Dr. Slaa, Mbowe wanguruma!

Dr. Slaa, Mbowe wanguruma!

Status
Not open for further replies.
Dk Slaa ataka mitambo ya Dowans itaifishwe siyo kununuliwa

Tausi Mbowe na Elias Msuya
Mwananchi
Date:3/26/2009

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa ameitaka serikali kuitaifisha mitambo ya Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans badala ya kujadili manunuzi yake.

Dk Slaa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada yakutopa taarifa ya kamati kuu kilichokutana kwaajili ya kuandaa mkutano wa baraza kuu.

Alisema kuwa mitambo ya Dowans ilirithiwa kutoka kwenye kampuni ya Richmond ambayo ilibainika bungeni kuwa ni ya kifisadi kwahiyo hakuna haja ya kuinunua tena bali kuitaifisha.

“Msimamo wangu siku zote ni kutaifishwa kwa mitambo ile na siyo kuinunua. Naishangaa serikali, kutaka kuinunua mitambo ya Dowans wakati mitambo ile ilishabainishwa Bungeni kuwa ni ya kifisadi. Kama mtu umekamata kitu chako cha wizi utakinunua tena?" alihoji

Akizungumzia malumbano kati ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Igunga Rostam Aziz, Dk Slaa alisema,


“Mradi wa kuzalisha umeme nimeushughulikia kwa miezi minane. Nilikwenda hadi kijiji cha Kisesida mkoni Singida ambako ndiko kampuni mbili za Power Pool East Africa ya Dk Mwakyembe na wenzake na Wind East Africa ya Rostam Aziz zimewekeza.

Kampuni ya Power Pool East Afrika ni ya wazalendo na imeshalipa fidia kwa wakazi wa kijiji cha Kisesida lakini ile ya Wind East Africa haijafanya hivyo, badala yake inabebwa na kiongozi wa ngazi za juu mkoani ambaye amekuwa akiwakejeli wanakijiji wa Kisesida. Ndiyo maana kuna kuwa na malumbano kati ya Rostam Aziz na Dk Mwakyembe,” alisema Dk Mwakyembe.

Akizungumzia tatizo la mgawo wa umeme ambalo litangazwa na Tanesco hivi karibuni, Dk Slaa alisema,

"Baada ya kubainika kwa kashfa ya Richmond, Rais Kiwete alitangaza kuwa suala la mgawo wa umeme litakuwa historia katika nchi hii, sasa mgawo huu unatoka wapi tena? nendeni mkamwulize,” alisema Dk Slaa.


Aidha alimshangaa Rais Kikwete kwa kuendelea kumwacha madarakani Mkurugenzi wa Tanesco, Idriss Rashid wakati anatuhumiwa kwa ufisadi,

"Dk Rashid alihusishwa na ufisadi alipokuwa Gavana wa Benki kuu. Tumeshatoa vilelezo vyote kuthibitisha jinsi alivyoshiriki kwenye ununuzi wa rada na ndiyo maana sasa hivi anashirkiana na Dowans ili kununua mitambo yake kiufisadi. Tunashangaa kwanini Rais Kikwete hamchunguzi, wala kumwajibisha.

Eti wanasema Serikali ya Uingereza inachunguza, wakati si kweli. Uingereza wanachunguza ushiriki wa BAE system siyo watu wetu,” alisema Dk Slaa.
 
Serikali ya Uingereza inachunguza wizi ulofanywa na raia wa Tanzania walioiba fedha za wananchi wa Tanzania?

Yalabi Toba!

Si mzaha.

Hii ni sawa na mtu mzima mwenye mke na watoto asikiapo njaa kutangaza kwamba ana mpango kabambe wa kushughulikia njaa yake kwani anataraji kupitia kwa mama yake mzazi ili anyonye.

Kuna mambo mengi hayaingii akilini yakatuwama kwa mfano;

1 Rais wa nchi kutoa msaada wa kiitifaki kuiba hazina ya taifa katika benki yetu kuu.

2 Kudhani kwamba kuna kundi la watu huko ughaibuni wasio Watanzania walio na uchungu mwingi sana juu ya Matatizo ya Tanzania, na pengine ni sehemu au ni jukumu lao kutatua au kutoa ufumbuzi na hawalali mpaka wapate suluhisho.

Ni aibu iliyo sawa na kutembea uchi kwa Rais wa nchi au serikali yake kutangaza kwamba upelelezi wa wezi walio raia wa Tanzania na walio iba mali ya wananchi wa tanzania unashughulikiwa na watu au nchi iliyowahi kuwa mtawala wake wa kikoloni miaka 48 ilopita.

Huu ni uchuro.

Tanzania kuna watu walizaliwa bila kuwa na sehemu inayoshughulikia aibu katika ubongo wao.

Mwe!
 
Last edited:
Lets wait and see,mahali panaponitatiza ni pale ambapo Dk Slaa and Mh Mbowe wanaweza kutofautiana na Mh Zitto kwenye suala la Dowans bila kuathiri mwenendo wa chama,hapo ndo nashangazwa,like i said...Lets wait and see.

Hili la msimamo wa chama ndilo tulilokuwa tukilipigia kelele kwa Wabunge wa CCM kule Bungeni kwa kuacha kutowa maamuzi yao kwa kuhofia uamuzi wa Chama chao. Naona kama tunakuwa Double standard katika hili.Wakati CCM wabunge wao wanatofautiana hatutizami mtizamo wa Chama badala yake tunatizama ushujaa wa wale tunaowabeba. Mwakyembe, Sitta, shelukindo wote ni wa CCM na tunajuwa msimamo wa CCM kuhusu hili lakini hatufanyi kuwa issue.

Suala la Zitto kutofautiana na msimamo wa viongozi wengine wa chama chake tunaona kuwa mgogoro ndani ya Chama. Kwa kweli mara nyingi nashangazwa na tunavyovutwa na hisia hata tukajisahau mitazamo yetu na matakwa yetu ni nini hasa.

Kwani kutofautiana kimawanzo ndani ya Chama kimoja ni haramu? Taratibu za kawaida ni kuwa hadi pale mnapoamuwa jambo kwa uwingi wa wahusika ndio linakuwa msimamo wa jumla uliokubalika.Sasa CHADEMA walikwisha towa tamko la uamuzi wa suala hili na Zitto akaenda kinyume baada ya chama chake kuamuwa msimamo? Nafikiri hilo halijafanyika sasa kwanini tuwe na hisia kuwa CHADEMA itaparaganyika kwa msimamo wa Zitto?

Aidha Zitto ni mjumbe wa kamati na ameshiriki katika maamuzi ya Kamati iliyotowa msimamo wa pamoja sasa Chama chake kinahusika na nini kwa hili? Nafikiri wajumbe wakutoka CCM ni wengi katika kamati ya Ziitto nao hawajajitokeza kupinga msimamo huo sasa tuseme hii CCM ni ya kina Mwakyembe au hawa waliokubali kununuliwa DOWANS kwani hatujuwi nani wanaokwenda kinyume na Chama chao.

Nafikiri uamuzi wa Zitto utabaki wa Zitto mpaka pale CHADEMA itakapomwelekeza naye akakaidi
 
- Whaaat Mwiba ni kiongozi wa juu wa CUF hii ni kweli au Sasa mzee thibitisha hili au kubali umekurupuka!
Inafaa umuulize yaani kugandamiza kidogo tu jamaa ameshaniona ni kiongozi wa juu tena wa Chama Cha Vita CUF ,hivi hakusikia kama siku CCM ikianguka ndipo nitakapojiunga nayo na kuwa mwanachama nambari one ili kuimarisha upinzani.

Tatizo tulilo nalo wananchi wapiga kura ni kupenda Chama na kuona mimi ni wa Chama fulani ,inaweza kukubalika ,lakini kukubalika kwenyewe isiwe umetekwa kimawazo au umetekwa uhuru wako kwa maana huyo mbunge hakuletei au kukumegea feza yeyote ile kutoka kwenye mshahara wake na kukugawia angalau ukanunue mkate na kupata kijio cha kila siku,wananchi waelewe kuwa wanayonafasi ya kumchagua mbunge au kiongozi kwa kumpima.

Uwezo wake katika kuhimiza maendeleo yanayoletwa na serikali yanawafikia wananchi ,ikiwa hafai basi unahamia kwa mwengine ,si lazima umchague mtu kutoka CUF au Chadema ingawa wewe ni wa vyama hivyo wakati hawaonekani kukuletea maendeleo ndio maana kunatokea nafasi ya kuwahoji na kuwauliza masuala wanaotetea au kuwania ubunge na nafasi zingine za uongozi.

Vyama haviwafahamishi wananchi juu ya kutumia kura yao kila msimu kwa kupima ni kitu gani mbunge waliemchagua amewaletea maendeleo ameonekana akiwa nao katika kupambana na matatizo pamoja na mahitaji ambayo yalihitajiwa juhudi za serikali.

Ni lazima wananchi wafahamu faida ya uwepo wa vyama viingi na kuwa wao ni wenye nguvu za kuweza kuchagua mtu badala ya chama.CCM wapo wabunge ni wachapa kazi na wanaonekana katika sehemu zao wakichanganyika na kuwasaidia wananchi si kwa kuwahonga fedha bali kuhakikisha kuwa mahitaji au shida zao zinazohusiana na serikali zinapatiwa ufumbuzi.

Kuna fununu kuwa Wananchi wa Pemba huenda wakawachagua wabunge kupitia Chadema kutokana na uongozi wa CUF kujitenga na hoja zao au kushindwa kulinda ushindi ,kwa sababu wananchi wa Pemba wameiwezesha CUF kutwaa ushindi wa Uraisi mara zote lakini mbinu za kuulinda ushindi huo hazikuonekana kwa Chama ,Chama kiliwaomba wananchi kura zao ,wananchi wakatoa kura hizo na kulinda ushindi huo ,hatua ya mwisho ambayo wanaoshiriki ni viongozi wa Chama wa juu wameshindwa kutetea ushindi huo ,hivyo inasemekana mara hii wasirudi kuomba kura kwani wameshindwa kura walizopewa ,sasa huenda kura zikaelekezwa Chadema ili kuwapa fursa viongozi wa Chadema kupambana na Sultani CCM katika kulinda ushindi watakao pewa.
 
Naona kuna makundi Slaa ,Mbowwe na Mwakiembe na upande mwengine kuna Lipumba ,Zito na kundi kubwa katika kikao cha juzi hivyo ni bora tukapata vyama vitatu ,Chadema CUF na Sultan CCM ,halafu tuweke uchaguzi wa haki tuone.

Mwakiembe aende Chadema ,Zittto akimbilie CUF na Sultani abakie kama alivyo akiwa na migogoro kibao ya takirima tuelekee uchaguzi mkuu ,Zitto anaweza kuipata nafasi ya kugombea Uraisi 2010 kupitia CUF ,naamini ni nafasi ambayo atapewa tu bila ya matatizo yeyote na asifanye mchezo wa kuamini kuwa Chadema watampatia sidhani kabisa kwanza kule Chadema kuna ukabila au mnaonaje ?

Unafahamu Katiba ya JMT inasema nini kuhusu umri wa mgombea kiti cha urais? Mwaka 2010 Mh Zitto atakuwa bado kufikisha umri unaoruhusiwa na katiba.

s 39.-(1) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama-
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Sheria ya Uraia.
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(d) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi,
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Labda kwanza tuzungumzie kubadili katiba ili kuwezesha vijana (chini ya miaka 40) kugombea nafasi hiyo nyeti.
 
Enhe......nimetega sikio kuona thread inaenda wapi....
Sina cha kuchangia acha tu niongeze mabandiko, lol
 
Mzee Mwanakijiji & Invisible,
Nafikiri huu sio tena wakati wa kutoa press conferences maana hazisaidii upinzani kabisaa. Hizi zinawaumiza zaidi CCM na ndio maana Malecela akawakataza wanaCCM wasizitumie na sio wapinzani.

Wapinzani inatakiwa sasa tuanze kuchukua hatua ngangari zaidi za kumuondoa au kummaliza nguvu Kikwete kama maandamano, migomo, mikutano ya hadhara n.k.

Hii ndio njia pekee iliyobaki maana kama tulivyomsikia Mzee Malecela ameshaeleza kuwa Kikwete anachoogopa ni upinzani ndani ya CCM na sio nje yake.

Yaani Mkulu nakuunga mkono 1000%.Maneno matupu hayavunji mfupa.
Niweke rekodi ili wachangiaji waweze kujua kilichozungumzwa na kimezungumzwa wapi.

Tangu jana CHADEMA wamekuwa na Kamati Kuu ya chama TAIFA na leo wanaendelea na kikao cha Baraza Kuu la Chama Taifa.

Hivyo basi kutokana na mikutano hiyo Kamati Kuu jana ilifanya maamuzi mengi juu ya mwelekeo wa chama na Taifa kwa ujumla.

Ni kweli jana wanachama 12 wa chama walifukuzwa uanachama kutokana na ripoti maalum iliyokuwa imetokana na KAMATI NDOGO YA KAMATI KUU iliyoundwa mwaka jana mwezi wa kumi na moja ikiwa inaongozwa na mwanasheria mahiri mzee Bob Makani.

Wajumbe wengine wa kamati hiyo walikuwa ni pamoja na ;
Prof.Baregu, Mustafa Akoonay ambaye ni wakili wa kujitegemea na mjumbe wa kamati kuu, Edson Mbogoro mwanasheria wa kujitegemea kutoka Ruvuma,Mama Chiku Abwao .

Makatibu wa kamati hiyo walikuwa ndugu Tundu Lissu akisaidiana na Halima Mdee.

Baada kazi ya kamati hiyo walifulkuzwa wanachama 12 ambao walikuwa wakijiita wanachama wa Dar es salaam huku wakuwa wanatumiwa na CCM kukivuruga chama.

Mtakumbuka pia kuwa wakati wa mchakato wa uchaguzi Tarime hawa jamaa ile wiki ya mwisho waliandamana kupinga chama kushiriki uchaguzi Tarime kwa hoja kuwa kilihusika kumuua Wangwe.

Kuhusu Rostam.
Leo Dr.Slaa kaamua kuuvunja mzizi wa fitna pale alipoweka wazi kile ambacho kinaendelea kati ya Rostam , Mwakyembe e.t.c kwa kuweka ukweli hadharani juu ya kampuni ya kuzalisha umeme ambayo inamilikiwa na Rostam inaitwa PE (POWER ENERGY).

Kampuni hii inalitaka eneo la kijiji kinaitwa Kisasida , na kampuni ya Rostam inamilikiwa kwa ubia wa yeye pamoja na Lowassa , na ndio maana utaona jinsi ambavyo mkuu wa mkoa wa Singida alikuwa mstari wa mbele kuibeba kampuni hii ya Rostam na Lowassa .

Hili limepelekea CHADEMA kumfikisha mkuu wa mkoa mahakamani na tangu jana alishapelekewa barua ya kusudio la kuburuzwa mahakamani baada ya kumtukana mwenyekiti wa kijiji hicho pamoja na viongozi wa CHADEMA kwenye mkutano wa hadhara.

Kampuni hii ya PE na ile ya wakina Mwakyembe wako kwenye kupigania kupata eneo kwenye kijiji hicho.

Mengine nitawaeleza zaidi baadae.

Katika yooote hilo la kumburuza RC mahakamani ndio la muhimu zaidi.Actions speak louder than words.
 
Hivi Tanzania hatuna sehemu za kusajili intellectual property? Kama vipi unamwacha anaiba plan/idea halafu unampiga bonge la suit.

Hakuna Mkuu.... Nchi hii iko kimtego mtego tu. Kila kitu kimekaa tayari kulipuka
 
Hi vita ndiyo kwanza inaanza, hata kama JK haogopi upinzani nje ya CCM mwisho wa siku atajua kuwa kuna nguvu kubwa ya watanzania walio nje ya chama chake ambao wanaweza kuamua hatma ya nchi hii!
 
wewee patamu hapo! chezo ndio kwanza linaanza..![/QUO

Watu wenye mawazo ya aina hii ndio wametufikisha hapa tulipa yaani nchi viongozi mafisadi na wasiojali maslahi ya watanzania.

Ni kosa kubwa sana kufananisha jitihada hizi za wapiganaji wetu kama akina W. Slaa na mchezo wa kuigiza. Hawaigizi,men at work bwana
 
Tupe hiyo audio,au bado unafuatilia.we are waiting for audio to discuss more on this topic
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom