Hii ni failure kubwa kwa Mwigulu Nchemba. Igunga ndiye alikuwa kinara wa kampeni sasa chali, Arumeru Mashariki alikuwa kinara wa kampeni nako alipigwa mweleka. Sasa CCM waangalie sana huyu jamaa, atazidi kuwapeleka kaburini mapema.
Kwanini msimshukie Magufuli? yeye ndie alikacha kwenda kupangua ushahidi! sasa hata mkikata rufaa Magufuli atakwenda kukanusha tuhuma za kauri zake za rushwa ya kujenga daraja la Ndutu?
tutakata rufaa haki itapatikana..
nakumbuka sana mh. Nape nnauye ndo alikuwa wa kwanza kuja kuzomea chadema hapa jf, tunataka aje atoe msimamo wake hapa tena baada ya hukumu hii. Kwa kweli siku ile alitumia maneno ambayo hakustahili kuyatumia kwa nafasi yake. Ningefurahi akija tena leo tumsikie mh sana.
.WANA BODI MNAMKUMBUKA HUYU KIJANA AMBAYE MWIGULU ALIMWAGIA TINDIKALI NA KUSINGIZIA CHADEMA?
MWIGULU ALIPATA LAANA KUANZIA HAPA HADI SASA ANAENDELEA KUUWA VIJANA KWA KUTUMIA PROPAGANDA KUWA CHADEMA NI CHAMA CHA VURUGU... AIBU KUUWA, KUUMIZA KISA MADARAKA YA KISIASA... SASA KAFIKA WAPI HUYO KAMFUMU?
![]()
MKAZI wa Igunga, Kada wa CCM, Mussa Tesha aliyekuwa nchini India kwa matibabu baada ya kumwagiwa tindikali usoni na watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADAEMA), wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo jimboni humo (Igunga) mwaka jana, akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam, baada ya kurejea nchini. Kulia ni Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba ambaye alikuwa Meneja wa Kampeni za CCM jimboni humo.
HUKUMU ya IGUNGA Leo..Kashinje Vs Kafumu,
....Kwakweli mpaka sasa hivi Mbunge wa CCM ameshindwa kumleta shahidi ambaye angetoa taswira njema kwa Ushindi wa Kafumu.
Kwani Bwana Magufuli, ambaye yeye ametajwa kwenye Kesi mara kadhaa; kwamba alikuwa akitoa Ahadi ambazo alikuwa akitoa
mbele ya Jukwaa..kwa hali hiyo Mgombea Wa Chadema anasema alikuwa anatoa Kama Nani? Waziri au mpiga Debe wa CCM?
Kwakweli Kesi imekaa patamu sana...kama Haki ikitendeka ...Basi Jimbo tutalajie kuwa Wazi katika Hukumu ya Leo..!!!
=======
UPDATES
=======
Magari ya polisi, gari la maji washa, naona ndo yanawasili hapa mahakamani, ila bado hatujaingia ndani ya ukumbi wa mahakama, pia watu bado si wengi sana.
Taarifa kuwa Dk Peter Kafumu amevuliwa ubunge ni za kufurahisha kutokana na rafu aliyocheza yeye na chama chake kushinda ubunge. Sasa si siri kuwa CCM imo njia panda kuhusiana jinsi ya kurejesha kiti hicho hasa ikizingatiwa kilichotokea Arumeru Mashariki. Je kudondoka kwa Kafumu ni haki kutendeka au maandalizi ya kumrejesha ugani Rostam Aziz?
Nina kila sababu ya kupata Konyagi leo! Remmy, tafadhali sn leo nitakuwa pale YENU BAR kuanzia saa 2.30 za usiku, nikukabidhi kabisa haya mananihii aisee!, usikose. sweetlady, nyie huko Arusha mnisubiri tu, nina zawadi zenu wote, najua lile kinywaji lako unalotumia ambalo lina Historia ya kumsababishia mtu fulani Brain Concussion!
Nina kila sababu ya kupata Konyagi leo! Remmy, tafadhali sn leo nitakuwa pale YENU BAR kuanzia saa 2.30 za usiku, nikukabidhi kabisa haya mananihii aisee!, usikose. sweetlady, nyie huko Arusha mnisubiri tu, nina zawadi zenu wote, najua lile kinywaji lako unalotumia ambalo lina Historia ya kumsababishia mtu fulani Brain Concussion!
chadema yashinda rufaa igunga.....dr kafumu kukata rufaa mahakama kuu....chanzo habari leo