Dr. Slaa & Lema waiangamiza CCM bila huruma

Dr. Slaa & Lema waiangamiza CCM bila huruma

Mkuu Ben,

Asante sana kwa taarifa, hii inatia hamasa magamba wengine kujiunga na CHADEMA tayari kwa harakati za ukombozi wa kweli wa Tanzania ya watu wapole, wastaarabu, wanyenyekevu, wakarimu, lakini siyo wanyonge!

Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki CHADEMA

MAPAMBANO YANAENDELEA
Yaani natamani ningekuwa maeneo husika...Mkuu J5 wako Arusha ujiandae....
 
524682_3724059142443_1304804641_33573091_457856436_n.jpg


487524_382072005145930_148053981881068_1381004_1734355057_n.jpg


serikali na ccm kama walifikiria kutokuwepo dr. Slaa kwenye bunge na hatimaye mizengwe ya kumtoa ubunge godbless lema ni mafanikio sasa hali imegeuka kilio na kusaga meno kwa serikali na chama chake ccm. Uhuru na nafasi waliyo nayo pamoja na ushawishi mkubwa, hali kadhalika mizengwe iliyotumika kumvua ubunge ndiyo chachu ya wananchi wengi kuwaona watu hawa ni wapigania uhuru wa kweli kama madiba wa bondeni.

Shibodo alisema makapa kusema maneno ya ovyo yasiyostahili kwa mtu mkubwa kama yeye ikiwemo matusi, dharau na dhihaka dhidi ya wananchi wa tanzania kupitia vyama vya upinzani yamewakasirisha sana watanzania, leo yametimia, moto huu kuuzima ipo kazi, na hadi kufikia 2015 ccm yatabaki mabua tu.




dr slaa na lema wanazidi kuchanja mbuga kuimarisha uhai wa chadema


go cdm go!
 
Hizi Picha ni Za Arusha hiyo hapo juu Ni viwanja vya fire na hiyo ya chini niwakati Dr. Slaa anakwenda kwenye mkutano Ambureni kwenye kampeni ya Nassari
 
Hongereni Kanda ya Ziwa, maana naona na wazee wapo katika mikutano ya Ukombozi
 
Simnaona wanavyokula fegha za maendeleo halafu wanasema kasungura kadogo cag kawaumbua haooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo mwisho wenu 2015 hamna maana kabisa nyinyi,hosptali hazina dawa wanafunzi wanakaa chini,nyinyi mnafanya sherehe za nanenane,miaka hamsini ya uhuru,hao ,watu mnao waonesha wangekuwa wamekufa mngeonesha miti,ng'ombe.
 
Kesho madiwani wanne na wenyeviti wa vitongoji 22.
Keshokutwa tutasikia Madiwani 50 kutoka Iringa, 50 Pwani, 50 Singida, 50 Tabora!

Yaani itafikia CHADEMA watazidiwa na mapokezi ya wageni sijui itakuwaje.
Makamanda karibuni CHADEMA karibuni kwenye harakati za Ukombozi.

Angalizo: CHADEMA Makao Makuu kadi zinahitajika kwa wingi sana, kwa mfano hapa Arusha zinahitajika kadi zaidi ya 2000 zinahitajika, watu wamedertermine kurudisha kadi za ccm tumeshindwa kuwapa za chama tumeishiwa!
Tumani Makene take into consideration plse!

Usisahau kabla ya mwaka kuisha pengine na wabunge wanne watano na mawaziri wawili bila kusahau wanachama waandamizi waliowahi kuwa viongozi hapo awali
 
Mods, nimejaribu kuweka summary ya hotuba ya dr.Slaa kwenye ile post ya Ben ambayo imeunganishwa na hii, mbona siioni? Ingewasaidia wengi kujua alichokisema dr. Tafadhali niisaidieni kuiweka hapa.
 
hatari iliyoje,ukiona njigi utadhani njege na ukiona njege utadhani njigi.Siku zote dalili za moto ni kufuka kwa moshi.Nguvu ya umma ni sauti ya Mungu.Mabadiliko ya kweli hayawezi toka ndani ya mfumo ule ule,kwa staili hii hata akija malaika kwa mfumo huu wa magamba naye anaweza akawa gamba,cha muhimu ni kuvunja mfumo dume na kusimika utawala ulioridhiwa na watu kwa harakati zao binafsi bila kuwabagua wala kuwabeza.

Hata siku moja haiwezi kutokea ukabadilisha chupa lakini mvinyo ule ule.CDM ni wakati wenu kutumia nguvu ya umma kama mlivyoanza na Mungu na kumaliza na Mungu.Kifo kinapofika mtu hukifuata yeye mwenyewe,CCM wamekifuata wenyewe kilchobaki tuwavishe sanda wakati wao umefika ili ifikapo mwaka 2015 tuhitimishe jukumu la kuzika.
 
Back
Top Bottom