DR. Mwakyembe na Natural Justice



Hili nalo ni tatizo kubwa miongoni mwetu na kama tunataka kupiga hatua lazima tubadilike.

Kama mtu unafahamu kitu kwanini usikiseme kwa ajili ya maslahi ya watu wengi unaishia kutoa vitisho vya hapa na pale, au ndo siasa za maji taka zenyewe!?

Hapa analaumiwa mwakyembe kwa kuficha baadhi ya mambo, na wewe engineer unaficha baadhi ya mambo, sasa ndio nini hii? Kwa maslahi ya nani?
 

Mwakyembe (na usomi wake wote) mpumbavu -sio mjinga-. As in idiot, and not ignorant. Kashasoma sana kupewa benefit of doubt ya ignorance, kawa muhadhiri wa kutumainiwa ati.

Hili linanifanya nijiulize sana kuhusu quality ya elimun yetu. Kama hata mhadhiri maarufu wa sheria anaweza kuchemsha hivi, tutegemee nini kutoka kwa sio tu wahadhiri wetu wapya, bali hata wahitimu wetu wapya.

Yoyote ambayo hujayasema katika ripoti, halafu ukasema "kuna mengine sijayasema katika ripoti" unakuwa ushayasema kwa namna moja ama nyingine. Unakuwa kama yule mkimbizi wa vita aliyelala chini ya nyasi, akasikia adui kauliza "kuna aliyebaki hai tumpe maji?". Akaamini na kujibu "Mimi nipo hai". Akamalizwa hapo hapo.

Kama kuna mambo hayaelezeki katika ripoti, huyazungumzii kabisa. Husemi hata kwamba hayaelezeki, kwa sababu ukisema tu hayaelezeki ushaanza kuyaelezea. Mwanasheria aliyebobea anatakiwa kuelewa hili a la "You have the right to remain silent, anything you say can and will be used against you".

Na kutoka hapo ( statement ya "kuna mengine sijayasema katika hii ripoti") unapata the worst of both words.

Wale waliotaka usiseme watakuona mbaya kwa sababu umesema kuna mengine hujayasema, ume spill beans kwamba kuna zaidi ya uliyoyasema.

Wale waliotaka useme watakuona mbaya kwa sababu umesema kuna mengine hujayasema ambayo wangetaka uyaseme.
 
Kwa nini Lowassa alijiuzulu? Kati ya mambo yote ambayo angeweza kufanya kwa nini aliamua kujiuzulu?
Kwa maelezo yake alijiuzulu ili kulinda heshima ya chama na serikali yake, Kama tunavyo jua ugongwa wa kulindana ulivyo ndani ya taifa
 


Kama EL anaamini kwamba kamati ya mwakyembe haikumtendea haki, kwanini asiombe bunge kurejea maamuzi yake juu ya scandal ya richmond?

Inawezekana alihamaki baada ya ripoti kusomwa na hakupata muda wa kutosha kutafakari, ndipo akaamua kujiuzulu na sasa amegundua kosa lake na anaweza kuweka mambo sawa na ukweli halisi ukajulikana. Mlio karibu nae ama mnaomtetea kwanini msimshauri airudishe mezani bungeni hoja ya richmond ili kukata mzizi wa fitna?
 
Kwa report ile wengi wanamkubli nami pia

Lakini tunayakujiuliza kwa nini hakuyasema yote ? ali acha kwa faida ya nani, mafisadi au... hapa ndipo panapo leta utata ktk weredi wake halafu anatishia, ni bora uamuzi wake wa kuichakachua report yake mwenyewe ungebaki siri yake kuliko kutuwekw ktk stress kila siku maana watu hatujui nini kingine cha ajabu ambacho kipo nyuma ya pazia

It is better akanyamaza tu
 
Kwa maelezo yake alijiuzulu ili kulinda heshima ya chama na serikali yake, Kama tunavyo jua ugongwa wa kulindana ulivyo ndani ya taifa


Kama Mwakyembe alificha baadhi ya mambo ili kumlinda JK,,,

EL naye alijiuzulu ili kumlinda JK,,,

Hii inathibitisha tabia ya kulindana jinsi ilivyokomaa na kuota mizizi hapa nchini.

Sasa anacholalamikia EL ni kitu gani ikiwa wote walifanya kazi ya kufanana ya kumlinda JK?
 
Mkuu si mtetei EL hata kidogo ninacho jaribu kudadisi ni kwa nini Dr Mwakyembe hakuyasema yote leo anakuja na kusema ninayo mengi moyoni

Hata kama kamati haikupewa jukumu la kumhoji PM lakini mazingira ya liwalazimu wamhoji kama walivyo fanya kwa wengine

Kumbuka kuwa EL ni mwanaCCM hawa wana desturi ya kulindana naye alijuzuru ili kulinda wengi walio nyuma yake The same done by Dr HM hapa naye kwa kulinda watu wengi ....Tujue wazi kuwa wanachokilinda si chema bali ni uovu tu that is all...
 
Kiranga,
Kumuita Mwakyembe mpumbavu unakuwa hujamtendea haki hata kidogo. Ni mambo mangapi wananchi tumepata kuyafahamu kupitia kamati aliyoiongoza? Je hayo ni ya kubezwa kiasi hicho?

Pamoja na kutoweka hadharani baadhi ya mambo, ambayo bila shaka alifanya hivyo kuinusuru serikali ya chama chake isiporomoke, kwakuwa naye ni mwana ccm lakini bado kuna mambo mengi tumejua kupitia ripoti ya kamati yake.

Kama EL ndiye mwerevu kuliko mwakyembe katika hili, kwanini hakujitetea bungeni alipopewa nafasi lakini akaamua kujiuzulu ili kuilinda serikali ya chama chake?
 


Kwanza tunakubaliana kwamba hawa wote mwakyembe na lowasa ni wanaccm na kila mmoja alifanya kile alichofanya kuilinda serikali ya chama chao na hususan JK.

Ikiwa mwakyembe alificha baadhi ya mambo kuilinda serikali ya JK na ccm. Lowasa naye aliamua kujiuzulu badala ya kujitetea ili kuilinda serikali ya JK na ccm. Sasa hapa ndipo najiuliza lowasa na watetezi wake wanalalamikia kitu gani?
 
100% nakubaliana nawe

Labda nijaribu kueleza za wanao mtetea EL

  • Nadhani wana mkubali zaidi EL kuwa ni kiongozi ambaye yupo tayari kufanya maazi magumu kwa manufaa ya walio wengi Maana hii nchi inahitaji kiongozi jasiri
  • Hawaamini kuwa EL pekee yake anasitahiri kubebeshwa lawama za Ufisadi ikiwa ile ilikuwa ni system ilikuwa na watu wengi kama alivyo sema huko NEC kuwa kila hatua Mkuu alijua kinachoendelea
  • Wanasema ndani CCM mtu anayeweza kuingoza hii nchi awe mchapa kazi hivyo EL ni mchapa kazi sijui kigezo wanachutumia (Haya ni badhi tu ya maoni ya watu humuhumu )
 
kweli kaka, nimekubali ...tuko pamoja.

Mkuu x-mass njema, kama uko tanzania tengeneza pilau ya asili , kama uko 'kule' duni nyingine najua umeishaisherekea mwezi wote huu....



nadhani haujasahau nikisema mwana kondoo ameshinda unajibu nini!

...tumfuate..
 


Kuna wakati elimu inabidi iwekwe kando busara ichukuwe nafasi,naamini Mh.Mwakyembe aliweka busara mbele ya taaluma yake,anastahili pongezi na si shutuma.
Ni ukweli uliowazi kuwa jeshi la mafisadi lisingekubali kuumbuliwa kirahisi namna ile,ufisadi ofisi yao kuu ipo magogoni unajua jinsi ambavyo Mwakyembe angefuata taaluma bila busara angefika hadi magogoni TZ pasingetosha.
 
Kuna masuala magumu kuyazungumzia kwa kuwa hatujui muhusika ana mawazo gani kichwani.
 
Wadau vp na yale madai ya RA,kwamba kamati ilipga mzigo zaidi ya siku ilzopewa...alitoa evidence ku prove hilo?coz nakumbuka wkt anaitwa yeye alikuwa nje ya tz!
 
Kwa nini Lowassa alijiuzulu? Kati ya mambo yote ambayo angeweza kufanya kwa nini aliamua kujiuzulu?


swali zuri sana! do you think he was stupid? he is smart and knew exactly what he was doing na hizi propagada zake uchwala za kwenda makanisani tena mpaka kwa wakatoliki na nabii joshua the guy knows what he is doing!!!
 

A chain is as strong as it's weakest link. Mtu makini hawezi kuandika ripoti halafu aka i undermine ripoti yake mwenyewe kwa kutuambia kwamba kuna mengine hajaandika. Kama hujayaandika huyaongelei.

Sasa ona alivyotengeneza a cloud of controversy. I mean these things are controversial enough even without such careless remarks, so why create even more controversy?

Kama kweli kaficha mengine ili kumnusuru JK/ chama, kwa kusema "kuna mengine sijaandika" alikuwa anatoa possibly self incriminating evidence, nchi za watu wanaofuata rule of law angeweza kuchunguzwa kama kafanya "cover up" na kama akibainika kafanya hivyo anacheza na lupango.
 

Mwenye busara anajua wapi pa kusema na wapi pa kukaa kimya, kipi cha kusema na kipi cha kukaa kimya.

Mwakyembe kwa kusema "kuna mengine sijayaandika humu" tayari kashatengeneza swali kwamba hichi ambacho hakijaandikwa ni kipi?

Inawezekana vitu ambavyo hajaandika hata si muhimu hivyo, lakini kwa sababu katuambia kuna vingine hajaandika tushaanza kufikiri a cover up na mambo mengine mabaya.

Ile kauli ya "kuna mengine sijaandika humu" si kauli ya mtu mwenye busara.
 
Sasa wewe unataka kumlazimisha mwenzako achangie kama unavyotaka, unachotakiwa wewe ni kuchangia si kukemea wanaochangia.
Kuna watu wanataka kulazimisha mtu mchafu awe safi na watu safi wawe wachafu..je nani atakubali hilo? Mimi sithubutu kula pesa ya mtu hata senti tano yake ....!
 
Mkuu ebu nambie unapoandika report ya kuchunguza uhalali wa Richmond wewe ungeandika hata vitu ambavyo vinatakiwa uchunguzi wa vyombo vya sheria?... Sidhani kama kuna report yoyote huandikwa hivyo na kama wewe utafanya hivyo mkuu wangu utakuwa umefanya kmakosa makubwa sana..

Mwakyembe alichokifanya ni kupeleka report na ingefikia mahala yeye kama shahidi kusema anayoyajua ndiyo mbele ya sheria kilichotakiwa afanye ama kama angekuwa mchunguzi binafsi wa swala lile. Na kusema kwake kuna mengine ambayo sijayaandika humu ni kielelezo tosha kwamba anabanwa na sheria tu lakini angeweza kuandika vitu zaidi ya report kile alichotakiwa kukifanya..


Makosa tumeyafanya sisi au niseme Bunge letu kukubali kumwachia Lowassa na wahusika wote kabla hajajibu report. Kisha kwa nini watu wanamtazama Lowassa tu wakati wapo wengi ambao walijiuzulu lakini nao walikuwa ktk sakata hili hili mathlan Msabah mbona hazungumziwi yeye ambaye halalamiki isipokuwa alisema alifanywa bangusilo kwa amri kutoka juu isipokuwa Lowassa.
 

Kama kuna ambayo yako "out of scope" unayaacha. Kuyaacha maana yake huyazungumzii. Huyazungumzii maana yake husemi hata "mengine nimeyaacha" kwa sababu speaking in context, hujayaacha, yako out of scope.

Ukishaanza kusema "mengine nimeyaacha" una imply yalikuwa "in scope" ukayaacha, kibaya zaidi husemi uliyoyaacha ni yapi na kwa sababu gani umeyaacha.

Unawapa watu mwanya kuanza ku speculate, hata kama umeacha vitu insignificant, watu wanaanza kuzoza sasa "Mnajua Mkwakyembe alivyosema kuna vitu kaacha kaacha nini? Kuna data zimemhusisha JK ndiyo kaziacha" etc.

Utawalaumu watu wakifikiri hivyo? Mwakyembe mwenyewe domokubwa kashindwa kua cat professionally kapanda mbegu ya doubt on his own integrity.

Kama mambo hayakutakiwa kusemwa, kwa nini kayasema (hata kwa kusema kwamba hayakutakiwa kusemwa kayasema tayari).

Anaweza kufanya kazi za national security huyu? Kuna kazi zingine hata unachoacha kusema kinaweza kuwaambia watu nini ni siri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…