Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
- Thread starter
- #961
SEHEMU YA 99
“Mmejifunza wapi Kiingereza?” aliuliza mwanafunzi mmoja aliyejulikana kwa jina la Amina.
“Tulipotoka!” alijibu Godwin.
“Aisee mnaongea vizuri sana. Nifundishe na mimi!”
“Nitakufundishaje sasa Amina? Huwezi kufahamu lugha pasipo kuiongea, wewe tuongee na utaifahamu mbele ya safari,” alijibu Godwin ambaye kwa kumwangalia, alionekana kuwa kijana mpole kupita kawaida.
Maisha yalikuwa ni tofauti, walizoea kula chakula kizuri katika shule waliyotoka lakini ndani ya shule hiyo, maisha yalionekana kuwa magumu mno.
Hawakuviona vyakula walivyokuwa wakila walipotoka, kila chakula walichokitaka ilikuwa ni lazima kulipia tofauti na kule ambapo gharama zilijumuishwa katika ada yao ya mwaka.
Mbali na kufahamu Lugha ya Kiingereza, pia walikuwa hatari katika somo la Kiswahili na Hisabati. Walifanya vizuri, walifaulu katika majaribio waliyokuwa wakipewa kila wiki.
Wakawa maarufu shuleni hapo, watu waliwafahamu kutokana na uwezo wao mkubwa waliokuwa nao kwenye masomo. Wanafunzi wengi waliwafuata na kuhitaji kufundishwa, hawakujiona, walijiona kuwa sawa na wanafunzi wote waliokuwa shuleni hapo.
Wakati hayo yote yakiendelea, bado Rosemary alijiona kuwa kwenye wakati mgumu, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea katika maisha yake. Moyo wake ulimuuma mno, kupoteza kila kitu lilikuwa pigo kubwa ambalo hakulitegemea kabisa.
Baada ya mwezi mmoja tangu ahamie Tandale hatimaye akapoka barua kutoka kwa mwalimu mkuu ambaye alipewa na serikali ambayo ilimfuta kazi ya ualimu shuleni hapo.
Alipoipokea na kuisoma, hakuamini kama kweli yeye ndiye aliyeandikiwa barua ile. Iliandikwa kwamba hakutakiwa kufundisha shuleni hapo, hakukuwa na sababu yoyote ya maana, ila kwa kifupi iliandikwa kwamba kulingana na matumizi makubwa, serikali iliamua kupunguza wafanyakazi wake.
“Nini? Nimefukuzwa kazi?” aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
Hakutaka kukubali, hapohapo akatoka ofisini na kwenda katika ofisi ya mwalimu mkuu, alipofika, akaambiwa asubiri kwenye benchi. Ndani ya dakika tano, akaambiwa aingie ndani.
“Mmejifunza wapi Kiingereza?” aliuliza mwanafunzi mmoja aliyejulikana kwa jina la Amina.
“Tulipotoka!” alijibu Godwin.
“Aisee mnaongea vizuri sana. Nifundishe na mimi!”
“Nitakufundishaje sasa Amina? Huwezi kufahamu lugha pasipo kuiongea, wewe tuongee na utaifahamu mbele ya safari,” alijibu Godwin ambaye kwa kumwangalia, alionekana kuwa kijana mpole kupita kawaida.
Maisha yalikuwa ni tofauti, walizoea kula chakula kizuri katika shule waliyotoka lakini ndani ya shule hiyo, maisha yalionekana kuwa magumu mno.
Hawakuviona vyakula walivyokuwa wakila walipotoka, kila chakula walichokitaka ilikuwa ni lazima kulipia tofauti na kule ambapo gharama zilijumuishwa katika ada yao ya mwaka.
Mbali na kufahamu Lugha ya Kiingereza, pia walikuwa hatari katika somo la Kiswahili na Hisabati. Walifanya vizuri, walifaulu katika majaribio waliyokuwa wakipewa kila wiki.
Wakawa maarufu shuleni hapo, watu waliwafahamu kutokana na uwezo wao mkubwa waliokuwa nao kwenye masomo. Wanafunzi wengi waliwafuata na kuhitaji kufundishwa, hawakujiona, walijiona kuwa sawa na wanafunzi wote waliokuwa shuleni hapo.
Wakati hayo yote yakiendelea, bado Rosemary alijiona kuwa kwenye wakati mgumu, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea katika maisha yake. Moyo wake ulimuuma mno, kupoteza kila kitu lilikuwa pigo kubwa ambalo hakulitegemea kabisa.
Baada ya mwezi mmoja tangu ahamie Tandale hatimaye akapoka barua kutoka kwa mwalimu mkuu ambaye alipewa na serikali ambayo ilimfuta kazi ya ualimu shuleni hapo.
Alipoipokea na kuisoma, hakuamini kama kweli yeye ndiye aliyeandikiwa barua ile. Iliandikwa kwamba hakutakiwa kufundisha shuleni hapo, hakukuwa na sababu yoyote ya maana, ila kwa kifupi iliandikwa kwamba kulingana na matumizi makubwa, serikali iliamua kupunguza wafanyakazi wake.
“Nini? Nimefukuzwa kazi?” aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
Hakutaka kukubali, hapohapo akatoka ofisini na kwenda katika ofisi ya mwalimu mkuu, alipofika, akaambiwa asubiri kwenye benchi. Ndani ya dakika tano, akaambiwa aingie ndani.