Dr Nchimbi ameunda Kamati sio Tume

Dr Nchimbi ameunda Kamati sio Tume

Tulianza kujadili uhalali wa TUME/KAMATI hii ya Nchimbi humu JF kabla hata ya Tundu Lissu. Namshukuru TL kwa kuliongea kisheria zaidi. Natamani wanaSIASA wetu wote wangekuwa wanapita humu.
 
kwenye jambo zito kama hili waziri anakurupuka na kuunda kamati ambayo haiwezi kuja na majibu yoyote, hili ni changa la macho
 
Wana habari wekeni clip ya Nchimbi hapa tusikie alisema anaunda nini
 
Sasa watu inabidi wamkubali TL kwani hata uhalali wa JAJI IHEMA aliwahi kusema ni questionable.Leo mimi nimeamini aliyosema GURU TL jaji ihema angekuwa makini angekataa kuteuliwa na Nchimbi na angetumia utaalam wake wa ujaji kumshauri kama alivyofanya TUNDU LISSU.KWELI JAJI IHEMA NI VODA FASTA. AHAAA WAMEKATA PEASA ZA MCHANGO WA ARUSI BORA NIJIUNGE CDM KWANI KUTUMA NI BUUUUUUUUUUUUUREE
 
Njaa kitu mbaya sana !! tazama ktk hiyo tume 'feki' mmoja wa wajumbe ni JAJI! ila kwa kuwa kuna hela hakuona kasoro yoyote, akakubali kuteuliwa na asiye na mamlaka kikatiba. kweli nimeamini lile neno “mambo haya wamefichwa werevu (jaji na magamba) na kufunuliwa wadogo hawa (mh lissu)”
 
Kutoa UHAI wa mtu ni suala la KIKATIBA zaidi. Mlinzi mkuu wa KATIBA ni RAIS wa JMT. Hauwezi kuunda kamati yenye nguvu sawa na zile za harusi, graduation na misiba kuchunguza jambo zito kama hili.

Walipouliwa wale wafanyabiashara wa madini aliyeunda TUME ni RAIS mwenyewe ingawa watendaji wake walimzunguka wakapeleka mahakamani watu wengine bila muuaji halisi!

Hili la Mwangosi pia linamtaka Rais aunde tume mbali na hiyo kamati ya waziri wake. Tunajua muuaji halisi hatapatikana ingawa anafahamika kwa kuwa silaha iliyotumika alikuwa nayo askari mmoja tu.

Tunahitaji jeshi jipya la polisi litakaloendana na mazingira ya sasa ya KISIASA nchini mwetu
 
Sasa watu inabidi wamkubali TL kwani hata uhalali wa JAJI IHEMA aliwahi kusema ni questionable.Leo mimi nimeamini aliyosema GURU TL jaji ihema angekuwa makini angekataa kuteuliwa na Nchimbi na angetumia utaalam wake wa ujaji kumshauri kama alivyofanya TUNDU LISSU.KWELI JAJI IHEMA NI VODA FASTA. AHAAA WAMEKATA PEASA ZA MCHANGO WA ARUSI BORA NIJIUNGE CDM KWANI KUTUMA NI BUUUUUUUUUUUUUREE
Jaji Ihema anaudhalilisha muhimili wa mahakama kwa kukubali uteuzi wa aina hii. Ngazi aliopo sio ya kuteuliwa na mwenye mamlaka chini ya Rais mwenyewe isipokuwa kama Rais atakasimu madaraka yake kwa aliyemteua.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na Mambo ya Nje, Mh saana Lowasa, anasemaje? Nilidhani angemwita IGP amuhoji kama askari wake wameandaliwa vizuri KIAKILI na kwa zana kali za kuzuia maandamano!
 
Kwanza na yeye anatakiwa achunguzwe,
 
Nawapenda sana makamanda wa CDM, ni wazalendo halisi. Hebu fikiria Waziri(!?) mzima ana wasaidizi na maandalizi ya kila aina ameitisha press conference akijagamba kuwa kaunda Tume. Hata alipoulizwa kwama atajuzulu akadai eti "akijiuzulu mtapata wapi waziri (kilaza?) kama yeye..." Then anasimama mwananchi mmoja, msomi kitaaluma, mzalendo wa ukweli anakosoa na kukataa ***** wa Waziri (special).

Ndani ya saa 24, Wizara bila kuomba radhi inakubaliana na hoja ya Mh. Lissu, na kwa unafiki na aibu wanaamua kubadili usemi. Bila Waziri/Wizara kujuliza yafuatayo:
1) Kwa vile sasa imeshuka hadhi na kuwa Kamati, je hadidu za rejea bado ni zile zile?
2) Je Wajumbe ni wale wale?na mwisho,
3) Je kuna haja ya hiyo Kamati kuundwa?

Jamani wana JF ni kwa nini tusisimame popote tulipo tumpigie makofi ya asante Mh. Lissu kwa dakika moja?

Makofi ya nguvu kabisaaaaa! Hii ndo safu ya Mnafiki Samweli Sitta ya kuongoza serikali! Nonsense...
 
Mtu ameongea kwenye TV na tumemuona na kumsikia, sasa bila aibu anasema hakuunda tume ila kamati, ni afadhali aseme ukweli kuwa yeye ni kiazi na hajui tofauti kati ya tume na kamati. Vinginevyo tutarusha hapa JF kipande chake anachosema nieunda tume
 
Kwani waziri Nchimbi akiomba radhi atapungukiwa na nini? Two wrongs does not one right! Kuunda tume au kamati ya kuchunguza mauji yaliyofanya na vyombo vya dola si kazi ya Nchimbi, yeye hamteui IGP wala RPC, hawa ni wateuliwa wa rais, aache uhuni hana mamlaka ya kuwawajibisha, sasa anawachunguza ili iweje? Hiyo kamati yake ya HARUSI ai call off!
 
Duuh.. Hii nchi inatawaliwa na Viongozi wasiojua katiba..? Mwl. Nyerere alituasa na tabia hii ya Viongozi kuchezea katiba huku wakiwa wameapa kuilinda katiba hiyo hiyo..!
 
TEH TEH TEH TEH
MIMI NAPITA TU!!!!!Akili ndogo inatawala akili kubwa. kazi ipo na tutaona na kusikia mengi kwa miaka 3 iliyobaki
 
Juzi nilijaribu kuandika elimu ya o-level ya nchimbi mods wakaiondoa lakini sasa wameelewa ni aina gani ya nchimibi wanayemtetea ni bora tukawafahamu viongozi wetu kama elimu zao ni questionable let the public know
 
Juzi nilijaribu kuandika elimu ya o-level ya nchimbi mods wakaiondoa lakini sasa wameelewa ni aina gani ya nchimibi wanayemtetea ni bora tukawafahamu viongozi wetu kama elimu zao ni questionable let the public know
Mkuu Nchimbi ana 'Phd'
 
Ili jamaa nilichojua ni kuvimba mashavu tu. Kichwani patupu! Anakurupuka kuunda kitu asichokijua! Duh ndio Viongozi wetu wa kututoa kwenye umasikini tulionao! Tumekwisha!
 


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI ALIUNDA KAMATI SIO TUME
Wizara ya mambo ya Ndani ya Nchi inapenda kutoa taarifa kwa Umma kuwa katika kikao chake na Waandishi wa Habari cha tarehe 4 Septemba, 2012, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi alitoa taarifa ya kuunda Kamati kuhusiana na vurugu zilizotokea katika Kijiji cha Nyololo, wilayani Mufindi, tarehe 2 Septemba, 2012 ambapo katika vurugu hizo mwandishi wa habari wa Channel Ten, Daudi Mwangosi alipoteza maisha.
Waziri Nchimbi alisema aliunda Kamati hiyo, (na siyo Tume), ili kumsaidia kupata majibu ya maswali yafuatayo, ambayo alisema hakuwa na majibu yake:
1. Nini kilikuwa chanzo cha kifo cha mwandishi wa habari, Bw. Daudi Mwangosi,
2. Kama upo uhasama kati ya waandishi wa habari wa Iringa na Polisi,
3. Kama ipo orodha ya waandishi watatu (3) waliopangwa kushughulikiwa na Polisi,
4. Kama ukubwa wa nguvu za Polisi zilizotumika ulikuwa sahihi,
5. Kama zipo taratibu zinazoruhusu Vyama vya Siasa kukata rufaa visiporidhika na maamuzi ya Polisi,
6. Kama kuna tatizo la mahusiano kati ya Polisi na Vyama vya Siasa.
Taarifa hii inatolewa ili kuweka sawa taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari vikimnukuu Mkurugenzi wa Masuala ya Sheria, Katiba na Haki za Binadamu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tindu Lissu akisema Chama chake hakiungi mkono Tume ya mauaji ya aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha televisheni cha Channel Ten, kwa madai kwamba imeundwa kinyume cha Sheria ya Tume za Uchunguzi ya Mwaka 1962 Sura ya 29, ambayo alisema kwa mujibu wa Sheria hiyo, tume zote za uchunguzi huundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kupitia taarifa hii, tunapenda kuuarifu Umma kuwa Waziri Nchimbi hakuunda Tume ila aliunda Kamati hiyo kwa Mamlaka aliyonayo kama Waziri na uundaji wa Kamati hii hauhusiani kwa vyovyote na matakwa ya Sheria ya Tume za Uchunguzi, Sura ya 32, Marejeo ya Mwaka 2002.
Utaratibu wa kutumia Kamati kutafiti jambo kwa kina kwa ajili ya kumshauri Waziri au kiongozi mwingine yoyote ni wa kawaida katika utendaji na utekelezaji wa majukumu ya umma.
Imetolewa na Isaac J. Nantanga
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
06 Sepemba, 2012

 
Back
Top Bottom