Dr. Slaa awatembelea Majeruhi wa Kijeshi

Dr. Slaa awatembelea Majeruhi wa Kijeshi

Rtackket

Member
Joined
Sep 24, 2013
Posts
74
Reaction score
373
Mwaka 1978, maelfu ya watanzania walijeruiwa katika vita vya Kagero wakijaribu kuilinda Tanzania. Hawa mashujaa HADI wa leo wengi wao wametelekezwa na serikali ya CCM. Wanaoshiriki kutunza amani chini ya umoja wa mataifa nao udhulimiwa haki zao mafao yao yanapoletwa nchini chini ya usimamizi wa CCM.

Chini ya utawala wa CHADEMA. Dhuluma zinazoendelezwa na serikali ya kidhalimu ya CCM itafikia tamati

Dr. Slaa yuko Marekani katika ziara maalum ya kujifunza inayoitwa "Vision Tanzania" itakayomuwezesha kujifunza mambo mbali mbali kwa manufaa ya watanzania. Dr. Slaa anaamini kwamba Tanzania ina uwezo wa kuwaudumia wananchi wake pamoja na wanajeshi wake ikiwa nchi itatumia rasimali zake kwa manufaa ya nchi na siyo kwa ajili ya wachache.

Dr. Slaa anaamini kwamba Tanzania inahitaji Serikali ya wananchi na siyo serikali ya watawala.

Dr. Slaa kwa unyenyekevu alikubali mwaliko kuwatembelea majeruhi katika hospitali kubwa ya kijeshi jijini Bethesda Maryland ambako alikula chakula cha mchana na majeruhi mbali mbali kutoka Vitani Afghanistan

Bila shaka, ni safari ya kihistoria. Dr. Slaa anawaomba watanzania wajitayarishie mabadiliko. Anawaomba vijana wote wame mstari wa mbele kusambaza habari njema za mabadiliko ili kumn'goa adui wa mtanzania CCM ! mama wa ufisadi

Re: Breaking News: Dr. Slaa, An Humble man of The People At US Walterreed

attachment.php

Dr. Slaa Alipowasili katika hospitali kubwa ya kijeshi ya Waltrereed Jijini Bethesda Maryland leo mchana
attachment.php


Mpiganaji (marine) akionyesha furaha yake kutembelewa na kiongozi wa aina yake. Eric aliumia nchini afghanistan. Eric licha ulemavu alioupata anaamini kwamba pamoja na matibabu anayoyapata, atarudia maisha yake ya zamani. Cha kusisimua zaidi ni uwezo wa kipekee wa muziki. Eric hivi karibuni atafanya tamasha kubwa sana jijini NY kuchangisha fedha kusaidia mayatima nchini Ethiopia. Eric amemuhadi Dr. Slaa kwamba atakuja Tanzania kufanya tamasha ya kuwasaidia mayatima !

attachment.php


Corry, moja ya majeruhi akiteta jambo na kiongozi huyu wa kipekee wa Tanzania.

attachment.php


Majeruhi, mashujaa wanamuziki wakipiga picha ya Pamoja na kiongozi wa CHADEMA. Mh. Slaa. Ingawa hawarudi kwenye hali yao ya kawaida. Wamemuahidi Dr. Slaa kwamba chini ya miaka miaka, miwili, Tamasha lao la kimataifa itakuwa Tanzania. Wameguswa na unyenyekevu wa Dr. Slaa

attachment.php


Lucas na familia yake, Moja ya maktari waliokuwa wakiwasaidia majeshi ya marekani nchini Afghanistan wakipiga picha ya pamoja na Dr. Slaa

attachment.php


Dr. Akiongea na moja ya majeruhi kwa huzuni kubwa. Huyu kijana alipoteza miguu yake yote na sasa hivi anafanya
mazoezi ya kutembea kutumia miguu bandia. Cha kusisimua ni kwamba, hawa vijana hawahitaji huruma. Wanajiona kama raia wengine. Wanaamini wakishajifunza kutembea wataingia uraiani, au watarudi jeshini kuendelea na maisha yao



 
Hebu wekeni mambo yenye tija na nchi, huruma yake kwa raia wa nchi nyingine waliopata madhara ya kivita kwa sababu ya sera zao sisi inatusaidia nini???!!!!!!

Humu ndani kuna shida nyingi sana na wanaohitaji faraja wapo wengi sana kamaliza kuwafariji hawa wetu???!!!

Sio kila alifanyalo kiongozi wote tutachukulia kama positive, mimi binafsi sioni tija ya hili tukio la huyu kiongozi kwa kweli.
 
Safi sana ni vizuri kujifunza kila siku maandalizi mazuri ya kuongoza nchi....i call him Papa!
 
.....Kweli ana unyenyekevu sana kwa Askari majeruhi wa Marekani,ila pale wale wa Tanzania walipouawa Sudan na Congo ata pole tu hakutoa....
 
Ni hatua nzuri inayoonyesha kukomaa kidiplomasia kwa Dr. Slaa. Kila la kheri angalia na mazuri yanayoweza kuja kuchochea juhudi za watz katika kujiletea maendeleo.
 
Slaa hatujamuoma kutembelea hospital za wanajeshi wa Tanzania. Anajipendekeza tu huko kutaka kitu kidogo.
 
Kumbe Dr. Anakifaa kikali namna hiyo! Ni wa ukweli kuliko hata dada yake na Habyarimana.
 
.....Kweli ana unyenyekevu sana kwa Askari majeruhi wa Marekani,ila pale wale wa Tanzania walipouawa Sudan na Congo ata pole tu hakutoa....

Acha Upotoshaji.Juzi Mwenyekiti wa Chama alihudhuria katika Msiba wa Askari wa Tanzania aliyeshambuliwa Huko DRC.
 
Acha Upotoshaji.Juzi Mwenyekiti wa Chama alihudhuria katika Msiba wa Askari wa Tanzania aliyeshambuliwa Huko DRC.

Dogo we si ni msomi kabisa?!,sasa hapa umeeleza nini?!jamaa kamzungumzia Dk Slaa wewe unamzungumzia Mbowe!dah.
 
Mleta mada jaribu kuwa objective kuhusiana na safari ya Dr. Slaa kama wewe una simama kama ni CHADEMA public relation official otherwise, mapambo yako unayompamba Dr. Slaa yanaonyesha kama ndiyo ameanza kupata International Exposure kwa sasa wakati Dr. Slaa alishawahi kuishi na kusoma katika nchi za magharibi na kikubwa zaidi aliaminiwa na wananchi asilimia zaidi ya 24 kutaka awe Rais wa nchi 2010, kwa maana kuwa walimuona tayari anayo hayo mapambo unayojitahidi kumpamba kwa sasa.

Halafu kwa mawazo yako unafikiri Marekani ni kila kitu kana kwamba sera za Marekani kiuchumi, kisasa na kijamii ndiyo mwarobaini wa maendeleo Tanzania kwa maana kwamba kujifunza sera hizo ni kutibu matatizo ya Tanzania.

'Vision Tanzania' ipatikane Marekani?. Mabandiko yako yanaonyesha uko nje ya reality kuhusiana na siasa za Tanzania.

Unapokuja na maneno kama "Vision for Tanzania, Dr. Slaa Takes America By Storm !" and "Delivers one of the greatest foreign policy yet from any African leader". Inabidi tukushangae wewe na kitengo chako katika safari ya Dr. Slaa.

Spinning zako zinamfanya Dr. Slaa aonekane kwa watu wenye fikra pana kama kibaya chajitembeza wakati ninaamini sivyo hivyo.

Ni angalizo tu na unaweza kukubali kutokubaliana kama unaona Vision for Tanzania inapatikana Marekani peke yake.
 
Hebu wekeni mambo yenye tija na nchi, huruma yake kwa raia wa nchi nyingine waliopata madhara ya kivita kwa sababu ya sera zao sisi inatusaidia nini???!!!!!!

Humu ndani kuna shida nyingi sana na wanaohitaji faraja wapo wengi sana kamaliza kuwafariji hawa wetu???!!!

Sio kila alifanyalo kiongozi wote tutachukulia kama positive, mimi binafsi sioni tija ya hili tukio la huyu kiongozi kwa kweli.

Lina tija kuliko Press Release ya Ikulu iliyosifia Rais Kukumbatiwa kisa aliuza raslimali za nchi kwa mikataba ya siri kwa namna isiyotofautiana na weledi wa kiwango cha Chifu Mangungo wa Msovero na Jasusi la Kikoloni Carl Peters!

Haujui katika nafasi yake Kama Mwenyekiti wa CCRBT kuna correlation gani katika ziara hiyo.Hutaki kufanya research wala kuuliza.Ni ku-punch keyboards tu na kubofya sent button.Really?
 
Slaa hakuhudhuria mazishi ya muhanga wa vurugu za Chadema Morogoro ambaye alizikwa kwao Tanga. Lakini ana huruma na wanajeshi wa Marekani waliothirika na vita ya Afganistan mpaka amefunga safari kuvuka bahari kwenda kuwapa pole!!!

Vituko...
 
Mbona vasco da gama wako alikwenda pale waltereed.Tulisema nini sisi?unataka tuweke picha zake?.
 
Dogo we si ni msomi kabisa?!,sasa hapa umeeleza nini?!jamaa kamzungumzia Dk Slaa wewe unamzungumzia Mbowe!dah.

Usomi ni kuzingatia protocal na pia mgawanyiko sahihi wa majukumu.Alienda Mwenyekiti Kwenye Msiba,je kwanini huyo msomi alazimishe Dr.Slaa aende au alihoji akiwa na malengo gani?
 
Slaa hakuhudhuria mazishi ya muhanga wa vurugu za Chadema Morogoro ambaye alizikwa kwao Tanga. Lakini ana huruma na wanajeshi wa Marekani waliothirika na vita ya Afganistan mpaka amefunga safari kuvuka bahari kwenda kuwapa pole!!!

Vituko...


Kwa sababu huko ndiko wanakotoa fedha zao nyingi kwa ajili y shughuli zao nyingi.
 
Olesaidimu,
Tumia akili uliyopewa bure na Mwenyeezi Mungu. Sikuenda Water Reed kufariji. Kufariji ni sehemu ya lazima ya mawasiliano Kati ya binadamu na binadamu. Water Reed ndiyo Hospitali kubwa ya kijeshi kwa Marekani yote. Inatumia teknolojia ya kisasa katika kutoa huduma ya matibabu. Inaona jinsi wapiganaji wao, miguu yote imekatwa lakini wanatumia miguu bandia kana kwamba hakuna kilichotokea. Ni binadamu wa ajabu tu atawaza Kama unavyowaza badala ya kujifunza teknolojia hiyo iwasaidie wapiganaji wetu. Dr Slaa siyo wa aina unayofikiri. Nenda CCBRT hospitali ambayo Dr Slaa ni mwanzilishi na Mwenyekiti uone huduma wanayopewa watanzania wenzako. Fikiria kabla hujatamka daima. Kuna taifa kufanya utafiti kabla ya kutoa tamko lolote. Nina hakika kwa kutembelea Water Reed Hoospital, Taifa letu litanufaika kwa kiwango kikubwa. Taifa linajengwa na watu wenye positive thinking. Watu wanaotafuta kila sekunde solutions kwa mazingira magumu yanayotukumba. Watanzania tushikamane, Hali yetu ngumu haitokani na maamuzi ya Mungu Bali ugumu wa mioyo yetu, above wa mipango yetu, kukosa vipau mbele. Fikiria wazee wetu wamepigania kukomboa Taifa letu toka Nduli Amini, Leo hawana miguu, wengine mikono, lakini wameachwa na kutelekezwa na Taifa walilotetea hata kwa kupoteza maisha Yao. Ushabiki hautufikishi mahali watanzania. Tulipokosea tukubali na turekebishe.





Hebu wekeni mambo yenye tija na nchi, huruma yake kwa raia wa nchi nyingine waliopata m


adhara ya kivita kwa sababu ya sera zao sisi inatusaidia nini???!!!!!!

Humu ndani kuna shida nyingi sana na wanaohitaji faraja wapo wengi sana kamaliza kuwafariji hawa wetu???!!!

Sio kila alifanyalo kiongozi wote tutachukulia kama positive, mimi binafsi sioni tija ya hili tukio la huyu kiongozi kwa kweli.
 
Back
Top Bottom