Dunia haina usawa

Dunia haina usawa

Nakubali sana kazi yako bibie, natumaini utashusha dinner hapa kabla kitanda hakijaita.
 
Jamani ni heshima tu kwani shikamoo nakunyima nini mm
Haya basi, ujue kwetu Mkuranga mtu akikuamkia Shikamoo kuna vingine huwezi kumuomba, kwa sababu kashakufungia njia kwa kukupa heshima hiyo.
 
Haya basi, ujue kwetu Mkuranga mtu akikuamkia Shikamoo kuna vingine huwezi kumuomba, kwa sababu kashakufungia njia kwa kukupa heshima hiyo.
Sasa mkuu me utaniomba nn jamani
 
Hii hadithi inahusiana na Serikali ya Ngosha kabisa yani na inalenga tarehe 26/04 ..... Mkwe njoo shusha mzigo
Yaan mule mule hakuna tofauti nahisi alitungiwa yeye
 
SEHEMU YA 63

Mapoto alipokea taarifa hiyo kutoka kwa mke wake, alishtuka, hakutegemea kupta taarifa kama hiyo. Aliwapenda watoto wake, alitaka wapate elimu bora ambayo ingewafanya kuwa watu fulani huko baadaye, walikaa nchini Marekani kwa miaka minne na muda huo ulikuwa ni wa kurudi nchini Tanzania.

Hakupenda lakini hakuwa na jinsi, akamwambia mke wake kwamba Godwin na Irene wangerudi nyumbani nchini Tanzania haraka iwezekanavyo na hivyo ndivyo ilivyofanyika, wakarudishwa.
Huko, kwa kuwa bado familia ilikuwa na pesa, wakapelekwa katika shule ya watoto wa matajiri kwa ajili ya kusoma darasa la saba na kuendelea. Uwezo wao haukushuka, bado waliendelea kuongoza darasani kitu ambacho kila mwalimu alikuwa akiwashangaa.

Wazazi wao waliwekeza katika elimu yao, waliamini kwamba ili watoto wawe na maisha mazuri ilikuwa ni lazima wasome katika shule nzuri na kufanya vizuri na ndiyo maana walifanya kila liwezekanalo kuhakikisha watoto wao wanapata elimu bora.

“Do you still want to be a pastor?” (bado unataka kuwa mchungaji?) aliuliza Rosemary huku akimwangalia Godwin.
“Yes! I will preach the world of God around the globe,” (Ndiyo! Nitalihubiri neno la Mungu dunia nzima) alijibu Godwin.

Hakuwa na ndoto nyingine maishani mwake zaidi ya kuwa mchungaji. Alimpenda Mungu, alitaka kumtumikia katika maisha yake yote hapa duniani.
Kila siku alikuwa mtu wa kusali tu, alipenda kujifungia chumbani kwake na kusali kama kawaida. Shuleni alipokuwa akisoma, kwenye begi lake ilikuwa ni lazima kuwa na Biblia, pale alipokuwa akipata nafasi alikuwa akisoma kitu kilichowafanya wanafunzi wengine wa darasa la saba kumuita kwa jina la mchungaji.

Rosemary alifarijika, moyo wake ulikuwa na furaha tele, alimpenda sana mtoto wake, Godwin. Kitendo cha kushika sana dini kilimfanya kuwa na mapenzi makubwa kwake.

Siku ziliendelea kukatika. Baada ya watoto wake kumalizia mtihani wa darasa la saba, siku moja akiwa sebuleni amekaa na watoto wake wakiangalia televisheni, akapigiwa simu na mtu ambaye hakumfahamu aliyekuwa nchini Marekani.
 
Mbona hii ctory based on true story?? Kinana wangu embu kunywa maji haya(in zakia meghi voice)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom