Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

ERIC SHIGONGO
DUNIA HAINA USAWA

IGP Ng’osha alichanganyikiwa, hakuamini kama mpigaji simu ambaye alijitambulisha kwa jina la Godwin alijua maovu yake yote ambayo kwake yalikuwa siri kubwa. Alibaki akitetemeka, ubabe wote aliokuwa nao ukatoweka na kuwa mdogo kama kidonge cha pritoni.
Aliogopa, alikuwa kiongozi wa jeshi la polisi Tanzania lakini alikuwa mbabe, aliyefanya mambo mengi ya chini, tena wakati mwingine kufanya mauaji kwa kuwa hara serikali yenyewe ilikuwa ya hovyo, iliyoongozwa na rais wa hovyo.
Akahisi kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake. Alimfahamu mtu huyo, alikuwa hatari, aliyaweka mambo mengi hadharani, watu walimsifia kwa kuwa kila alichokuwa akikiandika kilikuwa ni ukweli mtupu.
Pale alipokuwa amesimama, akahisi miguu ikikosa nguvu na kukaa kwenye kiti kiasi kwamba hata polisi wenzake wakabaki wakimshangaa.
“Mkuu!” aliita polisi mmoja kwa unyenyekevu mkubwa.
“Mfungueni huyo, hakikisheni mnaita waandishi wa habari na kuwaambia kwamba hakuwa na kosa,” alisema Ng’osha.
“Lakini mkuu...”
“Nimesema mfungueniiiiiii...” alisema kwa sauti kubwa iliyoonyesha kwamba hakuwa na utani juu ya lile alilokuwa akilitamka.
Kambili akatolewa katika chumba alichokuwa amefungwa, hakuelewa ni kitu gani kiliendelea kwani mateso aliyokuwa ameyapata siku hiyo hakuwahi kuyapata hapo kabla.
Waandish wa habari wachace wakaitwa na kupewa taarifa kwamba Kambili aliachiwa huru na kupelekwa nyumbani kwake. Alipofika, akatulia, mwili wake ulikuwa umevimba sana na kila wakati mkewe alipokuwa akimwangalia, alikuwa akilia tu kama mtoto.
Wakati akiwa hapo, akapokea simu kutoka kwa Godwin ambaye alimwambia kuwa kila kitu kilichokuwa kimetokea alikipanga yeye hivyo alitakiwa kufanya kila liwezekanalo, kuwaweka sawa wanachama wake kwani baada ya siku kadhaa, rais atatoka madarakani na yeye ndiye atakayekuwa rais.
“Mimi niwe rais?” aliuliza Kambili huku akiwa haamini.
“Ndiyo! Wewe ni mpambanaji sana, utakuwa rais wa nchi hii. Kesho mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Noel anakwenda kumkataa rais, huo ni mwanzo, akitoka huyo watakuja wengine na wengine, waambie wanachama wako huu ndiyo muda wa kugangamara, watakaoshindwa, achana nao. Nitahakikisha mpaka unaingia ikulu,” alisema Godwin kwenye simu.
“Unanichanganya! Yanawezekana vipi haya?”
“Fanya kwa nafasi yako. Ya nafasi yangu, niachie mimi,” alisema Godwin na kukata simu. Kambili akabaki akiwa hafahamu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
***
Haikuwa lengo la Noel kuwaita waandishi na kuwaambia kwamba hakuwa akiridhishwa na rais na hakutaka kumuunga mkono bali nyuma kulikuwa na kitu ambacho kingeweza kuiondoa familia yake duniani.
Alikuwa akiipenda, kwake, Sandra na mtoto wake walikuwa kila kitu, alikuwa radhi kupoteza kitu chochote kile maishani mwake ikiwemo kazi lakini si kuiona familia hiyo iliyokuwa ikimpa furaha wakati wa huzuni, upendo wakati wa kukata tamaa ikiondoka mikononi mwake.
Waandishi wa habari walikuwa wamekusanyika kwa wingi Habari maelezo, walitaka kusikia kile kilichomfanya mkurugenzi wa Usalama wa Taifa kuwaita mahali hapo na kutaka kuzungumza nao jambo muhimu.
Hakukuwa na mtu aliyekuwa akijua kilichokuwa kikiendelea, kila mmoja alikuwa na hamu ya kutaka kusikia kile ambacho Noel alikuwa tayari kukizungumza mbele ya waandishi wa habari.
Watu waliokuwa majumbani, walifuatilia moja kwa moja mkutano huyo katika televisheni na redio zao huku wale waliokuwa katika nchi mbalimbali wakifuatilia kila kitu katika televisheni zilizokuwa katika Youtube ikiwemo televisheni ya Global TV.
Baada ya waandishi wa habari wote kuwa tayari, Noel akaingia ukumbuni hapo na moja kwa moja kuelekea katika meza pekee iliyokuwa humo ambayo ilikuwa na viti kisha kutulia.
Siku hiyo alionekana kuwa tofauti, watu walimfahamu kama mtu aliyependa sana kutabasamu kila anapokuwa mbele ya waandishi wa habari lakini siku hiyo alionekana kuwa tofauti, uso wake ulionyesha picha mbaya kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
“Habari zenu,” alianza kwa kusalimia.
“Salama tu kiongozi,” wakaitikia waandishi wengine.
Moyo wake ulikuwa na dukuduku kubwa, aliwaangalia waandishi wale, kichwa chake kikaanza kufikiria kile ambacho magazeti na vyombo vya habari vingeandika juu yake. Alijua kwamba kungekuwa na watu ambao wangemlaumu hasa viongozi lakini aliamini kwamba asilimia tisini ya Watanzania wangemuunga mkono kwa sababu hakukuwa na wananchi wengi wakimpenda Rais Bokasa.
“Nimewaita kwa jambo moja tu. Najua wengi mnaona jinsi ninavyopambana, jinsi ninavyorekebisha mambo kutoka huku kwenda kule. Nimekuwa nikiwatumikia wananchi kwa nguvu zote, niliapa kufanya hivyo, na ninamshukuru Mungu kwa kuwa alinipa nguvu,” alisema, akanyamaza, akawaangalia waandishi na kuendelea:
“Ninawashukuru waandishi wa habari, mmekuwa pamoja nasi, tulipokosea, mlitusema, tulipopatia, mkatupongeza. Nimekaa na kuangalia hali ya nchi, kiukweli, nimeamua kuweka uamuzi mmoja. Sikulazimishwa, nimekaa na kuamua hivyo kwa manufaa ya Watanzania.,” alisema, kisha akanyamaza tena, akainamisha kichwa chake, baada ya sekunde kadhaa, akakiinua, machozi yakaanza kumlenga.
“Simuungi rais mkono!” alisema sentensi ambayo ilizua minong’ono mahali hapo, kila mtu aliyesikia hakuamini kama kweli sentensi hiyo ilitoka kwa mwanaume huyo ambaye kila siku alikuwa bega kwa bega kuhakikisha unyonyaji na unyanyasaji wa Rais Bokasa ukiendelea kwa wananchi, inakuwaje leo, tena kwa kujiamini atamke sentensi hiyo.
“Najua mmeshtuka. Nimeiangalia Tanzania, kule tunapoelekea, si pazuri, na hata hapa tulipo si pazuri kabisa. Nikiendelea kuweka msimamo wangu wa kumuunga mkono, nitakuwa nawaumiza Watanzania wengine. Nimenawa mikono yangu, simuungi mkono rais wetu. Sina imani naye hata kidogo,” alisema Noel, akanyamaza na kuwaambia kwamba alikuwa akikaribisha maswali mawili tu.
“Samahani mkuu! Umesema humuungi mkono rais, je, ni kweli suala la kukosa imani naye limeanza hili au kuna kitu nyuma ya pazia?” aliuliza mwandishi wa Gazeti la Uwazi.
“Hakuna kitu! Huwa sifanyi jambo kwa sababu ya mtu fulani. Huu ni muda wangu wa kutulia na familia yangu, naomba muelewe kwamba sijalazimishwa na mtu kuamua hivi,” alijibu Noel. Mwandishi wa Global TV naye akanyoosha mkono kuuliza swali.
“Nakumbuka kwenye Akaunti ya Mabadiliko ya Kweli, yule msumbuaji aliandika kwamba anampa rais miezi miwili kujiuzulu vinginevyo atapinduliwa, je, huu ni mmoja wa mkakati?” aliuliza mwandishi huyo, Amani Madebe.
“Huwa siingii kwenye mitandao ya kijamii, sijui chochote kinachoandikwa huko, sifuatilii, kama liliandikwa hilo, sijui chochote kile, ninachoomba ni kwamba ieleweke kuwa nimefanya hivi kwa ajili ya familia yangu, ninahitaji kukaa nayo, ila pia kwa jinsi Watanzania wanavyoishi, nadhani damu zao zitadaiwa mikononi mwangu,” alijibu Noel, hakutaka kuendelea, akasimama na kuondoka zake.
Wakati Noel akiwa amemaliza, Rais Bokasa alikuwa akikaribia Habari Maelezo, ndani ya gari alipokuwa akisikiliza mahojiano hayo yaliyokuwa yakiendelea, moyo wake ulimuuma, kijasho chembamba kikaanza kumtoka huku akiwa haamini kilichokuwa kikitoka mdomoni mwa Noel.
Alimwamini kijana huyo, alipambana naye hasa baada ya kufanya mauaji ya mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Kimwinyi aliyeuawa nchini Nigeria, aliamini kwamba huyo ndiye angeenda naye mpaka mwisho lakini mwisho wa kila kitu kilikuwa ni kuwaita waandishi wa habari na kuwaambia kwamba hakuwa na imani naye.
“Hivi kweli Noel anaweza kufanya uamuzi wa kijinga kama huu?” alijiuliza bila majibu.
Msafara huo ukafika mahali hapo, rais akashindwa kuteremka, alichokifanya ni kumwambia mlinzi wake kwamba msafara ugeuke na kuelekea ikulu kwani aibu aliyokuwa nayo ilikuwa kubwa mno na kuhisi kama alipakwa kinyesi usoni.
Haraka sana msafara ukageuka na kuondoka huku waandishi wa habari waliokuwa nje wakipiga picha kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
Hiyo ndiyo ilikuwa stori ya siku, gumzo la nchi nyingi kwamba hatimaye mkurugenzi wa Usalama wa Taifa hakuwa na imani na rais wake. Wengi walishangaa lakini kwenye mitandao ya kijamii alipokea sifa kwamba alikuwa mzalendo wa kweli na viongozi wengi walitakiwa kumuunga mkono kwa kile alichokuwa amekifanya.
“Yaani huyu jamaa nilikuwa simpenda, ila kwa hili alilolifanya, hakika yeye ni shujaa,” aliandika jamaa mmoja kwenye akaunti yake Facebook.
“Hata mimi! Huyu jamaa nilikuwa simpendi mno. Duuh! Leo imekuwaje mpaka kabadilika hivi?” alihoji jamaa mwingine kwenye posti hiyo.
Hakukuwa na mtu aliyejua sababu ya Noel kufanya hivyo, hawakujua kama familia yake ilitekwa na alifanya hivyo kama njia mojawapo ya kutaka wasiuawe. Siku hiyohiyo baada ya Noel kumaliza kuzungumza, Godwin akaandika katika akaunti ya Mabadiliko ya Kweli maneno yaliyosema: ‘Asipojiuluzu, atapinduliwa. Sijawahi kusema uongo’, posti ambayo ilizua mijadala mingi kwamba je, ni yeye aliyekuwa nyuma ya hilo? Hakukuwa na mtu aliyejua.
***
Halima alikuwa msichana mrembo, aliyekuwa na mvuto wa kumfanya mwanaume yeyote yule amfuate na kumchombeza kwa maneno matamu. Alikuwa mzungumzaji, alikuwa akizungumza na kila mtu aliyekuja mbele yake. Watu wengi walimpenda kwa kuwa tu hakuwa akijiona, alikuwa msichana ambaye alitoa tabasamu kwa kila mwanaume aliyesimama mbele yake.
Wanawake wengi wa Tandale wakatokea kumchukia, uzuri wake uliwachanganya na wengine kuhisi kwamba msichana huyo angewachukulia wanaume wao. Hawakutaka kumsalimia lakini hilo wala halikuwa tatizo kwa msichana huyo, kitu pekee alichokuwa akikiangalia kilikuwa ni kumpata mtu aliyemfanya kuwa hapo, Godwin.
Wanaume wakapeana taarifa, kama ilivyokuwa kwa mitaa mingine kwamba msichana mrembo anapohamia mtaani basi mitaa mingine wangejua nivyo ilivyotokea kwa Tandale. Wanaume kutoka Manzese, Mwananyamala na Magomeni wakafika mtaani hapo kwa ajili ya kumuona Halima ambaye alikuwa na sifa za kuwa msichana mrembo mno.
Kila aliyemuona, hakujutia muda wake aliopoteza, hakutaka kujuta kwa hatua aliyochukua ya kutoka mtaani kwake mpaka Tandale kwani msichana ambaye alibahatika kumuona siku hiyo aliingia ndani ya kichwa chake na kukiri kwamba Halima alikuwa msichana mrembo mno, msichana ambaye wengine walisema kwamba hakutakiwa kuishi Tandale bali Masaki kulipokuwa na wanaume wenye pesa.
Hakukuwa na mtu aliyejua sababu ya msichana huyo kuwa mahali hapo, wengi wakatamani kujua kwani kila siku asubuhi, alikuwa mtu wa kukaa ndani, hakutoka kwenda sehemu nyingine yoyote, hakuwa akifanya kazi kitu kilichowapa watu maswali mengi.
Vijana wengine wakajitoa kumfuatilia msichana huyo, walitaka kujua alikuwa nani na kwa nini aliamua kwenda kuishi mtaa huo na wakati alikuwa na uzri wa ajabu. Katika kufuatilia kwao wakagundua kwamba msichana huyo alikuwa kimada cha bwana mmoja mwenye pesa ambaye aliamua kumpangishia maeneo ya Tandale kwa kuwa tu hakutaka binti huyo achukuliwe na mwanaume yeyote mwenye pesa.
Mchana alionekana sista duu lakini kwa usiku alikuwa mtu mwingine kabisa, alitulia katika chumba chake huku akiwa na laptop yake akiangalia ni kwa jinsi gani angeweza kumtafuta mtu huyo.
Kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwasiliana na maofisa wa Usalama wa Taifa nchini Uswisi, FIS ambao walikuwa wakimwambia kitu gani cha kufanya na mahali ambapo walikuwa na wasiwasi wa kuwepo kwa mtu huyo.
“Umefikia wapi?” lilikuwa swali la kwanza kabisa.
“Bado ninaendelea kupeleleza, nahisi nitafanikiwa kumpata tu kwani bado nazoeana na watumbalimbali wa mtaa huu,” alisema Halima.
“Sawa. Jitahidi mpaka tufanikiwe.”
“Haina shida!”
Hakuacha kupeleleza huku na kule, alijitahidi kuendelea kuwapeleleza watu wengine ili afahamu mahali mwanaume huyo alipokuwa hapo mtaani. Wakati hayo yote yakiendelea ndipo akatokea kuzoeana na msichana mmoja mrembo ambaye alikuwa akifika sana hapo Fogo, Tandale.
Wakaanza kuzungumza, kwa muonekano, msichana huyo alionekana kuwa msomi kwani kila alipokuwa akifika huko, alikuwa na laptop yake katika begi kitu kilichowafanya kuanza kuzoeana kwa kuwa tu mara ya kwanza walipokutana, walionekana kuvutiana wenyewe.
“Unaitwa nani?” aliuliza msichana huyo.
“Naitwa Angelica,” alidanganya Halima.
“Ooh! Sawa. Mimi naitwa Winfrida!”
“Unaishi huku au?”
“Hapana! Huwa ninakuja kutembelea mpenzi wangu, nyumba hiyo hapo mbele. Anaitwa Godwin. Unamfahamu?” aliuliza Winfrida huku akitoa tabasamu pana.
Halima alipolisikia jina hilo, akashtuka, hakuamini kama kweli Winfrida alilitaja jina la mtu aliyekuwa akitafutwa sana ambaye alimfanya kufika mahali hapo. Alimwangalia msichana huyo mara mbilimbili huku akijiuliza kama lile jina la mtu aliyekuwa ametajwa mbele yake alikuwa ndiye aliyekuwa akimtafuta au mwingine.
“Angelica! Mbona umeduwaa?”
“Ooh! Samahani! Unajua nilikuwa na mpenzi wangu mwenye jina kama la mpenzi wako! Alifariki kwa ajali ya gari mwaka jana,” alisema Halima hapohapo kuyavuta machozi kwa nguvu zake zote na kuanza kulia kiasi kwamba Winfrida akamkumbatia kumpoza pasipo kujua ni kwa jinsi gani msichana huyo alijisikia baada ya kugundua kwamba mtu aliyekuwa akimtafuta, alikuwa mpenzi wake.
****
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania National, Bwana Kambili akawaita wenzake na kuanza kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea. Alikuwa na ushuhuda mkubwa kwamba kwa kila kitu walichokuwa wakikiona kikitokea katika kipindi hicho kilikuwa kimesukwa na mtu aliyeitwa Godwin ambaye alikuwa akitafutwa kila kona duniani.
Wengi hawakumwamini, kwanza walitaka kujua sababu ya kuachiwa kwake na polisi, yeye mwenyewe hakujua zaidi ya kuambiwa kwamba IGP Ng’osha aliamuru atolewe na waandishi wa habari kupewa taarifa. Kila mmoja alishangaa, wengi walimjua Ng’osha, alikuwa mwanaume mwenye roho mbaya kwa watu wa chama pinzani.
“Kwa nini aliruhusu kuondoka, yaani kirahisirahisi tu?” aliuliza katibu wa chama hicho, Bwana Walusanga Ndani.
“Sijajua! Mimi mwenyewe nilishangaa sana! Ila ukiachana na hayo, nimepigiwa simu na mtu anaitwa Godwin,” alisema Kambili.
Hapo ndipo alipoanza kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea na maneno aliyokuwa ameambiwa na mtu aliyempigia simu ambaye alijitambulisha kwa jina la Godwin. Kila mmoja alishangaa, hawakuona kama hilo lingekuwa jambo rahisi kutokea kwani pamoja na yeye kumiliki akaunti ile, pia alimwambia kwamba ndani ya siku chache Rais Bokasa angejiuzulu au kupinduliwa na wao kuchukua uongozi.
“Haiwezekani!”
“Jamani! Mimi ndiyo nimeambiwa hivyo! Tujipangeni kwa ajili ya kuichukua nchi hii,” alisema Kambili.
“Kuna ishara gani ambayo inaweza kutufanya tumuamini?” aliuliza Ndaki, alitaka kuamini baada ya kuona na si kuamini baada ya kuambiwa.
Kambili akawaambia kwamba kesho kungekuwa na kiongozi mmoja ambaye angewaita waandishi wa habari na kuwaambia kwamba hakuwa na imani na rais na hivyo kujitoa katika uongozi huo. Hakutakiwa kuwaambia ni kiongozi gani ila walitakiwa kujua kwamba kungekuwa na mtu ambaye angewaita waandishi wa habari na kuwaambia hivyo.
Hilo kidogo likawafanya viongozi hao kusubiri kuona kama jambo hilo lingetokea ili waanze kuamini. Siku hiyo ilipofika, wakaambiwa kwamba Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Bwana Noel alikuwa amewaita waandishi wa habari Habari Maelezo kwa kuwa kuna jambo alitaka kuzungumza nao.
Kilichotokea ndicho kilichowafanya kuamini kama Godwin angeweza kuwapeleka mpaka ikulu kwani kwa maneno tu kutoka kwa Kambili hawakuwa wameamini lakini kwa kile ambacho waliambiwa na kutokea, waliamini kwamba walikuwa wakienda ikulu, tena njia ilikuwa nyeupe kabisa, ishu ilikuwa ni kwao tu kujipanga na kwenda huko.
“Jamani! Iteni mikutano mzungumze na watu, waambieni kwamba tunakwenda ikulu. Kama tutakamatwa na kuuawa, acha tuuawe lakini tukawaambieni kwamba tunajiandaa kwenda ikulu,” alisema Kambili huku akiwaangalia wenzake kwa umakini kabisa kwani kwa jinsi alivyopigwa na macho yake kuvimba, hakuwa akiona vizuri.
“Tutafanya hivyo! Nadhani napo ni muda wa kupanga nani atakuwa makamu wa rais na nani atakuwa waziri mkuu!” alisema Ndani huku akionekana kuwa na hamu ya madaraka.
“Hilo tutapanga tukionana naye! Nadhani ni njia moja ya kufanikiwa katika hili. Nitawasiliana naye, nitapokea maelekezo kutoka kwake!” alisema Kambili.
****
Rais Bokasa alikuwa amechanganyikiwa, hakuamini kilichokuwa kimetokea, moyo wake ulimuuma, ulichoma kama mkuki, mtu ambaye alimwamini kwa nguvu zote, ambaye alikuwa akijua siri kubwa kutoka ikulu alikuwa amemkataa, hakutaka kufanya naye kazi kwa kuwa hakuwa na imani naye.
Hakutaka kukubali, alichokijua ni kwamba kulikuwa na mtu mwingine nyuma ya pazia ambaye alimshawishi kufanya jambo kama hilo, kwa sababu wanawake walikuwa na nguvu kwa waume zao, akataka kumtumia mkewe, Bi Stela kwa ajili ya kumshawishi mumewe na hatimaye kurudisha moyo nyuma.
Akamtuma Waziri mkuu mpaka nyumbani kwa Noel kwa lengo la kuzungumza naye lakini baada ya kufika huko akapewa taarifa kutoka kwa vijana wa Usalama wa Taifa waliokuwa wakilinda nyumba huyo kwamba hiyo ilikuwa siku ya pili mwanamke huyo hakuwa ameonekana.
“Amekwenda wapi?”
“Hatujui! Mumewe hataki kuzungumzia suala hilo hata kidogo,” alisema Andrew.
Waziri mkuu hakutaka kubaki nje, alichokifanya ni kuingia ndani kwa lengo la kuzungumza na Noel. Akakaribishwa mpaka ndani ambapo dada wa kazi akaenda kumuita bosi wake ambaye ndani ya dakika mbili, tayari alikuwa sebuleni.
Kwa jinsi macho yake yalivyoonekana, alionyesha kulia sana, yalikuwa mekundu huku kila wakati akivuta mafua yake kwa ndani. Waziri mkuu alibaki akimshangaa, hakujua kilichokuwa kikiendelea ila alihisi kwamba kulikuwa na jambo.
“Kuna nini?” aliuliza.
“Mheshimiwa Godson! Moyo wangu unaniuma sana,” alisema Noel huku akimwangalia waziri mkuu huyo.
“Kuna nini? Niambie kijana wangu. Umefanya maamuzi ya ghafla sana, niambie kuna nini,” alisema Bwana Godson.
“Ninaipenda sana familia yangu! Nadhani unajua hilo!” alisema.
“Ndiyo!”
“Nilikuwa tayari kufanya kila kitu kwa ajili yao.”
“Ndiyo!”
“Familia yangu siioni, sijajua ipo wapi! Ni ghafla tu siioni ndani, walinzi walisema aliondoka, alipokwenda, hakurudi, nimechanganyikiwa sana,” alisema Noel, akaanza kulia tena.
“Imetekwa?”
“Sijajua! Sijui chochote kile.”
“Niambie ukweli!”
“Sijui mkuu!”
Walizungumza mambo mengi, Bwana Godson alimuomba sana Noel arudi katika nafasi yake lakini mwanaume huyo alikataa na kusema kwamba siku zote angeendelea kubaki na msimamo wake, hakutaka tena kusikia kuhusu uongozi huo.
“Ni nani yupo nyuma yako?”
“Hakuna mtu, ila kurudi, siwezi kwa kweli,” alisema Noel.
Hakukuwa na kitu cha kumbadilisha, alibaki na msimamo wake kwamba kusingekuwa na kitu chochote cha kumrudisha kwani aliamini kwamba kama angefanya hivyo basi familia yake ingeweza kuuawa. Aliogopa na alipanga kubaki kwenye msimamo wake uleule mpaka pale ambapo angeona ni kitu gani kingeendelea baada ya hapo.
Baada ya siku mbili kupita huku kila mtu akiwa na maswali mengi juu ya uamuzi alioufanya Noel, mara waandishi wa habari wakapigiwa simu na Bilionea Kizota na kuambiwa kwamba walitakiwa kuonana naye nyumbani kwake kwani kulikuwa na mambo mengi alitaka kuzungumza nao.
“Bilionea Kizota? Kuna nini tena?” aliuliza mwandishi mmoja.
“Hatujui! Ila twendeni jamani. Si unajua yule ndiyo ameshikilia uchumi wa wafanyabiashara wengi. Twendeni,” alisema mwandishi mmoja, zaidi ya waandishi hamsini kutoka kwenye magazeti, mitandao na sehemu nyingine wakaanza kwenda huko, kila mmoja alikuwa akijiuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, walittaka kujua kama ni yaleyale kama ya Noel au yalikuwa mengine.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane siku zijazo.
 
Jackal nn tena mbona unataka umkamatishe mkombosi wetu Godwin kwa Halima, acha kabisaaaa icje tokea hilo.!!
 
ERIC SHIGONGO
DUNIA HAINA USAWA

IGP Ng’osha alichanganyikiwa, hakuamini kama mpigaji simu ambaye alijitambulisha kwa jina la Godwin alijua maovu yake yote ambayo kwake yalikuwa siri kubwa. Alibaki akitetemeka, ubabe wote aliokuwa nao ukatoweka na kuwa mdogo kama kidonge cha pritoni.
Aliogopa, alikuwa kiongozi wa jeshi la polisi Tanzania lakini alikuwa mbabe, aliyefanya mambo mengi ya chini, tena wakati mwingine kufanya mauaji kwa kuwa hara serikali yenyewe ilikuwa ya hovyo, iliyoongozwa na rais wa hovyo.
Akahisi kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wake. Alimfahamu mtu huyo, alikuwa hatari, aliyaweka mambo mengi hadharani, watu walimsifia kwa kuwa kila alichokuwa akikiandika kilikuwa ni ukweli mtupu.
Pale alipokuwa amesimama, akahisi miguu ikikosa nguvu na kukaa kwenye kiti kiasi kwamba hata polisi wenzake wakabaki wakimshangaa.
“Mkuu!” aliita polisi mmoja kwa unyenyekevu mkubwa.
“Mfungueni huyo, hakikisheni mnaita waandishi wa habari na kuwaambia kwamba hakuwa na kosa,” alisema Ng’osha.
“Lakini mkuu...”
“Nimesema mfungueniiiiiii...” alisema kwa sauti kubwa iliyoonyesha kwamba hakuwa na utani juu ya lile alilokuwa akilitamka.
Kambili akatolewa katika chumba alichokuwa amefungwa, hakuelewa ni kitu gani kiliendelea kwani mateso aliyokuwa ameyapata siku hiyo hakuwahi kuyapata hapo kabla.
Waandish wa habari wachace wakaitwa na kupewa taarifa kwamba Kambili aliachiwa huru na kupelekwa nyumbani kwake. Alipofika, akatulia, mwili wake ulikuwa umevimba sana na kila wakati mkewe alipokuwa akimwangalia, alikuwa akilia tu kama mtoto.
Wakati akiwa hapo, akapokea simu kutoka kwa Godwin ambaye alimwambia kuwa kila kitu kilichokuwa kimetokea alikipanga yeye hivyo alitakiwa kufanya kila liwezekanalo, kuwaweka sawa wanachama wake kwani baada ya siku kadhaa, rais atatoka madarakani na yeye ndiye atakayekuwa rais.
“Mimi niwe rais?” aliuliza Kambili huku akiwa haamini.
“Ndiyo! Wewe ni mpambanaji sana, utakuwa rais wa nchi hii. Kesho mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Noel anakwenda kumkataa rais, huo ni mwanzo, akitoka huyo watakuja wengine na wengine, waambie wanachama wako huu ndiyo muda wa kugangamara, watakaoshindwa, achana nao. Nitahakikisha mpaka unaingia ikulu,” alisema Godwin kwenye simu.
“Unanichanganya! Yanawezekana vipi haya?”
“Fanya kwa nafasi yako. Ya nafasi yangu, niachie mimi,” alisema Godwin na kukata simu. Kambili akabaki akiwa hafahamu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
***
Haikuwa lengo la Noel kuwaita waandishi na kuwaambia kwamba hakuwa akiridhishwa na rais na hakutaka kumuunga mkono bali nyuma kulikuwa na kitu ambacho kingeweza kuiondoa familia yake duniani.
Alikuwa akiipenda, kwake, Sandra na mtoto wake walikuwa kila kitu, alikuwa radhi kupoteza kitu chochote kile maishani mwake ikiwemo kazi lakini si kuiona familia hiyo iliyokuwa ikimpa furaha wakati wa huzuni, upendo wakati wa kukata tamaa ikiondoka mikononi mwake.
Waandishi wa habari walikuwa wamekusanyika kwa wingi Habari maelezo, walitaka kusikia kile kilichomfanya mkurugenzi wa Usalama wa Taifa kuwaita mahali hapo na kutaka kuzungumza nao jambo muhimu.
Hakukuwa na mtu aliyekuwa akijua kilichokuwa kikiendelea, kila mmoja alikuwa na hamu ya kutaka kusikia kile ambacho Noel alikuwa tayari kukizungumza mbele ya waandishi wa habari.
Watu waliokuwa majumbani, walifuatilia moja kwa moja mkutano huyo katika televisheni na redio zao huku wale waliokuwa katika nchi mbalimbali wakifuatilia kila kitu katika televisheni zilizokuwa katika Youtube ikiwemo televisheni ya Global TV.
Baada ya waandishi wa habari wote kuwa tayari, Noel akaingia ukumbuni hapo na moja kwa moja kuelekea katika meza pekee iliyokuwa humo ambayo ilikuwa na viti kisha kutulia.
Siku hiyo alionekana kuwa tofauti, watu walimfahamu kama mtu aliyependa sana kutabasamu kila anapokuwa mbele ya waandishi wa habari lakini siku hiyo alionekana kuwa tofauti, uso wake ulionyesha picha mbaya kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea.
“Habari zenu,” alianza kwa kusalimia.
“Salama tu kiongozi,” wakaitikia waandishi wengine.
Moyo wake ulikuwa na dukuduku kubwa, aliwaangalia waandishi wale, kichwa chake kikaanza kufikiria kile ambacho magazeti na vyombo vya habari vingeandika juu yake. Alijua kwamba kungekuwa na watu ambao wangemlaumu hasa viongozi lakini aliamini kwamba asilimia tisini ya Watanzania wangemuunga mkono kwa sababu hakukuwa na wananchi wengi wakimpenda Rais Bokasa.
“Nimewaita kwa jambo moja tu. Najua wengi mnaona jinsi ninavyopambana, jinsi ninavyorekebisha mambo kutoka huku kwenda kule. Nimekuwa nikiwatumikia wananchi kwa nguvu zote, niliapa kufanya hivyo, na ninamshukuru Mungu kwa kuwa alinipa nguvu,” alisema, akanyamaza, akawaangalia waandishi na kuendelea:
“Ninawashukuru waandishi wa habari, mmekuwa pamoja nasi, tulipokosea, mlitusema, tulipopatia, mkatupongeza. Nimekaa na kuangalia hali ya nchi, kiukweli, nimeamua kuweka uamuzi mmoja. Sikulazimishwa, nimekaa na kuamua hivyo kwa manufaa ya Watanzania.,” alisema, kisha akanyamaza tena, akainamisha kichwa chake, baada ya sekunde kadhaa, akakiinua, machozi yakaanza kumlenga.
“Simuungi rais mkono!” alisema sentensi ambayo ilizua minong’ono mahali hapo, kila mtu aliyesikia hakuamini kama kweli sentensi hiyo ilitoka kwa mwanaume huyo ambaye kila siku alikuwa bega kwa bega kuhakikisha unyonyaji na unyanyasaji wa Rais Bokasa ukiendelea kwa wananchi, inakuwaje leo, tena kwa kujiamini atamke sentensi hiyo.
“Najua mmeshtuka. Nimeiangalia Tanzania, kule tunapoelekea, si pazuri, na hata hapa tulipo si pazuri kabisa. Nikiendelea kuweka msimamo wangu wa kumuunga mkono, nitakuwa nawaumiza Watanzania wengine. Nimenawa mikono yangu, simuungi mkono rais wetu. Sina imani naye hata kidogo,” alisema Noel, akanyamaza na kuwaambia kwamba alikuwa akikaribisha maswali mawili tu.
“Samahani mkuu! Umesema humuungi mkono rais, je, ni kweli suala la kukosa imani naye limeanza hili au kuna kitu nyuma ya pazia?” aliuliza mwandishi wa Gazeti la Uwazi.
“Hakuna kitu! Huwa sifanyi jambo kwa sababu ya mtu fulani. Huu ni muda wangu wa kutulia na familia yangu, naomba muelewe kwamba sijalazimishwa na mtu kuamua hivi,” alijibu Noel. Mwandishi wa Global TV naye akanyoosha mkono kuuliza swali.
“Nakumbuka kwenye Akaunti ya Mabadiliko ya Kweli, yule msumbuaji aliandika kwamba anampa rais miezi miwili kujiuzulu vinginevyo atapinduliwa, je, huu ni mmoja wa mkakati?” aliuliza mwandishi huyo, Amani Madebe.
“Huwa siingii kwenye mitandao ya kijamii, sijui chochote kinachoandikwa huko, sifuatilii, kama liliandikwa hilo, sijui chochote kile, ninachoomba ni kwamba ieleweke kuwa nimefanya hivi kwa ajili ya familia yangu, ninahitaji kukaa nayo, ila pia kwa jinsi Watanzania wanavyoishi, nadhani damu zao zitadaiwa mikononi mwangu,” alijibu Noel, hakutaka kuendelea, akasimama na kuondoka zake.
Wakati Noel akiwa amemaliza, Rais Bokasa alikuwa akikaribia Habari Maelezo, ndani ya gari alipokuwa akisikiliza mahojiano hayo yaliyokuwa yakiendelea, moyo wake ulimuuma, kijasho chembamba kikaanza kumtoka huku akiwa haamini kilichokuwa kikitoka mdomoni mwa Noel.
Alimwamini kijana huyo, alipambana naye hasa baada ya kufanya mauaji ya mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Kimwinyi aliyeuawa nchini Nigeria, aliamini kwamba huyo ndiye angeenda naye mpaka mwisho lakini mwisho wa kila kitu kilikuwa ni kuwaita waandishi wa habari na kuwaambia kwamba hakuwa na imani naye.
“Hivi kweli Noel anaweza kufanya uamuzi wa kijinga kama huu?” alijiuliza bila majibu.
Msafara huo ukafika mahali hapo, rais akashindwa kuteremka, alichokifanya ni kumwambia mlinzi wake kwamba msafara ugeuke na kuelekea ikulu kwani aibu aliyokuwa nayo ilikuwa kubwa mno na kuhisi kama alipakwa kinyesi usoni.
Haraka sana msafara ukageuka na kuondoka huku waandishi wa habari waliokuwa nje wakipiga picha kila kitu kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
Hiyo ndiyo ilikuwa stori ya siku, gumzo la nchi nyingi kwamba hatimaye mkurugenzi wa Usalama wa Taifa hakuwa na imani na rais wake. Wengi walishangaa lakini kwenye mitandao ya kijamii alipokea sifa kwamba alikuwa mzalendo wa kweli na viongozi wengi walitakiwa kumuunga mkono kwa kile alichokuwa amekifanya.
“Yaani huyu jamaa nilikuwa simpenda, ila kwa hili alilolifanya, hakika yeye ni shujaa,” aliandika jamaa mmoja kwenye akaunti yake Facebook.
“Hata mimi! Huyu jamaa nilikuwa simpendi mno. Duuh! Leo imekuwaje mpaka kabadilika hivi?” alihoji jamaa mwingine kwenye posti hiyo.
Hakukuwa na mtu aliyejua sababu ya Noel kufanya hivyo, hawakujua kama familia yake ilitekwa na alifanya hivyo kama njia mojawapo ya kutaka wasiuawe. Siku hiyohiyo baada ya Noel kumaliza kuzungumza, Godwin akaandika katika akaunti ya Mabadiliko ya Kweli maneno yaliyosema: ‘Asipojiuluzu, atapinduliwa. Sijawahi kusema uongo’, posti ambayo ilizua mijadala mingi kwamba je, ni yeye aliyekuwa nyuma ya hilo? Hakukuwa na mtu aliyejua.
***
Halima alikuwa msichana mrembo, aliyekuwa na mvuto wa kumfanya mwanaume yeyote yule amfuate na kumchombeza kwa maneno matamu. Alikuwa mzungumzaji, alikuwa akizungumza na kila mtu aliyekuja mbele yake. Watu wengi walimpenda kwa kuwa tu hakuwa akijiona, alikuwa msichana ambaye alitoa tabasamu kwa kila mwanaume aliyesimama mbele yake.
Wanawake wengi wa Tandale wakatokea kumchukia, uzuri wake uliwachanganya na wengine kuhisi kwamba msichana huyo angewachukulia wanaume wao. Hawakutaka kumsalimia lakini hilo wala halikuwa tatizo kwa msichana huyo, kitu pekee alichokuwa akikiangalia kilikuwa ni kumpata mtu aliyemfanya kuwa hapo, Godwin.
Wanaume wakapeana taarifa, kama ilivyokuwa kwa mitaa mingine kwamba msichana mrembo anapohamia mtaani basi mitaa mingine wangejua nivyo ilivyotokea kwa Tandale. Wanaume kutoka Manzese, Mwananyamala na Magomeni wakafika mtaani hapo kwa ajili ya kumuona Halima ambaye alikuwa na sifa za kuwa msichana mrembo mno.
Kila aliyemuona, hakujutia muda wake aliopoteza, hakutaka kujuta kwa hatua aliyochukua ya kutoka mtaani kwake mpaka Tandale kwani msichana ambaye alibahatika kumuona siku hiyo aliingia ndani ya kichwa chake na kukiri kwamba Halima alikuwa msichana mrembo mno, msichana ambaye wengine walisema kwamba hakutakiwa kuishi Tandale bali Masaki kulipokuwa na wanaume wenye pesa.
Hakukuwa na mtu aliyejua sababu ya msichana huyo kuwa mahali hapo, wengi wakatamani kujua kwani kila siku asubuhi, alikuwa mtu wa kukaa ndani, hakutoka kwenda sehemu nyingine yoyote, hakuwa akifanya kazi kitu kilichowapa watu maswali mengi.
Vijana wengine wakajitoa kumfuatilia msichana huyo, walitaka kujua alikuwa nani na kwa nini aliamua kwenda kuishi mtaa huo na wakati alikuwa na uzri wa ajabu. Katika kufuatilia kwao wakagundua kwamba msichana huyo alikuwa kimada cha bwana mmoja mwenye pesa ambaye aliamua kumpangishia maeneo ya Tandale kwa kuwa tu hakutaka binti huyo achukuliwe na mwanaume yeyote mwenye pesa.
Mchana alionekana sista duu lakini kwa usiku alikuwa mtu mwingine kabisa, alitulia katika chumba chake huku akiwa na laptop yake akiangalia ni kwa jinsi gani angeweza kumtafuta mtu huyo.
Kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwasiliana na maofisa wa Usalama wa Taifa nchini Uswisi, FIS ambao walikuwa wakimwambia kitu gani cha kufanya na mahali ambapo walikuwa na wasiwasi wa kuwepo kwa mtu huyo.
“Umefikia wapi?” lilikuwa swali la kwanza kabisa.
“Bado ninaendelea kupeleleza, nahisi nitafanikiwa kumpata tu kwani bado nazoeana na watumbalimbali wa mtaa huu,” alisema Halima.
“Sawa. Jitahidi mpaka tufanikiwe.”
“Haina shida!”
Hakuacha kupeleleza huku na kule, alijitahidi kuendelea kuwapeleleza watu wengine ili afahamu mahali mwanaume huyo alipokuwa hapo mtaani. Wakati hayo yote yakiendelea ndipo akatokea kuzoeana na msichana mmoja mrembo ambaye alikuwa akifika sana hapo Fogo, Tandale.
Wakaanza kuzungumza, kwa muonekano, msichana huyo alionekana kuwa msomi kwani kila alipokuwa akifika huko, alikuwa na laptop yake katika begi kitu kilichowafanya kuanza kuzoeana kwa kuwa tu mara ya kwanza walipokutana, walionekana kuvutiana wenyewe.
“Unaitwa nani?” aliuliza msichana huyo.
“Naitwa Angelica,” alidanganya Halima.
“Ooh! Sawa. Mimi naitwa Winfrida!”
“Unaishi huku au?”
“Hapana! Huwa ninakuja kutembelea mpenzi wangu, nyumba hiyo hapo mbele. Anaitwa Godwin. Unamfahamu?” aliuliza Winfrida huku akitoa tabasamu pana.
Halima alipolisikia jina hilo, akashtuka, hakuamini kama kweli Winfrida alilitaja jina la mtu aliyekuwa akitafutwa sana ambaye alimfanya kufika mahali hapo. Alimwangalia msichana huyo mara mbilimbili huku akijiuliza kama lile jina la mtu aliyekuwa ametajwa mbele yake alikuwa ndiye aliyekuwa akimtafuta au mwingine.
“Angelica! Mbona umeduwaa?”
“Ooh! Samahani! Unajua nilikuwa na mpenzi wangu mwenye jina kama la mpenzi wako! Alifariki kwa ajali ya gari mwaka jana,” alisema Halima hapohapo kuyavuta machozi kwa nguvu zake zote na kuanza kulia kiasi kwamba Winfrida akamkumbatia kumpoza pasipo kujua ni kwa jinsi gani msichana huyo alijisikia baada ya kugundua kwamba mtu aliyekuwa akimtafuta, alikuwa mpenzi wake.
****
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania National, Bwana Kambili akawaita wenzake na kuanza kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea. Alikuwa na ushuhuda mkubwa kwamba kwa kila kitu walichokuwa wakikiona kikitokea katika kipindi hicho kilikuwa kimesukwa na mtu aliyeitwa Godwin ambaye alikuwa akitafutwa kila kona duniani.
Wengi hawakumwamini, kwanza walitaka kujua sababu ya kuachiwa kwake na polisi, yeye mwenyewe hakujua zaidi ya kuambiwa kwamba IGP Ng’osha aliamuru atolewe na waandishi wa habari kupewa taarifa. Kila mmoja alishangaa, wengi walimjua Ng’osha, alikuwa mwanaume mwenye roho mbaya kwa watu wa chama pinzani.
“Kwa nini aliruhusu kuondoka, yaani kirahisirahisi tu?” aliuliza katibu wa chama hicho, Bwana Walusanga Ndani.
“Sijajua! Mimi mwenyewe nilishangaa sana! Ila ukiachana na hayo, nimepigiwa simu na mtu anaitwa Godwin,” alisema Kambili.
Hapo ndipo alipoanza kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea na maneno aliyokuwa ameambiwa na mtu aliyempigia simu ambaye alijitambulisha kwa jina la Godwin. Kila mmoja alishangaa, hawakuona kama hilo lingekuwa jambo rahisi kutokea kwani pamoja na yeye kumiliki akaunti ile, pia alimwambia kwamba ndani ya siku chache Rais Bokasa angejiuzulu au kupinduliwa na wao kuchukua uongozi.
“Haiwezekani!”
“Jamani! Mimi ndiyo nimeambiwa hivyo! Tujipangeni kwa ajili ya kuichukua nchi hii,” alisema Kambili.
“Kuna ishara gani ambayo inaweza kutufanya tumuamini?” aliuliza Ndaki, alitaka kuamini baada ya kuona na si kuamini baada ya kuambiwa.
Kambili akawaambia kwamba kesho kungekuwa na kiongozi mmoja ambaye angewaita waandishi wa habari na kuwaambia kwamba hakuwa na imani na rais na hivyo kujitoa katika uongozi huo. Hakutakiwa kuwaambia ni kiongozi gani ila walitakiwa kujua kwamba kungekuwa na mtu ambaye angewaita waandishi wa habari na kuwaambia hivyo.
Hilo kidogo likawafanya viongozi hao kusubiri kuona kama jambo hilo lingetokea ili waanze kuamini. Siku hiyo ilipofika, wakaambiwa kwamba Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Bwana Noel alikuwa amewaita waandishi wa habari Habari Maelezo kwa kuwa kuna jambo alitaka kuzungumza nao.
Kilichotokea ndicho kilichowafanya kuamini kama Godwin angeweza kuwapeleka mpaka ikulu kwani kwa maneno tu kutoka kwa Kambili hawakuwa wameamini lakini kwa kile ambacho waliambiwa na kutokea, waliamini kwamba walikuwa wakienda ikulu, tena njia ilikuwa nyeupe kabisa, ishu ilikuwa ni kwao tu kujipanga na kwenda huko.
“Jamani! Iteni mikutano mzungumze na watu, waambieni kwamba tunakwenda ikulu. Kama tutakamatwa na kuuawa, acha tuuawe lakini tukawaambieni kwamba tunajiandaa kwenda ikulu,” alisema Kambili huku akiwaangalia wenzake kwa umakini kabisa kwani kwa jinsi alivyopigwa na macho yake kuvimba, hakuwa akiona vizuri.
“Tutafanya hivyo! Nadhani napo ni muda wa kupanga nani atakuwa makamu wa rais na nani atakuwa waziri mkuu!” alisema Ndani huku akionekana kuwa na hamu ya madaraka.
“Hilo tutapanga tukionana naye! Nadhani ni njia moja ya kufanikiwa katika hili. Nitawasiliana naye, nitapokea maelekezo kutoka kwake!” alisema Kambili.
****
Rais Bokasa alikuwa amechanganyikiwa, hakuamini kilichokuwa kimetokea, moyo wake ulimuuma, ulichoma kama mkuki, mtu ambaye alimwamini kwa nguvu zote, ambaye alikuwa akijua siri kubwa kutoka ikulu alikuwa amemkataa, hakutaka kufanya naye kazi kwa kuwa hakuwa na imani naye.
Hakutaka kukubali, alichokijua ni kwamba kulikuwa na mtu mwingine nyuma ya pazia ambaye alimshawishi kufanya jambo kama hilo, kwa sababu wanawake walikuwa na nguvu kwa waume zao, akataka kumtumia mkewe, Bi Stela kwa ajili ya kumshawishi mumewe na hatimaye kurudisha moyo nyuma.
Akamtuma Waziri mkuu mpaka nyumbani kwa Noel kwa lengo la kuzungumza naye lakini baada ya kufika huko akapewa taarifa kutoka kwa vijana wa Usalama wa Taifa waliokuwa wakilinda nyumba huyo kwamba hiyo ilikuwa siku ya pili mwanamke huyo hakuwa ameonekana.
“Amekwenda wapi?”
“Hatujui! Mumewe hataki kuzungumzia suala hilo hata kidogo,” alisema Andrew.
Waziri mkuu hakutaka kubaki nje, alichokifanya ni kuingia ndani kwa lengo la kuzungumza na Noel. Akakaribishwa mpaka ndani ambapo dada wa kazi akaenda kumuita bosi wake ambaye ndani ya dakika mbili, tayari alikuwa sebuleni.
Kwa jinsi macho yake yalivyoonekana, alionyesha kulia sana, yalikuwa mekundu huku kila wakati akivuta mafua yake kwa ndani. Waziri mkuu alibaki akimshangaa, hakujua kilichokuwa kikiendelea ila alihisi kwamba kulikuwa na jambo.
“Kuna nini?” aliuliza.
“Mheshimiwa Godson! Moyo wangu unaniuma sana,” alisema Noel huku akimwangalia waziri mkuu huyo.
“Kuna nini? Niambie kijana wangu. Umefanya maamuzi ya ghafla sana, niambie kuna nini,” alisema Bwana Godson.
“Ninaipenda sana familia yangu! Nadhani unajua hilo!” alisema.
“Ndiyo!”
“Nilikuwa tayari kufanya kila kitu kwa ajili yao.”
“Ndiyo!”
“Familia yangu siioni, sijajua ipo wapi! Ni ghafla tu siioni ndani, walinzi walisema aliondoka, alipokwenda, hakurudi, nimechanganyikiwa sana,” alisema Noel, akaanza kulia tena.
“Imetekwa?”
“Sijajua! Sijui chochote kile.”
“Niambie ukweli!”
“Sijui mkuu!”
Walizungumza mambo mengi, Bwana Godson alimuomba sana Noel arudi katika nafasi yake lakini mwanaume huyo alikataa na kusema kwamba siku zote angeendelea kubaki na msimamo wake, hakutaka tena kusikia kuhusu uongozi huo.
“Ni nani yupo nyuma yako?”
“Hakuna mtu, ila kurudi, siwezi kwa kweli,” alisema Noel.
Hakukuwa na kitu cha kumbadilisha, alibaki na msimamo wake kwamba kusingekuwa na kitu chochote cha kumrudisha kwani aliamini kwamba kama angefanya hivyo basi familia yake ingeweza kuuawa. Aliogopa na alipanga kubaki kwenye msimamo wake uleule mpaka pale ambapo angeona ni kitu gani kingeendelea baada ya hapo.
Baada ya siku mbili kupita huku kila mtu akiwa na maswali mengi juu ya uamuzi alioufanya Noel, mara waandishi wa habari wakapigiwa simu na Bilionea Kizota na kuambiwa kwamba walitakiwa kuonana naye nyumbani kwake kwani kulikuwa na mambo mengi alitaka kuzungumza nao.
“Bilionea Kizota? Kuna nini tena?” aliuliza mwandishi mmoja.
“Hatujui! Ila twendeni jamani. Si unajua yule ndiyo ameshikilia uchumi wa wafanyabiashara wengi. Twendeni,” alisema mwandishi mmoja, zaidi ya waandishi hamsini kutoka kwenye magazeti, mitandao na sehemu nyingine wakaanza kwenda huko, kila mmoja alikuwa akijiuliza ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, walittaka kujua kama ni yaleyale kama ya Noel au yalikuwa mengine.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane siku zijazo.
Lini tena
 
Jamani leteni mwendelezo huku, tumesharejea home
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom