Dr Slaa atingisha Kigoma Kaskazini

Dr Slaa atingisha Kigoma Kaskazini

Msafara wa Gwiji wa siasa Tanzania na Katibu mkuu CHADEMA Dkt. Wilbroad Slaa ndo unakatiza hapa Kigoma mjini, ishara ya vidole viwili inatanda kila mahali na maneno ya ''Dkt. Slaa huyo huyo...Chademaaaa....Chademaaaa''.

Msafara unaelekea Jimbo la Kigoma Kaskazini Mkutano wa Kwanza utakuwa Nyarubanga, kisha utaelekea mkutano wa pili.

Updates.....

Ndo twawasili Nyarubanga hapa. Akina mama wamejipanga barabarani pembeni kdg ya uwanja wanaimba kumpokea Katibu Mkuu Dkt. Slaa. Msafara umeshaingia uwanjani.

Red Brigade wako imara kweli kweli leo hapa. Wananchi wanasogea sogea. Naona ngoma hapa inachezwa na akina mama.

Updates No 2:

Dkt. Slaa anaingia kucheza ngoma na wenyeji hapa. Ngoma hii inachezwa na kikundi cha ngoma cha akina mama wa CHADEMA kuhamasisha wananchi kujiunga na CHADEMA hasa akina mama na vijana.

Naambiwa inaitwa Denga. Wananchi wanashangilia kumuona Dokta anaungana na akina mama kucheza Denga!

Updates No 3.....

Mkutano umeshafunguliwa na Mkiti Issa Kibaba. Waitara amemkaribisha Mratibu wa Kanda ambaye amezungumzia namna Kanda inavyojipanga kuhudumia wanachama na wananchi kwa ujumla.

Sasa anapanda Mkiti wa Kanda Shaaban Mambo, anazungumza kidogo kwa sbb ya dalili ya mvua kubwa. Sasa amepanda Dkt. Slaa.

Mvua imekuwa kubwa hapa. Wav wamevumilia kumsikiliza Dkt, ambaye ameamua kubadili kubadili mbinu ya mkutano badala ya kuendelea kuhutubia, anatoa nafasi ya maswali kwa wananchi ili wasiende mbali

Updates No 4.....

Watu 4 hadi sasa wameshauliza maswali na Dkt. Slaa anaendelea kujibu maswali yote 5, 3 yanayuhusu maamuzi ya Kamati Kuu kuwavua madaraka Zitto, Kitila na Mwigamba

Mengine 2 yanayuhusu Chadema na misingi yake. Dkt, anaendelea kufafanua, masuala yote yaliyoulizwa.

Mvua inazidi kuwa kubwa hapa. Dkt. Slaa anawauliza wananchi aendelee au afunge mkutano, wananchi wanasema aendelee. Anaendelea hapa.

Mvua kubwa iliyotanguliwa na ukungu mkubwa sana ktk eneo la mkutano imezidi kuongezeka.

Sehemu ya umati wa wananchi wametafuta miamvuli na kubaki karibu na jukwaa. Wengine wako jukwaa kuu, wengine wamekimbilia upenuni mwa nyumba kuendelea kusikiliza.

Mvua ktk eneo hili la mkutano ni kubwa sana, ingawa mbali kdg tu kutoka hapa hakuna ukungu wala mvua.

Updates No 5....

Kutokana na mvua kuzidi kuwa kubwa Wananchi wamemruhusu Dkt. Slaa ashuke jukwaani baada ya kuhutubia kama dkk 45.

Msafara unalazimika kuondoka kwenda mkutano wa pili.

Kuna utani unazungumzwa na baadhi ya wananchi kwamba ''wameshindwa njia zote sasa wameamua kujaribu hii...''.

Lakini Dkt. Slaa kabla hajaondoka jukwaani, aliwaambia wananchi kuwa mvua ni baraka, hivyo wasilaumu!

Picha chini ni kabla mvua haijaanza kunyesha:
attachment.php



Source: Afisa Habari Mkuu CHADEMA Tumaini Makene

DR SLaa...kweli ni tishio halisi kwa CCM!!! Mzee huyu utadhani anamiaka 18!! Mungu mlinde President wetu huyu!
 
itabidi makamanda tubadili mbinu za vita hii sio vita ya damu na nyama tena maana uko wameshindwa sasa ni vita katika ulimwengu wa roho juu ya wakuu wa giza juu ya wachawi,waganga,prof.maji malefu na wengine wengi
 
Kila la heri dr. Slaa, tunaombeni endeleeni kutupa updates za kutosha wakuu!
 
Well done Chadema. Vita na vikwazo ni vingi lakini hatimaye sisi wote Watanzania tutashinda. Magazeti yaliyo mengi kama vile MWANAINCHI,HABARI LEO na mengineyo, yote yako kinyume na harakati halali za Ukombozi dhidi ya UDHALIMU na UKANDAMIZAJI wa serikali ya CCM.
Vilevile vituo vya Televisheni haswa pia ITV sio rafiki wa kuzungumzia UKWELI kuhusu mikutano na matukio ya kisiasa ya Chadema haswa juu ya mikutano inayofanywa na Dr Slaa kule Kigoma.
Wote hao hawaoni uchungu wa UDHALILISHWAJI wa WANAINCHI unaofanywa na UFISADI wa CCM na serikali yake.

CHADEMA tusichoke kuwatetea Maskini na Wanyonge wa Nchi hii,na kuwapigania katika yale yote wanayoyaamini katika ustawi wa Maendeleo yao na ya Taifa kwa ujumla.

VIVA Dr.SLAA;VIVA CHADEMA:
 
Si bora yeye kuliko yule aliyejaladia hadi ulinzi wa majini kwenye kampeni za urais 2010? Nimekumbuka jinsi Kiongozi wa Brigedia ya ulinzi wa Majini alivyotishia hadi wagombea urais wengine kuwa atakayempinga JK atakufa ghafla......

Nilicheka sana kipindi kile nikasema kama presidaaa anaamini majini na ushirikina je wananchi ambao hatujaenda shule
 
wakuu kuna mtu ana habari alipo TUNTEMEKE?nataka aje aniambie mwaka hiyo picha ilipopigwa na wapi
 
Last edited by a moderator:
John Mrema, vipi kile kikao cha jana kilichoazimia kumdhuru kimwili Alex Kitumo? Kidahwe si mmekimbia baada ya mkutano kushindikana, ndio mmeamua kupika hizi picha? Pole sana. Hamna haja ya kuhangaika kuonyesha mafanikio ya ziara ya Dk Slaa Kigoma. We know Kigoma. Nyie mvueni uanachama Zitto ili uchaguzi mwingine uitishwe ili tuone nani mjanja.
 
Hakuna kurudi nyuma. Huu ni ujumbe tosha kwa mahasimu wa haki na maendeleo ya Watanzania
Hii nchi ni ya Watanzania na Watanzania wenyewe ndio sisi tulioamua kusimama nyuma ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Bravo Dr Slaa
 
  • Thanks
Reactions: MC
Tumeanza kuchanganyikiwa. Yaani badala ya kupambana na akina Kinana tupo busy kupambana na Zitto. Ni nani huyo aliyeturoga? Yaani Zitto amekuwa taasisi?
 
Hakuna kurudi nyuma. Huu ni ujumbe tosha kwa mahasimu wa haki na maendeleo ya Watanzania
Hii nchi ni ya Watanzania na Watanzania wenyewe ndio sisi tulioamua kusimama nyuma ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Bravo Dr Slaa

Kwa hiyo sasa hivi mpinzani wetu ni Zitto na sio CCM tena?
 
Back
Top Bottom