Dr. Slaa & Lema waiangamiza CCM bila huruma

Dr. Slaa & Lema waiangamiza CCM bila huruma

mtemiwao

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2010
Posts
384
Reaction score
46
Habari wana jf,nimepata habari toka kwa jamaa yangu alieko gta kuwa dr slaa na g.lema leo (mida hii)wanaeneza moto wa ukombozi kwa wakazi wa gta,kama kuna mwana jf aliyeko sehmu ya tukio tafadhali atupe live
 
Tanzania inakombolewa , PEOPLE'S POWER = CDM

Kila mwenye macho, masikio, haitaji kuambiwa au kuonyeshwa wakati umefika uliosubiriwa muda mrefu wa kuirudisha nchi mikononi mwa wenye nchi . Nilisubiri niko sekondari, sikupata, vyama vya upinzani vikaingia.

Nyerere akasema , ninaona chama pekee cha upinzani ni CHADEMA.

Na sasa CDM inachukua nchi, kila mtanzania halisi ni wakati wetu wa mwanzo mpya, hongera wapiganaji, tupo pamoja, kuwang'oa hawa magamba.
 
Mkutano umeshaanza,sasa kamaliza kuongea aliyekuwa diwani wa CCM kata ya Sombetini kabla ya kuhamia CDM ndugu Mawazo Alphonce na sasa kamanda Lema anapanda jukwaani.Watu ni wengi sana,hakika uwanja wa magereza umetapika,tutaanzisha thread kwa ajili ya picha hapo baadaye.
 
Kesho madiwani wanne na wenyeviti wa vitongoji 22.
Keshokutwa tutasikia Madiwani 50 kutoka Iringa, 50 Pwani, 50 Singida, 50 Tabora!

Yaani itafikia CHADEMA watazidiwa na mapokezi ya wageni sijui itakuwaje.
Makamanda karibuni CHADEMA karibuni kwenye harakati za Ukombozi.

Angalizo: CHADEMA Makao Makuu kadi zinahitajika kwa wingi sana, kwa mfano hapa Arusha zinahitajika kadi zaidi ya 2000 zinahitajika, watu wamedertermine kurudisha kadi za ccm tumeshindwa kuwapa za chama tumeishiwa!
Tumani Makene take into consideration plse!
 
Ee Mungu watie nguvu makamanda wetu, ukombozi utimie mapema, wananchi twateseka sana na haya maisha.
Teketeza ma-ccm yote, yametutesa sana, alafu mungu, saidia zile kura 71 zipatikane leo jioni.
Peopleeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeees!
Poweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeer
 
Mungu wetu anatupigania,kwa nia njema aliyokuwa nayo Dr na viongozi wengine na sisi tutashuhudia uhuru wa nchi yetu toka kwa mkoloni ccm.Tunaanza na Mungu,tunamaliza na Mungu
 
Update tafadhali,arusha na hapo ni mbali twawategemea ku2juza
 
Kama nilivyoahidi Jana kwamba nitawaletea Picha wakati ktano ukiendelea.Baada ya kikao cha Ndani kilichoahirishwa kwa muda ili kupata fursa ya mkutano wa Hadhara.Dr slaa amepokea madiwani wa CCM kutoka sengerema baada ya Chadema,pia diwani wa Sombetini-Arusha amesimama jukwaani na Kuhutubia.

IMG_4112.jpg

Dr Slaa akiongoza kikao cha ndani

IMG_4148.jpg

Mkutano wa hadhara

IMG_4145.jpg

Kwenye picha hapo juu Diwani Tabasamu(aliyevaa kombati wanaokumbatiana) akipokelewa na makamanda


IMG_4141.jpg IMG_4146.jpg
 
M4C songa mbele waambieni hata wakibana Bungeni kazi ipo palepale tu 2015.!
 
Kwenye picha hapo juu Diwani Tabasamu(aliyevaa kombati wanaokumbatiana) akipokelewa na makamanda
Mkuu naomba niulize, hilo kombati ameshona lini, au alikuwa nalo tayari nyumbani?
 
Kama nimekusoma vizuri una maana madiwani wawili wa Sengerema na mmoja wa Arusha Sombetini. Baada ya kikao cha bunge turudishiwe ile operation Twanga Kotekote tuwaraaaaammbeeeee hawa magamba.
 
Back
Top Bottom