Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 16,473
- 34,347
- Thread starter
- #21
MAHAKAMA IJITENGE NA MITEGO YA SIASA
Wananchi wakipoteza Imani na Mahakama, wakimbilie wapi?
Kwanza, tunapo ongelea kesi ya Mh Tundu Lissu hatuongelei kosa analotuhumiwa nalo, tunaongelea mwenendo wa taratibu zinazotumika. Kwa namna yoyote hatutaongelea suala linalohusu kesi yenyewe.
Hatua za awali (committal) zimekamilika, kesi imepeleka Mahakama kuu. Hadi sasa haijapangiwa tarehe
Malalamiko ya Wananchi ni kuhusu cheleweshajwi wa kesi uliochukua zaidi ya siku 100.Lissu alipokamatwa ni dhahiri kulikuwa na ushahidi wa kutosha, lakini kwa namna ya ajabu sababu za kuahirisha kesi zikatolewa kila siku na kupata baraka za Mahakama. Sura inayojitokeza ni Mahakama ''kusaidia'' ucheleweshaji kwa hisia za ''kutumika''
Kuna kesi mbili Mahakamani zikihusu CHADEMA. Kwanza hii inayomhusu Lissu kwasababu ni mwenyekiti wa Chama.
Pili, inayohusu mgawanyo wa rasilimali za CHADEMA. Kesi zote mbili zina chembe za siasa ndani yake.
Nchi inaelekea uchaguzi mkuu October. Endapo kuna ushiriki au kutoshiri uchaguzi hayo yanahusu Vyama na Taasisi zinazosimamia chaguzi.
Kilicho wazi, ni msimu wa siasa za uchaguzi , Wananchi kupitia taasisi zao wana haki ya kushiriki siasa bila vikwazo.
Ucheleweshaji wa kesi kwa visingizio au kutozingatia hali ya Nchi kunapelekea hisia mbaya dhidi ya mifumo ya haki.
Kwamba kuna mbinu zinatumiwa ''kuzuia'' baadhi ya Taasisi kushiriki katika siasa kuelekea uchaguzi
Mahakama isiingie katika mtego huo, kuna uwezekano wa kumaliza mashauri kwa njia za dharura kwa kuzingatia hali ya nchi. Hii ina maana maamuzi yatoke kwa kuzingatia sheria bila kuathiriwa na udharura au hali ya siasa.
Hilo linawezekana! hoja kubwa ni kupatikana kwa haki ikimaanisha hatma ya kesi bila kujali matokeo
Hukumu zikitoka Mahakama itajivua lawama za 'siasa' zinazoelekezwa kwake na Umma.
Si kazi ya Mahakama kujua endapo CHADEMA watashiriki uchaguzi au la, ni wajibu wa Mahakama kufanya '' informed decision'' ili kulinda integrity ya Tribunal.
In public perception, the integrity and sanctity of judicial system is at an all time low!
Kama Taifa tunazuiaje uharibu zaidi?
Wananchi wakipoteza Imani na Mahakama, wakimbilie wapi?
Kwanza, tunapo ongelea kesi ya Mh Tundu Lissu hatuongelei kosa analotuhumiwa nalo, tunaongelea mwenendo wa taratibu zinazotumika. Kwa namna yoyote hatutaongelea suala linalohusu kesi yenyewe.
Hatua za awali (committal) zimekamilika, kesi imepeleka Mahakama kuu. Hadi sasa haijapangiwa tarehe
Malalamiko ya Wananchi ni kuhusu cheleweshajwi wa kesi uliochukua zaidi ya siku 100.Lissu alipokamatwa ni dhahiri kulikuwa na ushahidi wa kutosha, lakini kwa namna ya ajabu sababu za kuahirisha kesi zikatolewa kila siku na kupata baraka za Mahakama. Sura inayojitokeza ni Mahakama ''kusaidia'' ucheleweshaji kwa hisia za ''kutumika''
Kuna kesi mbili Mahakamani zikihusu CHADEMA. Kwanza hii inayomhusu Lissu kwasababu ni mwenyekiti wa Chama.
Pili, inayohusu mgawanyo wa rasilimali za CHADEMA. Kesi zote mbili zina chembe za siasa ndani yake.
Nchi inaelekea uchaguzi mkuu October. Endapo kuna ushiriki au kutoshiri uchaguzi hayo yanahusu Vyama na Taasisi zinazosimamia chaguzi.
Kilicho wazi, ni msimu wa siasa za uchaguzi , Wananchi kupitia taasisi zao wana haki ya kushiriki siasa bila vikwazo.
Ucheleweshaji wa kesi kwa visingizio au kutozingatia hali ya Nchi kunapelekea hisia mbaya dhidi ya mifumo ya haki.
Kwamba kuna mbinu zinatumiwa ''kuzuia'' baadhi ya Taasisi kushiriki katika siasa kuelekea uchaguzi
Mahakama isiingie katika mtego huo, kuna uwezekano wa kumaliza mashauri kwa njia za dharura kwa kuzingatia hali ya nchi. Hii ina maana maamuzi yatoke kwa kuzingatia sheria bila kuathiriwa na udharura au hali ya siasa.
Hilo linawezekana! hoja kubwa ni kupatikana kwa haki ikimaanisha hatma ya kesi bila kujali matokeo
Hukumu zikitoka Mahakama itajivua lawama za 'siasa' zinazoelekezwa kwake na Umma.
Si kazi ya Mahakama kujua endapo CHADEMA watashiriki uchaguzi au la, ni wajibu wa Mahakama kufanya '' informed decision'' ili kulinda integrity ya Tribunal.
In public perception, the integrity and sanctity of judicial system is at an all time low!
Kama Taifa tunazuiaje uharibu zaidi?