Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

SEHEMU YA 40

“Alianguka? Alianguka? Ina maana atakufa? Irene mtoto wangu atak…” alisema Rosemary, hata kabla hajamalizia sentensi yake, presha ikapanda, akadondoka chini.

“Rose…Rose…Rose mke wangu,” aliita Mapoto huku akilia, manesi wakafika mahali hapo haraka sana, mapigo yake ya moyo yalianza kushuka, wakambeba na kumuweka kwenye machela, mwili wake ulimlegea, alionekana kama tayari alikwishakufa. Manesi wenyewe wakatingisha vichwa vyao kushoto na kulia kuonyesha kwamba inawezekana huo ulikuwa mwisho wa mwanamke huyo.
***

Mapoto alijipa moyo kwamba mtoto wake angeweza kupona na kurudi katika hali ya kawaida. Moyo wake ulikuwa na huzuni kubwa, kila alipokuwa akiikumbuka sauti ile ambayo aliamini kwamba ilikuwa ni sauti ya shetani, alijikuta akichukia moyoni mwake.

Hakuwa na tumaini jingine zaidi ya Mungu wake aliyekuwa akimuabudu. Kila saa alimwambia mke wake washikane mikono na kuanza kusali kwani aliamini kwamba Mungu angekwenda kufanya muujiza na hali waliyokuwa wakiipitia ilikuwa ni jaribu ambalo lilikuwa ni lazima walishinde.

“Mke wangu! Hili ni jaribu. Namuamini Mungu wangu, hawezi kukupa jaribu kubwa zaidi ya uwezo wako! Hili ni jaribu linalolingana na uwezo wetu, hatuna budi kulishinda,” alisema Mapoto huku akimwangalia mke wake ambaye macho yake yalikuwa mekundu mno kuonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa amelia sana.

“Amen!” alijibu mkewe, hakutaka kuzungumza maneno mengi kwani kila alipotaka kufanya hivyo, moyo wake uliuma zaidi.
Upasuaji ukaanza, baada ya kukichana kichwa cha Irene, wakaanza kutoa kipande cha fuvu ambacho kitaalamu huitwa Bone Flap na kisha kukiweka pembeni kwa ajili ya kuangalia ndani ya ubongo kuona kulikuwa na nini.

Wakati wakiendelea kufanya upasuaji huo bado walikuwa wakizungumza huku wakikiangalia kichwa hicho kwa makini kabisa ambapo huko wakaliona donge la damu likiwa limeganda katika ubongo wake, tena kwa kujificha ndani ya ubongo kwa mbali.

“Ooh my God!” (Ohh Mungu wangu) alisema Dk. Phillips huku akionekana kushtuka kwani donge lile lilionekana kuwa kubwa tofauti na walivyodhani.
 
SEHEMU YA 41

“What is it?” (kuna nini?) aliuliza nesi mmoja.
“This is brain hemorrhage,” (damu imevuja kwenye ubongo) alijibu Dk. Phillips japokuwa alijua kwamba aliwaambia hilo kabla.

Kila mmoja alishtuka, hawakuamini kusikia kwamba damu ilikuwa imevilia katika ubongo wa Irene kwa kiasi kikubwa. Lilikuwa tatizo kubwa ambalo kwa watu wengi waliokuwa wakipata tatizo hilo, asilimia themanini walikuwa wakifa kwani damu huwa na kawaida ya kusambaa kwa haraka sana katika ubongo kuliko sehemu nyingine yoyote ile.

Waliogopa, waliuona mwisho wa Irene ukiwa mikononi mwao kwani hata kama angepona ilikuwa ni lazima kupata matatizo mawili, iwe ugonjwa wa kusahau kila kitu kilichotokea katika maisha yake yote au nusu ya maisha lakini pia ilikuwa ni kupata ugonjwa wa kupooza ambao ungeyatesa maisha yake kitandani.

Japokuwa walikuwa wakisali kimoyomoyo lakini baada ya kugundua hilo, kila mmoja akatulia, wakaanza kuangalia, damu ilikuwa kwenye ubongo na kwa bahati nzuri sana kwa Irene ni kwamba lilikuwa donge moja la damu lililotulia ndani ya ubongo paspipo kusambaa.

“We have to remove it without soring a brain,” (ni lazima tuiotoe damu pasipo kuutonesha ubongo) alisema Dk. Phillips huku akiliangalia donge lile la damu.

“We have ten hours to perfom this craniotomy,” (tuna saa kumi za kufanya upasuaji huu wa kichwa) alisema Dk. Phillips, na mpaka kipindi hicho, tayari zilikuwa zimepita saa saba.
 
SEHEMU YA 42

Upasuaji ulikuwa ukiendelea, Dk. Phillips na wenzake hawakutoka ndani ya chumba kile, walijua kwamba nje kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakisubiri kuona ni kitu gani ambacho kingetokea ndani ya chumba kile.

Donge la damu halikutoka kirahisi, kila walipoligusa kwa maana ya kulitoa, lilihama na kuhamia sehemu nyingine kitu kilichowapa usumbufu mkubwa kwani mpaka wanakamilisha kulitoa, tayari walitumia saa sita na hivyo kuanza kurudishia fuvu taratibu.

Mpaka wanamaliza, walichukua saa kumi na mbili, walichoka, hawakuwa na matumaini kama Irene angepona kwani kila walipokuwa wakiangalia mashine ya Mult Parameter Monitor mapigo yake ya moyo yalionyesha kushuka kwa ghafla na kupanda.

“We have to pray for her,” (inabidi tumuombee) alisema Dk. Phillips.
Hawakuwa na jinsi, kadiri walivyomwangalia Irene kitandani pale walikiri kwamba mtoto huyo alikuwa akienda kufa. Hali yake ilitisha na kila walipomwangalia, mioyo yao iliwaambia kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa wake kuvuta pumzi ya dunia hii.

Baada ya kumaliza kusali, wakatoka na moja kwa moja Dk. Phillips kuwaita wazazi Irene ofisini kwake kwa ajili ya kuzungumza nao. Hakuwaficha, aliwaambia ukweli juu ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwamba binti yao alikuwa kwenye hali mbaya na kama wasingemuomba Mungu basi angeweza kufariki dunia kitandani hapo.

“Hatuna ujanja zaidi ya kusali sana, tukishindwa, basi atakufa kwani nisingependa kuwaficha, watu wanaopata tatizo hili, wengi hufa japokuwa kwa Irene tunajaribu kupambana,” alisema Dk. Phillips japokuwa alikuwa akizuiliwa kuwaambia ndugu wa wagonjwa maneno kama hayo lakini hakuwa na jinsi.
 
Naona hawataki kuniona jukwaa la siasa nikiingia tu hijo nikitoka lazima wanipe ban
Uckate tamaa inamaana kuna kitu wamekiona kwako lazima upambane siasa imekuwa sehemu ya maisha yetu japo wanatutisha
 
Uckate tamaa inamaana kuna kitu wamekiona kwako lazima upambane siasa imekuwa sehemu ya maisha yetu japo wanatutisha
Wanapoelekea watanipa life ban inabidi tu niwe makini walinipa ban za mfululizo
 
Wanapoelekea watanipa life ban inabidi tu niwe makini walinipa ban za mfululizo
Wapuuzi tuu kwani maana ya uhuru wa mtandao ni nini kama wamechoka watu wafunge limtandao lao tutaenda kwingine saifi jamiiforum haina tofauti na serikali ya Ngosha
 
Wapuuzi tuu kwani maana ya uhuru wa mtandao ni nini kama wamechoka watu wafunge limtandao lao tutaenda kwingine saifi jamiiforum haina tofauti na serikali ya Ngosha
Mkwe unapoelekea utanipa ban shunie mm nikishusha mgazeti wangu yaani ni kweli hawana tofauti kabisa mwanzo walinipa ban et nachochea maandamo mods hawapendi sikia habari za maandamnao na sio kwamba napost thread za maandamano hapana nacomment tu habari za maandamano

Mara ya pili ban imeniuma mpaka nikawaandikia thread kama hawataki niende jukwaa la siasa waniambie ban waliyonipa wamenionea kuna thread ilipostiwa jukwaa la siasa jf ya sasa sio kama ya zamani nikacomment jf ya sasa inabidi tukae kimya tu nikala ban sababu waliyonipa eti comment yangu nazuia wengine kuchangia hoja nazuiaje sasa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom