Dr. Slaa hatimaye aibuka


Haki ya nani hizi siasa ni kizunguzungu kitupu.
 

Mwacheni Dr Slaa apumzike ajitafakari alipo na alikotoka ajipime. Nina imani hawezi kuwa msaliti naelewa ni mkweli wala hanunuliki nategemea atatu suprise kwa ujio wake ili kuipa ushindi Ukawa. Hapo ndio ccm wote mwili utawalegea kwa mshangao.
 
Ukombozi hauwezi kusubili mtu mmoja mmoja akubaliane na wengi chadema inamhitaji dr slaa lakini watanzania wanamhitaji zaidi lowasa awe raisi wao ..............
 

Mkuu wanaopiga kelele humu ni wale team El eti kwamba watavuna members humu jf, ila kwa jinsi nnavyowajua wana jf hawashawishiki na maneno ya juujuu , matusimatusi, zomea zomea ,,, kuponda,, kejeli vinavyotumiwa na team el ili mradi tumuunge mkono bwana wao,
Wanawezaga kuwarubuni watu wasiofikiria hata kidogo lakini humu wanapiga kelele tu.

Nawaambia team El acheni tamaa, fanyeni kazi mpate kipato halali ,,,,, mmeitolea macho TZ yetu ,,,mnataka kuitafuna bila huruma.
Tutakuja kuwanasa tu..au mnadhani hela zitawaokoa?
 
"DK SLAA amefunguka kwamba dakika za mwisho MBOWE aliwaburuza na kulazimisha tumpokee LOWASA , hapo nikaona nikae pembeni. muda si mrefu nitaitisha press confrence kwani watu wanapotosha sana kuhusu mimi DK SLAA."
 
Kaka mkubwa tuwaache hao majirani hebu tuangalie maisha yetu yanavyokuwa magumu..maana ukiamka ni Lowasa Dr
. Slaa wakati hali zetu ni mbaya ktk mikakati yetu kushinda tena na tenaa
 
"DK SLAA amefunguka kwamba dakika za mwisho MBOWE aliwaburuza na kulazimisha tumpokee LOWASA , hapo nikaona nikae pembeni. muda si mrefu nitaitisha press confrence kwani watu wanapotosha sana kuhusu mimi DK SLAA."
Yeye aende anakoenda na ataenda yeye na familia yake. Sisi ni wafuasi wa chama siyo wa mtu , nafikiri majibu mmeyapata kwa LIPUMBA. Wasaidieni hao watu kiuchumi lakini sisi malengo yetu yako palepale kumwondoa mkoloni mweusi CCM oktoba.
 
yeye aende anakoenda na ataenda yeye na familia yake. Sisi ni wafuasi wa chama siyo wa mtu , nafikiri majibu mmeyapata kwa lipumba. Wasaidieni hao watu kiuchumi lakini sisi malengo yetu yako palepale kumwondoa mkoloni mweusi ccm oktoba.

leo unamkana dk
 
leo unamkana dk
Mimi siku zote ni mfuasi wa chama si mtu. Ukiwa mfuasi wa mtu je akifa utafanyaje? Kama yeye kachoka aende anakoenda au apumzike kama afanyavyo kwani umeona kazi zimesimama kwa yeye kutokuwapo? Kufa kufaana.
 
Chama kwanza mtu baadaye! Hakuna mtu maarufu zaidi ya chama! Akitaka afuate nyayo za Lipumba!
 
dr.slaa hebu shusha pumzi urudi tukijenge chama,hasa kipindi hiki cha uchaguzi.
 
"DK SLAA amefunguka kwamba dakika za mwisho MBOWE aliwaburuza na kulazimisha tumpokee LOWASA , hapo nikaona nikae pembeni. muda si mrefu nitaitisha press confrence kwani watu wanapotosha sana kuhusu mimi DK SLAA."

Kwahiyo?
 
Kadi yangu ya CDM imekuwa mzigo mzito sana kwangu kwa sasa, tokea gia ilipobadilishiwa angani, in the name of politics is the game of dynamics.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…