POMPO
JF-Expert Member
- Mar 12, 2011
- 6,690
- 2,402
Waziri Simba akiwa shahidi wa 16 kwa upande wa mshitakiwa alitoa ushahidi wa kula chakula na wanachama wa CCM katika Hospitali ya Nkinga Kata ya Inkiga. Alikiri kula na watu zaidi ya 50 hali ambayo mawakili wa mlalamikaji waliendelea kumhoji wakihusisha maneno aliyotamka kuwa ‘msimchague Kashindye kwani hana mke pia ni masikini', hata hivyo Waziri huyo alikanusha kutoa kauli hiyo.
Akiwa shahidi wa 15 upande wa washitakiwa, Rage alikiri kushiriki kampeni hizo za uchaguzi akipangiwa kata za tarafa ya Igulubi. Wakili wa mlalamikaji alimhoji shahidi huyo juu ya umiliki wa bastola na kwa nini alikuwa nayo katika mikutano ya kampeni ambayo alishiriki.
Rage alikiri kumiliki bastola na kuwa nayo katika shughuli nzima za kampeni wakati huo. Hata hivyo, alisema upepo ulimponza ulipopeperusha shati lake na bastola hiyo kuonekana hadharani na vyombo vya habari kumpiga picha sawia.
Akiwa shahidi wa 15 upande wa washitakiwa, Rage alikiri kushiriki kampeni hizo za uchaguzi akipangiwa kata za tarafa ya Igulubi. Wakili wa mlalamikaji alimhoji shahidi huyo juu ya umiliki wa bastola na kwa nini alikuwa nayo katika mikutano ya kampeni ambayo alishiriki.
Rage alikiri kumiliki bastola na kuwa nayo katika shughuli nzima za kampeni wakati huo. Hata hivyo, alisema upepo ulimponza ulipopeperusha shati lake na bastola hiyo kuonekana hadharani na vyombo vya habari kumpiga picha sawia.