Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

Jamani shunie, ulipita jukwaa gani hilo limikusababishia ban mamii
Sijui ni ya muda gani aisee
 
SEHEMU YA 35

Ilipofika asubuhi, majira ya moja, tayari walikuwa hospitalini kwa ajili ya kumjulia hali, kama walivyokuwa wamemuacha usiku uliopita ndiyo alikuwa vilevile, walihuzunika, walilia sana kwani kuna kipindi walihisi kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wa Irene, pale kitandani alipokuwa asingeweza kuinuka wala kufumbua macho yake.

“Ni lazima niwasiliane na Rosemary,” alisema Mapoto.
Hakutaka kujiuliza mara mbilimbili, hapohapo akachukua simu yake na kumpigia mkewe, hakutaka kumpa taarifa moja kwa moja, ilikuwa ni lazima amdanganye kwamba kuna kitu ambacho kingemfanya kusafiri na kwenda nchini Marekani haraka sana.

“Rosemary! Tumekukumbuka sana mke wangu,” alisema Mapoto mara baada ya kumpigia simu mkewe.
“Nimewakumbuka pia. Mnaendeleaje huko?”
“Huku sisi ni wazima sana. Watoto wapo shuleni, wamekukumbuka mno, kila siku wanakuulizia, ninahitaji uje huku, uwaone, uwafanyie sapraizi kwanza. Halafu pia kuna kitu,” alisema Mapoto.

“Kitu gani?”
“Kuhusu kujiuzulu. Kuna jambo nimelifikiria, ninataka uje tuweze kulizungumzia,” alisema Mapoto.
“Mmh!”
“Mbona unaguna sasa?”

“Hatuwezi kulizungumzia kwenye simu?”
“Hapana! Uje huku kwanza, uwaone watoto waliokukumbuka, halafu kuna sehemu tutakwenda, ni sehemu nzuri sana, huko, tutazungumza mambo mengi. Nadhani umekwishasikia Jiji la Hollywood!”

“Yeah!”
“I just want to take you there,” (nataka nikupeleke huko!)
“Ooh! Sawa. Ngoja niombe ruhusa. Ila naomba nisichukue mwezi kukaa huko!”
“Hilo usijali my Juliet,”
“Nashukuru my Romeo.”

Moyo wake ulimuuma, kuzungumza na Rosemary pasipo kumwambia ukweli kile kilichokuwa kimetokea kilimfanya kujihukumu sana moyoni mwake. Akakata simu, akaelekea pembeni ukutani na kuanza kulia kama mtoto.

Alijitahidi kujifanya kama mtu mwenye furaha kuzungumza na Rosemary lakini moyo wake ulimkatalia kabisa, hakufarijika na hata maumivu aliyokuwa nayo moyoni hayakupungua hata mara moja.
 
SEHEMU YA 36

“Itakuwaje akifika? Itakuwaje kama akigundua nimemdanganya? Atafanyaje? Mungu naomba umtie nguvu asipate tatizo lolote lile baada ya kupokea taarifa kuhusu Irene,” alisema Mapoto, akamchukua Godwin na kukaa naye kwenye kiti kilichokuwa nje ya chumba kile na kuanza kulia, kadiri muda ulivyozidi kwenda mbele, mioyo yao iliwaka moto kwa maumivu makali.

*** Moyo wa Rosemary ulikuwa na shauku kubwa ya kutaka kuwaona watoto wake, aliwapenda sana na kilipita kipindi kirefu pasipo kuwatia machoni mwake, alifurahi kwa kuwa alijua baada ya saa kadhaa, ndege ingetua na kuwaona watoto wake hao.

Aliona ndege ikienda taratibu, alikuwa na hamu kubwa ya kuwaona kwa mara nyingine, hakufikiria kama kulikuwa na jambo baya lililotokea ambalo lingemuumiza sana moyo wake.
Ndani ya ndege, alikuwa akiwasiliana na mume wake kwa kutumia barua pepe, kila sehemu alipofika, ilikuwa ni lazima amtumie barua pepe kuonyesha kwamba alikuwa njiani na muda wowote ule angefika nchini Marekani.

“Tumefika Heathrow nchini Uingereza, muda wowote ule tunaondoka kuja huko,” alisema Rosemary mara baada ya kupata muda wa saa mbili kupumzika kabla ya ndege kuendelea na safari.
“Ooh! Tunakusubiri kwa hamu kubwa. Kila mtu hapa nyumbani amekukumbuka sana,” alisema Mapoto, kwa jinsi sauti ilivyosikika, ilikuwa vigumu kugundua kwamba kulikuwa na jambo baya lililokuwa likiendelea.

Saa 4:45 usiku wakapanda ndege kuelekea nchini Marekani. Muda mwingi alikuwa akiwasiliana na mumewe kwa barua pepe, alitamani kufika nchini Marekani haraka sana kwani kilipita kipindi kirefu tangu siku ya mwisho kuwaona watoto na mume wake.
Upande wa pili, Mapoto alikuwa na mawazo tele, mke wake alikuwa njiani akielekea nchini Marekani, mpaka kipindi hicho hakuwa amemwambia ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

Moyo wake ulikuwa mzito, alimfahamu mkewe, alikuwa na presha, alijua kwamba kama angemwambia waziwazi basi angeweza kupata tatizo zaidi na hata kufariki kutokana na mshtuko mkubwa.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 37

Baada ya saa kumi, akaondoka nyumbani kwake na kuelekea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JFK uliokuwa hapohapo jijini New York. Alipofika, akatulia na kuanza kumsubiri mkewe.
Ubao ulisomeka kwamba ndege aliyopanda Rosemary ambayo ilikuwa ikitoka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow ingeingia mahali hapo majira ya saa saba mchana hivyo alitakiwa kusubiri.

Moyo wake haukuacha kumuomba Mungu, alitaka amtie nguvu mkewe mara baada ya kugundua kitu kilichokuwa kimetokea, hakutaka kumuona akipata tatizo lolote lile, alitaka kumuona akiwa kwenye hali ya kawaida japokuwa kile alichotaka kumwambia kilikuwa kitu kibaya, chenye kuumiza ambacho kwa mwanamke yeyote, mwenye mapenzi na watoto wake asingeweza kuvumilia.

Ilipofika saa saba, ndege hiyo ikaanza kutua katika uwanja huo, aliiona ikitembea ardhini, haraka sana akakimbilia bafuni, akanawa uso wake, hakutaka michirizi ya machozi ionekane, ilikuwa ni lazima kumuonyeshea mke wake furaha kubwa ili asiweze kugundua kitu chochote kile.

Alipotoka huko, akaelekea sehemu ya kuwasubiri wageni wanaoingia, alipomuona mke wake, akamsogelea na kumkumbatia kwa nguvu, hakutaka kuona akiondoka mikononi mwake.
“Nimekukumbuka mke wangu!” alisema Mapoto huku akiwa amemkumbatia zaidi.

“Nimekukumbuka pia mume wangu! Watoto wapo wapi?” aliuliza Rosemary.
“Unakumbuka nilikwambia nini?” aliuliza Mapoto huku akiachia tabasamu pana ambalo liliyaficha maumivu mazito yaliyokuwa moyoni mwake.
“Sapraiziiiii…” alisema Rosemary na kuachia kicheko.

“Yeah! Nataka washtuke kwa furaha kukuona,” alisema Mapoto huku akionekana kuwa na furaha mno.
Wakatoka nje ya jengo la uwanja huo na kuingia ndani ya gari, aliamua kuendesha yeye mwenyewe kwani alihitaji kujiweka bize na asiweze kumfikiria mtoto wake.
Njiani, walikuwa wakizungumza mambo mengi, kila mmoja alionekana kuwa na furaha mno.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika nyumbani ambapo Mapoto akaliingiza gari mpaka ndani na kumfungulia mlango mkewe.

Nyumba ilikuwa kimya, wakaelekea ndani na kumuita mfanyakazi ambaye tayari alimtengeneza kwa kile kilichokuwa kikiendelea, alichokifanya ni kumwambia akawaite watoto.
 
SEHEMU YA 38

“Daktari alikuja na kumchukua Irene, alikuwa akilalamika kuumwa kichwa,” alisema mfanyakazi wa ndani.
“Nilijua tu! Jana amecheza sana! Na hii si mara ya kwanza,” alisema Mapoto, aliongea kama utani ili mkewe asiweze kufikiria kitu kibaya.

“Na Godwin?”
“Yule asingeweza kubaki. Wale watoto wanavyopendana! Ni hatari! Ngoja tujiandae twende tukamuone na kuwachukua. Naamini akikuona tu, na kichwa kitapona,” alimwambia mkewe ambaye hakuonekana kuwa na hofu yoyote ile.

Wakaondoka na kuelekea bafuni, huko, Rosemary alimkumbatia mumewe, kwa kipindi kirefu hakuwa amekutana naye, alilikumbuka joto lake, alitamani sana afike na kuonana na mume wake huyo japo wachangie kitanda kama ilivyokuwa nchini Tanzania.

Mapoto hakuwa na hamu yoyote, hisia zote za kufanya mapenzi ziliondoka mwilini mwake, alipokuwa akimwangalia sana mkewe, taswira ya Irene aliyokuwa amelala kitandani ilimjia kichwani mwake, machozi yalipoanza kutiririka, akafungua bomba la mvua na kuyaruhusu maji kummwagikia.

“Una nini?” aliuliza Rosemary huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Sina kitu chochote.”
“Hebu uruhusu mwili wako! Utanifanya nijisikie vibaya kwamba una mwanamke mwingine,” alisema Rosemary huku akimwangalia mumewe usoni.

Hakuwa na jinsi, hakuwa na hamu yoyote ile lakini ili kumridhisha mkewe ilikuwa ni lazima afanye kile alichotaka kifanyike. Wakakumbatiana, walikaa kwenye hali hiyo kwa dakika kumi na tano kisha kutoka bafuni.

Wakajiandaa na kisha kuondoka nyumbani hapo kwa ajili ya kwenda hospitalini kumuona Irene aliyekuwa amelazwa kwa kupoteza fahamu baada ya kuanduka kutoka kwenye kiti.

Hawakuchukua muda mrefu wakafika huko, wakamuona daktari na kuzungumza naye, kwa kuwa na yeye alikuwa akijua kilichokuwa kikiendelea, akawaita ndani ya ofisi yake na kuwaambia kwamba mtoto wao hakuwa amepata tatizo, lilikuwa dogo sana la kichwa.

“Huwa anakuwa anaumwa kichwa mara kwa mara?” aliuliza daktari.
“Ndiyo! Huwa anaumwa mara kwa mara, tena hasa baada ya kuja kuishi huku, nahisi ni matatizo ya kubadili hali ya hewa” alidakia Mapoto kwani alijua kama asingeingilia, mkewe angekataa hilo.
 
SEHEMU YA 39

“Sawa. Ndiyo maana! Tumempa chumba apumzike kwanza. Mkitaka kumuona, mnaruhusiwa, ila mtatakiwa kuwa kimya, amepumzika,” alisema daktari.
“Sawa.”
Wakatoka ndani ya ofisi hiyo na kuanza kuelekea katika chumba alicholazwa Irene. Mapigo ya moyo wa Mapoto yalikuwa juu kwa kiwango kikubwa, alikuwa na hofu kubwa kwa kuhisi kwamba inawezekana mkewe angegundua kile kilichokuwa kimetokea Irene mara baada ya kumuona kitandani hapo.

Walipokifikia chumba hicho, wakaufungua mlango na kuingia ndani. Irene alikuwa kimya kitandani, waliambiwa kwamba alikuwa amepumzika hivyo hata Rosemary alivyomuona mtoto wake kitandani pale, hakuonekana kuwa na hofu kabisa.

“Nafikiri baadaye atakuwa kwenye hali ya kawaida,” alisema daktari.
“Tunashukuru sana!”
Mpaka kufikia hapo, wakawa na uhakika kwamba walifanikiwa kuutuliza moyo wa Rosemary, hakuonekana kuwa na presha, aliamini kile alichokisema mume wake.

Wakatoka na kukaa kwenye viti vilivyokuwa nje ya chumba kile, walikuwa wakizungumza huku Mapoto akijitahidi sana kujiweka katika hali ya kawaida.
Baada ya dakika kadhaa, dereva wake, James akafika hospitalini hapo akiwa na Godwin.

Alipomuona mama yake, akamkimbilia, alipomfikia, wakakumbatiana huku Godwin akilia kwa maumivu makali kiasi kwamba Rosemary alishangaa.

“Unalia nini?”
“Irene…Irene…”
“Amefanya nini?” aliuliza Rosemary.
“Anaumwa kichwa tu. Godwin njoo kwa baba,” alisema Mapoto huku akimchukua Godwin.

“Hebu subiri kwanza. Godwin, Irene amefanya nini?” aliuliza.
“Atakufa! Mwalimu amesema Irene atakufa, alianguka darasani,” alisema Godwin huku akimwangalia mama yake, Rosemary aliposikia maneno hayo, akahisi kama alipigwa na shoti ya umeme, akayapeleka macho kwa mume wake, Mapoto alibadilika, machozi yakaanza kumlenga, akayainamisha macho yake chini kwani hata kukutanisha macho na mkewe aliogopa.

“Irene alianguka darasani? Atakufa? Alianguka darasani au anaumwa kichwa?” aliuliza Rosemary huku akimwangalia mume wake.

“Nisamehe mke wangu!”
“Niambie! Ukweli ni upi?”
“Ire..Irene…Iren…”
“Niambie amefanya nini?” aliuliza mke wake kwa sauti ya juu, tayari machozi yalianza kumtoka, maumivu aliyoyasikia moyoni mwake kipindi hicho hayakuweza kuelezeka.
“Alianguka!”
 
nimecheka yaan ban napewa za kuonewa aisee nahisi kuna mod anajifunzia ban kwangu hataki kabisa nifike jukwaa la siasa
Usiende kule baki na wazee wa arosto hukujana nimekusearch mpaka kwa darubini sikuoni.
 
nimecheka yaan ban napewa za kuonewa aisee nahisi kuna mod anajifunzia ban kwangu hataki kabisa nifike jukwaa la siasa
Pole na karibu tena, kule uwe unasoma tu then unapita zako
 
Usiende kule baki na wazee wa arosto hukujana nimekusearch mpaka kwa darubini sikuoni.
Hahahah acha tu tena juzi walitoka nifungulia khaa bada ya masaa machache napewa ya siku mbili sijui kama nitaweza kutoingia jukwaa la siasa yaan
 
Hahahah acha tu tena juzi walitoka nifungulia khaa bada ya masaa machache nawepa ya siku mbili sijui kama nitaweza kutoingia jukwaa la siasa yaan
Ukitaka kuingia jukwaa lile nitumie hata PM
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom