Dr Tulia Ackson Miaka yote aikuwa wapi?

Dr Tulia Ackson Miaka yote aikuwa wapi?

Hauwezi kumtetea, haya mambo hayajanza leo. Lowassa alifanya hivi hivi, akijadai anasaidia jamii wakati anafanya kampeni kimya kimya.
Lowassa ilikuwa anafanya hivyo baada ya kupitishwa na chadema,au mwaka gani? Kingine,yeye lowassa alikuwa ni mbunge bhana,kwahyo huenda aliyafanya hayo kutumia nafasi hiyo,ila sidhani kama amemfikia dokta.
 
Lowassa ilikuwa anafanya hivyo baada ya kupitishwa na chadema,au mwaka gani? Kingine,yeye lowassa alikuwa ni mbunge bhana,kwahyo huenda aliyafanya hayo kutumia nafasi hiyo,ila sidhani kama amemfikia dokta.

Kwani uyu sio mbunge? Lowassa alifanya yote hayo akiwa Ccm na alikua anakanywa na Nape kila mara.
 
Siyo kweli mzunguko wa pesa ni mdogo Tanzania nzima utaongezekaje tukuyu jielewe
Hao watu karibu 3,000 watakaoshiriki hayo mashindano watalala wapi?watakula nin na wapi?watakunywa nin na wapi? Na bado huoni tu ongezeko la mzunguko wa pesa utakaochochewa na mashindano?
 
Halafu Ngunangwa baada ya kuuliza swali hilo, akabwagwa!
 
Basi Dodoma. Ombi langu ni kuwa mashindano yawe ya nchi nzima!
Miongoni mwa lengo la Tulia Trust kwa sasa kupitia mashindano halo ni kuvutia utalii kusini mwa Tanzania na labda ndio sababu yanafanyika huko.
 
Wakuu natanguliza salamu ,

Naomba kuweka wazi kabisa kwamba mimi ni mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya , Wilaya ya Kyela , kijiji cha Kajunjumele ,utamaduni wa Kyela na Rungwe unashabihiiana kwa kiasi kikubwa sana , wakazi wengi wa Wilaya hii ni Wanyakyusa , japo kuna makabila mengine.

Tunazo ngoma za asili ambazo kwa uchache ni Mang'oma , Ipenenga , Samba nk , na tumecheza ngoma hizi kwa miaka mingi bila msaada wa hela ama chochote kutoka kwa yeyote , kama kuna aliyetoa chochote basi alitoa kama vile PDG Ndama Mutoto wa ng'ombe anavyowapa wanamuziki wa FM ACADEMIA .

Sasa cha kushangaza mwaka huu amezuka mfadhili wa ngoma za asili aitwaye Tulia Ackson , Huyu tetesi zinadokeza kwamba lengo lake si kufadhili ngoma za asili , maana alikuwepo miaka yote na alikuwa na uwezo kama huu wa leo , lakini hakufanya hivi , taarifa zinaonyesha kwamba amelenga kurubuni wakazi wa Rungwe ili achaguliwe mbunge uchaguzi ujao .

Mbinu hii ya kizamani haikubaliki , na naomba kuchukua nafasi hii kuwaasa wana Rungwe kumuogopa huyu mama kama ukoma .

Dr Tulia aliyeingia bungeni na kubebwa kwa mbeleko ya chuma hadi kwenye unaibu spika , amekuwa mstari wa mbele kudhalilisha na kunyanyasa wabunge wa upinzani , amezima mijadala mingi yenye tija ili kuokoa chama chake , huyu hawezi kuwa msaada wa Akina Mama wauza ndizi na maziwa wa ushirika au Kiwira , hafai hata kuwa Mwenyekiti wa kijiji cha Makandana , hafai .

Dr Ngunangwa aliwahi kuwauliza waliokuwa wanajipitisha kwenye jimbo lake huko Njombe na kutoa zawadi za baiskeli nk , kwamba WALIKWINA ? yaani kwa kiswahili , MIAKA YOTE WALIKUWA WAPI ?

Nakala ya uzi huu imfikie JOHN MWAMBIGIJA .
Kwa bahati nzuri nawaaminia sana Wanyakyusa. huwaga hawakosei
 
Kila kitu kina tarehe moja Ya kuanza usiwe mtumwa wa historia. Yesu alizaliwa kwenye hori la ngombe lakini Maisha yake hakuishi na kukulia kwenye holi la ngombe .Tulia kyala akutule go ahead
Mbinu zenu za kishamba zimestukiwa kudadeki !
 
Mbona Mr Sugu aliingia kwa gia ya kuendeleza Hiphop Mbeya na hatukusikia yote hayo,na kuna wengine wamekuwa maarufu kwa kutukana viongozi,mwache Tulia atulie na amang'oma yake.Hata asipoleta hiyo mipalaano Tu;ia atakuwa mbunge tu .Mambo ya watu wa CCm waachie wenyewe kama vile mambo ya Chadema mlivyoachiwa wenyewe kikolo.
Uzoefu huo ndio unatufanya tusituke
 
Siyo kweli mzunguko wa pesa ni mdogo Tanzania nzima utaongezekaje tukuyu jielewe
Hivi hata mgeni akilala tukuyu guest house hajaongeza mzunguko wa hela? Huyo mgeni anakuwa kaingiza pesa mpya ambayo tukuyu ilikuwa haipo kwenye mzunguko kupitia wenyeji . Tulia akileta watu elfu tatu toka nje Ya tukuyu wataingiza mamilioni ya pesa mpya kwenye mzunguko ambazo hazikuwepo Kabla ya tamasha. Wewe inaonyesha ni Muuza sura tukuyu usiye na mchango wowote wa kuongeza mzunguko mkubwa wa pesa tukuyu. Huelewi hata maana ya kuongeza mzunguko wa pesa kwa watu wengi tukuyu ni nini na inafanyikaje? Inaonyesha elimu yako ya hapa na pale Kama ya mbunge kubenea . Mambo makubwa Kama ya kubuni mbinu za kuongeza mizunguko ya pesa kwenye eneo kwa watu wengi tukuyu waachie wasomi wabunifu waliokubuhu Kama DK. Tulia nkamu gwangu wewe Kama una elimu ya kuunga unga mpishe Dk Tulia. Kuna methali inasema mwenye nguvu mpishe. Mpishe Dk Tulia asaidie mzunguko wa pesa uongezeke tukuyu maruhuni wewe. Tukuyu inahitaji waongeza mzunguko wa pesa sio mabwege wasiojua mzunguko wa pesa unaweza ongezwaje Kama wewe
 
Aacha kupofuka kwa Kanga za kuchezea ngoma, yeye ni wakitaifa kama lengo sio jimbo mwambie afanye yanahusu kutaifa kuliko kulenga jimbo, na ya kitaifa wala hayaitaji mtaji mkubwa kama anaotumia kwenye Ngoma.
Hata hujui unachobishia
 
Mi siwapendi CCM ila kama huyo Tulia anataka ubunge wa Rungwe atawafaa sana kuliko Sauli.
 
Tulia aogopwe jamana...! Nikimkumbuka toka enzi za bao la mkono "Mita 200", sitaki hata kumsikia..!

Mnafiki sana
Huyu aliyetimua wananchi kwenye vituo vya kuhesabia kura eti leo anarudi kudanganya wananchi kwa ufadhili wa ngoma za asili !

Hatudanganyiki !
 
Mkuu unabishana na bavicha hawana akili hao usipoteze nguvu bure kuwajibu
Utafiti umedhihirisha kwamba Bavicha , ndio taasisi pekee ya vijana inayotikisa ukanda wa Maziwa makuu , Kamanda Mambosasa anawafahamu tangu alipokuwa Dodoma .
 
Kwa mfano aliwahi kufaa kwenye nini ?
Mtu aliyefika cheo cha naibu spika anakuwa na influence kubwa sana. Akiwa mbunge wao sauti ya wana Rungwe itafika mbali sana. Haya mambo ya kuwa na wabunge mediocres kama wakina sauli siyo kabisa.
 
Kama dar es salaam tu mzunguko wa hela mdogo sembuse tukuyu
hapo jamaa anazungumzia pesa ya siku mbili tatu itaongezeka mifukoni mwa watu kwa sababu ya biashara na mambo mengine kutokana na kuwapo kwa wageni mbalimbali.pia ishu ya utalii hapo itahusika
 
Back
Top Bottom