Dr. Kafumu (CCM) avuliwa ubunge Igunga!

Dr. Kafumu (CCM) avuliwa ubunge Igunga!

mwaka 20o9 nilikuwa na shughuli zangu katika bank ya nbc tawi la chuo kikuu cha dar-es salaam.
Baada muda akaingia magufuli,wakati huo akihangaikia na phd yake pale udsm, na kuanza kupiga soga na mtu mmoja.baadaye kidogo akaingia dkt wa kike mhadhiri udsm ambaye hajaolewa mpaka sasa.(naomba nisimtaje jina). Sasa magufuli alipomwona huyo mwanataaluma baada ya kusalimiana akamwuliza ,tena kwa sauti ya juu ,kiasi cha kila mtu aliyekuwepo ndani kusikia :''vipi umeshapata mchumba?''
nilimtazama huyo mwanataaluma na uso wake ulionyesha wazi kufaidhaika sana...kwa mtazamo wa baadhi ya wadau waliokuwepo pale, magufuli alikuwa amefanya utani usiopendeza na unaodunisha heshima ya mtu hasa jinsia ya kike.nami nilifadhaika sana.
Binafsi sikufurahishwa na kauli ya namna hiyo tena kutolewa na mtu wa hadhi ya waziri wa serikali.
Ni kweli kabisa magufuli ni mropokaji tena asiyechukua muda kupima kauli zake.hana busara wala hekima ingawa amepita shule.
ni vema tukumbuke kumpongeza
prof.abdalah safari kwa kuwa ndiye aliyekuwa akiiwakilisha chadema katika hiyo kesi.

bolded red sina cha kusema, lakini napendekeza tumfanyie harambe ya kumshukuru kwa uwakilishi uliotukuka. Mungu amjalie maisha marefu zaidi
 
huyu profesa abdala safari nilimvulia kofia pale alipotoa jibu kuhusu sekeseke la kuvuliwa hijabu kwa mama dc. Unajua alijibuje lile vumizo lililoanikizwa na ccm kuwakuvuliwa hijabu kwa mama huyu ni udhalilishaji wa kidini.
Profesa huyu yeye mwenyewe akiwa ni mwislamu wa swala tano ajibuje alipoulizwa? "iacheni mahakama iamuwe kama alichovuliwa mama dc ni hijabu au ni mtandio". kesi haikwenda mahakamani.

kesi iliienda mahakaman, na kama kawa CHADEMA walishinda kesi ile. Iliamuliwa kama sijakosea mwezi uliopita, mwezi wa saba
 
Prof. Abdala Safari deserves to be a law maker .... isn't it?
 
huyu hakimu kaongea ukweli ambao wenzake wanauficha. Big up kwake lakini sina imani na magamba kama watamwacha hivi hivi hawakawii kumtengenezea zengwe.
Nchi maskini ambayo haiachi kufanya uchaguzi kila kukicha kwa kutumia ela ya walipa kodi. Kweli tanzania ni mr.bean kwa majirani zetu.
 
Dah! Na zile mil 400 zake masikini ailizotoa majuzi, dah! Wanaigunga watamkumbuka kwa hilo
 
Maskini mwigulu nchemba.kumbe kazi ya kubebeshwa fuko la note kama punda ilikuwa ya bure.namuonea huruma.
 
Jaji Mary Nsimbo Shangali wa Mahakama kuu kanda ya Tabora kwa ujasiri mkubwa na kujiamini alisema hoja zilizothibitishwa na Mahakama na ambazo zimetumika kutengua matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Igunga ni hizi zifuatazo:

v Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alitumia nafasi yake ya uwaziri kutoa ahadi ya ujenzi wa Daraja la Mbutu ambalo lilikuwa ni moja ya kero kubwa kwa wananchi wa Jimbo la Igunga Dk Magufuli akiwa katika moja ya kampeni za uchaguzi huo, alitumia nafasi ya uwaziri kwa kuwatisha wapigakura wa jimbo hilo kwa kusema kama hawatamchagua mgombea wa CCM, watawekwa ndani.

v Jaji Shangali alitaja hoja nyingine iliyotumika kufuta matokeo hayo kuwa ni kauli ya Imamu Swaleh Mohamed wa Msikiti wa Ijumaa Igunga, kuwatangazia waumini wa msikiti huo kuwa wasikichague Chadema, kwa kuwa baadhi ya viongozi wake wamemdhalilisha Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatuma Kimario

v Hoja nyingine ambayo Jaji Shangali aliikubali ni ugawaji wa mahindi ya kuwawezesha wakazi wa Igunga kukabiliana na njaa wakati wa uchaguzi huo kwamba ulitumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa kuwashawishi wananchi wawapigie kura. Jaji huyo alihoji iwapo wakazi wa Jimbo la Igunga walikuwa na njaa sana wakati wa uchaguzi huo kiasi cha viongozi wa Serikali kuona kuwa ulikuwa wakati mwafaka wa kugawa mahindi hayo

v Alisema hoja nyingine ni Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama kudai kuwa Chadema kilileta makomandoo katika uchaguzi huo na kupanga kuuvuruga.

v Jaji Shangali aliendelea kueleza kuwa Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage alitangaza kuwa mgombea wa Chadema alikuwa amejitoa katika uchaguzi huo, jambo ambalo Mahakama imeridhishwa na ushahidi uliokuwa ukitolewa.

vKuhusu hoja ya upande wa utetezi kwamba mgombea wa Chadema, Kashindye alipaswa kupeleka malalamiko hayo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), alisema siyo ya msingi yanayoweza kumzuia mlalamikaji kupeleka malalamiko hayo katika Mahakama Kuu na hakuna kifungu chochote kinachomzuia mlalamikaji kufanya hivyo.

 
na huu ni ushindi wa Nape kwani walimkataa kushiriki kampeni Igunga

hapa heshima itapatikana tu
 
Hayo ndio matokeo ya kutaka kushinda at any cost. Wahusika walikuwa wanajua walichokifanya ni makosa kama Magufuli, na ndio sababu hakufika mahakamani hata baada ya kuombwa lakini waliamua kupuuza kwa ajili ya kupata ushindi ili wajiridhishe kuwa wananchi bado wanawapenda na matokeo ndio haya aibu tupu.

Waliodharirika hapa ni Kafumu mwenyewe Aden Rage, Katibu Mkuu wa CCM na TAKUKURU kwa kushindwa kuwakamata waliokuwa wakigawa mahindi na ukitaka kujua taasisi hii imeoza na inakula pesa za kodi za wananchi bure, hata baada ya CHADEMA kufikisha mahakami ushahidi wa baadhi ya viongozi wa CCM kugawa rushwa TAKUKURU haitowafuata kuwafungulia mashitaka licha ya mahakama kuwatamka kuwa ni watoa rushwa.
 
Huo ndo umakini wa Mwanasheria wa kujua namna ya kuandaa hoja, lakini mbona suala hili linafanana na la Segerea kwa ujumla wake.

Majimbo mengi nyinyiemu walishinda kwa hila lakini wajue haki haipotei kamwe na ndo mana hata mahudhurio bungeni hayaridhishi.
 
Huo ndo umakini wa mwanasheria wa kujua namna ya kuandaa hoja, lakini mbona suala hili linafanana na la Segerea kwa ujumla wake.Majimbo mengi nyinyiemu walishinda kwa hila lakini wajue haki haipotei kamwe na ndo mana hata mahudhurio bungeni hayaridhishi.

Hawakai bungeni wako busy kufanya transenction bank ya fedha walizokopa kwa ajili ya kuhonga kipindi cha kampeni za 2010
 
Mwenye kumbukumbu ya haraka alifahamishe, Tundu Lisu alimsemaje huyu jaji? Nataka nijue kama analysis ya Lisu ina mantiki
 
Jamani tutake tusitake haki ya mtu haipotei sana sana ni muda tu utasogea. Kinachotakiwa ni kutokukata tamaa. CCM wamekuwa na tabia kwamba hata wakichakachua anayeshindwa hawezi kudai au kushitaki kwa kuwa huwa wengi wetu hatuna uwezo hasa wa kifedha. Wabunge, madiwani hata serikali za mtaa walichakachua. La msingi tunakoelekea upeo wa uelewa wa wananchi unaongezeka kwa hiyo haki inachukua mkondo wake. Tungojee rufani ya Ubunge Arusha mjini itakuwaje! HAKI UWE RAIS, WAZIRI, MBUNGE, DIWANI, HAKIMU, MWALIMU, KASISI, SHEHE, BABA, MAMA, POLISI ETC itakuweka huru na utakuwa na utulivu ktk maisha yako!
 
Safi sana, mie edward lowasa, nape, mzee makamba, rostam, andrew chenge na mafisadi wengine tumefurai sana kwan kafumu hakuwa chaguo letu mafisadi tunaoifisadi nchi hii
 
Mwenye kumbukumbu ya haraka alifahamishe, Tundu Lisu alimsemaje huyu jaji? Nataka nijue kama analysis ya Lisu ina mantiki

Tukisema wanawake wengi ni MALAYA NA MACHANGUDOA ina maana na MKEO/MPENZIO yupo kundini.?
 
Back
Top Bottom