Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

SEHEMU YA 102

Hakukuwa na maisha ya raha wala furaha, majonzi ambayo alikuwa nayo tangu mumewe afariki dunia ndiyo yaliendelea kila siku. Umasikini ukaanza kumnyemelea Rosemary na familia yake.

Alijaribu kuwafuata ndugu zake na ndugu wa mume kwa ajili ya kuwaomba msaada lakini wakati huo kila mmoja alimkimbia, hakutaka kumsaidia, hawakukumbuka wema waliokuwa wakifanyiwa na familia ya Mzee Mapoto, kwao, chuki na majivuno yalitawala moyo yao.

Hilo lilikuwa pigo kubwa kwa Rosemary, hakuwa na pesa ya kutosha na ilikuwa ni lazima ailee familia yake, watoto wake waliokuwa kidato cha tatu waendelee kusoma lakini hakujua angepata vipi pesa.

Alipokwenda benki kuchukua pesa zilizobaki, akakuta akaunti yake ikiwa imefugwa na alipouliza, hakupewa majibu ya kuridhisha hata kidogo. Mkononi hakuwa na kitu, alikuwa mweupe kabisa, shilingi elfu ishirini aliyokuwa nayo ndiyo fedha pekee iliyobaki ambayo ilitakiwa kuyaendesha maisha yake na familia yake.

Alilia, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya. Kwa kuwa alikuwa uswahilini, akaanzisha genge siku hiyohiyo. Ulikuwa ni uamuzi wa haraka, watu walimshangaa, waliomfahamu, walimuonea huruma kwani alishuka chini kabisa na kuanza maisha ambayo hakuwahi kufikiria hata siku moja kwamba angeyaishi.

Godwin na Irene waliporudi nyumbani, walishangaa, mama yao alibadilika zaidi, walijua kwamba alikuwa na mawazo tele, moyo wake uliumia lakini siku hiyo alionekana kuwa tofauti kabisa.

Godwin akamfuata mama yake na kumuuliza kilichofanya kuwa katika hali hiyo lakini mwanamke huyo hakumjibu chochote zaidi ya kutoka nje na kwenda gengeni.

“Hili genge ni letu?” aliuliza Godwin huku akionekana kushangaa.
“Ndiyo!”
“Umelijenga leo?”
“Ndiyo!”
Godwin aliumia mno, hakuongea tena, akaelekea ndani na kulala kitandani. Moyo wake ulimuuma mno, aliyakumbuka maisha ya raha waliyokuwa wakiishi zamani, aliyakumbuka maisha ya nchini Marekani baba yake alipokuwa hai, kitendo cha kutoka katika maisha yale na kuwa na maisha waliyokuwa nayo yalikuwa ni mabadiliko ya haraka ambayo hakuamini kama kungekuwa na mtu mwingine duniani ambaye angekuwa na mabadiliko ya maisha kwa haraka kama waliyokuwa nayo
 
SEHEMU YA 103

Moyo wake ukawaka kwa hasira, alijua dhahiri kwamba kulikuwa na mtu aliyesababisha hayo yote. Roho ya kichungaji aliyokuwa nayo, ikatoka, akagubikwa na hasira nzito, hasira ya kisasi ambayo aliamini kwamba ni lazima ahakikishe wale waliowafanya kuwa katika hali ile wanakufa mara moja.

Hakutaka kuwa na huruma tena, aliikumbuka mistari kadhaa ya Biblia iliyohusu ghadhabu kali ya Mungu kwa mtu atakayelipiza kisasi, alijua fika kwamba kisasi chochote kile kilitakiwa kuachwa kwa Mungu aliye hai.

Hakutaka kukubali, aliona kama Mungu akichelewa kulipa kisasi, iwe isiwe ilikuwa ni lazima kulipa kisasi kwa mikono yake mwenyewe.
“Mungu! Nimekutumikia tangu nikiwa mdogo, nilitamani sana niwe mchungaji kama Bonke, ila siwezi, sitaki kuwa mchungaji tena, ni lazima niwe muuaji kwa kila mtu aliyemfanya mama yangu kuwa katika hali hii,” alisema Godwin kwa hasira huku machozi yakimtoka.

Walipaswa kumsaidia mama yao kazi ya kuuza genge. Kila walipokuwa wakitoka shuleni, walifikia kuuza genge. Mwanzoni walijisikia aibu lakini kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele, walizoea na hatimaye kukubaliana na hali halisi kwamba yale yalikuwa maisha yao.

“Amina! Natakiwa kurudi nyumbani haraka sana,” alisema Godwin, alikuwa akimwambia rafiki wake wa kike aliyeitwa Amina.
“Ila si mara moja tu! Tunakwenda halafu tutawahi kurudi!” alisema msichana huyo.

“Hapana! Tufanye siku nyingine. Siwezi kumuacha mama akiuza genge peke yake,” alisema Godwin.
“Lakini Irene si yupo?”
“Haijalishi! Na yeye pia anatakiwa kupumzika Amina,” alisema Godwin.
“Please!” (tafadhali)
“Am I understood?” (nimeeleweka?)
“A little bit,” (kidogo tu)

Amina alisimama akimwangalia Godwin, alimpenda mvulana huyo lakini alishindwa kumwambia ukweli. Alikuwa kijana mpole ambaye hakuonekana kuzungumza jambo lolote kuhusu mahusiano ya kimapenzi.

Alijaribu kumuonyeshea ishara zote kwamba alikuwa akimpenda lakini Godwin hakuonekana kabisa kuelewa. Alikuwa bize na masomo, maisha ya nyumbani kwao yalikichanganya mno kichwa chake.
 
Ona sasa watu hawa si wema kabisa, yaani wamesababisha hata mtoto Godwini mwenye moyo wa upole awe na moyo wa maangamizi na visasi.! Eee Mungu msaidie mtoto huyu ugeuza moyo wake wa upole, upendo na huruma.!!
 
SEHEMU YA 103

Moyo wake ukawaka kwa hasira, alijua dhahiri kwamba kulikuwa na mtu aliyesababisha hayo yote. Roho ya kichungaji aliyokuwa nayo, ikatoka, akagubikwa na hasira nzito, hasira ya kisasi ambayo aliamini kwamba ni lazima ahakikishe wale waliowafanya kuwa katika hali ile wanakufa mara moja.

Hakutaka kuwa na huruma tena, aliikumbuka mistari kadhaa ya Biblia iliyohusu ghadhabu kali ya Mungu kwa mtu atakayelipiza kisasi, alijua fika kwamba kisasi chochote kile kilitakiwa kuachwa kwa Mungu aliye hai.

Hakutaka kukubali, aliona kama Mungu akichelewa kulipa kisasi, iwe isiwe ilikuwa ni lazima kulipa kisasi kwa mikono yake mwenyewe.
“Mungu! Nimekutumikia tangu nikiwa mdogo, nilitamani sana niwe mchungaji kama Bonke, ila siwezi, sitaki kuwa mchungaji tena, ni lazima niwe muuaji kwa kila mtu aliyemfanya mama yangu kuwa katika hali hii,” alisema Godwin kwa hasira huku machozi yakimtoka.

Walipaswa kumsaidia mama yao kazi ya kuuza genge. Kila walipokuwa wakitoka shuleni, walifikia kuuza genge. Mwanzoni walijisikia aibu lakini kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele, walizoea na hatimaye kukubaliana na hali halisi kwamba yale yalikuwa maisha yao.

“Amina! Natakiwa kurudi nyumbani haraka sana,” alisema Godwin, alikuwa akimwambia rafiki wake wa kike aliyeitwa Amina.
“Ila si mara moja tu! Tunakwenda halafu tutawahi kurudi!” alisema msichana huyo.

“Hapana! Tufanye siku nyingine. Siwezi kumuacha mama akiuza genge peke yake,” alisema Godwin.
“Lakini Irene si yupo?”
“Haijalishi! Na yeye pia anatakiwa kupumzika Amina,” alisema Godwin.
“Please!” (tafadhali)
“Am I understood?” (nimeeleweka?)
“A little bit,” (kidogo tu)

Amina alisimama akimwangalia Godwin, alimpenda mvulana huyo lakini alishindwa kumwambia ukweli. Alikuwa kijana mpole ambaye hakuonekana kuzungumza jambo lolote kuhusu mahusiano ya kimapenzi.

Alijaribu kumuonyeshea ishara zote kwamba alikuwa akimpenda lakini Godwin hakuonekana kabisa kuelewa. Alikuwa bize na masomo, maisha ya nyumbani kwao yalikichanganya mno kichwa chake.
SEHEMU YA 102

Hakukuwa na maisha ya raha wala furaha, majonzi ambayo alikuwa nayo tangu mumewe afariki dunia ndiyo yaliendelea kila siku. Umasikini ukaanza kumnyemelea Rosemary na familia yake.

Alijaribu kuwafuata ndugu zake na ndugu wa mume kwa ajili ya kuwaomba msaada lakini wakati huo kila mmoja alimkimbia, hakutaka kumsaidia, hawakukumbuka wema waliokuwa wakifanyiwa na familia ya Mzee Mapoto, kwao, chuki na majivuno yalitawala moyo yao.

Hilo lilikuwa pigo kubwa kwa Rosemary, hakuwa na pesa ya kutosha na ilikuwa ni lazima ailee familia yake, watoto wake waliokuwa kidato cha tatu waendelee kusoma lakini hakujua angepata vipi pesa.

Alipokwenda benki kuchukua pesa zilizobaki, akakuta akaunti yake ikiwa imefugwa na alipouliza, hakupewa majibu ya kuridhisha hata kidogo. Mkononi hakuwa na kitu, alikuwa mweupe kabisa, shilingi elfu ishirini aliyokuwa nayo ndiyo fedha pekee iliyobaki ambayo ilitakiwa kuyaendesha maisha yake na familia yake.

Alilia, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya. Kwa kuwa alikuwa uswahilini, akaanzisha genge siku hiyohiyo. Ulikuwa ni uamuzi wa haraka, watu walimshangaa, waliomfahamu, walimuonea huruma kwani alishuka chini kabisa na kuanza maisha ambayo hakuwahi kufikiria hata siku moja kwamba angeyaishi.

Godwin na Irene waliporudi nyumbani, walishangaa, mama yao alibadilika zaidi, walijua kwamba alikuwa na mawazo tele, moyo wake uliumia lakini siku hiyo alionekana kuwa tofauti kabisa.

Godwin akamfuata mama yake na kumuuliza kilichofanya kuwa katika hali hiyo lakini mwanamke huyo hakumjibu chochote zaidi ya kutoka nje na kwenda gengeni.

“Hili genge ni letu?” aliuliza Godwin huku akionekana kushangaa.
“Ndiyo!”
“Umelijenga leo?”
“Ndiyo!”
Godwin aliumia mno, hakuongea tena, akaelekea ndani na kulala kitandani. Moyo wake ulimuuma mno, aliyakumbuka maisha ya raha waliyokuwa wakiishi zamani, aliyakumbuka maisha ya nchini Marekani baba yake alipokuwa hai, kitendo cha kutoka katika maisha yale na kuwa na maisha waliyokuwa nayo yalikuwa ni mabadiliko ya haraka ambayo hakuamini kama kungekuwa na mtu mwingine duniani ambaye angekuwa na mabadiliko ya maisha kwa haraka kama waliyokuwa nayo



Smart911
 
SEHEMU YA 104

Siku hiyo ya Jumamosi Amina alimwambia kwamba alitaka kwenda naye katika Ufukwe wa Coco lakini kijana huyo hakutaka kabisa kumuelewa.

Alimwambia wazi kwamba alitakiwa kurudi nyumbani baada ya mitihani ya wiki kumalizika,
Amina aliumia lakini hakuwa na jinsi kwani hata Godwin alivyokuwa akionekana, ilionyesha kabisa hakuwa sawa.

Hakumbishia, akabaki akimwangalia wakati Godwin akiungana na Irene kurudi naye nyumbani.
Njiani, kila mmoja alikuwa kimya, walisoma tu kwa sababu walihitajika kusoma lakini ukweli wa mambo ni kwamba vichwa vyao havikuwa sawa kabisa. “Irene!” aliita Godwin.
“Abee!”

“Kuna mtu amesababisha haya yote, katika kila kitu kinachotokea, kuna mkono wa mtu,” alisema Godwin huku akimwangalia Irene.
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Maisha yamebadilika kwa kasi sana.

Hakuna mabadiliko yanayotokea kwa kasi namna hii! Umesoma historia, ni nani alikuwa na maisha yenye mabadiliko ya kasi kama yetu? Hakuna kabisa, nina uhakika hapa kuna mkono wa mtu,” alisema Godwin huku akimwangalia Amina.

“Tumuachie Mungu tu!
“Tumuachie Mungu? Yaani Mungu ashuke aje kudili na watu hao?” aliuliza Godwin.
“Sasa tutafanyaje?”

“Irene! Tutachelewa! Sijaona sababu ya kumsubiri Mungu na kudili na watu hao na wakati ametupa nguvu, akili, sasa unahisi Mungu ametupa za nini? Kukaa nazo tu?” aliuliza Godwin.

“Sijakuelewa unamaanisha nini?”
“Ni lazima tuue!”
“Tuue?”
“Irene! Hiyo ndiyo njia rahisi ya kufanya. Ili amani ipatikane, ni lazima tuue kama kisasi kwa kile tulichofanyiwa!” alisema Godwin huku akimwangalia Irene.

“Tumeokoka lakini!”
“Sizungumzii wokovu! Nazungumzia mauaji!
“Godwin!”
“Irene! Wakati mwingine amani inatakiwa kupatikana kupitia vita! Utakuwa tayari kuua?” aliuliza Godwin.

“Siwezi kuua!”
“Mimi nitaua! Nitakapomgundua mtu aliyesababisha haya yote, nitaua!” alisema Godwin.

Irene hakumuunga mkono Godwin, alibaki kimya huku akimwangalia.

Alimuona Godwin ambaye hakumzoea kabisa katika maisha yake, alibadilika, roho ya kutamani kuwa mchungaji iliondoka moyoni mwake na kuingiwa na roho ya kutamani kuua.
 
SEHEMU YA 105

Kila alipokaa, alifikiria ni kwa jinsi gani angefanya mauaji. Alijua dhahiri kwamba kwa kila kitu kilichokuwa kimetokea, kulikuwa na mtu aliyesababisha hayo yote.

Irene hakutaka kumwambia mama yake, alinyamaza huku kila alipokuwa akimwangalia Godwin manano yale aliyomwambia yaliendelea kujirudia kichwani mwake.

Maisha yaliendelea, walizidi kupigika, wakati mwingine biashara ya genge ilikuwa ngumu, walilala bila kula, walivumilia kwa kuamini kwamba kuna siku maisha yangekuwa na uafadhali kama kipindi cha nyuma lakini hilo halikuweza kutokea.

Baada ya kuishi kwa miezi sita, hatimaye kodi ya nyumba ikamalizika na hivyo mwenye nyumba kumuita Rosemary na kumpa taarifa kwamba alitakiwa kulipa.
“Nitalipa mwisho wa mwezi huu!” alisema Rosemary.

“Sawa. Usiniangushe basi!”
“Haina shida baba!”
Hakujua ni kwa namna gani angepata kodi hiyo, biashara ilikuwa ngumu na kila alipoifanya, pesa aliyoipata ilikuwa ni ya kula tu.

Aliamini kwamba ni lazima angefukuzwa nyumbani hapo na famiia yake hakutaka hilo litokee, alitamani kulizuia lakini hakuwa na jinsi.

Baada ya mwezi kumalizika, baba mwenye nyumba akamfuata na kuhitaji pesa yake ya kodi, hakuwa nayo na hivyo kuwapa saa arobaini na nane kuondoka nyumbani hapo.

Hawakuwa na pa kwenda, Rosemary aliyafikiria maisha yake baada ya hapo. Saa arobaini na nane ambazo ni sawa na siku mbili zilipomalizika, wakafukuzwa nyumbani hapo.

Rosemary alilia, aliomba msaada wa kuongezewa siku lakini mwenye nyumba hakutaka kuwaelewa. Watu walikusanyika, waliwaonea huruma lakini hawakujua ni kwa jinsi gani wangeweza kumsaidia.

Hawakuchukua kitanda, walichukua baadhi ya vyombo vyao vya chakula na kuondoka nyumbani hapo. Waliviinamisha vichwa vyao, kila mmoja alikuwa akilia.

Godwin alizidi kuwa na hasira tele, maisha waliyokuwa wakiyapitia yalimfanya kuwa na hasira zaidi juu ya mtu aliyesababisha wao kuwa mahali hapo.

“Nitamuua! Nitamuua mtu yeyote aliyesababisha haya!” alisema Godwin, wakati huo walikuwa njiani wakielekea Mwananyamala, hawakujua ni mahali gani walitakiwa kwenda kuishi.

Waliamini kama wangefika huko, wangejua sehemu ya kuishi, hata kama ingekuwa barabarani, kwao kusingekuwa na shida yoyote ile.
 
Kama Shunie akiniruhusu hii hadithi niwe natupia ndefundefu kila siku!
 
SEHEMU YA 106

Rosemary akiwa na watoto waliendelea na safari ya kuelekea Mwananyamala. Japokuwa walikuwa wakipita barabarani, hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba walikuwa wao.

Walichoka, maisha yaliwapiga kupita kawaida.
Walikuwa na utofauti mkubwa na wa zamani, walionekana watu dhaifu waliopitisha siku nyingi bila kula. Ilikuwa ni aibu kwa Rosemary, wakati mwingine alikuwa akichukua khanga yake na kuufunika kidogo uso wake.

Safari yao hiyo iliishia Mwananyamala karibu kabisa na hospitali ambapo kwa pembeni kulikuwa na mti mkubwa huku kukiwa na watu waliokuwa wakitengeneza masofa.

Wakatulia chini ya mti huo, hawakutaka kugundulika hivyo muda wao mwingi walificha sura zao. Walitaka kulala pembeni ya ukuta wa hospitali hiyo, hawakuwa na sehemu ya kwenda, kutoka katika maisha ya kifahari na kutamani hata kulala nje ya hospitali hiyo kwao yalikuwa mabadiliko makubwa mno.

Wakati wakiwa mahali hapo, muda mwingi watu waliokuwa wakipita karibu na eneo hilo walikuwa wakiwaangalia sana. Walishangaa, kwa eneo hilo haikuwahi kutokea hata siku moja watu wa mitaani au hata machokoraa kwenda kukaa mahali hapo.


Rosemary akagundua kwamba kama wangeendelea kukaa mahali hapo ilikuwa ni lazima wagundulike kama walikuwa wao, hivyo walichokifanya ni kuondoka huku tayari ikiwa saa kumi na mbili jioni.


Walipotaka kwenda ilikuwa ni Mikocheni. Rosemary alikumbuka kwamba zamani alipokuwa akipita kwa gari huko aliwaona wanawake wakiwa na watoto wao wakiishi mitaani kwa kujenga kibanda na kuendelea kuishi. Kama walivyokuwa watu hao, na yeye alitaka kwenda huko na watoto wake kwa ajili ya kuyaanza maisha hayo.


Kutoka Mwananyamala mpaka Mikocheni ilikuwa ni umbali mrefu, walipita katika njia ya Mtaa wa Mama Zakaria ambapo waliunganisha nayo mpaka Makumbusho.


Hapo, wakasonga mbele mpaka walipofika Sayansi ambapo wakachukua njia inayoelekea Rose Garden ambapo kwa mbele kidogo wakaachana na barabara ya lami na kuchukua barabara ya vumbi ambayo iliwapeleka mpaka sehemu iliyokuwa wazi, majani mengi kidogo ambapo hapo ndipo walipotaka kuyaanza maisha yao upya.......
 
SEHEMU YA 107

“Hapahapa panatosha,” alisema Rosemary huku akiliweka chini begi lake la nguo.
“Mama! Tunafanya nini hapa?” aliuliza Godwin.

“This is our new home,” (hapa ni nyumbani kwetu kupya!)
“A new home?” (nyumbani kupya?)
“Ndiyo!”

Hiyo ndiyo ilikuwa nyumba yao mpya, hawakubishana na mama yao, alikuwa mwanamke shupavu ambaye alikuwa tayari kupambana kwa ajili ya watoto wake hao.

Kwa kuwa giza lilikwishaanza kuingia, Rosemary akatandika kanga chini kwa lengo la kulala. Hakukuwa na mtu aliyelala, kila mmoja alikuwa akiyafikiria maisha yake, jinsi walipotoka mpaka kuwa mahali hapo.


Yalikuwa ni maisha yaliwaumiza, yaliyowasikitisha ambapo kwa Godwin kila siku alijiapiza kwamba ni lazima alipe kisasi, hata kama ingechukua miaka mingapi.

Walikesha, ilipofika asubuhi, wakatoa vyombo vyao vya kupikia. Kila mtu aliyekuwa akipita mahali hapo aliwashangaa, watu wengine, matajiri waliokuwa wakielekea kazini walisimamisha magari yao na kuanza kuiangalia familia hiyo.

Hilo liliwashangaza kila mmoja. Huo ulikuwa mtaa wa matajiri, kila jumba lililojengwa lilikuwa la kifahari, hawakujua watu hao walitoka wapi na kwa nini waliamua kuhamia hapo na wakati kulikuwa na sehemu nyingi za watu masikini ambapo wangeweza kwenda.


Hakukuwa na mtu aliyejua kwamba hiyo ilikuwa familia ya Mapoto. Kila walipokuwa wakimwangalia Rosemary, alijitahidi sana kuuficha uso wake, hakutaka mtu yeyote agundue kama wameanza maisha mapya.

Hakukuwa na shule tena, Irene na Godwin walitakiwa kusahau kila kitu kuhusu kusoma na kilichokuwa kimefuata ni kuendelea kuishi maisha ya mtaani huku wakitakiwa kutoka nyumbani na kwenda mitaani kuomba kwa ajili ya pesa za kumsaidia mama yao.


“Irene! Tumekuwa ombaomba mitaani! Kweli?” aliuliza Godwin, alikuwa amechanganyikiwa kupita kawaida.

“Godwin! Kila kitu kinatokea kwa sababu, hujui ni sababu gani imemfanya Mungu kuamua kutupa maisha haya, cha msingi ni kumshukuru kwa kila jambo,” alisema Irene.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom