Mimi binafsi huwa ninafurahishwa na yote uchangiayo bungeni. Hakika Dr. Slaa wewe ni mpiganaji. Mpigania haki za watanzania maskini wanaozidi kufukarishwa kila kukicha. Karibu sana JF. Kama walicyosema wengi hapo awali, kuna wengine humu kazi kwao ni kuvuruga na kukatisha tamaa. Ila naamini uko strong kukabiliana na ya humu JF kwa vile umeweza kuvumilia purukushani za bungeni bila kujali unaungwa mkono ama la, ili mradi uliamini kile ulichokisema ni sahihi na ni kwa maslahi kwa taifa.