Usiwadharau mkuu, hii mbona ni kawaida sana kwa upande wa saikolojia? Ukimnyanyasa mtu kwa muda mrefu anaona ni sawa tu/inakua mazoea. Kwa Wana-Igunga waliolia inawezekana wanaona ni sawa kutawaliwa na kunyang'anywa rasilimali zao na Rostam) na wamepoteza identity yao kabisa wanaogopa change. Chukulia mwanamke au mwanaume aliyekuwa abused muda mrefu; unaweza ukampeleka mpaka kituo cha polisi lakini akakataa kufungua kesi, leave alone kuwa witness. Hawa watu for more than 15yrs wameshaharibiwa "psychologically" wanaona bila CCM hawawezi kuishi. Tunahitaji watu wakuwaambia na kuwaonyesha change is necessary and is possible; it is desperately needed now in places like Igunga. Igunga deserve a better leader/MP.Wakiona kwa vitendo mind zao zitafunguka taratibu.
La msingi hapa nikuwaambia wanaigunga Rostam Aziz kaonewa. Ufisadi anaotuhumiwa ulimhusisha hata JK,familia yake,viongozi karibu woote wa CCM. Sasa ni kwa nini Rostam Aziz afanywe mbuzi wa kafara. NEC yao inawatuhumu watu watatu tu. Mbona inawaacha vigogo wote walionufaika na EPA. Je na wakurugenzi wa Halimashauri ambao wamefisidi fedha kwenye miradi yote ya maendeleo hao sio mafisadi? Fisadi ndani ya CCM ni hao watatu tu?