Naibu waziri wa makazi na mbunge wa Ilemela katoa somo zito la kukabiliana na msongamano Mwanza. Kasema ili kukabiliana na msongamano wa magari, Barabara ya Airport Igombe kayenze Sangabuye Kongolo hadi Magu inapaswa kuwekwa lami, Ili abiria wanaoshuka na ndege waendao Magu Lamadi Bunda hadi Musoma hawatahitaji kupita mjini kati.
Barabara ya Ilemela Kiseke hadi Buswelu nayo inapaswa kuwekewa lami, hii itasaidia watu watokao Ilemela na Airport kwenda Buswelu na Igoma haitawalazimu kwenda mjini kati, kwa kweli huyu mama anaona mbali sana, sasa tunaomba wakuu hebu wayafanyieni kazi mawazo ya huyu mbunge wetu.
Pia, Kasema serikali inapaswa kuharakisha kukamilisha uwanja wa mwanza ili uwe International, watalii sasa wapitie Mwanza badala ya KIA kwani kutoka mwanza hadi serengeti ni km 160 tu wakati kutoka KIA hadi serengeti ni 360km, hii itawapunguzia sana gharama watalii na kuwafanya kutopoteza muda mwingi barabarani. Hongera sana.
Barabara ya Ilemela Kiseke hadi Buswelu nayo inapaswa kuwekewa lami, hii itasaidia watu watokao Ilemela na Airport kwenda Buswelu na Igoma haitawalazimu kwenda mjini kati, kwa kweli huyu mama anaona mbali sana, sasa tunaomba wakuu hebu wayafanyieni kazi mawazo ya huyu mbunge wetu.
Pia, Kasema serikali inapaswa kuharakisha kukamilisha uwanja wa mwanza ili uwe International, watalii sasa wapitie Mwanza badala ya KIA kwani kutoka mwanza hadi serengeti ni km 160 tu wakati kutoka KIA hadi serengeti ni 360km, hii itawapunguzia sana gharama watalii na kuwafanya kutopoteza muda mwingi barabarani. Hongera sana.