Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Dr.Charles Kitima na wewe umenunuliwa?

Bimkubwa, maada ni hi, kwanini Dr. Charles Kitima awe kimya? Najua we sikuzote hua unaongozwa na chuki, lakini jikite kwenye maada, kama huwezi kuchangia hi, weka uzi wako unaomuhusu Tundu Lissu ili tuchangie huko.
Tundu muongo, mnafik, mzandik.
 
Mkuu,
Huyo Dr. Kitima hawezi kuongea kwasababu anajua ukweli wote.

Inaelekea kuna watu walimwambia amependekezwa na alitaka kuwemo kwenye hiyo tume. JK ana majina ya waliopendekezwa na ndio maana kajiamini mpaka kutumia lugha nzito dhidi ya Lissu.

Ukiwa na ushahidi unakuwa na nguvu zote za kuongea. Si unaona Lissu alianza na CET na sasa anasema Dr. Kitima na sio CET tena.
Kuna mtu kamdanganya Lissu hapo na yeye badala ya ku confirm na wahusika akaenda kumwaga desa lake kama lilivyo.

Hao Maaskofu, asingeteuliwa mtu wao ungewasikia wakiongea; sio waoga hao.
Dr.Kitima ni miongoni mwa watu ambao mara kwa mara huwa anaalikwa Star tv katika vipindi mbalimbali na niseme ukweli tu huwa navutiwa sana na michango na kauli zake kwenye vipindi anavyoalikwa na kwakweli siku zote huwa anakuwa "outspoken".Mara nyingi anakuwa ni mtu wa kuikosoa serikali bila woga wala hofu,naamini wale ambao huwa mnamfuatilia katika luninga mtakubaliana nami.

Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.

Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?

Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.

Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.

Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.

Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!
 
Unaweza kaba koo taasisi kubwa za kidini zenye hadhi kubwa kama TEC na CCT? Pigana vita kote usisigee hizo taasisi kama CHADEMA inataka ipigwe chini nzima nzima uchaguzi 2015 pamoja na huyo Tundu Lisu isogeze vita zake kwenye hizo taasisi.Hizo taasisi ni moto wa kuotea mbali hasa kwa wanasiasa uchwara.

Huyo Padre katima na huyo mwingine wa CCT ni watu wadogo sana CCT na TEC hata kama waliiiona list ya wajumbe walioteuliwa katika hatua za awali haikuwa ndio fainal viongozi wa juu ambao ni maaskofu walikuwa na uwezo wa kuweka majina mengine tofauti na hilo la DR.katima na mwenzie yaliyopendekezwa bila kuwajibika kurudisha feedback kwa huyo Dr.KATIMA kwa kuwa kwa mfumo wao hawajibiki kwa junior.

Sasa kama huko mbele kwa mbele hakuona jina lake mtu wa kumwuuliza sio Tundu Lisu na hiyo kamati au Raisi .Na Chadema WAJIFUNZE Kuwasiliana na wakubwa wa taasisi za kidini kama raisi anavyofanya wakiiga staili hii ya tundu lissu ya kuwasiliana na kuchukulia serious hoja ya mtu mdogo wameisha.Raisi alichosema ni sahihi anajua alikopata majina.

Pole Tundu lISSU ULIYEPATA majina kwa DR.katima.
Ndio maana mmetuma watu ili waongee na wakubwa wa CCT na TEC ili wasaidie kumwokoa rais baada ya kuona ameumbuliwa ehe! Tunawamulika kwa macho mawili na watu mliowatuma tumewaona! Kazi kuishi kisanii tu......
 
Amri ya 7 inawakataza WAKIRISTO kusema UONGO. Nina amini kabisa mwakilishi wa baraza la maaskofu (TEC) hawezi kusema uongo mbele ya kamati ya katiba ya Bunge.

Aliyesema uongo hapa anajulikana, lakini kwa kuwa ni MFALME bado anadanganywa kwamba nguo alizovaa zimempendeza ili hali yuko UCHI wa mnyama.

Kama TEC, CCT na walemavu wasingekuwa wamesema hayo mbele ya kamati ya Bunge ya katiba. Believe me Pindi Chana asingemu-spare TL angekwisha mmaliza siku nyingi.

Akili za kuambiwa changanya na za kwako!
 
Tundu muongo, mnafik, mzandik.

ww ni janga,ck zote ww ni mbabaishaji huna uwezo wa kujibu hoja.
kazi yako kushinda mtandaoni sijui ndio kazi yako.
FICHA UPUMBAVU WAKO USIFICHE HEKIMA NA BUSARA ZAKO
 
Hivi kwa akili ya kawaida Maaskofu wachague Mjumbe wao alafu wachezewe faulu??kisha wanyamaze!!! lazima pangechimbia,Lisu ukimwangalia usoni tu unajua hayuko sawa.kama hana radhi za Wazee wake basi alizaliwa njiti.
 
Kuna sakata gani kati ya jk na lisu lisu ni mnafiki,mzandiki na mmbea kuliko kawaida tangu jk amwambie ukweli mnahangaika sana kumcover lakini hamtaweza lisu ni mnafiki daima.
 
Tusihukumu bila ushahidi.

Je, ikithibitika Jk ndio muongo,mnafiki na mzandiki utasema nini?

Kwanini watu hamuhoji ukimya wa hizi Taasisi?

Nasi tusiwe wanafiki!

Ithibitike mara ngapi? mimi mwenyewe nina ushahidi wa kutosha kwamba Kikwete ni Muongo na Mnafiki, kuna siku tumeenda kumsikiliza, alivyo mnafiki baada ya kuona Watanzania walio wengi maisha yao ni magumu ila yeye na familia yake wapo vema akaamua kudanganya kwamba akichaguliwa atafanya maisha bora kwa kila Mtanzania lakini mimi nilishtukia tu kwamba huo ni unafiki na uongo kabisa, kikwete hana ujanja wa kufanya maisha bora kwa kila Mtanzania, kama Maraisi wa Marekani wenyewe wameshindwa kufanya maisha bora kwa kila Mmarekani sembuse Kikwete? Muongo mkubwa
 
ndio maana CCM inayumba kwa kukosa mtu wa kutoa taarifa sahihi,Nape anaongea yake,Bulembo anaongea yake
 
alishanunuliwa siku nyingi wewe waona leo ndo hujue hivyo ndo yuko kimya wala hataki bughudha
Dr.Kitima ni miongoni mwa watu ambao mara kwa mara huwa anaalikwa Star tv katika vipindi mbalimbali na niseme ukweli tu huwa navutiwa sana na michango na kauli zake kwenye vipindi anavyoalikwa na kwakweli siku zote huwa anakuwa "outspoken".Mara nyingi anakuwa ni mtu wa kuikosoa serikali bila woga wala hofu,naamini wale ambao huwa mnamfuatilia katika luninga mtakubaliana nami.

Lakini ninachoshangaa ni kwanini mpaka leo yuko kimya juu ya sakata hili la Kikwete na Tundu Lissu kuhusu uteuzi wa mjumbe wa TEC kwenye tume ya katiba.Dr.Kitima ndie alietajwa na mh.Lissu kuwa aliiambia kamati ya bunge ya katiba,sheria na utawala kuwa mtu alieteuliwa na Raisi kuingia katika tume hiyo hakupendekezwa na TEC.

Sasa Dr. unashindwa nini kusema hadharani juu ya hili?

Hata hivyo,inawezekana hawezi kuongea bila idhini ya TEC kuhusu jambo hii.

Itakuwa ni jambo la ajabu Taasisi ya kidini kushindwa kusema ukweli au kuficha ukweli.

Watanzania tuachane na Jk na Lissu na badala yake tuzikabe koo hizi Taasisi.Haiingii akilini kuwajadili Tundu Lissu na Kikwete bila kuhoji ukimya wa hizi Taasisi.

Kitu kingine cha kujiuliza ni mbona hawakuhoji uteuzi wa wajumbe hao mara baada ya majina ya wajumbe wa katiba mpya kutangazwa??!!
 
Kuna sakata gani kati ya jk na lisu lisu ni mnafiki,mzandiki na mmbea kuliko kawaida tangu jk amwambie ukweli mnahangaika sana kumcover lakini hamtaweza lisu ni mnafiki daima.

Tupe uthibitisho wa haya unayoyasema!

Hivi ina maana hiyo kamati ya bunge inayoongozwa na mbunge wa CCM Pindi Chanya ingeacha kweli kumuumbua Tundu Lissu kama alichosema kilikuwa ni uongo??!!

Unataka kuniambia Pindi Chanya alietetea hoja hii bungeni angeshindwa kutumia mwanya huu kujisafisha na kumuumbua Lissu??

Tumia tu akili ya kawaida utapata majibu labda uwe mvivu wa kufikiri.
 
kumbuka jk naye aliambiwa tu huenda waliomwambia ndo wazandiki na wfitini.
 
ww ni janga,ck zote ww ni mbabaishaji huna uwezo wa kujibu hoja.
kazi yako kushinda mtandaoni sijui ndio kazi yako.
FICHA UPUMBAVU WAKO USIFICHE HEKIMA NA BUSARA ZAKO

"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."
 
Bimkubwa, maada ni hi, kwanini Dr. Charles Kitima awe kimya? Najua we sikuzote hua unaongozwa na chuki, lakini jikite kwenye maada, kama huwezi kuchangia hi, weka uzi wako unaomuhusu Tundu Lissu ili tuchangie huko.

"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."
 
"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."

Madam pengine unapenda ku-cut na ku-paste
 
"Siyo tu kauli ya Mheshimiwa Tundu Lissu ni uzushi na uongo mtupu, bali pia ni ya unafiki, fitina na uzandiki wa hali ya juu."

"... (K)wa Mheshimiwa Tundu Lissu kudai kuwa mapendekezo ya TEC na CCT hayakuheshimiwa ni uongo wa mchana usiokuwa na kichwa wala miguu."

Ukweli ni upi? tupe fact ili tuone uzandiki wake na unafiki wake basi maana mnatalk talk tu
 
Back
Top Bottom