Dr Kitila Mkumbo for CHADEMA Presidency!

Dr Kitila Mkumbo for CHADEMA Presidency!

Siasa si hesabu. Kama hujui kwamba hoja ya ukaskazini inatumika kuididimiza chadema basi una tatizo. Hata leo tu soma Tazama uk 2 imeandikwa kama ifuatavyo:" Kauli hizo za mjumbe wa kamati Kuu ya chadema zimetafsiriwa na wachambuzi wa mambo ya kisiasa kwamba ni uthibitisho wa dhahiri dhidi ya tuhuma za muda mrefu kwamba chama hicho si cha kitaifa kama viongozi wake wanavyotaka kuwaaminisha watanzania, bali ni chama cha ukoo na watu wa kaskazini tu" Mwandishi ameandika utumbo mtupu ila sasa watanzania wengi wanayaamini haya. Ili kuwakata kilimilimi wapuuzi kama hawa, weka M/kiti ambaye si wa kaskazini. Hata kenya watu wanamshauri Uhuru Kenyatta asigombee maana rais anayemaliza muda wake ni Mkikuyu. pamoja na kwamba ni maarufu sana akipuuza ushauri huu utamgharimu. hii ni political tactic. Kuna tofauti kati ya ukweli na siasa.
hivi wewe na kwa ufahamu wako bado unasoma TAZAMA? Hilo mbona watanzania wengi wanalijua ni gazeti la kuichafua CDM na wanamageuzi wa kweli.. sasa unafikiri ukaskazini ni tatizo au kukosekana uongozi bora wenye mafanikio ndio tatizo kubwa? Yawezekana magamba wanaogopa mtu kutoka kaskazini ataipaisha hii nchi kimaendeleo.. (hizo ni fikra zangu).
 
Hivi mtoa hoja alikuwa anamaanisha Kitila agombee urais wa CDM au urais wa nchi??? Naona wachangiaji wengi hamkumwelewa!! Kwa jinsi alivyoandika anamaanisha kuwa Kitila amrithi Mbowe nafasi ya uwenyekiti wa CDM kama hatagombea kwenye next party General election!!

Kwa sasa CDM hakuna mwingine kama Slaa kwa Urais!!!
 
Kwanza ni ruhkusa kwa watu kujadili juu ya kesho yao ili waanze kutafakari juu ya makosa ambayo yamefanyika katika vipindi vingi vya kiutawala wa nchi hii toka uongozi wa mwl Nyerere ututoke uliotoa dira ya dhana nzima ya kiuongozi kuwa ni kuonyesha njia.Kuna watu wanajaribu kumbeza mleta hoja juu ya values za Dr kitila kuwa ama mgombea urais ama kuwa kiongozi mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Kiufipi Dr KItila ana value zote za kuwa kiongozi wa watu katika ngazi yoyote ya kiutumshi wa ummah,nenda miaka ya nyuma alipoongoza Taasis ya Daruso utapata rekodi yake,njoo katika nafasi yake ya umoja wa wahadhiri kama makam M/kiti UDASA utapata rekodi yake,lakini pia utapata rekodi yake katika nafasi yake ya ukuu wa Idara ya Psychology pale mlimani,waulize wahadhiri na wanafunzi he is derivering.
Kuna watu wanadhani unaweza kuwa na sifa za kiuongozi katika kuongoza watu halafu uwezo huo ukufunge katika mipaka ya ubunge tuu,huku hawajui kwamba hata Rais anaongoza Taifa ambalo ni watu,mbunge naye anaongoza Taifa ambao ni watu.Hebu niambieni juu ya uzoefu wa Mwl Nyerere kuwa Rais nini kilimuwezesha ni ubunge,ubalozi,ualimu ama uwezo na uzalendo????hebu nielezeeni juu ya Mzee Mandela ni ubunge,uwaziri,ubalozi au ni uwezo na uzalendo???toka Nyerere ang'atuke hatujawahi kupata Rais Mwadilifu kama yeye japo hakuwahi kuwa waziri au mbunge wa Butiama!!Miaka mingi tumepatia kuchambua wale wote waliokuwa waandishi wake wa habari,mawaziri wake na wengine washauri wake wa kisiasa tukidhani kwamba labda watakuwa wameambukizwa uwezo,uzalendo na uadilifu!!! kumbe aah wapi all of them are " African crew of Bandity" japo wanauzeefu wa kutosha wa kuishi na mwl Nyerere,uzoefu wa kiutendaji lakini siyo uzoefu wa uzalendo,uadilifu na uthubutu wa kiuwezo.Mwl Nyerere hakuwahi kuwa mzoefu wa uongozi wa juu,ubunge au uwaziri zaidi ya uwezo,uadilifu,uzalendo na uthubutu bado aliweza kufanya maamuzi mazito yaliyo ifanya Tanzania ing'are katika jamii ya kimataifa.,misingi yote ya Taifa hili tunaililia juu ya ukabila,udini,mapengo ya kitabaka,mshikamano wa kitaifa ulijengwa na mtu ambaye kabla ya hapo alikuwa haijui ikulu wala uzoefu wa kibunge,bali yote haya aliyajenga kwa silaha ya uzalendo,uadilifu na uwezo vitu ambavyo kwa anaye mfahamu dr Kitila hawezi kuvibishia.
Watanzania miaka KARIBU 35 YA CHAGUZI ZETU Tumeendelea kudiriki kuendelea kulewa na baadhi ya bandit leaders eti kwasababu wamewahi shika nafasi kubwa zilizo nyingi huku tukisahau kwamba mwl Nyerere aliyejenga misingi ya mishikamano ya Taifa hili alikuwa na silaha ya uadilifu,uzalendo na uwezo na siyo umaarufu wa vyeo vingi vya kisiasa.,tunaompinga mtu eti kwa sababu hajawahi kuwa mbunge tujitathimini kwa swali la kwamba Ndg Mwinyi alikuwa Rais wa Zanzibar kabla ya uRAIS muungano vipi aliweza kukidhi matarajio ya uadilifu wake,uzalendo wake na uwezo wake???bado tulirudia circle ile ile mwaka 1995 tukamchagua Mr Clean Benjamin Mkapa kwa dhana ya aliwahi kuwa Mwandish wa Habari wa Mwl,Ubalozi,uwaziri katika nafasi mbalimbali[uzoefu kibao wa kimataifa] tumeona uzalendo wake,uadilifu wake na uwezo wake kwa miaka aliyoongoza na kutawala Taifa hili.,bado tukazidi kujenga imani ya nguvu kwamba huyu ndg Kikwete ana uzoefu wa miaka mingi kichama na kiserikali kwa kushika nafasi mbalimbali za kitaifa na kimataifa tukijua uzoefu wa kilevi ndicho kinacholisibu Taifa hili,tukasahau juu ya uzalendo wa mtu,uadilifu wake na uwezo wake!!!hatimaye tunakuja kuja kuwa mashuhuda wa Bandit Cabinate na Bandit Government
Bado tunaelekea 2015 tunauliza juu ya Kuwahi kuwa waziri Dr kitila baadala ya Kuwahi kuwa Mzalendo na Kuwahi kuwa mwenye uwezo!!!!!!
kama kweli tutakuwa tunaendelee kuwatafuta marais kwenye baraza la mawaziri,Bungeni na ngazi zingine za watu kuwa AU au UN kuwa ndiyo pekee walio na suluhu ya kansa ya uongozi basi nitaamini kwamba kweli kila jamii hustaili uongozi wa stairi yake.kwamba Vichaa huo na kiongozi kichaa,kwamba majambazi huwa na kiongozi jamazi,kwamba waelewa huwa na viongozi waelewa.
Mjadilini Dr Kitila kwa uwezo wake,uadilifu wake na uzalendo wake na siyo ubunge wake au uwaziri wake na pengine ujumbe wake wa UNO.asante.
 
Siasa si hesabu. Kama hujui kwamba hoja ya ukaskazini inatumika kuididimiza chadema basi una tatizo. Hata leo tu soma Tazama uk 2 imeandikwa kama ifuatavyo:
" Kauli hizo za mjumbe wa kamati Kuu ya chadema zimetafsiriwa na wachambuzi wa mambo ya kisiasa kwamba ni uthibitisho wa dhahiri dhidi ya tuhuma za muda mrefu kwamba chama hicho si cha kitaifa kama viongozi wake wanavyotaka kuwaaminisha watanzania, bali ni chama cha ukoo na watu wa kaskazini tu" Mwandishi ameandika utumbo mtupu ila sasa watanzania wengi wanayaamini haya. Ili kuwakata kilimilimi wapuuzi kama hawa, weka M/kiti ambaye si wa kaskazini. Hata kenya watu wanamshauri Uhuru Kenyatta asigombee maana rais anayemaliza muda wake ni Mkikuyu. pamoja na kwamba ni maarufu sana akipuuza ushauri huu utamgharimu. hii ni political tactic. Kuna tofauti kati ya ukweli na siasa.

Aisee nilikuwa sijakufahamu vizuri.........asante kwa kuwa muwazi ila siafiki hoja yako
 
Nakiri simfahamu vizuri huyo jamaa.
isipokuwa tunataka rais mwenye sifa moja kuu kwamba:-
1. ANA MAAMUZI YALIYONYOOKA [YASIYOFUATA UPEPO, YAANI MWENYE KUSIMAMIA ANACHOKIAMINI/AU ALICHOSHAURIWA NA KUKIKUBALI]
 
Kweli wehu mpo wengi humu! Yaani katika watu wote tulio nao mnamuongelea Kitila Mkumbo kwa Urais lazima mtoa mada anfikiri kwa kutumia masaburi!!!

mambo vipi mkuu.Tupe mafanikio katika ziara yako kanda ya ziwa!
 
Huu upuuzi unajengeka miongoni mwa watu kuwa watu wa kaskazini hawafai kuwa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania ni upofu na ufinyu wa mawazo, soma katiba sifa za kugombea urais ni zipi msikurupe kutoa mada za kipuuzi huku mkivunja katiba?? Mtu anayeingiza ukabila, udini ukanda katika suala la urais au uchaguzi wowote wa kisiasa ajue anavunja katiba na anapaswa kuadhibiwa kwa sheria zilizopo!! Huyu Dr. Mkumbo hana mdomo?? mwacheni muda ukifika atatoa uamuzi kwa kutumia haki yake ya kikatiba lakini msimsemee na kuanza kumhusisha na ukanda na ukabila!!!!

Mkuu nimekukubali. Kwani watu wa kaskazini wana nini? Hii ipo kwenye CCM na CDM why? huu ni ubaguzi ambao hauwezi kukubalika hata kidogo.
 
Endeleeni kugombana hivyo hivyo..mi nawashauri Mr. Sugu agombee.
Kwanza siyo wa kaskazini.
Pili anafahamika sana na majority ya watanzania.
Tatu,,,,ongezea wewe

Uko viloba nini?
 
Sredi yote imekosa mantiki kwa kuleta ubaguzi wa kikanda!!!!
Hii inaonesha wivu juu ya watu wa kandaya kanda ya kaskazini but ukweli unabaki pale pale watu wa kanda ya kaskazini ni wachapakazi ndo sababu kwao kuna maendeleo!!!

kuna maendeleo kuliko wapi?
 
Dr.slaa awe m/kiti chadema taifa & dr.kitila kumbo awe katibu mkuu wa chadema na alipwe kama anavyolipwa dr.slaa kwa sasa,hivyo chadema itatisha nchi nzima.
wewe mbilimbi unajua majukumu ya katibu mkuu???
kwa nini usiseme Kitilia awe mwenyekiti na SLAA abaki kwenye ukatibu???
katibu mkuu ndye injini ya chama
 
Yaani ukisoma comment karibu zote hapa utagundua ni kwa nini watanzania wengi wamezoea kuvurunda mambo, mtoa mada kavurunda kwa title yake! Lakini kwa mtu wa kiwango chochote kile akisoma ataelewa, sasa ajabu angalia wakuu hapa wamekomaa na urais wa nchi..

Uvivu wa kusoma ili uelewe tanasoma tu kama kasuku!
 
Msaliti mkubwa aliwahi kutusaliti tukidai mikopo wizara ya elimu ya juu..

Siwezi kumsahau huyu bonge ya opportunistic...

Huyo bado sana ..mwepesi sana anatumika vibaya
 
Msaliti mkubwa aliwahi kutusaliti tukidai mikopo wizara ya elimu ya juu..

Siwezi kumsahau huyu bonge ya opportunistic...

Huyo bado sana ..mwepesi sana anatumika vibaya

nilishakudharau siku nyingi kwa sababu wewe ni mtu unaendekeza sana udini!
 
Back
Top Bottom