wish mgemjua huyu ulimboka vizuri msingembeza na kumsema vibaya kwa mimi niliyefanya nae kazi namuelewa vizuri tu ni dr mzuri sana na fanisi kwenye kile anachokifanya but mbali na hiyo mishahara hduma ni mbaya kwasababu vifaa hakuna huko mahospitali sm time unaingia kazini unamuangalia mgonjwa hata hujui uanzie wapi sababu tu vifaa hakuna ukiandikia report unaambia fungu hakuna sasa kama serikali haina fungu mimi mfanyakazi nimsaidieje huyu raia kwa namna hii wataendelea kufa ndugu zetu huku hao waliomng'oa meno wanaenda kutibiwa india.
Nafikiri yeye aliwakilisha tu madai ya wafanyakazi wote wa sekta ya afya lkn luck was not on his side yeye akaonekana mbaya na mwenye kuchochea zaidi. Laiti vifaa vingekuwepo utendaji wa kzi ungekuwa rahisi sana na mishahara isingekuwa big deal sana watu wangeelewa. Ila tatizo mishara duni, bado vifaa hakuna,wagonjwa wanalala chini,dawa hazitoshi huyohuyo dr anatibu zaidi ya idadi anayotakiwa kutibu
We unanyofolewa mpaka m n y e o, kwa nini usiwe mpole???
comment yako inareflect makuzi uliyopata toka kwa waliokuzaa/kulea.
Kwenzako huko. Ndugu zetu walikufa then unaleta ujinga uijinga kumtetea zoba mwenzako.
shujaa aliyehongwa na serikal akasahau kuwa ilijuea llllkuwa afe yeye, chezea hela, sasa shavu hilooo, mwana garajat wa njaa huyo, akina mandela hawatatokea tena
ulimboka ni bonge la mshamba.i was very wrong to think he was a real activist/hero kumbe boya tuu.alishindwa kusimamia alicho kianzisha bada ya kurejea toka SA.ccm wakamtekenya kidogo nae akatekenyeka na sasa kalegea kabisa.nchi hii bhana hakuna mtu real karibu wote ni ma-pretender.nyambafffff uli.
Hii ndiyo Tanzania....Hata shetani ataitwa shujaa.....Hata wasomi wamrkuwa wanyama....utu nyuma atiiiii......UKITAKA KUPATA VIDONDA VYA TUMBO FIKIRIA SIASA......MAY SOMEONE's GOD SAVE US ALL.......
umefanya nae kazi wapi?
Huduma zenyewe zinahusu mhudumu makini........dawa za bure wanatuuzia,mgonjwa mahututi wanampuuzia....Aisee mtu asiniambie kitu.....These people are sooooo cruel...
Kadoda wewe umeshawahi kupigania haki yeyote? Ulifikia wapi katika mapambano yako? Usifikirie kua kudai haki ni kitu rahisi hivyo. Tusiwakatishe tamaa wapiganaji wakat wewe unakaa oficn unacomment tu watu wana risk maisha yao kwa ajili ya wengi. Hali ya afya Tz ni mbaya kuliko unavyoweza kufikiri. Tatizo letu tumeaminishwa kua hiyo ndiyo hali tunayostahili kua nayo, na hatutakiwi kujilinganisha na mataifa mengine kwani wao wameendelea zamani.hivi kweli tunashindwa kununua vitanda kwa wajawazito? Hatuwezi kununua oxygen concentrators au dawa za emergency? Hivi vyote ni mataifa yaliyoendelea tu ndo wana afford kununua? Inapofika swala la maslahi ya viongozi na ununuzi wa magari yao na furniture za ofisi zao,tunalingana na mataifa yaliyoendelea.
Hali halisi ni kua watu walikufa wakati wa mgomo, kwakua madaktari hawakuwepo na wanaendelea kufa na wataendelea kufa kwa sababu hakuna vifaa na madawa .tofauti na wakati wa mgomo, sasa hakuna anayetangaza vifo vinavyotokea, lkn tujue either sisi au ndugu zetu ni victim wa hali mbaya ya afya
Ndugu yangu nafikiri wakati wa mgomo wewe hukuwa na mgonjwa hospitali. Nafikiri wengi wetu tuliokuwa na wagonjwa hatukukubaliana nao.
afadhali unisaidie tofauti ni kwamba kipindi cha mgo ndo watu walionekana wanakufa sasa hawafi au,angali wangejua wagonjwa wanavyokufa wasingeongea pumba mambo ni mengi sana wanakufa sababu tu hakuna tu hakuna chemikali maabara ya kufanya culture ili tatizo la mgojwa lijulikane,wanakufa sababu hakuna oxygen wodini mpaka ukaazime wodi ya jirani,wanakufa eti sababu docta on call ni mmoja na ana wodi tano kwa usiku mmoja, wanakufa sababu hakuna hata BP machine ya kugundua huyu ana pressure kwakweli inasikitisha sana simlaumu ulimboka na bado natamani atokee shujaa ambaye ataweza kupigania hizi haki pengine na utendaji kazi utakuwa mzuri huku mahospitalini. sitasahau siku mama mjamzito alinifia mikononi maana hata sikujua nianzie wapi ni usiku wamanane dr ni mmoja akisaidiwa na intern dr na wote walikuwa kwenye operation ya dharura kaja mama wa watu ana bleed ajabu pressure iko juu ,dawa zimeisha na phamarcy sijui ndo walikosa huko msd basi ni ukame tu vitanda vimejaa mwenzangu niliyenae zamu ndo anazalisha mama mwingine niko peke yangu mama wa watu analia sina kifaa hata kimoja chakuweza kumsaidia wodi haina simu hata umpigie dr aje na hata ukipiga ndo hawezi kuja maana yupo katikati ya op. Kweli it was bad sitasahau ilibidi nivae majukumu yasiyo yangu na kuwatuma dawa ndugu zake wakanunue nje maana niliona kifo cha huyu mama kiko karibu so kuwaondoa wale ndugu angalau wasishuhudie akifa but no way walikuja wakakuta ameshakufa kiukweli walitukana sana kama vile kosa ni lakwangu
pengine haki walizokuwa wakigombea wakina ulimboka zingetimizwa mambo kama haya yasingekuwepo. saa hizi raisi wetu yupo marekani kaenda kuchek afya tu wakati watoto wanalala watano kitanda kimoja asee inauma sana.
Kama shujaa anaitwa shetani. Basi Tanzania hakuna wasomi
Aisee... safari ni ndefu.
na haijulikani tutafika lini maana hakuna matumaini pengine tukafia njiani kabla yakuona wenyeji wetu
Wenyeji wetu ni kina nani?
Watt na vitukuu wstakavoishi
Tapeli alikuwa anayafuta umaarufu ameupata
shame on you poor tanzanian with empty brain, mtaendelea kufa kwa kipindupindu na malaria mpaka mshike adabu wakat wwaume zenu na wakuu wenu wakienda uk SA na india