Wana Ukumbi,
Mtendaji mkuu wa CHADEMA, Dr Slaa, kwa sasa ana kadiriwa kuwa na miaka zaidi ya 70 (kwa mujibu wa wazee wenzake wa Karatu). Hivyo kutokana na umri huo mkubwa, kunamfanya Dr Slaa kushindwa kutekeleza majukumu yake kwa ufasaha na kumfanya aonekane mzigo kwenye chama!
Kutokana na lawama na manung'uniko mengi ya wanachama wa CHADEMA juu ya mwenendo wa chama chao. Dr Slaa amefanyiwa tathmini na kugundulika kuwa kwa sasa hawezi tena kuendana na kasi ya CHADEMA hivyo ameombwa kujiuzuru na kupisha wengine wenye uwezo.
Baada ya taarifa hizi kutolewa, chanzo changu cha habari kilifanya jitihada za kumtafuta Dr Slaa na kuzungumza nae juu ya kutakiwa kujiuzuru; Dr Slaa alikiri kweli umri umeenda, lakini alisema hilo halina mahusiano na utendaji kazi wake!
My take,
Hivi kweli umri wa mtu hauna mahusiano na utendaji kazi!??? Kweli Dr Slaa amezeeka sasa!