Priorities mazee.
Hapa mtu angeweka chart ya "Unaweza kutumiaje dola milioni sita za Kimarekani" tungelia.
Kuanzia madawati ya shule, kama unakwenda kwa estimate za dawati la uhakika la shilingi 100, 000 na exchange rate ya dola moja kwa shilingi 1500 for simplicity's sake. Dola milioni sita ni shilingi bilioni tisa, katika shilingi bilioni tisa unapata madawati tisini elfu.
Madawati tisini elfu tungekuwa tumebadili kabisa picha za wanafunzi wanaokaa chini nchi nzima.Sijui hata kama mahitajin yetu yanafikia hapo.
Hii inamaanisha hizi habari za kusema kwamba hatuna pesa, nchi masikini ni uongo.Kama nchi inaweza kutumia $ 6 m kuleta timu ya Brazil, then suala si umasikini, suala ni priorities kama anavyosema mazee mbebabox hapo juu.
Hapo sijaenda kwenye tiba na huduma nyingine za jamii.
Watu wenye UKIMWI wanachukua zaidi ya nusu ya vitanda vilivyopo mahospitalini Tanzania. Kama unatumia figures hizo hizo za madawati kwa vitanda vya hospitali Tanzania ingeweza kuongeza vitanda 90,000 vya hospitali kwa pesa hizi. Tungeweza kumaliza tatizo la vitanda hospitalini, au hata kama tusingemaliza tatizo hili, tungelipunguza vizuri sana.
Tuna magonjwa, tuna UKIMWI (imebidi niuweke tofauti na magonjwa mengine kutokana na ulivyo tishio) tuna ujinga (Tanzania inarudi nyuma katika kufuta ujinga) kuna umasikini.
Kuna kuwapatia watu maji, kuna kuwapatia watu umeme, kuna kuwapatia watu pembejeo, kuna kuwapatia watu ajira viwandani, kuna elimu, kuna miundombinu, kuna lishe kuna maswala lukuki.
Less than 29% of the rural Tanzanian population has access to clean water. And these are Ministry of Water figures so you know to take them with a pinch of salt, the real figure is probably less than half of that.
Sisi tunaenda kulewa mvinyo wa mamilionea!
Leo hii tunashabikia kutumia hela zote hizi kwa siku moja tu. Hivi watu wanatumia akili hapa?
Yaani tunafanya mambo utadhani hatuna external debt ya about $ 6 billion ?
Priorities.