Dr. Magufuli, tafadhali badili hotuba

Dr. Magufuli, tafadhali badili hotuba

Mpeni maneno ya kuwa anahutubia ili ayakariri
 
Atabadili vipi wakati hana ambition wala vision ya urais???? Kwani mleta mada hujui magufuli alilazimishwa na wazee??
 
Kuna watu wamezaliwa kwa ajili ya kutumwa tu, ukimtuma kufanya jambo hakosei. Watu wa namna hii huona fahari kutumwa. Ni kama walivyo wanyampala gerezani. Ubaya wa watu aina hawawezi kujituma wao - hawana akili ya kubuni jambo na kulisimamia mpka likazaa matunda. Magufuli ni sample nzuri ya watu hawa. Akiwa rais sijui atakuwa anatumwa na Big Ben au yule Sungura mjanja wa msoga.

eti "SUNGURA MJANJA WA MSOGA"... umetisha
 
kauli hii sitawaangusha kwani ulikuwa umewabeba? bora hata ya pinda wapigwe tu imempindua kuwa hana maadili.
 
aliselema hadija aliselema hadija..nilichukua fomu kimya ....nikatafuta wadhamini kimya....nitakuwa mtumishi wenu..naahidi sitawaangusha
 
Sasa unaelekea 'kuboa'. Unarudiarudia maneno yale yale kila mahali unapohutubu,kwanini? Badili hotuba. Badili maneno. Kuanzia ukumbini Dodoma; uwanjani Dodoma, Dar es Salaam na hata Zanzibar, umekuwa ukisema: 'Sitawaangusha,nitakuwa mtumishi wa wote'. Na jana pia umeyarudia maneno hayo hapa Lumumba. Kurudiarudia kunaonesha kufilisika. Usifike huko.

Nafahamu na nakufahamu kuwa una maneno mengi. Unaweza kubadili maneno na hata kuyaleta matamu kuliko hayo. Kama huo ni msemo wako sawa.

Lakini,badilikabadilika kimaneno ili uvutie. Shauriyo, utapoteza wasikilizaji kwakuwa tu watakuwa wanasikia yale yale. Badilika Tingatinga!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam


Abadili maneno atayatoa wapi wakati mwenyewe alichokua fomu ya uraisi kwa kuigiza sasa jumba limemuangukia wakati hakujipanga siumeona hata kuchukua fomu jana ilibidi mzee ampeleke kazi kwelikweli
 
Ni dhahiri kabisa Mhe. Magufuli hajui matatizo ya watanzania kwa kusema ni masuala ya boda boda na mama ntilie. Kweli Mhe. imepita siku zote tangu uchukue form na hadi kuteuliwa hujui watanzania unaotaka kuwaongoza wana matatizo gani. Sikuskia mambo muhimu yote ambayo wanahangaika nayo zaidi ya ajira ambalo ni janga la dunia nzima. Kajipange upya la sivyo utapigwa asubuhi kabla ya misaa ya kwanza. Acha kukariri kila kitu, nchi hii sio barabara ulizokuwa una kariri miaka nenda miaka rudi.
 
Rais sio maneno ni vitendo liache jembe


Hilo jina la jembe umempa nyie na likingia kutu (hasa huu ukanda wa pwani) msilaumu mtu. Wenye kumbukumbu mnakumbauka kuna mzee alipewa fagio la chuma, maji ya pwani yakalitia kutu likashindwa kufanya kazi sembuse jembe! Hata hivyo sisi tuliosoma naye (Mkwawa) tulimfahamu kwa jina la BOILER, kwa tabia yake ya kutoa maneno yasiyo na maana (aka vapour).

Hivyo kurudiarudia maneno haishangazi kwani kazi ya boiler huwa habadiliki ni kutoa uvuke uleule!
 
tatizo hilo si magufuli peke yake mpaka lowassa analo pia tatizo hilo linachangiwa na ccm yani maswala ya chama ni nape, mangula, na yule msomali ktk kuzunguka mikoani kukijenga chama ktk mikutano mbalimbali yenye watu wengi ndo unapata experience ya kuongea leo kama chama cha chadema wote wanajua kuongea coz wanafanya mikutano mingi na kupata experience ya kuongea
Mkuu umenena vema. Nimemsikiliza Magufuri,kuhutubia mzito,nimemsikiliza Lowasa kuhutubia mzito. Wote maneno wanayatafuta. Tena kwa uchunguzi wangu,aheli ya magufuri kuliko Lowasa. Tunaenda kwenye kampeni,one mistake one goal.
 
HA HA HA HAAAA nimeecheka sana eti hakujiandaa kuwa rais teh hata mimi ananiboa sana eti nitakuwa mtumishi wa watu kwani hana washauriii???
 
na kama atajaribu kuja na ule ukatuni wake wa kutaja kilomita za barabara,hapo ndio nitamuona hamnazo.
 
Hilo jina la jembe umempa nyie na likingia kutu (hasa huu ukanda wa pwani) msilaumu mtu. Wenye kumbukumbu mnakumbauka kuna mzee alipewa fagio la chuma, maji ya pwani yakalitia kutu likashindwa kufanya kazi sembuse jembe! Hata hivyo sisi tuliosoma naye (Mkwawa) tulimfahamu kwa jina la BOILER, kwa tabia yake ya kutoa maneno yasiyo na maana (aka vapour).

Hivyo kurudiarudia maneno haishangazi kwani kazi ya boiler huwa habadiliki ni kutoa uvuke uleule!

Mh!! Unaonekana hukusoma huki Mkwawa. Boiler ndiyo nini na maana yake nini au ulikuwa unataka kusema boarer?
 
Utumishi hauhitaji kulemba maneno usofiwe,hilo siyo shairi,hizo ni feelings za mtendaji,ccm hatuangalii ulembaji wa maneno au sura,tunakisema kile tunachokiweza,magufuri ni raisi wa watanzania mkubali mkatae,yaani kwa wale wavivu na wamjini mjini ishu imebuma jiandaeni kurudi mikoa yenu msio na physical address
 
Lakini huku mitaani tunaambiwa baada ya lowasa kutoingia tano,timu lowasa ndiyo ikaamua kumnchinjia baharini membe,na kumpigia kura magufuli,ili wote wakose.na kwamba hata magufuli hakuwa chaguo la jk.sasa Kama ndiyo hivyo kweli alikuwa hajajiandaa.kuchukua form hata prof kalokola alichukua,form sio issue sasa.
 
Hatatuangusha...kama ametubeba vile...hahaaaaaaaaa
 
Back
Top Bottom