Dr. Kafumu (CCM) avuliwa ubunge Igunga!

Dr. Kafumu (CCM) avuliwa ubunge Igunga!

Ah Daraja la Mbutu ndo limemtoa mtu mjengoni.

LEKA DUTIGITE
 
ni kumshukuru mungu kwamba amesimama mwenyewe na haki imepatikana igunga ccm wameangukuia pua poleni sasa sijui kwa haya nape nauye atasemaje.daima ppls powerrrrrrrrrrrrrrr

hilo ZUZU nape litajikausha kama halijaona vile, kwani lina akili basi hilo li-nape???
 
Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Igunga amefunguka na kusema kuwa hakuwa na imani na jaji kwa kuwa aliegemea upande wa CHADEMA na matokeo yake ameipa CHADEMA ushindi.

Dk. Kafumu ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa yeye siyo mbunge tena na ataendelea na kazi yake ya utafiti wa madini.

source EAT
Mungu mkubwa dr. Kafumu hakua chaguo la wananchi.
 
Daraja la MBUTU na bastola ya Rage vimemmaliza baba wa watu. Yaani Rage alikuwa anaona ujiko kweli kupanda jukwaani na bastola, kumbe watu wanamchora tu. Aibu hata kwa wanasimba
 
Kuna kitu bado sijaelewa hapa wakuu .....
Kwa Dr. Kafumu kushindwa kesi je, tunarudia uchaguzi tena Igunga, ama ni by default Mwl. Kashindye anachukua Ubunge wa Igunga??

Hakimu ameaiagiza tume ya uchaguzi kuanza taratibu za kuandaa uchaguzi. Igunga jiandaeni kuona tena helikopta za CCM A, B na CDM. Wenye guest houses anzeni kupiga rangi, neema yaja, na wale wenzangu na mimi waficheni wake zenu, Chemba lazima lipite huko
 
Alidandia treni kwa mbele...teh teh teh! Siasa hizi si za kufuatilia kwa professionals wa aina yake.
 
Let the man go. By the way ameshaandika history kuwa alishawahi kuwa member of parliament maishani mwake. Ova.
 
Hadithi inayokuja,Ni ya Sungura sikia,...Hadithi uliyongoja,Leo ninakuletea.... Alitoka siku moja,njaa aliposikia,..Siku ile akaenda,porini kutembelea...Akayaona matunda mtini yameenea....Sungura akayapenda mtini akasogea,...Karuka tena karuka,Matunda hakufikia,mkononi hakutia Sungura nakuambia..SIZITAKI MBICHI HIZI sungura nakuambia,NAONA NAFANYA KAZI BILA FAIDA KUJUA.

Hii inanikumbusha na kale ka recent slogan.... "Tumteke kwa maslahi gani..."
 
Lakini anastahili sifa na heshima kwa kuamua kuishia kivyake.
anajuta kuifahamu ccm, ya majipwande, imemfanya aonekane kama mtu ambaye hakunda shule na sasa hivi anasikitika kweli madini kutosaidia watanzania, labda wazii wa sasa atamkumbuka kwenye ufalme wake, yaani akijiangalia anaendeshwa na nape, mwigula etc amechoka kweli kweli anajiuliza hivi mimi nimelogwa?
 
masikini kumbe hakuwa na imani na jaji hivi majaji huteuliwa na mwenyekiti wa chama gani? nayeye ni chama gani? bora angenyamaza kama aishe

Anaendelea kudhihirisha matamshi yaliyotamkwa na Tundu Lissu juu ya majaji wasio na sifa na vigezo, lkn hao hawakujiteua bali kuna mtu mmoja tu ndiye aliyewapa shavu naye ndiye m'kiti wa Kafumu
 
Bado nawalilia ndugu zetu walopigwa, kuteswa, kumwagiwa tindikali na kuuawa kwa ajili ya kukuweka wewe bungeni.
Bado tunayakumbuka matusi yenu na dharau kwa watanzania as if Mungu alipoiumba Tanzania alikiumba na chama cha mapinduzi kitawale.
Kafumu, mmesababisha watu wajane na mayatima. Kuwa mbunge hamkutakiwa kumwaga damu.

HAMKUTAKIWA KUUA ILI MUWE WABUNGE.
 
Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Igunga amefunguka na kusema kuwa hakuwa na imani na jaji kwa kuwa aliegemea upande wa CHADEMA na matokeo yake ameipa CHADEMA ushindi.

Dk. Kafumu ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa yeye siyo mbunge tena na ataendelea na kazi yake ya utafiti wa madini.

source EAT
Msomi uchwara,amegundua hilo baada ya kupigwa chini.
Sizitaki mbivu hizi teh! teh! teh!
 
Safari hii walisahau kumpenyezea muhishimiwa judge hukumu ya kuwabeba kama ile ya Arusha mjini na kule kwa Mahanga wakiamini hakimu atafanya bussiness as usual
 
asitudanganye aende fasta kukata rufaa kwani ccmabwepande hawako tayari kuingia kwenye uchaguzi kwani bado mzimu wa arumeru mashariki haujawaacha
 
safi sana yanajisafishanyenyewe jimbo letu hilo wamezidi zuluma haoooo??? chama cha wanaume kinaingia:flypig:
 
Haya tena kazi kwenu wana igunga msifanye tena makosa kuchagua gamba.Mungu kaamua kesi hiikwa haki
jifunzeni kwa wenzenu Arumeru chagueni CDM.
 
Mara baada ya kutolewa hukumu iliyotengua ubunge wa Dr. Dalali Kafumu, mbali na mambo mengine amenukuliwa akisema,''MIMI SIO MBUNGE WA IGUNGA TENA NA SASA NARUDI KWENYE KAZI YANGU YA UTAFITI WA MADINI'' huku akiwa na simanzi na hali ya kukata tamaa kabisa.

Hii ikiashiria hana mpango wa kukata rufani au kugombea tena japokuwa chama chake huenda kikamlazimisha kukata rufani kwa maslahi ya chama kuepuka kulikosa jimbo hilo kwa urahisi.

Sababu kadhaa zinaelezwa kuwa zimechangia hali hiyo:

1/Kususiwa kesi hivyo kujikuta anapigana vita mwenyewe(eg. kitendo cha magufuli kukataa kwenda kutoa ushahidi)

2/Gharama kubwa ya muda na pesa iliyoiingia kuupata ubunge lakini pia kuutetea mahakamani na pia kwa wananchi.(Ubunge kwake haulipi)

3/Kusutwa na dhamira yake(Hakufurahichwa na aina za hila zilizotumiwa na chama chake ili yeye awe mbunge)

4/Kuongezeka kwa Chuki dhidi yake na chama chake kutoka kwa wananchi wa jimbo lake(Amejaribu kutumia fedha zake nyingi ili kuwaridhisha wapiga kura wake lakini bado wameendelea kumnyoshea kidole)

5/Hakuwa mtu mwenye furaha toka ameupata ubunge

6/Hana uhakika wowote wa kurudi bungeni iwe kwa mahakama ya rufaa, uchaguzi kurudiwa ama 2015.
 
Back
Top Bottom