Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

SEHEMU YA 95

Hakukuwa na siri tena, watu wa serikalini wakagundua kwamba mtu aliyenunua nyumba ya Mapoto hakuwa Othman kama ilivyojulikana bali alikuwa Bilionea Matiku ambaye hakutaka kujulikana.

Hilo lilionekana kuwa tatizo, watu ambao walitaka kumuona Rosemary akiteseka hawakutaka kubaki kimya, walichokifanya ni kumuita Othman kwa ajili ya kuzungumza naye.

Walitaka kufahamu utajiri wake mkubwa aliokuwa nao mpaka kununua nyumba hiyo. Biashara zake hazikuwa kubwa, hawakuamini kama angeweza kununua nyumba hiyo kwa bei kubwa. Alipofuatiliwa zaidi kuhusu biashara zake akagundulika kwamba hakuwa mnunuaji wa nyumba hiyo.

Akakamatwa na kuwekwa selo, huko, akalazimishwa kusema mtu aliyekuwa nyuma ya mpango wa kununua nyumba ile. Waliomuuliza ni kama hawakuwa wakifahamu lakini ukweli ni kwamba walifahamu kila kitu, walijua kwamba Bilionea Matiku ndiye aliyetoa kiasi cha fedha kununua nyumba hiyo.

Walikasirika, walitaka kumuonyesha Matiku kwamba walikuwa na nguvu hivyo walichokifanya ni kuanza kumsumbua katika biashara zake. Magari ya kampuni zake yalikuwa yakikamatwa hovyohovyo, alipandishiwa kodi kubwa bila sababu maalumu. Kila alipokuwa, alikuwa akifuatiliwa, kila alichokuwa akikifanya ripoti ilipelekwa katika kitengo cha juu.

Baada ya siku kadhaa, polisi wakatumwa kwenda kumkamata kwa kisingizio cha kufahamu kwamba alikuwa akifahamu kuhusu mauaji ya Juma yaliyokuwa yamefanyika Kawe.

“Hamuwezi kuja kunikamata kiholelaholela tu kama mmekuja kumkamata mbeba mizigo sokoni,” alisema Matiku huku akiwaangalia polisi waliofika nyumbani kwake.

“Unafikiri mabilionea wapo juu ya sheria?” aliuliza polisi mmoja.
“Arrest warrant yenu ipo wapi?” aliuliza Matiku.
“Hii hapa!’

Matiku akaichukua na kuanza kuangalia, akaisoma na kukubaliana nao kwamba alitakiwa kwenda nao kituo cha polisi.

Hata kabla hajafika mbali akawasiliana na mwanasheria wake kwa ajili ya kufika kituoni ili hata kama kingetokea kitu chochote kile, ajue nini cha kufanya.
 
SEHEMU YA 96

Njiani, hakukuwa na mtu aliyezungumza lolote lile, kila mmoja alikuwa kimya. Kumkamata Bilionea Matiku ilikuwa ni amri kutoka ngazi ya juu hivyo walitakiwa kumkamata kwa gharama yoyote ile.
Alipofikishwa katika Kituo Kikuu cha Polisi, akapelekwa katika chumba maalum cha mahojiano na kuanza kuhojiwa, kwa kuwa lengo lao lilikuwa ni kumlaza kituoni hapo, wakamlaza.

Matiku alijua kwamba kulikuwa na mtu nyuma aliyekuwa akifanya mambo hayo yote, aligundua kwamba sababu ya mambo hayo ni kwa sababu tu alimsaidia mwanamke mjane wa Mapoto ambaye alikuwa akichukiwa na serikali iliyokuwa madarakani kipindi hicho.

Kukamatwa kwake ikawa ni stori kubwa, kila mtu akaanza kulizungumzia jambo hilo, wengi waliona kabisa kwamba polisi walitumwa kwani kwa sababu iliyowekwa wazi kwamba ndiyo iliyosababisha bilionea huyo kukamatwa haikuonekana kuwa na mashiko hata kidogo.

“Huu ni uonevu ujue,” alisema jamaa mmoja.
“Kwani geni lipi? Au umetusahau Waafrika?” aliuliza jamaa mwingine.
Wakati Bilionea Matiku akisota sero ndicho kipindi ambacho Rosemary alikuwa nje na watoto wake, hakujua ni sehemu gani alitakiwa kwenda. Moyo wake ulikuwa kwenye majonzi mazito, hakuamini kile kilichotokea, aliwapenda watoto wake, alitamani sana wapate elimu bora lakini kila kitu kilionekana kubadilika.

Akasimama pale alipokuwa, aliwaangalia watoto wake, Irene na Godwin, moyo ulimuuma mno lakini hakuwa na la kufanya. Akawashika mikono na kuondoka nao mahali hapo huku akiwa na kadi yake ya benki ambayo ilikuwa na kiasi cha shilingi milioni tano tu.

“Mama! Tunakwenda wapi?” aliuliza Godwin huku akimwangalia mama yake ambaye mashavu yake yalilowanishwa na machozi.

“Tunakwenda sehemu nyingine,” alijibu.
“Na hapa nyumbani vipi?”
“Twendeni! Nitawaambia kila kitu!”
Hawakuwa na jinsi, mama yao ndiye alikuwa kila kitu, wakaondoka mpaka walipofika Msasani ambapo Rosemary akaingia katika kibanda cha ATM na kutoa kiasi cha shilingi laki tano na kuondoka mahali hapo.
 
Nimetia timu hapa.. Mambo ni motoo.. Huyo rais ni sawa na jiwe tuu, roho mbaya..
 
SEHEMU YA 97

Safari yao iliishia Tandale Kwa Mtogole. Alihitaji chumba cha kuishi na watoto wake. Hawakuwa na fedha za kutosha hivyo alijua kwamba kama angechukua chumba katika mtaa wa watu wenye uwezo mkubwa ni lazima angeshindwa kulipia au kukwamba katika baadhi ya matumizi na ndiyo maana akaamua kwenda Tandale.

“Unataka chumba? Vipo vingi sana! Unahitaji cha kiasi gani?” aliuliza dalali.
“Hata efu arobaini!”
“Sawa. Twende!”
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa maisha mapya yeye na watoto wake. Kutoka kuishi maisha ya kifahari Masaki mpaka Tandale yalikuwa ni mabadiliko ya haraka sana, kutoka juu na kushuka chini kwa kasi kubwa.

Wakakabidhiwa chumba, hakikuwa kikubwa sana, kilikuwa kidogo ambacho kilikuwa katika nyumba iliyokuwa na wapangaji wengi.Kabla ya kufanya kitu chochote kile, Rosemary akakaa chini, akaikunja miguu yake na kukiingiza kichwa katikati ya miguu hiyo na kuanza kulia. “Mungu! Kwa nini? Kwa nini imekuwa hivi? Mbona ghafla sana?” aliuliza Rosemary huku akilia. Mbele ya maisha yake aliliona giza kubwa likiwa limetanda.

*** Mpaka muda huo Bilionea Matiku hakujua ni mtu gani alikuwa nyuma ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Moyo ulimuuma, alijuta kwa kile alichokuwa amekifanya, alijua kwamba kila kitu kilisababishwa na wema wake wa kumsaidia Rosemary na ndiyo maana mwisho wa siku jambo hilo lilitokea.

Nje, watu hawakunyamaza, kila mmoja alizungumza lake. Wapo waliodai kwamba serikali ilikuwa nyuma ya kila kitu lakini pia wapo waliosema kwamba inawezekana kweli bilionea huyo alihusika katika mauaji hayo.

Baada ya siku kadhaa akafikishwa mahakamani, watu wengi walijaa, walitaka kusikia ni kitu gani kilichokuwa kimetokea. Upande wa jamhuri ukasimamisha mashahidi wake na kwa upande wa Bilionea Matiku akasimamisha mashahidi wake ambao walikuwa mahali hapo kwa ajili ya kumtetea tu.

Waandishi wa habari hawakukosa, walikuwepo mahakamani hapo, walikuwa na hamu kubwa ya kutaka kufahamu kitakachotokea siku hiyo. Kama ilivyokuwa kawaida, kwa siku ya kwanza, kesi ikasikilizwa na kurudishwa rumande ambapo aliendelea kushikiliwa.
 
SEHEMU YA 98

Mitaani, kelele hazikuisha, kila mtu alikuwa akizungumza lake, kelele za kuilaumu serikali ziliendelea kusikika kila kona kiasi kwamba kila mmoja akajua serikali ilikuwa imehusika katika tukio hilo.

Baada ya wiki mbili, kesi ikarudishwa tena. Iliendelea kama kawaida, mashahidi walisimama lakini baada ya kuzungushwa sana hatimaye mwisho wa siku Matiku kushinda kesi hiyo.

“Nilisingiziwa, najua nini cha kufanya,” alisema Matiku huku akionekana kuwa na hasira mno.
Wiki moja baada ya kutamka maneno hayo akapigiwa simu na mtu asiyemfahamu ambaye alimwambia kwamba alitakiwa kuachana na kila kitu kilichokuwa kimetokea na mbaya zaidi aliambiwa kuachana na Rosemary kwani vinginevyo angepata tatizo kubwa katika biashara zake.

Aliogopa, alijua kabla kwamba kumsaidia mwanamke huyo ndipo kulipokuwa na tatizo kubwa hivyo akaachana naye na kufanya mambo yake kwa kuamini kwamba watu aliotaka kupambana nao walikuwa na mkono mrefu.

Rosemary hakupokea tena misaada. Hakuwa na pesa za kutosha kwa maana hiyo asingeweza kuendelea kuwasomesha watoto wake katika shule za kitajiri na hivyo kuwapeleka katika shule nyingine za watu wa chini, na shule ambayo ilimjia kichwani mwake kipindi hicho ilikuwa ni Royal Land, shule binafsi iliyokuwa Manzese jijini Dar es salaam.

Maisha yalikuwa tofauti, yalibadilika kwa kasi kubwa, kila alipokuwa akiwaangalia watoto wake, hakuamini kama alishuka kwa kasi kubwa na kuwa hapo alipokuwa.
Hakuacha kulia, aliumia sana na hata kazini alipokuwa akifanya kazi, walimu wenzake walimuonea huruma na kila siku wakawa na kazi ya kumfariji kwa kumwambia kwamba huo haukuwa mwisho, kama ni majaribu, Mungu alimuwekea mlango mwingine wa kutokea.

Uwezo wa Godwin na Irene haukuishia katika shule ya matajiri walipokuwa wakisoma bali uliendelea mpaka katika shule hiyo waliyokuwa wamehamia.

Ilikuwa ni shule ya watu wa chini maarufu kama Kayumba, hakukuwa na wanafunzi waliokuwa na uwezo mkubwa kuzungumza Kiingereza, kitendo cha wao kuzungumza lugha hiyo kwa ufasaha kiliwafanya wanafunzi wengine kuwaona watu wa ajabu na wenye uwezo mkubwa.
 
Hahahaha!! Nilifungiwa ndani kisa hizi mvua.. Simu ikatumbukizwa kwenye maji na nguo zikarowekwa..
Hahaha kwahiyo hapo mwepesi halafu avatar yako jamani umegoma kuibadili kabisa inanitisha
 
Hahahahaha!! Vingine kama vipi.!?
Hahhaha tater bana halafu jana mmu kuna mtu anatumia taiter nikajua wewe nisimshkuru kwa kubadili avatar atakuwa kanishangaa sana yule kaka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom