DOWANS waisamehe TANESCO deni lote!

DOWANS waisamehe TANESCO deni lote!

tutakuja kulia kwa hii ishu ya dowans mpaka basi mi nawambi

tukitumia tu mitambo yao twafa....maana lazima deni lijilipe....kama tunasema bigi no na tuseme sasa na sio kusubiri
waiingie mkataba mpya
 
Ni mambo mengi JK kateleza ila hili nchi inajiendesha yenyewe...hatuna Rais
 
Si uliiona nyomi ya jana Mwanza?
Unafikiri hawana hakiri kabisa?
Sasa wametambua kuwa upepo unawaendea vibaya wanajaribu kujiosha.
Msimamo uleule kwa CHADEMA mpaka kieleweke.

kweli waliona ndio maana wame-act effectively.

lakini huo msamaha ni wa kweli?
lazima kuwe na reason behind the scene.
Either wameona wapretend kuwa wamesamehe then wainunue kwa bei maradufu huku wakilipana deni lao juu kwa juu

Jamani Nothing goes with Nothing
 
Hii yote, ni gia ya kuipigia upatu Dowans, ipate kazi nyingine ya kuzalisha umeme! Baadae mtasikia, mitambo yao inanunuliwa au imekodishwa na Tanesco ili kumaliza mgao! Ukweli ni kuwa, Dowans hawana pa kupeleka hiyo mitambo, wala hawana sehemu nyingine wanapofanya kazi au wanapoweza kupata kazi ya kufua na kulangua umeme, zaidi ya Tanzania. Huyu Makamba ni dalali tu!

Huo ndio mpango halisi uliopo kwa sasa kwa hiyo kama hujui basi elewa hilo ndilo lililopo kwenye table
Unadhania jamaa ni wajinga wasamehe tu na waondoke?
lazima wawe wamepewa donge jingine nono la kuwekeza zaidi kwenye nchi ya wadanganyika
 
Mi sasa hivi sitaki kusikia ishu ya hela, ninachotaka ni umeme. Walipe, wasilipe, najua hakuna kitakachobadilika chini ya serikali ya mafisadi...
Mjukuu wangu acha kukata tamaa mapema hata jioni haijafika wee
A coward people always die before their time
We will fight till the end,
Dr.Slaa amewapa siku 9 lasivyo ataitisha maandamano nchi nzima

 
wanazodai ni zaidi ya walizosamehe,sasa wangetaka walipwe yote ingekuwaje?kweli siasa ni mchezo mchafu
 
Basi mwanangu ngoja nikusimulie hadith ili ulale eee,

Hapo zamani za kale ilikuwa hiviii;

Dowans inadai Tanesco fidia ya bilioni kadhaa kwa mujibu wa hukumu ya ICC......Hatuna namna ni lazima tulipe hilo deni....wanaharakati wapinga malipo ya Dowans..... CC ya ccm waagiza serikali isilipe Dowans kwanza isubiri uamuzi wa mahakama.....UVCCM wadai wamtukana PhD wa ukweli kuhusu umiliki wa Dowans.....Ngeleja: Kikwete siyo mmiliki wa Dowans.....Kikwete: Siwafahamu wamiliki wa Dowans (Lakini serikali yake inasema ni lazima walipwe)......Kafulilia apeleka hoja binafsi bungeni....Dowans wasajili tuzo yao mahakama kuu.....Wanaharakati wasajili pingamizi mahakama kuu kuhusu tuzo ya Dowans.....January amwandikia Ngeleja barua.....January achakachuliwa kuwa M/kiti wa Kamati ya nishati.......Ngeleja atoa kauli ya serikali Bungeni.....January asema mitambo ya Dowans iwashwe....Ali Hadaiwi aongea na wahariri wa habari bila kamera (na simu zao pia zilikuwa hazina kamera).....Ali Hadaiwi akagua mitambo......Ali hadaiwi atinga Ikulu.....Dowans yaisamehe Tanesco deni (lakini wanadai nyingi kuliko walizosamehe).....

oooo mtoto mzuri unasinzia ee, basi tutaendelea na hadithi kesho eee, lala salama ee.
Ahsante sana Gurudumu kwa kutuhadithia Hadithi nzuri na ya kupendeza
basi nakwenda kulala salama etiii
 
Huyo munai ni wa wapi hapa Tanganyika??? Natamani tuanze kuwapiga mawe hawa wahusika wote, sababu mambo yao ya gizagiza tu. Anaishi wapi huyo?
usiwe na hofu mjukuu tutakupa taarifa ASAP baada ya intelijensia yetu kupata majibu kamili
tutamchunguza toka anaingia na anapotoka
we are still monitoring the situation
 
By Kambarage:

Sikilizeni WADANGANYIKA wenzangu. January Makamba ni wakala wa mafisadi. Amepewa ubunge na Rostam Aziz na Edward Lowassa ili wamtoe William Shellukindo aliyetoa uamuzi kamati ya ubunge ichunguze Richmond. Pia wamemuweka kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ya Bunge ya Nishati na Madini ili kufanikisha ufisadi wa Richmond/Dowans na uporaji mwingine mkubwa kwenye umeme na madini.

Ndiyo maana siku zote January anazungumzia Dowans eti kama mitambo hiyo ndiyo suluhisho pekee la tatizo la umeme Tanzania. Gridi ya taifa ina upungufu wa 230MW. Dowans inaweza kuzalisha maximum 100MW. Hivyo hata Dowans ikiwashwa, mgao wa umeme bado utaendelea.

Mpango uliopo ni kuwa eti Dowans wajidai wamesamehe kulipwa tozo ya 100bn/- ya ICC halafu wawashe umeme na kuwauzia Tanesco. Lengo ni kusaini mkataba wa miezi 3 na Tanesco wa kununua umeme.

Baada ya kuisha kwa mkataba huu wa miezi 3, kamati hiyo hiyo ya January itaiagiza Tanesco na Wizara ya Nishati na Madini inunue mitambo ya Dowans ili kukidhi tatizo la nishati.

Hivyo basi, ule mpango wa kifisadi wa siku nyingi wa kununua mitambo ya DOWANS utarudi kwa mlango wa nyuma na kuungwa mkono na wenyeviti kadhaa wa kamati za Bunge wakiongozwa na January Makamba, Zitto Kabwe, John Cheyo, Augustine Mrema, nk.

Kweli sisi Wadanganyika tutaendelea kuliwa mpaka kiama chini ya utawala wa CCM na mawakala wao kwenye kambi ya upinzani.

Nimeukubali uchambuzi wako. Hiyo siasa iliyochezwa bungeni ya kubadilisha maana ya kambi rasmi haikuwa bure. Ni kutokana na maana mpya ndio tukawapata kina John Cheyo na Lyatonga kama wenyeviti. Na Cheyo alisema atampigia debe mmoja kutoka CDM ambaye naamini ni huyu dogo kibaraka wao Zitto. Mmmh - Mambo ya mafisadi hayo! natamani kufa ...!
 
Suala sio kusamehe, lazima kuna kitu kimefanyika ili mambo yapoe. Kuna siri hapo imefichwa usikute tumelazimishwa kuwatumia Dowans kwa miaka kibao.
 
Nakumbuka TRA walizuia mitambo hiyo isihamishwe kwa vile Dowans wanadaiwa kodi. Nina uhakika hilo deni la kodi bado hawajalipa na tukawabana huenda hata hayo wanayosamehe hayafikii kodi hiyo.
TRA najua mnapitia humu jamvini, watembeleeni hao matapeli tujue kama wamelipa kodi yetu.
 
Kwani tuliwaomba watusamehe; tumewaambia hatuwalipi na majenereta yao hatununui wakitaka wakayauze Oman huko. Kwani wanogopa nini wakati kuna kesi zimefunguliwa mahakamani kupinga hiyo tuzo? Wanaogopa kushindwa kwenye mahakama zetu?
 
Hapa JahK, hapa Lowesha,
Hapa Rost, hapa Al Adaiwi
Hapa kiiNgeleja hapa Jahnuwari
Hapa chao, hapa zao!
Wapi chetu walwa!?
a?
 
Hii inawezekana ikawa danganya toto tu. Watanzania tuwe macho, wanaweza kutoa taarifa hizi but behind the curtain wakalipwa.
Maandamano ya wananchi nayo yamesaidia kutoa changamoto kwa serikali ya kishikaji ya CCM.

Tanzania kila kitu kinawezekana kabisa, tatizo ni maamuzi. Watanzania wameandamana kupinga ongezeko la bei ya sukari, serikali imesharukia na kudai itapunguza. Tuyaongeze haya maandamano hadi kieleweke, sisi ndiyo wenye nchi. They have to obey what we WANT.
 
Kwani tuliwaomba watusamehe; tumewaambia hatuwalipi na majenereta yao hatununui wakitaka wakayauze Oman huko. Kwani wanogopa nini wakati kuna kesi zimefunguliwa mahakamani kupinga hiyo tuzo? Wanaogopa kushindwa kwenye mahakama zetu?

Mkuu uliwahi kusoma simulizi za gaidi mmoja zamani anaitwa Carlos? Nahisi ama kuna jambo kubwa tayari hawa mafisadi wameshafanya kupata pesa yao hivyo sasa wanajisiemea "bakini na hiyo tuzo yenu sisi tumepata zaidi"
 
Wamesamehe sababu wamesoma alama za nyakati. They couldn't keep up with the lies as paying them would have compromised a lot. a lot that had been built on unnecessary lies.
Hili ni fundisho kwa mafisadi na vibaraka vyao.
 
Kwa taarifa ya Radio Tumaini, leo asubuhi saa 3, Dowans wamekubali kusamehe shirika la TANESCO deni la Bil 94. Hii naona ni habari njema. Kitu ninachojiuliza ni sababu ipi iliyopelekea hatua hiyo kutoka kampuni ya DOWANS kufikia uamuzi huo kwa sasa.

Mimi naona ni kichekesho tu ila kuna 'hidden agenda' kubwa si bure, na ulaji kama kawaida kwa wakubwa wa wizara na wengineo
 
Back
Top Bottom