Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Unaweza kaba koo taasisi kubwa za kidini zenye hadhi kubwa kama TEC na CCT? Pigana vita kote usisigee hizo taasisi kama CHADEMA inataka ipigwe chini nzima nzima uchaguzi 2015 pamoja na huyo Tundu Lisu isogeze vita zake kwenye hizo taasisi.Hizo taasisi ni moto wa kuotea mbali hasa kwa wanasiasa uchwara.

Huyo Padre katima na huyo mwingine wa CCT ni watu wadogo sana CCT na TEC hata kama waliiiona list ya wajumbe walioteuliwa katika hatua za awali haikuwa ndio fainal viongozi wa juu ambao ni maaskofu walikuwa na uwezo wa kuweka majina mengine tofauti na hilo la DR.katima na mwenzie yaliyopendekezwa bila kuwajibika kurudisha feedback kwa huyo Dr.KATIMA kwa kuwa kwa mfumo wao hawajibiki kwa junior.

Sasa kama huko mbele kwa mbele hakuona jina lake mtu wa kumwuuliza sio Tundu Lisu na hiyo kamati au Raisi .Na Chadema WAJIFUNZE Kuwasiliana na wakubwa wa taasisi za kidini kama raisi anavyofanya wakiiga staili hii ya tundu lissu ya kuwasiliana na kuchukulia serious hoja ya mtu mdogo wameisha.Raisi alichosema ni sahihi anajua alikopata majina.

Pole Tundu lISSU ULIYEPATA majina kwa DR.katima.

Mbulula hawaishi nchi hii.
Poor you.

Kitima amesema hayo mbele ya kamati ya katiba ya bunge.

Hajamwambia Lissu wakiwa bar.

What is wring with people of this land?!
 
Tusihukumu bila ushahidi.

Je, ikithibitika Jk ndio muongo,mnafiki na mzandiki utasema nini?

Kwanini watu hamuhoji ukimya wa hizi Taasisi?

Nasi tusiwe wanafiki!

Jiulize kwanini Tundu hajagusia kiini cha kuitwa muongo alipoitisha "press"?
 
TEC huwa hawatoi matamko ya hovyo hovyo kujibizana na wanasiasa
 
Tangu nifahamu kitu bunge sijawahi kuona mbunge kama Tundu Lissu. Anaposimama kuongea spika au naibu lazima abadilike sura, wabunge wa CCM wanaanza kushauriana counter attack. Zaidi ni kwamba hata mkuu wa nchi anamwogopa, anatumia nguvu nyingi kumchafua huku anakubali hoja zake zinazungumzika. Kama Lissu mnafiki kwa nini JK anaogopa kusaini muswada
 
TEC huwa hawatoi matamko ya hovyo hovyo kujibizana na wanasiasa

Bila shaka mnafurahia ukimya huu ili mtu wenu asiumbuke!

Hakuna siri chini ya jua!

Ni swala la muda tu kabla hatujamjua ni nani mnafiki,muongo na mzandiki.
 
msemaji wa.TEC ni askofu Mufumbusa au rais wa.baraza la maaskofu Tz askofu.Ngalalekumtwa wa Iringa.

Hao ndio mngewalaumu ila dr kitima ni padri wa kawaida sema cheo uVC wa saut ndio kilimpa umaarufu
 
Jiulize kwanini Tundu hajagusia kiini cha kuitwa muongo alipoitisha "press"?

Lissu kaongea kama mwanasheria kwa kueleza source ya taarifa alioitoa na hakuita waandishi kupiga porojo za "nimeambiwa","nimearifiwa" n.k.

Sasa wewe unataka aeleze kiini cha uzushi na uzandiki yeye atakitoa wapi??!!
 
Dr.Kitima ni miongoni mwa watu ambao mara kwa mara huwa anaalikwa Star tv katika vipindi mbalimbali na niseme ukweli tu huwa navutiwa sana na michango na kauli zake kwenye vipindi anavyoalikwa na kwakweli siku zote huwa anakuwa "outspoken".Mara nyingi anakuwa ni mtu wa kuikosoa serikali bila woga wala hofu,naamini wale ambao huwa mnamfuatilia katika luninga mtakubaliana nami.

Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.

Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?

Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.

Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.

Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.

Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!

Unapaswa kujua kuwa Dr. Kitima si msemaji wa TEC, na kama aliongea na Lissu basi waliongea kama marafiki ukizingatia wote wanatoka mkoa mmoja na jimbo moja, na hasa ukizingatia kuwa Dr. Kitima yupo mapumzikoni Singida baada ya kustaafu nafasi yake kule SAUT Mwanza. TEC ina uongozi wake na ina taratibu zake za kutoa taarifa na si kwa kukurupuka kama mnavyotaka. Kama kweli TEC walitoa malalamiko basi lazima yapo maandishi kwani TEC ambayo waliyawasilisha. Tatizo la wanasiasa wengi ni pale mtu anapotoa maoni yake binafsi na kuamua kwa maksudi kuyahusisha na taasisi anayotoka.

Uongozi wa TEC ni huu
1)The President of the Conference is Most Rt. Rev. Tarcisius Ngalalekumtwa. 2) Pro-President is Most Rt. Rev. Severine NiweMugizi
3) The General Secretary is Rev. Fr. Raymond Saba
 
Kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kuandika kipuuzi kama ulivyoandika hapo! Hivi wewe unamfikia dk Kitima hata kwa punje? Je unamfikia Lissu hata kwa nukta? Acha ushabiki wa akili za juha... Ukweli utakuweka huru.. Acha kuwa -----...
Wee hujui kitu,unamjua Kitima?au unafurahi kumuona akiendesha harakati?
Uwe unafuatilia mkuu,Kitima anaongea sana kuhusu serikali,wakati yeye mwenyewe kakiibia chuo mahela mengi,na katapeli vitu vingi,waulize watu waliosoma SAUT miaka ya 2009 hadi 2012,watakwambia
 
sasa nakutukana kama lusinde kule bungeni tayari nimekutukana.

"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."
 
mi siyo PS wa Dr. Fr. Kitima ila ninachojua ni kuwa huyu bwana yupo Ujerumani kwa sasa.....na aliisha hama kutoka mwanza ameenda kuanza ujenzi wa chuo kipya cha SAUT huko Mkulanga-Pwani
ni hayo...
 
...hahahaaa kweli kamanda lisu kawashika pabaya,mmeambiwa,mmesikia,mnadhani,labda,huenda,nahisi...

"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."
 
Bila shaka mnafurahia ukimya huu ili mtu wenu asiumbuke!

Hakuna siri chini ya jua!

Ni swala la muda tu kabla hatujamjua ni nani mnafiki,muongo na mzandiki.

TEC hawajawahi kifanya kazi kwa shinikizo la jf wala CDM,CCM,CUF na yeyote yule wakiona inafaa watatoa tamko au unawesa pia ukamshauri pia Lissu akaenda ofisi za akatuletee huo ushahidi
 
Last edited by a moderator:
Sidhani kama yeye ni msemaji wa TEC. Labda kama nimechanganya madesa.
 
"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."

Heri mnafiki kuliko anayesema fulani mnafiki au muongo bila kuthibitisha uongo huo au unafiki huo. Daima onyesha uongo wa muongo kwa kueleza ukweli wa jambo lenyewe. La sivyo wewe utakuwa mwongo zaidi na dhambi yako itakuwa kubwa zaidi.
 
TEC hawajawahi kifanya kazi kwa shinikizo la jf wala CDM,CCM,CUF na yeyote yule wakiona inafaa watatoa tamko au unawesa pia ukamshauri pia Lissu akaenda ofisi za akatuletee huo ushahidi

Kwa jambo kama hili huwezi kusubiri shinikizo bali wanatakiwa watumie busara.

Mbona wakimwagiwa tindikali hawachelewi kutoa matamko??!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom