yaliyolewa na Watu walikamatwa!

Juzi, timu ya Yanga imesherhekea Ubingwa wa Ligi kuu kwa kufanya mkusayiko mkubwa eneo la Kariakoo.
Mkusanyiko wa Yanga ni mkubwa kuliko wa CHADEMA kwasababu Yanga ina mashabiki wa aina zote.
Maduka na shughuli za Biashara zilisimama kwa 'nature' ya tukio na wingi wa watu

Hatukusikia kiongozi yoyote wa Serikali au Jeshi la Polisi akikemea mkusanyiiko wa Timu ya Yanga.

Ikiwa mkusanyiko ndio ''subject na Factor'' ni sheria gani iliyotumika kuzuia CHADEMA na ikatoa ruhusa kwa Yanga SC? Hiawezekan kuwa na nidhamu kwa siku, tukio na wakati kwa kuchagua.

Nidhamu ni msumeno unaokata mbele na nyuma. Kwa hili la Kariakoo, nidhamu(discipline) iko wapi?
Integrity and credibility ya viongozi wa Mkoa ipo wapi! nani anawaamini tena kwa ''dicipline' hii

Tukio la pili ni la Wabunge waliojulikana COVID-19 ambao kisheria CHADE,A na kupitia mahakama imethibitisha ubatili wa Uanachama hivyo kupoteza sifa ya Ubunge kwa mujibu wa Katiba ya nchi.

Spika wa Bunge, Msajili wa vyama, Tume ya Uchaguzi zote zikafumbia macho ubatili wa sheria
Nidhamu (discipline) ya kusimamia sheria zilizotungwa na Bunge ipo wapi?

Baada ya Bunge kuvunjwa , Wabunge wa COVID waliokuwa '' bila chama'' wamejiunga na CCM na kuchukua Fomu za kutafuta ridhaa ya Ubunge.

Kuna maswali hapa! Ikiwa Ofisi ya Spika na Msajili wa Vyama na Tume ya Uchaguzi hazijui COVID wapo fungu gani, hivi walikuwa Bungeni kwa sheria gani? Je, ni 'the law of the jungle' iliyotumika?

Ikiwa Ofisi ya Spika inawatambua kama Wabunge wa CHADEMA, na sasa wamechukua Fomu za CCM, na ikiwa uhai wa Bunge upo, hawa COVID wanapiga kura kwa tufuru ya Chama gani? CHAMA HEWA, CHADEMA au CCM?

Ukitazama yote utabaini jambo moja, hatuna nidhamu ya kujitawala.

Tunaishi kama wanyama mwituni na sheria zinazotuongoza ni zile za ''the law of the jungle''.
Hili ni tatizo kubwa sana katika nchi yetu na si unique, nchi masikini hili ni sehemu ya modus operandi.

Inahitajika katiba itakayosimamia nidhamu kwanza! ili nidhamu isimamie nidhamu kila mahali

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
HOJA ZA ASKOFU GWAJIMA NA BALOZI POLEPOLE ZIJIBIWE, ZISIPIGWE MARUNGU.
HUKO ''SITE'' GWAJIMA NA POLEPOLE WANAELEWEKA !


Rejea bandiko#10 tukieleza hoja za Askofu Gwajima na sasa kuna hoja za Balozi Polepole, hazijajibiwa!

Tulieleza, Gwajima ana makando kando yake lakini hoja zake zijibiwe kwa hoja na si kutazama makando kando.
Vivyo hivyo, Balozi PolePole ana makando kando lakini hoja zake zijibiwe kama alivyoziwasilisha

Pamoja na makando kando, Gwajima kaoenkana ''shujaa'' si kwa kugusa tatizo la jamii.
Ndivyo ilivyo kwa Polepole ambaye kama Gwajima amegusa tatizo la jamii. Wote wanazungunzia UTEKAJI.

Kuna matatizo mengi ya Wananchi, linalosumbua Jamii kwa sasa ni kupotea watu na utekaji.
Gwajima na Polepole wanapokuwa 'wawakilishi wa Wananchi'' wanakuwa mashujaa ''by default'' kwasababu Bunge lilisusa wajibu, likawatelekeza Wananchi.

Spika alipozima mjadala wa utekaji na kupotea watu hakuisaidia Serikali, matokeo yake ndiyo haya! wanao ongelea ''contemporary matter'' ndio mashujaa.

Mwalimu Nyerere ''alipita na kuona foleni za sukari''. Siku iliyofuata Nyerere akaita mkutano Diamond Jubilee kueleza tatizo si ukosefu bali usambazaji. Nyerere alijua yapo matatizo lakini la sukari ndilo tatizo la wakati uliopo.

Zambia iliingia katika matatizo kwa kupandisha bei ya mkate. Wananchi hawakudai 'steak au Cake , maziwa au asali''
Mkate ndilo tatizo la jamii, lilipopuuzwa na Watwala, ukazuka mtafaruku mkubwa

Hakuna kutafuta mchawi kwa yanayotokea nchini kwasababu zilizo wazi;

1. Kukosa mkakati wa kutangulia '' pre emptive strategy''. Laiti utekaji na kupotea watu kungejadiliwa Bungeni leo Gwajima na Polepole pengine wasingekuwa na hoja. Kwavile Bunge halikutaka, wawili hao ni mashujaa ''by default''

2. Vyombo vinavyopaswa kuishauri serikali yaliyo katika jamii haviko makini. Au, vinadhani '' Nyundo ni suluhu ya kila tatizo linalohusu msumari''. Kwamba hoja zinazimwa kwa maguvu na mitutu bila kujua ni ''confounding factor''

3. Kutodhibiti hali '' damage control''. Kwamba uharibifu unakabiliwa kwa werevu si uharibifu zaidi. Jamii ina tatizo la utekaji, vyombo vinapokwenda ''kuteka'' au kuzuia hoja za utekaji kusemwa ni kuharibu zaidi ya uharibifu uliotokea!

Balozi Polepole ameeleza hoja nyingi, ya pili kubwa ni uchaguzi wa CCM. Tuliongelea katika uzi huu kwamba hata wakati wa Chama kimoja haikuwahi kutokea mkutano mkuu kupitisha wagombea halafu kurudi nyuma kutafuta utaratibu wa kuhalalisha. CCM walichokifanya '' the end justifies the means''

Polepole anasema Katiba ilikiukwa kama Wana CCM wengine wanavyolalamika chini chini. CCM wanaliona tukio hilo kama ''utekaji' mwingine wa Demokrasia.

Anachosema Polepole, haiwezekani CCM ikahubiri kuitetea Katiba ya Nchi wakati haifuati Katiba yake.
Yaani CCM inakosa ''moral compass'' ya kuhubiri taratibu , kanuni na sheria kwasababu haina maadili.

Tunasisitiza, hata kama makando kando ya Gwajima na Polepole yataibuliwa kuanzia chekechea hadi walipo sasa , ikiwa hoja zao zinazogusa Umma hazitajibiwa hakuna atakayeisikiliza Serikali.

Viongozi watambue, Gwajima na Polepole si tatizo la Wananchi, tatizo la Wananchi ni hoja zao ! Jibu si kukimbizana nao bali HOJA ZIJIBIWE KWA HOJA.

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
BALOZI POLEPOLE ''ALINUKUU'' MANENO YA RAIS MSTAAFU KIKWETE
HILI LA CCM LIMEWAPA NGUVU WAPINZANI MBELE YA USO WA JAMII

Hoja alizojadili Balozi Polepole ni uchaguzi wa CCM wa mkutano mkuu Dodoma. Polepole anasema taratibu na Katiba ya CCM ilikiukwa, akatole mfano wa iwapo Mkutano mkuu unaweza kuchagua Mbunge!

Hoja za Polepole zinashambuliwa na kujibiwa kwa dhihaka, si kwa uhafifu au potofu bali CCM hawana hoja ya kujibu (counter arguement)

Kuna video ya Vijana wa CCM wakinukuu ibara za katiba zinazotaka majina 3 yawasilishwe.
Vijana wanasema moja ya hayo 3 ni la Mwenyekiti wa sasa , hakuna ukiukwaji wa Katiba!!! Wanakubali taratibu hazikufuatwa lakini wanahalalisha tu kwasababu!

Jamii haikumbuki kabla ya Polepole hajatuhuma, Rais Mstaafu Kikwete alisema kuna ukiukwaji wa Taratibu

Akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu Kikwete alisema '' ...Sasa kama tunaamua , tumeamua! Kilichobaki ni kushauri wale wanaojua taratibu za kisheria. Bunge lishavunjwa, Tume ya uchaguzi ikaita wagombea wanataka utaratibu upi ili tujue ni utaratibu upi uliokuwa sahihihi ili tusije tukapata complications ya sheria halafu tukapoteza ... 2005 Mkutano mkuu wa uteuzi ulifanyika mwezi Mei, ndipo nilipoteuliwa of course tulifuata mchakato....... Tufanye uamuzi kwa misingi ambayo haitaonekana tumekiuka saana taratibu''

Kikwete anajua unahitajika ushauri wa kisheria kwa maana taratibu zimekiukwa, akaonya CCM isije ikapata complications. Kikwete akasisitiza, wanaojua sheria washauri ili CCM ijue utaratibu upi ni sahihi.

Kikwete akakiri 2005 walifuata mchakato uteuzi wake ulikuwa Mei, kwamba hakuna mchakato uliofuatwa.

Rais Mstaafu akasisitiza CCM ifanye uamuzi kwa misingi ambayo haitaonekana imekiuka Saaaana taratibu.

Kikwete anajua taratibu zimekiukwa, alichotaka ni kuona hazikiukwi saaana, lakini zimekiukwa.
Kikwete anatueleza kuna kitu kinaitwa kamimba kadogo ''little pregnancy''.

Ni ima kuna mimba au la! hakuna kitu katikati ya hicho! kwahiyo kukiuka saana haina maana! ni ukiukwaji tu

Ukumbi ulipoulizwa ulizomea! .CCM wanakubali utaratibu ulikiukwa , tatizo nani wa kumfunga paka kengele?

Balozi Polepole alichokisema ni aliyosema Kikwete, kama kusema hivyo ni kosa, nasi lilianza na Rais Kikwete.
Mitaani kuna hoja ya kimtaani, kwamba, lini Wagombea wa CCM walichukua Form?Si walichangiwa!

Hayo ni mambo ya CCM na Serikali yake, lakini yana impact kubwa katika jamii.
Kwamba, kama CCM haiwezi kufuata taratibu za Katiba yake katika chaguzi, vipi CCM hiyo itasimamia serikali yake kuhakikisha uchaguzi huru na haki? Hizi ndizo hoja za Wapinzani na zinashadidia hoja yao kwama NRNE.

CCM inakabiliwa na mtihani, si kukimbazana na akina Polepole ambao ni wengi ingawa hawasemi bali kukabiliana na hoja mbili. CC,M itashinda uchaguzi pengine kwa kishindo cha asilimia 99.

1. CCM haitakuwa na uhalali ''legitimacy'' ndani yake na kitakachoendelea ni kunyukana tu.
2. CCM na serikali zake hazitakuwa na uhalali ''Political legitimacy'' ndani ya jamii hata kama wangeshinda kwa haki.

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
ITV NA MZEE BUTIKU
WATANZANIA WANAPOSHINDWA KUTAFSIRI KAULI

Sakata la CCM na Mkutano mkuu linapamba moto , wakongwe wakitoa maoni.
Majuzi, Mzee Butiku, aliyefanya kazi na Mwalimu Nyerere kwa miaka 21 alihojiwa na kituo cha Televisheni cha ITV
Kuna yaliyojitokeza katika majadiliano hayo

1. Mzee Butiku hakutaka kuizodoa CCM '' critic', alichagua maneno kwa auangalifu
Mwandishi aliyemhoji,kama ilivyo kwa Waandishi wa Tanzania alishindwa ''kumchokonoa'' ili kupata habari zaidi

Mzee Butiku alisema '' lazima uchaguzi ufanyike ili tupate viongozi halafu mageuzi yatafuata baada ya kupata uongozi '' . Akaendelea kusema tutafanyaje mabadiliko Nchi ikiwa haina viongozi''

Mwandishi alipaswa kumuuliza kuhusu hoja za ''uwanja sawa wa uchaguzi'' ili kupata viongozi wanaotakiwa.
Kwa muundo uliopo hoja za Wanaotaka mabadiliko zinaanza na upatikanaji wa viongozi, hivyo mzee hakuwa sahihi

Mzee hakuwa sahihi pia kwasababu Katiba inaruhusu Rais kuongeza muda wa Bunge na Serikali. Imewahi kutokea alipofariki Makamu wa Rais Dr Omar Juma. Wapinzani wanakubaliana na hoja ya kuahirisha uchaguzi.

2. Mwandishi alishindwa kumdadisi kwa vile Mzee anataka mabadiliko baada ya uchaguzi je anakubaliana na kauli ya Reforms ya taratibu za uchaguzi? na kama ni hivyo kwanini zisianze reforms ili tupate viongozi .

3. Mzee Butiku alisema maneno mazito, kwa bahati mbaya Watanzania si wa tu wa kusikiliza au kusoma kwa utulivu.

Mzee Butiku alisema '' Read my lips'' pale alipobainisha kwamba uchaguzi wa CCM Dodoma ulikuwa na dosari.
Mzee akaonyesha kosa lililpotokea akisema '' ...Mkutano Mkuu hakuna kipengele kinachoruhusu private motion''

Mzee Butiku ana maanisha agenda za Mkutano mkuu huandaliwa mapema, mkutano mkuu wa January haukuwa na agenda ya Wagombea Urais, ilikuwa kosa kuleta ''private motion'' kisha kuitekeleza.

Akina Balozi Polepole wanasema kilichofanyika ni uhuni. Maana yake kulikuwa na ukiukwaji wa Katiba dhahiri shahiri.

Reading Butiku's lips and between the lines, kuna message! Kwamba the whole process was sham and flawed

Ikiwa Chama Tawala kinatenda haya 'within'' kwanini hoja za Wapinzania wanaoungwa mkono na baadhi ya CCM insiders zisiwe na mashiko? Kwamba, unacheza rafu mazoezini hali ipoje wakati wa mechi?

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
WIKI YA MAUZA UZA!
YA CHAUMMA NA ACT WAZALENDO
TINBAIJUKA NA MSIBA WA NDUGAI

Wiki imekuwa na kasi kwa matukio. Vyama vya CHAUMMA na ACT wameteua Wagombea wa Urais.
CHAUMMA ikimteua Salum Mwalim( naibu katibu Mkuu wa CHADEMA) na ACT wakimteu Luhanga Mpina.

Ni mambo ya kushangaza kwamba hao wanaweza kushinda kiti cha Urais kwa sifa zao na mazingira yaliyopo
Kwamba CHAUMMA na ACT zinaweza kulinda kura za Urais! kwamba wanaweza kuhinda mifumo iliyopo

Mpina Luhanga anakubalika jimboni kwake, laiti angepigania kurudi Bungeni ingeleta maana. Hata hivyo, kwa mzingira yaliyomkata Ubunge kabla ya kura, vyombo visingemuacha apate nafasi hiyo.

Kinachoonekana ni Mpina kuwa katika siasa ili asipotee ! akijiandaa kwa ''next move''. Huenda ni Sumaye, Lowassa au Membe kwa sura nyingine. Hili si geni hata kidogo

Kisiasa ni tatizo kubwa. ACT na CHAUMMA vinatoa uhalali wa kisiasa kwa CCM kwamba uchaguzi ni huru na wa haki. Vyama vinategemea fadhila kupata viti na kuanza kujijenga kwa ruzuku.

ACT na CHAUMMA vinategema kura za Urais kupata ruzuku. Vyama vinajua havina mategemeo yoyote ya ushindi.

Kwa wanaosema ACT na CHAUMMA ni CCM(B) na (C) ni vigumu sana kuwapinga
Ni vyama masilahi vikisalati '' fair play'' . Ni vyama vinavyovizia lakini havina Upinzani wa asili. Ni vyama mamluki vikipigania masilahi binafsi na si umma. Ni matawi ya CCM

Wiki hii kumetokea msiba wa Spika aliyejiuzulu Mh Job Ndugai. Katika maombelezo, Mbunge wa Zamani Mh Anna Tibaijuka ameeleza kuhusu tukio la kupigwa risasi kwa Mh Lissu.

Mama Anna anasema Ndugai alimweleza kwamba '' ni maelekezo' kutoka juu ! kwa maana alipewa maagizo kuhusu hatima ya Lissu, kiti chake cha Ubunge n.k. Kwa ufupi Ndugai alimweleza Tibaijuka kwamba ana maelekezo ya Serikali kuhusu Tundu Lissu!

Jambo hili linamaliza ubishi uliodumu kwa muda mrefu kuhusu shambulio la Tundu Lissu. Leo ;
1. Inafahamika kwanini Kamati ya Bunge iliyoundwa haikutoa taarifa
2. Inafahamika kwanini Polisi hawakufanya uchagunguzi
3. Inafahamika kwanini Dereva wake alikuwa kisingizio na alitafutwa pengine apangwe!
4. Inafahamika nani aliratibu na kutekeleza mpango ikiwemo viongozi walio ongoza msafar

Taarifa ya Mama Tibaijuka imeacha watu wengi wakiwa ''uchi''
Balozi wa Tanzania Marekani aliyesema haikuwa serikali
Waliodai hazikuwa risasi halisi bali '' rubber bullet''
Waliodai uchunguzi unasubiri dereva
Waliosimama kudai ni 'inside job' ya CHADEMA

Maombelezo ya Mama Tibaijuka kwa Spika Ndugai ni machache, lakini yamemaliza ubishi kuhusu shambulio la Lissu, waliohusika na cover up. Kwa hili, Mama Tibaijuka ashukuriwe ! ametenda haki kuufahamisha umma kilichotokea.

Kama Taifa tunaelekea wapi?
 
YANAYOTOKEA MAHAKAMANI YANATISHIA AMANI
VIONGOZI WA MAHAKAMA MPO WAPI?


Kuna wimbo wa Wanasiasa ''kudumisha amani, kulinda amani n.k.'' wakielewa hakuna silaha inayolinda amani
Viongozi wanajua Amani ni matokeo ya HAKI inayopatikana kupitia sheria tulizojiwekea kama jamii.

Bila sheria na haki , kama Wanadamu na Watanzania tutaishi kwa sheria za mwituni '' rule of the jungle'' zinazotoa fursa kwa wenye nguvu. Kwamba Simba, Tembo n.k. wana haki na wengine ni Wanyonge.

Maisha ya mwituni ni ya kukimbizana, kuvugana na kuwindana kila siku. Kuna nyakati Wanyama wanyonge hujilinda, huungana kukabliana na ukandamizaji! Ni maisha ya mashaka na hofu uchao na mawio

Wananchi wanapoteza imani na Mahakama ni kujidanganya kwamba kuna Amani.
Kunaweza kuwa na ukimya lakini si Amani.

Miaka ya karibuni Mahakama zimepoteza imani kwa Wananchi.
Kwanza, kwa mara ya kwanza Tanzania , Jaji Mkuu aliteuliwa kwa muda ''probation period' hadi pale Wapinzani walipopiga kelele Bungeni. Jambo la kusitikisha , Jaji aliyeteuliwa kwa muda alikubali hilo litokee akiwa Profesa

Jaji mkuu huyo hakujua ni ''precedent'' ya kuvuruga Mhimili wa Mahakama, akapiga magoti Mahakama ikidhalilishwa kwasababu tu alitaka cheo bila kujua madhara ya kitendo hicho kwa Taifa na Nchi kwa ujumla

Huo ukawa mwanzo wa Mahakama na Taaluma ya sheria kupoteza heshima na hadhi na kuwa idara au tawi

Mfanyabiashara maaurufu alisema '' Makampuni ya nje yangependa mashauri katika mahakama za Kimataifa, Mahakama za ndani zinaagizwa kwa simu... '' akimaanisha mamlaka zenye nguvu zaidi ya Mahakama

Kesi inayoendelea ya Tundu Lissu inatuonyesha matundu na ubovu wa mfumo wetu wa kusimamia HAKI kupitia mahakamani. Lissu amefikishwa mahakamani tangu akamatwe siku 100 ziizopita.

Kabla ya kumkamata waendesha mashtaka walijiridhisha kuna kosa na ushahidi wa kumshtaki Tundu Lissu.

Tangu wakati huo upande wa mshtaka umeomba kuahirishwa kesi kwasababu za kipuuzi zisizohitaji hata cheti cha sheria kuzibaini. Ni sababu zinazotia aibu Taifa kwa yoyote anayefuatilia kesi hiyo kitaifa na kimataifa.

Jambo baya ni Mahakama inaposimama na upande wa mshtaka kuendelea na udhalili wa sheria.
Ni kama vile Mahakama imepewa maagizo kwamba kesi hiyo ifanyiwe mzaha zaha kupoteza muda

Lissu ni kiongozi, kuelekea uchaguzi mkuu Mahakama ilipaswa kuona haja ya kutoa haki kwa wakati. Kiongozi wa upinzani kuwa mahabusu kunamuathiri kama Binadamu, Mwenyekiti, chama na Jamii kwa ujumla.

Tundu anapaswa kupewa haki ya kesi kuendeshwa kwa haki, uadilifu na weledi sio ubabaishaji na udhalili unaoonekana Mahakamani. Mfumo wa sheria nchini umedhalilika na kupotesha heshima

Uongozi wa mahakama upo kimya ukitaza uvurugwaji wa sheria na haki kana kwamba ni makubaliano.
Viongozi wa Mahakama waliwahisema ''... majaji watoe haki kwa kuzingatia mihimili mingine''

Upande wa Mahakama na Serikali wasichikona ni hatari iliyopo mbele yetu.

Wananchi watakapochoshwa na ukandamizwaji wa haki hakuna Amani na hakuna atakayekuwa salama, si Majaji, Mahakimu, waendesha mashtaka, Polisi au magereza. Tumeyaona Nchi ngingine!

Kama Taifa aibu hii tunaivumiliaje?
 
Back
Top Bottom