Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,547
- 41,059
Wiki hii imekuwa ya majonzi makubwa, ambapo Watanzania wenzetu zaidi ya 60 huko Hannang wamepoteza maisha, mamia wameumia. Lakini pia wapo walionusurika ambao maisha yao yamevurugwa na majanga.
Mengine ya pembeni ambayo hayakustahili kuwepo, nayo yakajitokeza. Badala ya kushikamana na kuhuzunika na wenzetu hawa, polisi wajatia dosari kwa kuonesha hata maafa yanakuwa mali ya vyama vya siasa.
LAKINI wakati haya yakiendelea kuna roho ziliendelea kuumia kimya kimya kutokana na Makamu wa Rais Dr. Mpango kutoonekana kwa muda mrefu, huku taarifa za kusikitisha na kuogofya zikisambaa, bila ya taarifa rasmi ya kuwatuliza watu. Wengine walisema, yu mgonjwa mahtuti, na wengine walienda mbali zaidi.
Katilati ya simanzi hizi, inakuja faraja. Dr. Mpango ameonekana Kanisani kwenye ibada.
Sijawahi kuwa karibu naye, wala sijawahi kukutana naye ana kwa ana, lakini habari zilizokuwa zikisambaa kuwa huenda yu mgonjwa sana au pengine hayupo katika Ulimwengu huu wa mwili, zilinipa simanzi, sawa na wale walio karibu nami katika maisha ya kila siku. Shukrani nyingi kwa Mungu, yeye atujaliaye uhai na kuweka neema katika mema yote tuyatendayo, na anayesafisha maovu na mapungufu yetu.
Nilipoona picha yake leo akiwa Kanisani, machozi ya furaha yalinitoka. Maana maneno yaliyokuwa yamesambaa yalikuwa yamenivunja sana moyo, na mara kadhaa nilipata simanzi na hasira kwa Serikali kwa nini haijali hisia za watu.
Kama alikuwa anaumwa au alikuwa mwenye afya njema, kama alikuwa nchini au nje ya nchi, kwangu hayo yote si muhimu kwa sasa. Lililo muhimu, Dr. Mpango yu mzima, bado yupo pamoja nasi.
Mungu azidi kumjalia maisha marefu yenye afya njema, furaha na amani moyoni mwake, na zaidi ajaliwe hekima ya kumzuia kujishikamanisha na uovu wowote hasa unaoweza kusababishwa na nafasi yake. Maana kuna wakati madaraka yanakupeleka karibu zaidi na ibilisi.
Kama kweli alikuwa anaumwa, na sasa amepona, kwa hiari yake, na wala hakuna ubaya, akafanya kama alivyofanya Rais mstaafu Kikwete alipotoka kwenye matibabu US. Japo najua itakuwa ngumu kwa mpango, maana kufanya hivyo ataona kama anamdhalilisha PM.
Dr. Mpango, kama mwumini mwenzangu, siyo kama Makamu wa Rais:
Kristo bwana wetu, aliteseka, hata kufa kwaajili yetu. Katikati ya mateso aliwapa msamaha watesi wake. Hakuwa na sababu ya kuteswa na hata kuuawa na wanadamu duni, bali aliyafanya hayo kutuonesha wanadamu tunavyotakiwa kuenenda katika maisha yetu. Mwisho Kristo alimshinda shetani, akayashinda mauti, mauti ya mwili na Roho. Bila kujali yaliyosemwa juu yako, yawe mema au mabaya, samehe na sahau yote, badala yake uombe neema ya kushiriki ushindi wa Kristo.
Dr. Mpango ni miongoni mwa watu ambao ningekuwa na access naye, ningefarijika sana kuonana naye. Lakini kujua tu kuwa yu mzima, ni zawadi kubwa ya kutosha.
Mengine ya pembeni ambayo hayakustahili kuwepo, nayo yakajitokeza. Badala ya kushikamana na kuhuzunika na wenzetu hawa, polisi wajatia dosari kwa kuonesha hata maafa yanakuwa mali ya vyama vya siasa.
LAKINI wakati haya yakiendelea kuna roho ziliendelea kuumia kimya kimya kutokana na Makamu wa Rais Dr. Mpango kutoonekana kwa muda mrefu, huku taarifa za kusikitisha na kuogofya zikisambaa, bila ya taarifa rasmi ya kuwatuliza watu. Wengine walisema, yu mgonjwa mahtuti, na wengine walienda mbali zaidi.
Katilati ya simanzi hizi, inakuja faraja. Dr. Mpango ameonekana Kanisani kwenye ibada.
Sijawahi kuwa karibu naye, wala sijawahi kukutana naye ana kwa ana, lakini habari zilizokuwa zikisambaa kuwa huenda yu mgonjwa sana au pengine hayupo katika Ulimwengu huu wa mwili, zilinipa simanzi, sawa na wale walio karibu nami katika maisha ya kila siku. Shukrani nyingi kwa Mungu, yeye atujaliaye uhai na kuweka neema katika mema yote tuyatendayo, na anayesafisha maovu na mapungufu yetu.
Nilipoona picha yake leo akiwa Kanisani, machozi ya furaha yalinitoka. Maana maneno yaliyokuwa yamesambaa yalikuwa yamenivunja sana moyo, na mara kadhaa nilipata simanzi na hasira kwa Serikali kwa nini haijali hisia za watu.
Kama alikuwa anaumwa au alikuwa mwenye afya njema, kama alikuwa nchini au nje ya nchi, kwangu hayo yote si muhimu kwa sasa. Lililo muhimu, Dr. Mpango yu mzima, bado yupo pamoja nasi.
Mungu azidi kumjalia maisha marefu yenye afya njema, furaha na amani moyoni mwake, na zaidi ajaliwe hekima ya kumzuia kujishikamanisha na uovu wowote hasa unaoweza kusababishwa na nafasi yake. Maana kuna wakati madaraka yanakupeleka karibu zaidi na ibilisi.
Kama kweli alikuwa anaumwa, na sasa amepona, kwa hiari yake, na wala hakuna ubaya, akafanya kama alivyofanya Rais mstaafu Kikwete alipotoka kwenye matibabu US. Japo najua itakuwa ngumu kwa mpango, maana kufanya hivyo ataona kama anamdhalilisha PM.
Dr. Mpango, kama mwumini mwenzangu, siyo kama Makamu wa Rais:
Kristo bwana wetu, aliteseka, hata kufa kwaajili yetu. Katikati ya mateso aliwapa msamaha watesi wake. Hakuwa na sababu ya kuteswa na hata kuuawa na wanadamu duni, bali aliyafanya hayo kutuonesha wanadamu tunavyotakiwa kuenenda katika maisha yetu. Mwisho Kristo alimshinda shetani, akayashinda mauti, mauti ya mwili na Roho. Bila kujali yaliyosemwa juu yako, yawe mema au mabaya, samehe na sahau yote, badala yake uombe neema ya kushiriki ushindi wa Kristo.
Dr. Mpango ni miongoni mwa watu ambao ningekuwa na access naye, ningefarijika sana kuonana naye. Lakini kujua tu kuwa yu mzima, ni zawadi kubwa ya kutosha.