Dr. Slaa, Mbowe wanguruma!

Dr. Slaa, Mbowe wanguruma!

Status
Not open for further replies.
- Wamtetea Dk. Mwakyembe katika sakata la umeme
- Wamshukia vibaya Rostam...

Zaidi naja kukupasheni... Looking for the Audio version of this(these) Press Conference(s)

Inatia moyo kuona kwamba Dr Slaa na Mbowe wameweka pembeni tofauti zao za kiitikadi na Mwakyembe na kuamua kumtetea. Hivi ndivyo inatakiwa iwe kwamba wakati mwingine tunaweza kabisa kukubaliana na wanachama wa vyama vingine katika kutetea maslahi ya Taifa pamoja na kuwa kuna tofauti kubwa kisera katika vyama hivyo. Hongera sana Dr Slaa na Mbowe.
 
Nilibahatika kumsikia Dr Slaa leo asubuhi akihojiwa kwa njia ya simu na watangazaji wa kipindi cha Power Breakfast cha CLOUDS FM. Alipoulizwa kuwa mbona kunakuwa kama kuna 'kutofautiana' kuhusiana na suala la Dowans kati yake na mh Zitto,alijibu kuwa yeye HATOFAUTIANI wala HAKUBALIANI na Zitto kwani anaelewa kuwa kamati mbili za bunge zilizotoa misimamo inayokinzana kuhusu Dowans itakuwa imefanya hivyo kutokana na 'data' walizonazo.Akasisitiza kuwa kuna 'taarifa' kwa sasa hatuna(hadi hapo kamati zitakaposoma ripoti bungeni) hivyo mjadala umebase kwenye hisia/hearsay na sio facts.
Kwangu mimi niliona kama Dr amespin tu.Kweli Slaa huyu akawa hadi leo hana facts kuhusiana na hili????Only on this one Dr,siamini kama ameshindwa kuzipata.
 
Na Mwakyembe nasikia ameamua kuwatolea uvivu kabisa... liwalo na liwe.. Sasa kina Mbowe hawakumsikiliza mzee Malecela jana? Kasema malumbano yakome, mbona hayakomi!! maana nasikia kuna msurururu wa mikutano ya waandishi sitoshangaa kesho ikawa "double dose"

Mkuu MKJJ, Kauli ile ya Mzee Malecela ililengwa kwa viongozi wa CCM. Ila ina maana tofauti kabisa kwa Upinzani. Kwa wanaozijua siasa za Bongo, kauli ile ina ishara njema sana kwa wapinzani. Tusibiri tuone yatakayofuata.
 
Sikonge eneo linaitwa kijiji cha KISASIDA kipo wilaya ya singida mjini , ndio hapo hapo kamapuni ya wakina Mwakyembe na Rostam wanataka kupata eneo.

Kuhusu hii ya wakina Rostam , ukweli ni kuwa Rostam aliiba mradi huu kwa watanzania ambao walifanya utafiti kuhusu kuzalisha umeme wa upepo , lakini walipoanza harakati za kutafuta pesa baada ya study yao kufanyika walijikuta wanaangukia mikononi wa Rostam , ndipo alipowaambia kuwa kama wanataka wanapaswa kusajili kampuni mpya ili awape pesa , na aligoma kutoa pesa kwenye ile ya awali ambayo sasa inamilikiwa na wakina Mwakyembe.

Mwakyembe kusikia wameenda kuchukua pesa kwa Rostam , ndipo alipowaeleza wenzake wazi kuwa hatapenda kuwa sehemu ya mradi huo na wao kwa kuwa wametoka wote eneo moja waliamua kumtii na kujitoa kwenye mikono ya Rostam na ndipo alipoamua kuendelea na mapambano kwa ajili ya kuhakikisha kuwa anazalisha umeme yeye kwenye kijiji hicho.

Kuna baadhi ya watu (singependa kuwataja) ambao wamewahi kunieleza kuwa ubunifu wa miradi yao (project research na plans) ilichukuliwa na RA na kuanzishwa nae, kwa kuwa tu walikwenda kwake kupata support na wao hawakuambulia chochote. Inaelekea hiyo ndio tabia yake.
 
- Wamtetea Dk. Mwakyembe katika sakata la umeme
- Wamshukia vibaya Rostam...

Zaidi naja kukupasheni... Looking for the Audio version of this(these) Press Conference(s)

Mkuu tuletee hizo nyingine,ile ya Dk Malecela sijaisikia lakini vipande nilivyopata vimenichosha kabisa,wanaturudisha nyuma,lakini kwasababu 2010 iko karibu,ni muhimu tukawasikilza...Shukran kamanda.
 
- Wamtetea Dk. Mwakyembe katika sakata la umeme
- Wamshukia vibaya Rostam...

Zaidi naja kukupasheni... Looking for the Audio version of this(these) Press Conference(s)

Asante mkuu, sasa tunasubiri taarifa zaidi
 
Kuna baadhi ya watu (singependa kuwataja) ambao wamewahi kunieleza kuwa ubunifu wa miradi yao (project research na plans) ilichukuliwa na RA na kuanzishwa nae, kwa kuwa tu walikwenda kwake kupata support na wao hawakuambulia chochote. Inaelekea hiyo ndio tabia yake.

Hivi Tanzania hatuna sehemu za kusajili intellectual property? Kama vipi unamwacha anaiba plan/idea halafu unampiga bonge la suit.
 
Lets wait and see,mahali panaponitatiza ni pale ambapo Dk Slaa and Mh Mbowe wanaweza kutofautiana na Mh Zitto kwenye suala la Dowans bila kuathiri mwenendo wa chama,hapo ndo nashangazwa,like i said...Lets wait and see.
 
Hivi Tanzania hatuna sehemu za kusajili intellectual property? Kama vipi unamwacha anaiba plan/idea halafu unampiga bonge la suit.

Kiranga, kuzuia kitu kisitokee ni mbadala makini zaidi kuliko kuacha kitokee ili "ukomoe". Ukiwa unaamini kwenye zero tolerance kama kigezo cha intelligence, basi hamna budi kuitumia hiyo intolerance katika kuzuia maovu yasitokee.

Mkuu hebu fikiria.... je mmoja kati ya wale wanaotaka kufanya hiyo 'sting operation' akipoteza maisha (kwani hili ni jambo ambalo hutokea) akiwa na evidence ambayo ndiyo ingekuwa muhimu katika kufanikisha hilo bonge la law suit dhidi ya huyo mwizi wa IP?!... si ndiyo yaweza kuwa basi kabisa kwani watakuwa wamechelewa na evidence ya kushinikiza imepotea?!
 
Ukiangalia vema utaona kuwa, kulikuwepo mpango wa siku nyingi wa Lowassa na RA kujaribu kuhodhi nguzo kadhaa za uchumi ikiwa ni pamoja na umeme.

Hebu angalia hii set up, halafu tuanze ku-connect dots;

  1. Vijana wa Lowassa, Waziri na Naibu Waziri, wamewekwa Wizara ya Nishati na Madini badala ya wazoefu kama Prof. Mwandosya n.k.
  2. Classmate na best wa Lowassa, Masebu, kawekwa kuwa mkurugenzi wa EWURA (Energy and Water Utilities Regularory Agency), na ndiye hivi sasa mshauri mkubwa wa Ngeleja.
  3. Sayore, home boy wa Lowassa, ndie Board Chairman wa EWURA
  4. Dr. Rashid, Mwangaliaji maslahi ya Lowassa tokea Vodacom, ndiye Mkuu wa Tanesco.

Kwa hiyo ni wazi kuwa Richmond ilikuwa tu ni mwanzo wa Lowassa kutaka kuimiliki Tanesco. Yeye EL na watu wake wanataka wawe ndio TANESCO, and they are very close to realise their ambitions.
 
Makaa ya Mawe.
sio kweli Naibu waziri wa nishati ni mtu wa Lowassa,kumbuka mkasa wa Malima,spika na Mengi bungeni utajua Lowassa hakuwa na Malima.
 
Naona kuna makundi Slaa ,Mbowwe na Mwakiembe na upande mwengine kuna Lipumba ,Zito na kundi kubwa katika kikao cha juzi hivyo ni bora tukapata vyama vitatu ,Chadema CUF na Sultan CCM ,halafu tuweke uchaguzi wa haki tuone.

Mwakiembe aende Chadema ,Zittto akimbilie CUF na Sultani abakie kama alivyo akiwa na migogoro kibao ya takirima tuelekee uchaguzi mkuu ,Zitto anaweza kuipata nafasi ya kugombea Uraisi 2010 kupitia CUF ,naamini ni nafasi ambayo atapewa tu bila ya matatizo yeyote na asifanye mchezo wa kuamini kuwa Chadema watampatia sidhani kabisa kwanza kule Chadema kuna ukabila au mnaonaje ?
 
Naona kuna makundi Slaa ,Mbowwe na Mwakiembe na upande mwengine kuna Lipumba ,Zito na kundi kubwa katika kikao cha juzi hivyo ni bora tukapata vyama vitatu ,Chadema CUF na Sultan CCM ,halafu tuweke uchaguzi wa haki tuone.

Mwakiembe aende Chadema ,Zittto akimbilie CUF na Sultani abakie kama alivyo akiwa na migogoro kibao ya takirima tuelekee uchaguzi mkuu ,Zitto anaweza kuipata nafasi ya kugombea Uraisi 2010 kupitia CUF ,naamini ni nafasi ambayo atapewa tu bila ya matatizo yeyote na asifanye mchezo wa kuamini kuwa Chadema watampatia sidhani kabisa kwanza kule Chadema kuna ukabila au mnaonaje ?

Mbowe mchagga na Slaa Muiraq ni wakabila dhidi ya Zitto Mha? Umekula nini leo mkuu? Maana sioni connection ya topic hii nahayo makapi hapo juu...Na sasa unashauri Mwakyembe Mnyakusya ajiunge na ukabila huo dhidi ya Zitto,acha headache mkuu,si lazima utype tuu.
 
Naona kuna makundi Slaa ,Mbowwe na Mwakiembe na upande mwengine kuna Lipumba ,Zito na kundi kubwa katika kikao cha juzi hivyo ni bora tukapata vyama vitatu ,Chadema CUF na Sultan CCM ,halafu tuweke uchaguzi wa haki tuone.

Mwakiembe aende Chadema ,Zittto akimbilie CUF na Sultani abakie kama alivyo akiwa na migogoro kibao ya takirima tuelekee uchaguzi mkuu ,Zitto anaweza kuipata nafasi ya kugombea Uraisi 2010 kupitia CUF ,naamini ni nafasi ambayo atapewa tu bila ya matatizo yeyote na asifanye mchezo wa kuamini kuwa Chadema watampatia sidhani kabisa kwanza kule Chadema kuna ukabila au mnaonaje ?

Mwiba tafadhali acha kuchoma mada, ukabila kwani Mbowe na Slaa ni kabila moja?

Hapa tuna anagalia nani wako serious kutetea maslahi ya walala hoi siyo mambo ya fulani katokea kabila gani, awe mdigo mdengereko, mtindiga mkwele kama anatetea maslahi yetu kabila lake is non of our business! Labda hizo sera kazipeleke kwa watani wajadi nyayo..
 
Makaa ya Mawe.
sio kweli Naibu waziri wa nishati ni mtu wa Lowassa,kumbuka mkasa wa Malima,spika na Mengi bungeni utajua Lowassa hakuwa na Malima.

Malima ni kijana wa wanamtandao ambao kiongozi wake ni Lowassa. Inasemekana Lowassa alijaribu tu kumtia mkwara Mengi ili asihangaike na Malima kwa kisingizio kuwa wabunge waliokuwa wamhukumu Malima walikuwa wameshahongwa.

Hebu fikiria kwa Waziri Mkuu mzima kuwa na nyeti za wabunge wake kupewa rushwa bila kuzifanyia kazi, lakini hapo hapo aliweza kumwambia Mengi ni legit kweli?

Lowassa alijipanga siku nyingi tokea enzi za Kikwete kuitawala nchi kiuchumi na kisiasa. Na ameweza kuwanunua wengine wengi kwenye ulindo wake.

Nikupe mfano mdogo tu, unamkumbuka na yule dada wa kirangi aliyekuwa DAWASO aliyemsingizia Mwakyembe kuwa mwizi wa maji nyakati za Richimond-gate? Uliza naye yuko wapi hivi sasa, Tanesco...

Tuendelee ku-connect dots utaona zitakapoishia.
 
Malima ni kijana wa wanamtandao ambao kiongozi wake ni Lowassa. Inasemekana Lowassa alijaribu tu kumtia mkwara Mengi ili asihangaike na Malima kwa kisingizio kuwa wabunge waliokuwa wamhukumu Malima walikuwa wameshahongwa.

Hebu fikiria kwa Waziri Mkuu mzima kuwa na nyeti za wabunge wake kupewa rushwa bila kuzifanyia kazi, lakini hapo hapo aliweza kumwambia Mengi ni legit kweli?

Lowassa alijipanga siku nyingi tokea enzi za Kikwete kuitawala nchi kiuchumi na kisiasa. Na ameweza kuwanunua wengine wengi kwenye ulindo wake.

Nikupe mfano mdogo tu, unamkumbuka na yule dada wa kirangi aliyekuwa DAWASO aliyemsingizia Mwakyembe kuwa mwizi wa maji nyakati za Richimond-gate? Uliza naye yuko wapi hivi sasa, Tanesco...

Tuendelee ku-connect dots utaona zitakapoishia.

Unamzungumzia Badra? huyu dada ndo amehama kiajabuajabu nashangaa kusikia sasa yupo Tanesco... sasa huyu dada wa kirangi ana uhusiano gani na Lowassa?
 
Unamzungumzia Badra? huyu dada ndo amehama kiajabuajabu nashangaa kusikia sasa yupo Tanesco... sasa huyu dada wa kirangi ana uhusiano gani na Lowassa?

Natumaini ni huyo huyo Badra, maana alitoka DAWASCO then akatimkia TANESCO.

Haya maswali mazuri sana, maana ndo unapata kila kitu kwa jinsi watu walivyo na data.

Kuna mahali niliona Game Theory akirusha salaam hewani kwenda kwa huyu dada. May be GT nae anaweza kuwa na full info. Pamoja na hayo Makaayamawe inabidi atuweke sawa ili twende pamoja!
 
Sasa mnaposema CUF chama cha waarabu hivi Lipumba ni muarabu ?

Yaani wengine hamjui kabisa kuzungumza siasa ,siasa haina dini wala rangi ni kugandamiza tu.

Zitto kama mtamuangalia siku hizi picha haziendani na Chadema kwa kuwa alichokigundua Chadema ni kuwa hawana muelekeo wana matatizo ya ndani kwa ndani ,na wasemaji wa kubwa Chadena ni Slaa na Mbowe ,Zitto alikuwa mmoja wao lakini wameanza kumueka pembeni na amesikika kuwa hagombei tena ubunge kwa maana hagombei tena Chadema .

Unajua Chadema kinaonekana ni Chama cha watu wawili tu ,Mbowe na Slaa bila ya wao hakuna anaeweza kuzungumza na kuvutia wateja au wananchi ,mkutano unakuwa hovyo kabisa hauna kichwa wala miguu ni kama mkutano wa CCM kukosa TOT.
Zitto hawezi kuusema ukweli wake kwa sasa lakini kwa tuonavyo kuna tofauti kubwa imeanza kujitokeza ambazo zinaonyesha kuwa sio wanalindana bali wanawindana kila mmoja anataka aonekane yeye ni top kuliko mwenziwe hawana umoja kama tuonavyo katika CUF ,maana katika CUF kila mmoja ni kivutio kumshinda mwenziwe ,awepo jukwaani na ni jambo ambalo linawafanya wananchi wawe kwenye msimamo mzuri sana ,kwa kuwa atakaewahutubia basi anawatosheleza kabisa ,hilo halina ubishi kwa ushahidi kuwa inawezzekana miezi kupita humuoni mwenyekiti wala katibu kupanda majukwaani ,ni vijjana tu wanasema na kurapu kuliko wakubwa zao ,ila kwenye Chadema ni Mbowe na Slaa ,sio nawazarau hapana kinachihitajika ni kuwapisha wengine na kuwapa elimu ya uzungumzaji katika majukwaa ya kisiasa ,yapo memngi ya kuwavutia wananchi na si kuhusu mafisadi jambo ambalo limeanza kuchujuka na kuondoa mvuto,siku zinakwenda tumebakishwa na mafisadi yaani CCM wametuachia pelemende ya kijiti tumungunye katika mikutano hatuna jipya ,au uongo Chadema hawana jipya zaidi ya kusakama fisadi mmoja mmoja.

Sasa kama unavyoona wamejikita ndani ya UCCM upinzani unamtetea kada wa CCM how comes ,siasa za upinzani kila siku mnaambiwa
usijaribu kujiweka hata dakika moja kwenye Chama Tawala ,naweza kusema Zitto alifanikiwa kuchonganisha ndani ya CCM na kuzidisha matatizo akiigawa CCM mapande mawili ,alikuwa amefanikiwa kabisa lakini akina Slaa na Mbowe wamempiga na chini kweli au uongo ? Wao wapo na Mwakiembe wakimkandamiza Rostam wakati Mwakiyembe nae ana lake limemkaa shingoni na lilikuwa limeanza kushika kasi ,Mbowe na Slaa wamekuwa watetezi ,hivi kuna upinzani hapo ?

Zitto alikuwa ,naamini kabisa akijua gemu aliyokuwa akiicheza na kwa kweli ilianza kushika kasi ,CCM ilikwisha gawika ,serikali bunge mvutano mtupu ,sasa tujiulize yote yamekwenda wapi ?

Serikali ingenunua kwa wakati ule ingewezekana baadae kuibana kwa kuzitazama sheria za bunge ,tayari kungekuwepo na mtafaruku mwengine ,upinzani ungerudi kwa wananchi na kuwambia mnaona serikali yetu haifuati sheria ,kwani sheria hii na hii inasema hivi ,hapo ingewezekana kubambikiza mambu kibao ,kwa sasa ni vigumu kwani gemu imeshavurugika. Siasa sii mchezo mchafu ila unachezwa kwa triki na mitego ya uangalifu kabisa ,maana ilikuwa tayari Kikwete ameshatoa agizo kuwa panunuliwe ,kuna kitu alisema ambacho kiliashiria kuwa sheria zikiukwe au zisizuie kitu kama hivyo ,Na sita nae akajibu kuwa kama wapo wenye ubavu na wanunue lakini tusije tukaonana maadui hapa Bungeni kitu kama hivyo,ila kwa sasa mtego umeshateguliwa na imebaki makelele tu ,kubadilisha upepo.
 
Naona kuna makundi Slaa ,Mbowwe na Mwakiembe na upande mwengine kuna Lipumba ,Zito na kundi kubwa katika kikao cha juzi hivyo ni bora tukapata vyama vitatu ,Chadema CUF na Sultan CCM ,halafu tuweke uchaguzi wa haki tuone.

Mwakiembe aende Chadema ,Zittto akimbilie CUF na Sultani abakie kama alivyo akiwa na migogoro kibao ya takirima tuelekee uchaguzi mkuu ,Zitto anaweza kuipata nafasi ya kugombea Uraisi 2010 kupitia CUF ,naamini ni nafasi ambayo atapewa tu bila ya matatizo yeyote na asifanye mchezo wa kuamini kuwa Chadema watampatia sidhani kabisa kwanza kule Chadema kuna ukabila au mnaonaje ?

Mwiba kwa habari ya ukabila Chadema umechemka maana nawe umeingia kwenye ule mtego wa Sultani kwamba hiki ni chama Chadema ni cha kikabila na chako Kafu ni cha kidini! je tuamini hivyo?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom