Dr. Ulimboka azimwa

Dr. Ulimboka azimwa

Kwa habari nilizo nazo, Dr. Ulimboka anapaswa kuwa mwangalifu na hao wakubwa wa serikali. Damage aliyoisababishia hii serikali na idara nzima ya TISS ni kubwa mno, na kwa uhakika, kuna watu wameapa "Hawatamsamehe".

Hakuna shirika lolote la kijasusi ulimwenguni linaloweza kuvumilia mtu aliye na siri zake bila control ya namna fulani. Yeye kuahidi kukaa kimya haiwahakikishii majasusi wetu kuamini kuwa daima atakaa kimya. Dawa ya hili katika mashirika yote, huwa ni kumalizana ili kuwa na uhakika kuwa ushahidi umekufa. Ndiyo maana, wakati wa Coup de'tat, rais anayeingia huwa anawamaliza waliomsaidia mmoja baada ya mwingine kwa sababu hawezi kuwa salama kwa kuwa na subordinates wanaofahamu udhaifu wake.

Ni suala la muda tu, Dr. Ulimboka ama atapoteza uwezo wa kusema wala kuandika; au atalazimika kuandika taarifa ya uwongo na kisha apotezwe kisha taarifa hiyo itumiwe kuisafisha serikali; au tu - atapotea na huo utakuwa mwisho wa hadithi hii. Worst scenario ni pale atakapojengewa mazingira ya kuchukiwa na wenzake, kisha amalizwe na ndipo wenzake watakaposingiziwa kuwa ndiyo wamemmaliza ili kulipiza kisasi cha kusalitiwa. Kukaa karibu na Dr. Ulimboka ni risk sana kwa sasa.

Mimi si nabii wala mtoto wa nabii!

Bila ubishi wewe ni NABII tena aliyetumwa na MUNGU. Naprint huu uzi kwa ajili ya kumbukumbu binafsi server ya JF ik collapse.
 
Kwa kile kipigo hatathubutu kuwataja, maana akitaja tu kesho wanakata shingo kabisa
 
Mnataka aseme ili tuje humu kwa majina feki kumgongea "like" huku akiishi kwa mashaka bila msaada? Tunataka kujua nini zaidi ya kilichomtokea?

Tuliambiwa ripoti itatoka haraka kurudisha imani kwa wananchi mpaka leo kuna wanaharakati au wanahabari wanaohoji mbona ripoti imechelewa na hiyo kamati haijamhoji hata mtuhumiwa mmoja! Madaktari ndio wasaliti namba moja wa Dr Ulimboka!

Ulimboka aseme nini zaidi ya aliyokwisha sema tena alitaja mpaka majina!

That's it! Ulimboka aseme nini zaidi na kwa matokeo yapi bora? Siye Watanzania tukisikia hicho "tunachotaka akiseme", tutakifanyia kazi na kuleta mabadiliko yanayotakiwa? Au itaishia kuwa ushabiki tu. Migomo yote inayeyuka kwa vitisho haba. Wapiganaji wa kweli wakisimama "kulianzisha" wengine tunaishia kuwa watazamaji na hata, wakati mwingine, kuingiza falsafa za kuipa "benefit of doubt" serikali. Na hapa naona maajenti wa watawala wanasherehekea kweli kwa ile hoja yao kwamba "kila mtu na lwake; ukikubali kutumika utaishia kupata kipondo na hakuna atakayekuwa na wewe". And it works!

Siku watawala watakapoaminishwa kwamba ukimfanyia mnyonge hata mmoja kama walivyomfanyia Dr. Ulimboka basi ujue utakuwa umewasha baruti kama ilivyotokea kwa Mohammed Bouaziz wa Tunisia, watakuwa na tahadhari sana na kuchezea wananchi. Lakini sio hivi tulivyo sasa. Tunataka kauli? Zile picha na maelezo ya awali baada ya Dr. kuokotwa msitu wa Mabwepande ukijumlisha na makala ya Mwanahalisi (ambayo imetisha) ni kauli tosha kabisa kwa madaktari, wanaharakati na yeyote yule anayetaka kuiwajibisha serikali kwa kuendesha utawala wa hofu (reign of terror). Zaidi ya hapo ni kutaka kuendekeza "uswahili". Bora Dr. sasa ajikalie kimya. Amekwishasema - kwa vitendo!
 
hivi kuna sehemu ulimboka alisema anawajua waliomteka au yeye alisema walikuwa wanaonakana kama watu wa state, mapolisi mana walijitambulisha hivyo?
 
Tumeshasema habari za Dr. Ulimboka zimetuchosha hapa JF pelekeni Issa Michuzi Blog hizo habari

Umechoka wewe Mfuasi wa magamba; sisi tunatamani amani ya kweli nchini tunaendelea kupashana habari hadi kieleweke.
 
duh sasa itakuwaje jamani??? anyway thank God he is back and fine
 
....Haya yote nilijua yatatokea tu.

....Dr.ULIMBOKA alivyorudi nilikuta msafara wa .......? ukielekea ........?

....Moyo ulishtuka kuona hali hiyo kwa kuwa si KAWAIDA kwa siku kama ile....

....Tatizo la WA-AFRIKA hawana UJASIRI...Ndo' maana WENGI WETU ni waogA hata katika kufanya MAAMUZI yao wenyewe wanasubiri WASHAURIWE....
 
Kwa muoga huenda kicheko na kwa shujaa huenda kilio,na kunguru muoga hukimbiza ubawa wake.
 
Umechoka wewe Mfuasi wa magamba; sisi tunatamani amani ya kweli nchini tunaendelea kupashana habari hadi kieleweke.

Magamba lakini ninakutawala wewe usiye na magamba. Wewe ni manyoya nini?
 
Aisee baba yangu pesa na haadi za madaraka ni mbaya ni bora 2 wangemuua 2 kuliko kuwepo hai then hataki kusema ukwali
 
Mmmh! Maneno yameniingia haswaa! Najiuliza mimi binafsi zaidi ya kulalamika nimechukua hatua gani?
Kwa hili ninakubaliana nawe JJB, bora anyamaze yaishe. Sisi tunaotaka aseme sio kwa sababu yoyote zaidi ya kutaka kusoma umbea tu. Watanzania sote tumemsaliti Dr.Ulimboka na wanaharakati wote waliowahi kuthubutu kulenga jiwe la kwanza lakini sisi tukaficha mikono yetu.

Moja ya maneno na rai aliyoitoa Dr. baada ya kudhulumiwa afya na uhuru wake yalikuwa kuwataka Madaktari wenzake (na Watanzania kwa jumla) kuwa yeye yamemfika yaliyomfika, lakini waliobaki wanendelee na mapambano; matokeo yake, Madaktari walifanya nini na Watanzania tumefanya nini?

Baada ya Mwanahalisi kulezea kile ilichokijua na kuwataja watu na ubini wao na nambari zao za simu, Watanzania tumefanya nini? Tuseme Dr. Ulimboka aje na habari zile zile za Mwanahalisi, Watanzania tutafanya nini? Kama tuwatendaji kweli na sio wambea tu, tuchukue hatua juu ya yale ambayo tayari tunayajua kabla ya kutaka mengine mapya.

Tumwache Dr. apumue na sisi tuendelee na woga na blah blah blah zetu. Uchune Dokta, uchune!
 
sisi tuliopigania maisha yake kipindi rama anataka kummalizia pale moi anatuona mafala sio!!!!

Tumejitoa mpaka kuhatarisha usalama wetu kwa ajili yake, huyu ulimboka vipi!!!


Madaktari wenzake wakajitolea kufa na kupona, wakahakikisha inapigwa harambee fasta, akapelekwa sauzi tena chini ya ulinzi mkali, yote kwa ajli ya maisha yake, hiyo yote igeuke kuwa bure jamani! hapana haifai hata kidogo, kama unavyosema bila support hiyo saa hizi angekuwa historia, tena ndio kesi ingeisha kiulaini kabisa. post namba 30 hapo juu mohamedi tantawi anasema tumwache apiganie uzima wake, huo uzima angeupata wapi bila support ya hao anaotaka kuwasaliti sasa (kama ni kweli). Halafu kumbuka mohamedi, hili siyo suala la kisiasa tena ni suala la ubakaji wa haki za binadamu,

Pia lazima muelewe kwamba siri haiwezi kufichwa daima, huwa inamkereketa mtu kuisema, kwa hiyo ataitoa kwa mtu wake wa karibu na kumwambia usimwambie mtu, na huyo naye atampata mshikaji wake atamwambia na kumpa masharti kama hayo ya kutomwambia mtu... yani ni kama mtandao wa 'tuko wangapi' unavyokuwa. sasa kwa kuhofia hilo sidhani kama....

Huyu dokta asitake kutuzingua hapa aseme kilichomkuta atakuwa salama zaidi kwa sababu watesi wake hawatakuwa na haja naye tena baada ya ukweli kuwa umewekwa wazi labda kama ni kwa ajili ya kulipa kisasi tu baada ya kuumbuliwa, na sijuji huko alikokuwa anakutana nao kama hawajamwambukiza kitu.
 
Last edited by a moderator:
Ni bora Dr akinyamaza tu,He is a strong man,amejaribu kupigana vita akiwa kiongozi akidhani yuko na wanajeshi kabambe.Amejikuta akibaki peke yake.Amejitoa hadi kupigwa kipigo cha kifo lakini hata katika kauli katika kitanda chake cha nusu kifo alisema "Damu yangu iwe chachu ya kuongeza mapambano",ameenda akarudi na kukuta usaliti,wamemwacha tangu siku nyingi leo wanamwambia aongee,kwa lipi hasa.Amejitoa kwelikweli,ni ngumu sana kwa kizazi chetu hichi na kwa Tanzania hii iliyojaa ubinafsi kupata mtu kama yeye anayeweza kusimama kwa maslahi ya wengine.Hatasahaulika.He did something,wengi kati yetu hatuwezi kufanya hayo.He is a hero.

Dr Ulimboka pumzika baba,Ulichofanya kinatosha.Watanzania bado sana kutetea haki zetu.Ukisema utaendelea kupigana vita peke yako.Watakumaliza.Wakati mwingine mtu anaweza kutoa maisha yake kwa ajili ya watu wengine,lakini sio kwa Watanzania.Hicho cha kujitoa hivo aliweza Yesu tu.Wewe ni binadamu baba,acha,tunza familia yako,fanya proffesion yako.Unaweza usiwe salama sana kwa sababu unajua mengi.Ikiwezekana ondoka nchini ukawe mkimbizi.MUNGU ana mpango na maisha yako Dr Ulimboka.

Sometime choosing to be a coward ni vizuri kama muda bado haujafika.Kwa wale wakristo wanajua kua Pale Yesu alipoingia katika sinagogi na kuwatangazia watu kwamba yeye ndo masihi,walimzonga wakitaka kumpiga huenda kumuua,lakini alichoropoka kati yao.Kwa nini,Muda ulikua bado.
 
Siyo kama amezimwa bali baada ya tafakuri mwanana aliyoifanya kuhusu kadhia nzima na jinsi ilivyomfikisha hapo, ametambua kuwa mwisho wa yote hatma yake na ya familia yake imo mikononi mwake yeye mwenyewe...na haipo mikononi mwa hao wanaojiita wanaharakati, ambao km walivyo duniani kote wanatumia watu km akina Ulimboka km turufu la muda kukidhi mahitaji ya muda.

Na wakishayapata hao wanaondoka zao bila ya kujali athari walizomsababishia kinara wao! ndio siasa za kila uchao karne hii ya viini macho!. Na ukizubaa kidogo tu umeumia! lakini wenzako watakuwa wameshapa mradi wao!.


Kwa hiyo akikaa kimya ndio atakuwa amejihakikishia maisha marefu ili aweze kuitunza familia yake? anyways, at the end of the day he is the desicion maker. hata asiposema poa tu, bona Mwa Kay hakusema/hajasema?
 
Anyamaze, asinyamaze, aseme, asiseme ni uamuzi wake! Msimsumbue!
 
Kama kweli Dr.Ulimboka anafanya mawasiliano na watu wazito(vigogo) wa serikali kwa kumhadaa kuwa anyamaze maana swala lake linashughulikiwa basi hakuna kesi tena!

Hawa jamaa wako very smart kwenye kumafanya manipulation ya mambo. Nina uhakika kabisa kuwa kile kikundi kilichokuwa kimeandaliwa kummaliza na kwa bahati ya Mungu akaweza ku-survive kwa muujiza wa Mungu bado kinafanya kila mbinu za kumfikia kwa mbinu za hali ya juu.

Kama hawa jamaa TISS/Vigogo wa serikali watashindwa kumweka sawa kwa maana ya kumnyamazisha kwa rushwa ya namna yoyote ile iwe pesa au cheo fulani basi hatua ya mwisho itakuwa kummaliza kwa kumuua! Nina mashaka sana na security ya huyu Dr.Ulimboka. Maana hata hawa vigogo wanaoenda kuzungumza naye yawezekana kabisa wako kazini kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kummaliza.

Ushauri wangu kwa huyu Dr. Ulimboka ni kuamua moja: Kuweka mambo hadharani kwa kusema ukweli wote anaoujua kuhusu walio mteka halafu aishie majuu kama mkimbizi wa kisiasa. Kukaa kimya kwake naona ni hatari zaidi kuliko kama atajitokeza na kuweka ukweli hadharani.

Ni afadhali akafanya hivyo na akaomba hifadhi ya kisiasa kama mkimbizi katika nchi za Ulaya au USA. Kuendelea kukaa kimya hakutamsaidia! TISS huwa hawana msamaha na hawasahau. Watamzubaisha na kumlaghailaghai lakini mwisho wa siku they'll strike back! Kina Sokoine,Kombe,Kolimba,Amina Chifupa na wengineo wako wapi?

Dr.Ulimboka watch out,the hunters are after you.
 
Ulimboka, ni dhambi kubwa kuudanganya uma wa watu wote waliolia kwaajiri yako na kukuona kama mpigania haki,then leo unanunuliwa.fanya maamuzi mazuri la sivyo hautokaa kwa amani rohono mwako.hata mungu hapendi.
Shauri yako.

MamaJack, huhitaji kuwa Dr. Ulimboka kutetea maslahi fulani, hata wewe unaweza kutetea unaloamini na kuwa mfano au ukawa role mode wa wengine. Kwa kipindi chote ambacho Dr. alikuwa kwenye matatizo tumefanya nini especially kwa familia yake..... Talking is cheap
 
Akisema atakuwa ameusaliti uhai wake. Kipi Bora? Sifa za kijinga au Uhai wake?

Vyovyote atakavyofanya HAYUKO SALAMA katika nchi hii. Aseme asiseme watahatarisha maisha yake tu ikiwezekana na familia yake. Serikali yoyote duniani iko tayari kutumia pesa nyingi na hata ikibidi kugharimu uhai wa watu ili kuepuka kuchafuka na siri za nchi kuvuja ikiwemo usalama wa taifa.
 
Kama kweli Dr.Ulimboka anafanya mawasiliano na watu wazito(vigogo) wa serikali kwa kumhadaa kuwa anyamaze maana swala lake linashughulikiwa basi hakuna kesi tena!

Hawa jamaa wako very smart kwenye kumafanya manipulation ya mambo. Nina uhakika kabisa kuwa kile kikundi kilichokuwa kimeandaliwa kummaliza na kwa bahati ya Mungu akaweza ku-survive kwa muujiza wa Mungu bado kinafanya kila mbinu za kumfikia kwa mbinu za hali ya juu.

Kama hawa jamaa TISS/Vigogo wa serikali watashindwa kumweka sawa kwa maana ya kumnyamazisha kwa rushwa ya namna yoyote ile iwe pesa au cheo fulani basi hatua ya mwisho itakuwa kummaliza kwa kumuua! Nina mashaka sana na security ya huyu Dr.Ulimboka. Maana hata hawa vigogo wanaoenda kuzungumza naye yawezekana kabisa wako kazini kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kummaliza.

Ushauri wangu kwa huyu Dr. Ulimboka ni kuamua moja: Kuweka mambo hadharani kwa kusema ukweli wote anaoujua kuhusu walio mteka halafu aishie majuu kama mkimbizi wa kisiasa. Kukaa kimya kwake naona ni hatari zaidi kuliko kama atajitokeza na kuweka ukweli hadharani.

Ni afadhali akafanya hivyo na akaomba hifadhi ya kisiasa kama mkimbizi katika nchi za Ulaya au USA. Kuendelea kukaa kimya hakutamsaidia! TISS huwa hawana msamaha na hawasahau. Watamzubaisha na kumlaghailaghai lakini mwisho wa siku they'll strike back! Kina Sokoine,Kombe,Kolimba,Amina Chifupa na wengineo wako wapi?

Dr.Ulimboka watch out,the hunters are after you.

Well said,..... Lakini inaonekana imeshakuwa ni matatizo ya Dr. Uli na familia yake sasa. Kwa hakika ndio wanaoumia. Haya wazalendo... sasa akimbie nchi ???
 
Back
Top Bottom