Dr SLAA: Wana TABORA mtuunge mkono

Dr SLAA: Wana TABORA mtuunge mkono

Wanyamwezi wanatia AIBU sana wana mlilia FISADI!

Walikodiwa wale, wakapewa chao ili wajidondoshe na kupiga yowe zisizokuwa na manufaa kwa taifa.
Mafisadi wananguvu sana chini ya anga!

Kaandaa waliaji kwanza kabla hajatangaza.

Bado EL na yule mzee wa vijisenti na wenzao wote watatoka mmoja mmoja
 
Mimi ni mnyamwezi na nafahamu mazingira na khulka za wanyamwezi, juu ya alichofanya Rostam...CCM ISAHAU JUU YA USHINDI WA HAKI KATIKA MKOA WA TBR ktk chaguzi yoyote ijayo. Ni doa na pigo kubwa sana kwao CCM TBR, waila kwa wasioufahamu vema mkoa ule...wanaweza kudai kwamba CCM inaweza kuwa hai kwa miaka 10 ijayo.
Dr Slaa mnapaswa mmuweke mtu ambaye ni kweli anatoka TBR, asipandikizwe mtu kinadharia kuwa ni mzawa wa TBR...wale hawachelewi kumsusa. Pelekeni mtu asilia ya mkoa ule na walau anajua lugha ya kinyamwezi na shupavu, MTASHINDA.

Kauli hiyo naiogopa kwa ka-element ka tribalism!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nadhani CCM watambana Mu-Iran kupiga kampeni zao maana akikataa pingu yake na uraia mashakani huo ndio mtindo wa CCM uwa wanakuwa na watu wenye weakness iliiwe rahisi kwao kuwafanya kama wanavyotaka, hapo RA lazima atalazimishwa kuzunguka Igunga nzima kupiga kampeni za CCM na kama CCM itashindwa na wakathibitisha kuwa ni hujuma yake utasikia siyo raia na na kesi zake hapo zote utazisikia mahakamani.
 
kama daktari wa ukatoliki slaa ni maarufu agombee igunga. mrema alishinda temeke kwa kishindo.

slaa sio lolote kwa mrema. akigombea igunga atashindwa.
 
Yaani mkija Igunga hata mimi ccm nitawapigia kura lakini sitahama chama kwani haya yote ni nguvu na jasho lenu WANA CHADEMA kuwafichua mafisadi

Mkuu maneno yako ni mazito na angalau wewe mwana CCM umeona ukweli kwamba kama si Chadema na list of shame CCM hata leo hawawezi kumtaja Rostam kama fisadi .Asante sana na kulikomboa Taifa lako sin lazima uhamie Chadema .Bakia huko huko na uwap shule ma CCM wezako.Wewe ni mwana CC kama mwalimu maana ume elewa ila ma CCM kama Sitta ni mzigo kwa Taifa.
 
kama daktari wa ukatoliki slaa ni maarufu agombee igunga. mrema alishinda temeke kwa kishindo.

slaa sio lolote kwa mrema. akigombea igunga atashindwa.
Red:katoliki wanawanyima rahaaa sana,maana unaweka maneno ambayo ayana maana.
Ficha upumbavu wako,usifiche hekima yako
Sio lazima kila thridi uchangie.
 
Naitwa matumbo bin matumbo,ni mzaramo niliebadili kabila jana saa 7 mchana kuwa mnyamwezi.. Napenda kujitokeza mbele yenu wana jamvi kutangaza nia ya kugombea ubunge wa jimbo la igunga kwa tiketi ya chama cha magamba..

Ni msomi niliyebobea hasa kwenye sanaa ya maigizo ,nna shaada ya kwanza toka royal colege-kariakoo/msmbaz,pia digrii ya uzamivu ya cookery toka kingston online international university-jamaica,..pia nna p.h.d ya siasa toka muslim university of mbumbumbus-moro..najua wengi sasa awalali wakitokwa udenda na nafas hii ila nawaomba wasahau kwani nimeshaaidiwa na mfalme wa igunga rost tamu kumwakilisha/kumrithi..nitarudi kumwaga sera,ngoja kwanza nikameze pilton km waziri tyson ili nipate nguvu ..
 
Sijakuelewa hapo kidogo ndugu mdau, ni<em><strong> North Mara</strong></em> au?
 
cdm hawakubaliki Tabora, huku cuf ndio wapo wengi, cdm wawaunge mkono cuf, vinginevyo jimbo litarudi magamba.
 
Mbona muiran aliweza kuwa mbunge kwa miaka kibao? Sema waweke mislamu kwa vile TBR inawaislamu kibao!
.Huo udini ni wako mwenyewe sasa unataka kusingizia watu bure.Si useme tu.....
 
Ingependeza kama cdm wangemuanguasha huyu fisadi kwenye uchaguzi, sasa kajiondokea mwenyewe ndio watu wanataka kujaribu bahati? Mkaribishe Rostam uanachama cdm mtayachukua majimbo mengi sana; kwa taarifa yenu, karibu nusu ya wabunge wa ccm wamesaidiwa kifedha na uyu jamaa hadi hapo walipo.
 
Naitwa matumbo bin matumbo,ni mzaramo niliebadili kabila jana saa 7 mchana kuwa mnyamwezi.. Napenda kujitokeza mbele yenu wana jamvi kutangaza nia ya kugombea ubunge wa jimbo la igunga kwa tiketi ya chama cha magamba..

Ni msomi niliyebobea hasa kwenye sanaa ya maigizo ,nna shaada ya kwanza toka royal colege-kariakoo/msmbaz,pia digrii ya uzamivu ya cookery toka kingston online international university-jamaica,..pia nna p.h.d ya siasa toka muslim university of mbumbumbus-moro..najua wengi sasa awalali wakitokwa udenda na nafas hii ila nawaomba wasahau kwani nimeshaaidiwa na mfalme wa igunga rost tamu kumwakilisha/kumrithi..nitarudi kumwaga sera,ngoja kwanza nikameze pilton km waziri tyson ili nipate nguvu ..

Hivi ile tabia uliacha kabisa ulipotoka seminary? Maana yule RECTOR alikupenda sana!
 
Mbona muiran aliweza kuwa mbunge kwa miaka kibao? Sema waweke mislamu kwa vile TBR inawaislamu kibao!

Unapozungumza Igunga usichukulie sasa ni Tabora kwa ujumla wake. Wananchi huko wengi hawana dini za kigeni kwa taarifa yako. Wengi wanaabudu dini za mababu. Hivi unalijua kabila linaitwa Wataturu? Wako kwa wingi! Hivyo tofautisha na wale wa Tabora mjini ambako ndo kuna Waislamu wengi.

Nimesikia wengine eti wanasema Igunga ni Wanyamwezi! Kwa taarifa wananchi wa Igunga ni mchanganyiko, yaani Wasukuma, Wanyamwezi na Wataturu.
 
Infact CDM badala ya kufikiria swala la uraisi wajipange kuanzia sasa ktk swala la kupata majimbo.

CDM na vyama makini vya upinzani wajipange kwa kuwaandaa watu kushika nafasi za ubunge. Kwa utaratibu wa nchi yetu inaitajika kuwa na wabunge wengi wa upinzani ili kuleta mabadiliko ya kweli!
 
Mtanisamehe bure lakini jana nimewadharau sana wana Igunga, kweli vya bure gharama!! na kwa mentality ile hakuna haja ya kupoteza fedha kwenye uchaguzi, wamuombe tu tajiri wao awatangazie Kibaraka wake atakayewaongoza wana Igunga kwa niaba yake.

Usiwadharau mkuu, hii mbona ni kawaida sana kwa upande wa saikolojia? Ukimnyanyasa mtu kwa muda mrefu anaona ni sawa tu/inakua mazoea. Kwa Wana-Igunga waliolia inawezekana wanaona ni sawa kutawaliwa na kunyang'anywa rasilimali zao na Rostam) na wamepoteza identity yao kabisa wanaogopa change. Chukulia mwanamke au mwanaume aliyekuwa abused muda mrefu; unaweza ukampeleka mpaka kituo cha polisi lakini akakataa kufungua kesi, leave alone kuwa witness. Hawa watu for more than 15yrs wameshaharibiwa "psychologically" wanaona bila CCM hawawezi kuishi. Tunahitaji watu wakuwaambia na kuwaonyesha change is necessary and is possible; it is desperately needed now in places like Igunga. Igunga deserve a better leader/MP.Wakiona kwa vitendo mind zao zitafunguka taratibu.
 
Nimesikia wengine eti wanasema Igunga ni Wanyamwezi! Kwa taarifa wananchi wa Igunga ni mchanganyiko, yaani Wasukuma, Wanyamwezi na Wataturu.

Mkuu unaelewa unachokisema? Kuna Wanyamwezi wa Dakama (Tabora) na Wanyamwezi wa Sukuma (Shinyanga na Mwanza). Sasa sijui kama ulielewa ulichokua unaandika.
 
Yaani mkija Igunga hata mimi ccm nitawapigia kura lakini sitahama chama kwani haya yote ni nguvu na jasho lenu WANA CHADEMA kuwafichua mafisadi[/QUOTE]

Nadhani umekomaa. Hata mwl. Nyerere katika uhai wake alimpigia kura mbunge wa upinzani naye akabaki CCM.
 
Poleni sana, Mwacheni Rostam afanye biashara. Tulieni muweke mgombea makini.
 
ndio manake cdm tuna twanga kote kote kama vp tuji pange tu chukue jimbo au co wa dau?
 
Back
Top Bottom