punainen-red
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 1,731
- 451
Huyo munai ni wa wapi hapa Tanganyika??? Natamani tuanze kuwapiga mawe hawa wahusika wote, sababu mambo yao ya gizagiza tu. Anaishi wapi huyo?
Huyo munai ni wa wapi hapa Tanganyika??? Natamani tuanze kuwapiga mawe hawa wahusika wote, sababu mambo yao ya gizagiza tu. Anaishi wapi huyo?
Tanesco wakikubali huo msamaha watakuwa wamekubali kushindwa katika kesi na pingamizi walilolitoa litakuwa halina maana. Anayekubali msamaha ni yule aliyekili kosa. Hawa mafisadi ni wajanja sana wakati kesi iko mahakama kuu wanajifanya eti kutoa msamaha! kwa nini wasisubiri kesi iishe?Dowans sasa yalainika, wafuta deni kwa Tanesco
Na Richard Makore
25th February 2011
Sasa wataka walipwe tu Sh. bilioni 36![]()
![]()
January Makamba
Kampuni ya Dowans Tanzania Limited ya kufua umeme wa dharura ambayo ilishinda kesi dhidi ya Tanesco katika Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) na kupewa tuzo ya Sh. bilioni 94, sasa imelainika na imetangaza kusamehe deni hilo.
Uamuzi huu ambao unatangazwa baada ya kuwapo kwa malumbano makali nchini juu ya hukumu ya ICC na kiasi cha fedha kilichotolewa, sasa Dowans wanataka Tanesco ilipe tu Dola za Marekani milioni 24 (Sh. bilioni 36 tu). Fedha hizo ni gharama halisi ya umeme uliouzwa kwa Tanesco.
....................................Hata hivyo Dowans imesema licha ya kutoa msamaha huo, Tanesco bado imeshindwa kujibu kama imeukubali msamaha huo au la ili mazungumzo yaanze.
Munai alidai fedha wanazolidai shirika hilo kwa sasa zinakaribia Sh. bilioni 99 badala ya Sh. bilioni 94 za mwaka jana.
Alisema ongezeko hilo limetokana na kampuni ya Dowans kuitoza Tanesco kila siku Dola za Marekani 11, 800 (Sh. milioni 15.3) kama gharama za kuweka mtambo hata kama hauzalishi umeme na kwamba nyongeza ya gharama hizo ilianza kutozwa kila siku tangu Juni 15, mwaka 2010 hadi sasa.
Alisema deni la Sh. bilioni 94 liliishia Juni 14, mwaka 2010 na baada ya hapo limekuwa likiongezeka siku hadi siku. Munai aliwaambia waandishi wa habari walioambatana na kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuwa kampuni yake haina tatizo kuhusu kusamehe deni hilo, lakini Tanesco muda wote imekuwa haitaki kukubali msamaha huo.
Aliongeza kuwa ikiwa Tanesco na Serikali watakataa kupokea msamaha huo nje ya mahakama na wao wataacha sheria iendelee kuchukua mkondo wake.
Munai alisema mkataba kati ya Dowans na Tanesco unasema kuwa ikiwa pande hizo mbili zitatofautiana na zikaenda kwa msuluhishi maamuzi yatakayotolewa yatatakiwa kuheshimiwa na pande zote na hakuna upande utakaoruhusiwa kukata rufaa.
Kwa mujibu wa mkataba huu, Tanesco haiwezi kukata rufaa kwa kuwa kipengele hicho kinawazuia na wao wanajua, lakini hajui ni kwanini hawataki kuwaambia wananchi ukweli, alisema.
CHANZO: NIPASHE
Na kweli DOWANS ni kama DAYS OF OUR LIVES unaona mchezo unaelekea kuisha mara inaanza episode mpya
I MUST BE DREAMING!!
Eti wakuu..
Huyu Munai ni kama nani pale Dowans? na alikuwa wapi siku zote hizo...
Basi mwanangu ngoja nikusimulie hadith ili ulale eee,
Hapo zamani za kale ilikuwa hiviii;
Dowans inadai Tanesco fidia ya bilioni kadhaa kwa mujibu wa hukumu ya ICC......Hatuna namna ni lazima tulipe hilo deni....wanaharakati wapinga malipo ya Dowans..... CC ya ccm waagiza serikali isilipe Dowans kwanza isubiri uamuzi wa mahakama.....UVCCM wadai wamtukana PhD wa ukweli kuhusu umiliki wa Dowans.....Ngeleja: Kikwete siyo mmiliki wa Dowans.....Kikwete: Siwafahamu wamiliki wa Dowans (Lakini serikali yake inasema ni lazima walipwe)......Kafulilia apeleka hoja binafsi bungeni....Dowans wasajili tuzo yao mahakama kuu.....Wanaharakati wasajili pingamizi mahakama kuu kuhusu tuzo ya Dowans.....January amwandikia Ngeleja barua.....January achakachuliwa kuwa M/kiti wa Kamati ya nishati.......Ngeleja atoa kauli ya serikali Bungeni.....January asema mitambo ya Dowans iwashwe....Ali Hadaiwi aongea na wahariri wa habari bila kamera (na simu zao pia zilikuwa hazina kamera).....Ali Hadaiwi akagua mitambo......Ali hadaiwi atinga Ikulu.....Dowans yaisamehe Tanesco deni (lakini wanadai nyingi kuliko walizosamehe).....
oooo mtoto mzuri unasinzia ee, basi tutaendelea na hadithi kesho eee, lala salama ee.
Haitoshi tunataka mitambo itaifishwe kwanza nasikia wanadaiwa na benki karibu bil.100 halafu pia walikuwa hawalipi kodi.
Kwa taharifa ambazo mimi ninazo ni kwamba Dowans wapo tayari kuisamehe Tanesco lakini kwa masharti maalumu.
Bado hawajawasamehee ila wapo tayari endapo watakaa na kuzungumza na Tanesco wanatakiwa wayakubali hayo masharti ya kifisadi.