Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Tundu muongo, mnafik, mzandik.

Kwani shetani akimuita mtu kuwa (huyo mtu) ni "muongo, mnafiki, mzandiki" kuna ubaya gani? Nitatishika Bwana Yesu akiniita maneno hayo, sio shetani aslaani!
 
Dr.Kitima ni miongoni mwa watu ambao mara kwa mara huwa anaalikwa Star tv katika vipindi mbalimbali na niseme ukweli tu huwa navutiwa sana na michango na kauli zake kwenye vipindi anavyoalikwa na kwakweli siku zote huwa anakuwa "outspoken".Mara nyingi anakuwa ni mtu wa kuikosoa serikali bila woga wala hofu,naamini wale ambao huwa mnamfuatilia katika luninga mtakubaliana nami.

Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.

Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?

Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.

Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.

Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.

Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!

Sasa mansubiri huruma ya TEC kumuokoa LISSU? imekula kwenu, na wala msiingize TEC kwenye siasa.
 
lisemwalo either linaukweli or uwongo no matter what lisu ni mwongo wa kupindukia, mie ni mwanangu wa kalibu sana ila hakishikilia kitu chake hakiachii kwa kuwa huwa anasema tz bado ni wadhaifu sana, wakijua umesoma ata uwadanganye wanakubali kilahisi.

'''''nimeambiwa''''
 
Wewe changia mada kwa kujibu hoja na siyo kumtajataja mtu, nina mashaka na uelewa wako au la hujui unalolifanya ndo maana hoja zako siku zote ni majina ya watu tu na siyo maudhuhi.

ha ha ha we ndo kalagabao kabisaa.title ya mada ni jina la mtu.ungeanza kumkosoa mleta mada.ye ashachangia we thibitisha lisu sio mzandiki.kumbuka dunia ni watu sio matofari
 
Wewe changia mada kwa kujibu hoja na siyo kumtajataja mtu, nina mashaka na uelewa wako au la hujui unalolifanya ndo maana hoja zako siku zote ni majina ya watu tu na siyo maudhuhi.

Naona umepewa jibu zuri kabisa post #66 , unalo zaidi?
 
Vitu vingine haviitaji Ph D kujua ukweli. Kama Tindu aliongopa kuhusu Muswada, kwanini Mh JK anaurudisha tena Bungeni? Tuacheni ushabiki, ukweli always uibuka juu

aisee kumbee itakua TEC wamemshinikiza eti?
 
Vitu vingine haviitaji Ph D kujua ukweli. Kama Tindu aliongopa kuhusu Muswada, kwanini Mh JK anaurudisha tena Bungeni? Tuacheni ushabiki, ukweli always uibuka juu

Sikiliza usiwe punguani, muswaada umejadiliwa bungeni, kama mnaona una matatizo ulitaka aurudishe wapi? Kwani ule wa kwanza mlipoenda kumuona Ikulu aliurudisha wapi?

Muswaada umepita unakwenda hatua ya kusainiwa, unasainiwa, unarudishwa bungeni, kama mnataka marekebisho nendeni mkajadili marekebisho bungeni. Hizo ndio kanuni, hakuna longo-longo hapo.
 
Unaweza kaba koo taasisi kubwa za kidini zenye hadhi kubwa kama TEC na CCT? Pigana vita kote usisigee hizo taasisi kama CHADEMA inataka ipigwe chini nzima nzima uchaguzi 2015 pamoja na huyo Tundu Lisu isogeze vita zake kwenye hizo taasisi.Hizo taasisi ni moto wa kuotea mbali hasa kwa wanasiasa uchwara.

Huyo Padre katima na huyo mwingine wa CCT ni watu wadogo sana CCT na TEC hata kama waliiiona list ya wajumbe walioteuliwa katika hatua za awali haikuwa ndio fainal viongozi wa juu ambao ni maaskofu walikuwa na uwezo wa kuweka majina mengine tofauti na hilo la DR.katima na mwenzie yaliyopendekezwa bila kuwajibika kurudisha feedback kwa huyo Dr.KATIMA kwa kuwa kwa mfumo wao hawajibiki kwa junior.

Sasa kama huko mbele kwa mbele hakuona jina lake mtu wa kumwuuliza sio Tundu Lisu na hiyo kamati au Raisi .Na Chadema WAJIFUNZE Kuwasiliana na wakubwa wa taasisi za kidini kama raisi anavyofanya wakiiga staili hii ya tundu lissu ya kuwasiliana na kuchukulia serious hoja ya mtu mdogo wameisha.Raisi alichosema ni sahihi anajua alikopata majina.

Pole Tundu lISSU ULIYEPATA majina kwa DR.katima.

Mwongo sana wewe hujui hata channel of communication ya hizo taasisi sasa nani wa kufyekwa na hizo taasisi kama sio Mh sana Jakaya Kikwete aliyeweka watu anaowafahamu yeye na wasio toka taasisi hizo taja nani toka taasisi hizo kati ya wajumbe 30 wa tume saa zingine fikiria kwanza
 
Sikiliza usiwe punguani, muswaada umejadiliwa bingeni, kama mnaona una matatizo ulitaka aurudishe wapi? Kwani ule wa kwanza mlipoebda kumuona Ikulu aliurudisha wapi?

Muswaada umepita unakwenda hatua ya kusainiwa, unasainiwa, unarudishwa bungeni, kama mnataka marekebisho nendeni mkajadili marekebisho bungeni. Hizo ndio kanuni, hakuna longo-longo hapo.

kwa Kifupi Mwenyekiti wa CCM amedeclare kwamba wabunge wake ni maamuma , muswada unapitishwa unakuwa sheria baada ya Raisi kusaini halafu inarudishwa bungeni bila hata kutumika jibu ni kwamba wabunge wa CCM aka akina ndiyooooooooooooooooooooooo, hawako kwa ajili ya wananchi ila kwa ajili ya matumbo yao
 
Wewe akili ya Lissu na Kitima unaona zipo sawa?hawa wote wapenda sifa na camera hwana kitu........
Nadhani hawa watani zangu huwajui. Kitima hajawi kushika namba 2 na kama sikosei alikuwa na 1 pointi 5,
si udaktari wa sheria wa kupewa kausotea ulaya na UDSM. Usijadili mtu kwa kuwa unachuki nae.
 
"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."

msichanganye mada. Dr Tundu Lissu alichosema ni kwamba Alshaimaar Kwegir hakupendekezwa na walemavu bali kikwete alimteua kwa mapenz yake binafsi. Hapo ndipo jk akamuita kuwa ni muongo na mnafiki. Sasa niambie unafiki wa Lissu ni upi. Ina maana kwamba Alshaimaar alipendekezwa na walemavu akawawakilishe? Acheni wivu wa kike na uvivu wa kufikiri!
 
Nadhani hawa watani zangu huwajui. Kitima hajawi kushika namba 2 na kama sikosei alikuwa na 1 pointi 5,
si udaktari wa sheria wa kupewa kausotea ulaya na UDSM. Usijadili mtu kwa kuwa unachuki nae.

Dr kitima is a great schoolar ana degree ya theology na PHD ya laws.tatizo sio kitima ni tundu lisu.inaonekana hakua na dhamira njema.Kwani mpaka xaxa TEC wako kimya.tutabaki tunamwamini rais mpaka TEC waongee Tofauati.much respect to TEC
 
Sikiliza usiwe punguani, muswaada umejadiliwa bingeni, kama mnaona una matatizo ulitaka aurudishe wapi? Kwani ule wa kwanza mlipoebda kumuona Ikulu aliurudisha wapi?

Muswaada umepita unakwenda hatua ya kusainiwa, unasainiwa, unarudishwa bungeni, kama mnataka marekebisho nendeni mkajadili marekebisho bungeni. Hizo ndio kanuni, hakuna longo-longo hapo.

Kuna vitu vingine kusaini ni sawa na kuweka "najisi" katika document ya serikali!

Raisi makini hasaini upuuzi kwani ana haki ya kusaini au kutosaini!
 
Back
Top Bottom