Dr. Magufuli, tafadhali badili hotuba

Dr. Magufuli, tafadhali badili hotuba

Bado yupo puzzled. Hata arogwe vipi hataweza kupata maneno mbadala...ashukuru tu wana CCM wao hawajali hico, wanachoangalia ni muongeaji amevaa nguo za rangi gani.
 
yaani Magufuli amakuwa mgombea kwa bahati mabaya tu lakini kiukweli hafai na hakujiandaa kabisa kuwa Rais..Na hivi anashindana na EL hakuna rangi ataacha kuona mwaka huu..Itafahamika tu mbona ...Yaani ubunge anaukosa na urais anaukosa...mwaka huutunaandaika historia ...
 
Ukweli haujifichi, pale Dodoma alionekana akiwahamasisha wadau wa EL kwa kuimba 'aliselema' dalili kwamba naye anaamini bila mchango wa huu upande mambo yatakuwa magumu.
Dr. Magufuli ni mtendaji mzuri tena sana na ndio maana mara nyingi alikuwa akipishana na watendaji wa serikali. Kwa kugombea urais kupitia chama hiki yatamtokea ya Jaji Ramadhani. Tusubiri tuone.
 
mi sielewi kwann watu mnasema hakujiandaa,angechukua fomu ya kugombea kama hakujiandaa?kama mnataka maneno,sera,mipango yake tuanze kumjaji siku 17 sijajazo kampeni zitakapoanza
 
Akili yako ni finyu sana!! Wanaweza kukusaidia ebu msaidieni kwa nini kule kanisani tunakaririshwa mafungu ya biblia !! Kwani Baba yako anarudia kila siku kukusihi umsikilize maagizo yake!
 
Kuna watu wamezaliwa kwa ajili ya kutumwa tu, ukimtuma kufanya jambo hakosei. Watu wa namna hii huona fahari kutumwa. Ni kama walivyo wanyampala gerezani. Ubaya wa watu aina hawawezi kujituma wao - hawana akili ya kubuni jambo na kulisimamia mpka likazaa matunda. Magufuli ni sample nzuri ya watu hawa. Akiwa rais sijui atakuwa anatumwa na Big Ben au yule Sungura mjanja wa msoga.
 
Magufuli hakujiandaa kuwa mgombea Rais na ndo maana sera zake ni nyepesi kama bua LA mhindi
 
Magufuli bado sana kisiasa. Amezoea kukariri simple data na tarakimu fulani, hana kitu cha kumshawishi mpiga kura. Hili ndio tatizo la kumpa mtu kugombea nafasi ambayo hakujiandaa nayo.
Lakini huenda wanaCCM wengi wamemuonya asiongee maneno mengine maana jamaa ana kiburi fulani na anaweza kuropoka maneno ya kuudhi kwa watu.
Mfano, issue ya wakazi wa kigamboni wapige mbizi, Bomoa tu nyumba zenye kuwekwa alama ya X nk.
 
Back
Top Bottom