Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
- Thread starter
- #321
SEHEMU YA 69
Rosemary alilia kwa uchungu, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kile alichoambiwa kwenye simu kwamba mume wake mpendwa, Mapoto alikuwa amefariki dunia.
Hakuishia kulia tu, baada ya muda akapoteza fahamu na mtu wa kwanza kabisa kumsaidia alikuwa mfanyakazi wa ndani ambaye akawaita majirani zake na walipofika, wakambeba na kuondoka naye kuelekea katika Hospitali ya Upendo wa Mungu iliyokuwa Masaki jijini Dar es Salaam.
Godwin na Irene walikuwa na hofu, hawakujua ni kitu gani kilitokea kwa mama yao, waliogopa, wakati mwingine nao walikuwa wakilia kwa kuamini kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa mama yao mpendwa.
Hospitalini hapo, mfanyakazi wa ndani hakutaka kuwaambia kilichokuwa kimetokea, alihisi kwamba mwanamke huyo alikuwa amefariki na kama angewaambia watoto hao ilikuwa ni lazima kulia sana kitu ambacho hakutaka kabisa kukiona kwani moyo wake uliwaonea huruma.
Rosemary aliwekewa dripu, aliendelea kulala hospitali na baada ya saa moja, akayafumbua macho yake na kuanza kuangalia huku na kule. Hakuelewa alikuwa wapi, ilikuwaje mpaka dripu kuning’inia juu yake lakini baada ya kukumbuka kilichokuwa kimetokea, akaanza kulia tena, kumbukumbu juu ya mume wake zikamrudia kitu kilichomfanya kuwa kwenye huzuni kubwa.
“Mume wangu amekufa…” alisema huku akimwangalia nesi ambaye alionekana kushtuka.
“Mumeo amekufa?”
“Ndiyo! Nilipigiwa simu na kuambiwa hivyo. Mungu! Kwa nini umemchukua mume wangu?’ aliuliza Rosemary na kuanza kulia tena.
Kitendo cha nesi yule kuambiwa hivyo, akatoka ndani ya chumba kile na kuelekea katika ofisi ya daktari na kumwambia hali aliyokuwa nayo mgonjwa. Nesi huyo hakuishia hapo, akachukua simu yake na kuwaambia marafiki zake kwamba Balozi Mapoto alikuwa amefariki dunia nchini Marekani.
“Amefariki! Wewe nani kakwambia huyo ubuyu?” aliuliza rafiki yake kwenye simu.
“Mkewe.”
“Umeonana naye?”
“Amekuja hapa hospitali akiwa amepoteza fahamu, na yeye ndiye aliyesema kwamba mumewe amefariki,” alisema nesi huyo.
“Jamaniiii! Huyo ndiye niliyetaka kumpa kura yangu mwaka kesho,” alisema rafiki yake huyo.
Rosemary alilia kwa uchungu, moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kile alichoambiwa kwenye simu kwamba mume wake mpendwa, Mapoto alikuwa amefariki dunia.
Hakuishia kulia tu, baada ya muda akapoteza fahamu na mtu wa kwanza kabisa kumsaidia alikuwa mfanyakazi wa ndani ambaye akawaita majirani zake na walipofika, wakambeba na kuondoka naye kuelekea katika Hospitali ya Upendo wa Mungu iliyokuwa Masaki jijini Dar es Salaam.
Godwin na Irene walikuwa na hofu, hawakujua ni kitu gani kilitokea kwa mama yao, waliogopa, wakati mwingine nao walikuwa wakilia kwa kuamini kwamba huo ndiyo ulikuwa mwisho wa mama yao mpendwa.
Hospitalini hapo, mfanyakazi wa ndani hakutaka kuwaambia kilichokuwa kimetokea, alihisi kwamba mwanamke huyo alikuwa amefariki na kama angewaambia watoto hao ilikuwa ni lazima kulia sana kitu ambacho hakutaka kabisa kukiona kwani moyo wake uliwaonea huruma.
Rosemary aliwekewa dripu, aliendelea kulala hospitali na baada ya saa moja, akayafumbua macho yake na kuanza kuangalia huku na kule. Hakuelewa alikuwa wapi, ilikuwaje mpaka dripu kuning’inia juu yake lakini baada ya kukumbuka kilichokuwa kimetokea, akaanza kulia tena, kumbukumbu juu ya mume wake zikamrudia kitu kilichomfanya kuwa kwenye huzuni kubwa.
“Mume wangu amekufa…” alisema huku akimwangalia nesi ambaye alionekana kushtuka.
“Mumeo amekufa?”
“Ndiyo! Nilipigiwa simu na kuambiwa hivyo. Mungu! Kwa nini umemchukua mume wangu?’ aliuliza Rosemary na kuanza kulia tena.
Kitendo cha nesi yule kuambiwa hivyo, akatoka ndani ya chumba kile na kuelekea katika ofisi ya daktari na kumwambia hali aliyokuwa nayo mgonjwa. Nesi huyo hakuishia hapo, akachukua simu yake na kuwaambia marafiki zake kwamba Balozi Mapoto alikuwa amefariki dunia nchini Marekani.
“Amefariki! Wewe nani kakwambia huyo ubuyu?” aliuliza rafiki yake kwenye simu.
“Mkewe.”
“Umeonana naye?”
“Amekuja hapa hospitali akiwa amepoteza fahamu, na yeye ndiye aliyesema kwamba mumewe amefariki,” alisema nesi huyo.
“Jamaniiii! Huyo ndiye niliyetaka kumpa kura yangu mwaka kesho,” alisema rafiki yake huyo.