Dr. Slaa ashindwa kung'ara Shinyanga

Dr. Slaa ashindwa kung'ara Shinyanga

tata mura

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2012
Posts
275
Reaction score
49
Katika hali isiyokuwa ya kutarajiwa Katibu mkuu wa Chadema na wapambe wake wameshindwa kuonyesha manjonjo yao kwenye kampeni yao ya kumnadi mgombea wao wa udiwani kama walivyo kuwa wanatarajia. Hata kama mnafuatilia waliokuwa wanatujuza waliishia kutuletea picha za kiongozi huyo maarufu wa kisiasa akiwa sokoni tu.
 
Thibitisha mkuu, usituletee hisia zako kudanganya Watanzania.
 
wapi hapo sasa kwenye majonjo uliyotegemea?
 
Eti ameshindwa kufanya manjonjo!


Manjonjo??? Hebu thibitisha unayoyasema kwa umma!
 
CHADEMA SIO CHAMA CHA WANENGUAJI HATA UTARAJIE KUONA MANJONJO YAO, CHADEMA KINAMWAGA SERA TU.

Kama unataka kuona manjonjo nenda kwenye mikutano yenu magamba utawakuta ZE COMEDY, WANAUMEFAMILY, TAARABU(T.O.T) na wasanii wengine kibao wakionesha manjonjo kwa lengo la kuwasahaulisha watanzania matatizo yao ya ugumu na kupanda kwa gharama za maisha yanayoendelea kuwakabili kwa miaka 50 sasa.
 
kwani kikwete huwa anafanya manjonjo yapi? hivi kwenye siasa kuna manjonjo?.
Dr. Slaa anafanya kweli hana manjonjo wala kulemba ndo maana alikuacha kwenye mataa. mia
 
Wapuuzi wengi hupenda kusifiwa haya kwa wadiostahili,wapuuz huchukia ukweli. Call a spade a spade and not a big spoon. Acheni ujuha, km kiongoz wetu hakuleta hamasa ktk kiwango kilichotarajiwa bac tutafte njia ya kutatua tatzo na sio kutaka kusifiwa mda wote km serikali ya sisiem
 
Katika hali isiyokuwa ya kutarajiwa Katibu mkuu wa Chadema na wapambe wake wameshindwa kuonyesha manjonjo yao kwenye kampeni yao ya kumnadi mgombea wao wa udiwani kama walivyo kuwa wanatarajia. Hata kama mnafuatilia waliokuwa wanatujuza waliishia kutuletea picha za kiongozi huyo maarufu wa kisiasa akiwa sokoni tu.
hivi wew unajua kuwa SHINYANGA YOTE ipo mikononi mwa CDM? subiri uone matokeo ya uchaguzi.
 
eeee, makubwaaa, kwani huwa CDM wanafaya manjonjo gani ambayo huko Shinyanga hawakufanya???? Funguka mkuu!
 
Mbona watanzania tunakuwa na mioyo ya kupakwa mafuta na viburudisho vya hii dunia na kutufanya tupoteze utu na haki zetu....nilifanikiwa kutembelea shinyanga siku za usoni ukitoka nje kidogo ya mji maisha hayafai..maji 0%,miundombinu 0%.kwa maana hyo ukija na uzi wa kushindwa kuonesha manjonjo kwenye kampeni unaturudisha nyuma ambako siko tunapo focus.
 
CHADEMA ni chama cha siasa, wala si cha manjonjo.
Kama wewe unataka manjonjo utayapata CCM.
wana jezi za Yanga, wana bongo fleva, wana TOT, wana waarabu kama Rostam Azizi, wana Wahindi kama Dewji, na mashangangingi kibao, full manjonjo na madoido
Katika hali isiyokuwa ya kutarajiwa Katibu mkuu wa Chadema na wapambe wake wameshindwa kuonyesha manjonjo yao kwenye kampeni yao ya kumnadi mgombea wao wa udiwani kama walivyo kuwa wanatarajia. Hata kama mnafuatilia waliokuwa wanatujuza waliishia kutuletea picha za kiongozi huyo maarufu wa kisiasa akiwa sokoni tu.
 
Back
Top Bottom