AHAAAA hapo mkuu ndiyo hasa nilikuwa namaanisha yaani mtelezo kwa mtelezo sasa sijui nani atamtelezea mwenzake, msimamo umeshatoka wa nchi na raisi alisema hayo mbele ya hadhara ya waheshimiwa , kingine ambacho ni ziada ya hili ni kuwa usije ukakuta muheshimiwa ana ajenda na mataifa mengine kwa rwanda. nalisema hili nikiwa na hoja moja kagame tangu siku nyingi alikataa kuwa pamoja na hao FDRL ki masikilizano na baadhi ya mataifa yalimuunga mkono akiwamo baba wa taifa , iweje leo mtu anafufua kitu kilichozikwa siku nyingi , hapo ndipo naanza kuikubali hoja ya dr.slaa kwa upande mwingine utofauti wa kikwete na kagame usije kutuingiza katika vita. lakini kama nchi tuwe wamoja kwa hili
Mkuu nikueleweshe tu kuwa taarifa zilizopo kwenye publica domain sasa kuhusu mauaji ya Rwanda ni tofauti ya zile zilizokuwepo wakati ule wa 1990s. Mengi yaliyokuwa yamefichwa sasa yako wazi, hata Gen. Romeo aliyekuwa kamanda wa UNAMIR amekiri kwenye speech zake na kitabu chake kuwa alikuwa 'fooled' na propaganda za RPF, lakini amekuja ku-realize nao ni wauaji tu. FDLR-FOCA ilianzishwa 2000, ingawaje wapiganaji wake wengine walikuwa ni ex-FAR.
Baada ya genocide ya Rwanda, pia kwa kutumia taarifa ambazo ni biased, Kagame alijinufaisha na genocide kupata misaada na kutumia kama fimbo kuwanyamazisha wapinzani wake nje na ndani ya Rwanda. Alipoingia Congo kwenye vita ya kumtoa Mobutu, Tanzania pia tulihusika, lakini baada ya Kabila kuwa madarakani ilidhirika kuwa dhamira ya Rwanda ni tafauti. Ukumbuke kuwa wanajeshi wa Tanzania walikuwa Congo ili kufundisha jeshi jipya la taifa hilo (hii haikuwa ishara nzuri kwa Rwanda, kwa vile walitaka waache wanajeshi wao wabaki Congo kwa wingi kwa vile uchumi wao haukuweza kubeba gharama zao). Kwa mara ya kwanza hapo, Tanzania na Rwanda zilipishana misimamo. Pili wahutu wengi sana waliuawa kwa kisingizio cha kuwatafuta ex-FAR.
Baada ya Kabila kutoa tamko la kufukuza wanyarwanda wote jeshini (hii ilitokea wiki chache tangu Tanzania kuondoa wanajeshi wake Congo, kwa vile inteligencia ilionesha hali kuwa sio shwari, upepo mbaya ulikuwa ukivuma ndani ya jeshi la Congo). Kilichofuatia unakijua, ambapo ni kufukuzwa kwa kina James Kaberebe na akina Bizima Karaha. Kabarebe akamkalia kooni Kagame ili wampindue Kabila, lakini Kabila akatumia utu uzima kutafuta marafiki wapya ikiwemo ex-FAR, na makundi mengine ikiweo ALiR I na ALiR II ili kupigana na Rwanda. Njama za Rwanda zikashindwa ingawaje wakafanikiwa kumuua Kabila binafsi. Tanzania haikuunga mkono jambo hilo.
Mambo mengi hayo yako kwenye public domain, labda nije direct kwenye swali lako. Ni kuwa mtizamo wa amani mashariki ya Congo umebadilika, ndio maana nchi za maziwa makuu, AU pamoja na SADC wamesema sasa basi. Jaribu kufikiri, ikiwa FDLR ingekuwa na shida na ukweli ungekuwa wazi kwanini UN Intervention Brigade kwenye mandate yao wasiambiwe wa-deal na FDLR badala yake M23 ndio wametajwa wakati wengine wamekuwa mentioned in general?