osangobantu
New Member
- Mar 30, 2011
- 4
- 4
Ana wakati mgumu,sio Rahisi kihivyo,tusubiri atakaeteuliwa na CCM,Kama ni Membe,kazi ni nyepesi,kama magufuli,kazi ni pevu.
Habari Wakuu.Ninaleta kwenu Dr.W.P Slaa The Special Thread.Uzi huu una malengo makubwa mawili
- Kumshawishi Dr.Slaa aone umuhimu wa kuomba ridhaa ya kugombea urais kupitia UKAWA.Na vilevile kuwashawishi UKAWA waone busara ya kumptisha Dr.Slaa kupeperusha bendera ya UKAWA.
- Kuweka pamoja katika JF harakati za Dr.Slaa(kama atapitishwa) kuanzia kuchukua fomu,harakati zote za kipindi cha kampeni mpaka kusimikwa na kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
View attachment 258204View attachment 258206Mambo 10 Kuhusu Dr.Wilbroad Slaa
Dr.W.P Slaa
View attachment 258227
Mama Maria Nyerere akimsihi jambo Dr.Slaa
1. Anachokisimamia
Dk Slaa anasimamia maadili, uadilifu, umakini na uwajubikaji katika uongozi wa nchi na utendaji serikalini.
Dk. Slaa anaamini kuwa Watanzania wanaweza kuleta mabadiliko wanayoyataka wakipata uongozi bora na thabiti.
2. Kuzaliwa, elimu ya msingi na sekondari
Dk. Slaa alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1948 katika Wilaya ya karatu. Alipata elimu ya msingi katika shule za Karatu na Kwermusi (Mbulu) kati ya mwaka 1958 na 1965. Alisoma elimu ya sekondari katika Shule za Dungâunyi Seminari na Itega Seminari kati ya mwaka 1966 na 1971.
3. Mafanikio ya DK. Slaa kielimu na Kitaaluma
Dk. Slaa ana shahada na atashahada zifuatazo.
Sharada ya Uzamivu (PhD) katika Sheria ya kanisa kutoka Chuo kikuu cha St. Urban, Rome.
Stashahada ya Theolojia kutoka Kipalapala Seminari.
Stashahada ya falsafa kutoka Kibosho Seminari.
Stashahada ya Afya ya Macho kutoka Kituo cha Kimataifa cha Macho.
4. Mafanikio ya Dk . Slaa kikazi na kitaalamu
Dk. Slaa amefanya kazi katika maeneo na sehemu mbalimbali. Baadhi ya nyadhifa alizoshika na kazi alizofanya ni hizi zifuatazo:
Mkurugenzi Mtendaji, Chama cha Wasioona Tanzania, 1992 â 1998
Katibu Mkuu, Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), 1985 â 1991
Mkurugenzi wa Maendeleo (Jimbo Katoliki la Mbulu), 19977 â 1979 na 1982 â 1985
Padri wa Kanisa Katoliki kuanzia 1977 hadi 1991
5. Vitabu alivyoandika
Utimilifu wa Msichana (1977) na Utimilifu wa Mvulana (1977)
Expediency and Exigency Liturgical Legislation (1981)
6. Ufasaha katika lugha nane (8)
Dk. Slaa anajua kuzungumza na kuandika lugha nane za kimataifa zifuatazo:
Kiswahili, Kiingereza, Kilatini, Kiitaliano, Kijerumani, Kihispania, Kireno na Kifaransa.
7. Uzoefu wa Dk. Slaa Kisiasa
Dk. Slaa ana uzoefu wa musa mrefu katika shughuli za kisiasa. Baadhi ya nyadhifa alizoshika ni hizi zifuatazo.
Mbunge wa karatu kwa miaka 15 kutoka 1995 hadi 2010
Katibu Mkuu wa CHADEMA, 2002 hadi sasa
Makamu Mwenyekiti Taifa wa CHADEMA, 1998 â 2002
Mjumbe wa Kamati Kuu na Baraza Kuu wa CHADEMA kutoka 1995 hadi sasa
8. Uzoefu wa Dk. Slaa KItaifa na Kimataifa
Dk. Slaa ana uzoefu mbalimbali kitaifa na kimataifa kama ifuatavyo.
Mjumbe w akuwakilisha Bunge la Tanzania katika Bunge la Afrika,Carribean na Pcific-FU (ACP-EUC Joint Assembly), 1996 â 2000.
Mjumbe kamati ya Uongozi (ACP-EU Joint Assembly)
Mjumbe katika Bunge la SADC kutoka 1998 hadi 2010
Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge la SADC(Inter Parliamentary Cooperation and Capacity Building Committee) kutoka 1998 hadi 2010.
Nibu kiongozi wa kamati ya Upinzani Bungeni, 2006-2010
Mwenyekiti Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Bunge la Tanzania 2008-2010
9. Mafanikio kisiasa na kiutendaji
Dk. Slaa amekuwa mbunge wa karatu kwa miaka 15 mfululizo.
Karatu ni moja ya wilaya hapa nchini zenye maafanikio makubwa ikiwamo miundo mbinu bora, maji na huduma nyingine za kijamii, Dr. Slaa anataka kutumia uzoefu wake wa miaka 15 ya ubunge wa Karatu na uongozi madhubuti wa ukatibu mkuu CHADEMA, kwa ajili ya taifa zima.
Ndiye katibu Mkuu aliyefanikiwa zaidi kuijenga CHADEMA kwa kushirikiana na viongozi wengine ameweza kuipitisha CHADEMA katika changamoto mbalimbali na kukifanya kuwa chama kilicho tayari kushika uongozi wa taifa.
Bila kujali vitisho vya watawala aliibua rasmi kafsha za ufisadi mbaya kuliko zote zilizowahi kutokea hapa nchini zikihusisha wizi wa fedha za umma katika Benki kuu. Madai yake mazito Bungeni yalimlazimisha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu nchini kutoroka nchini.
10.Zaidi ya yote Dr.Slaa anajua maisha ya watanzania wa kawaida na mateso yao ya kila siku
Kuhusu List of Shame
Karibuni
Ana wakati mgumu,sio Rahisi kihivyo,tusubiri atakaeteuliwa na CCM,Kama ni Membe,kazi ni nyepesi,kama magufuli,kazi ni pevu.
habari njema kwa watanzania[h=3][/h]
![]()
Baada ya jina la katibu Mkuu wa Chadema Dk Wibroad Slaa likiwa limeteuliwa na UKAWA kuwa mgombea wake wa nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
Dakika chache zilizopita kwenye ukurasa wa twitter wa Dr Slaa kathibitisha kuteuliwa na UKAWA.
CREDIT:MILLARDAYO
niliogopa ku-pre empty hii kituMambo gani yameiva mkuu; fafanua.
[h=3][/h]
![]()
Baada ya jina la katibu Mkuu wa Chadema Dk Wibroad Slaa likiwa limeteuliwa na UKAWA kuwa mgombea wake wa nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
Dakika chache zilizopita kwenye ukurasa wa twitter wa Dr Slaa kathibitisha kuteuliwa na UKAWA.
CREDIT:MILLARDAYO
ni mwisho mwaka huu kuongozwa na mafisadi.ona wanavotapanya pesa huko DodomaTanzania haiongozwi na Shahada za DINI.
huyu anaongea manini?Wapinzani tupooooooo. CCM wameshamaliza game. Jamani wametuuuwa Ila kwa kuwa Tanzania ni moja basi si shida kama tukapata magufuli